Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 253

۞تِلۡكَ ٱلرُّسُلُ فَضَّلۡنَا بَعۡضَهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖۘ مِّنۡهُم مَّن كَلَّمَ ٱللَّهُۖ وَرَفَعَ بَعۡضَهُمۡ دَرَجَٰتٖۚ وَءَاتَيۡنَا عِيسَى ٱبۡنَ مَرۡيَمَ ٱلۡبَيِّنَٰتِ وَأَيَّدۡنَٰهُ بِرُوحِ ٱلۡقُدُسِۗ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ مَا ٱقۡتَتَلَ ٱلَّذِينَ مِنۢ بَعۡدِهِم مِّنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَتۡهُمُ ٱلۡبَيِّنَٰتُ وَلَٰكِنِ ٱخۡتَلَفُواْ فَمِنۡهُم مَّنۡ ءَامَنَ وَمِنۡهُم مَّن كَفَرَۚ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ مَا ٱقۡتَتَلُواْ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ يَفۡعَلُ مَا يُرِيدُ

Hao Mitume baadhi yao tumewatukuza zaidi kuliko wengine. Katika wao wapo ambao Allah alisema nao, na baadhi yao amewatukuza daraja mbalimbali. Na Isa mwana wa Mariamu tukampa hoja zilizo wazi, na tulimpa nguvu kwa Roho Takatifu. Na kama Allah angetaka, wasingelipigana waliokuja baada yao, baada ya kuwafikia hoja zilizo wazi, na lakini walihitilafiana. Basi wapo miongoni mwao walioamini, na wapo miongoni mwao waliokufuru. Na kama Allah angelitaka, wasingelipigana na lakini Allah hufanya ayatakayo



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 254

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَنفِقُواْ مِمَّا رَزَقۡنَٰكُم مِّن قَبۡلِ أَن يَأۡتِيَ يَوۡمٞ لَّا بَيۡعٞ فِيهِ وَلَا خُلَّةٞ وَلَا شَفَٰعَةٞۗ وَٱلۡكَٰفِرُونَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ

Enyi mlioamini, toeni katika vile tulivyowapeni kabla haijafika siku ambayo haitakuwa na mauzo wala urafiki wala uombezi, na makafiri ndio wenye kudhulumu



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 255

ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ ٱلۡحَيُّ ٱلۡقَيُّومُۚ لَا تَأۡخُذُهُۥ سِنَةٞ وَلَا نَوۡمٞۚ لَّهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۗ مَن ذَا ٱلَّذِي يَشۡفَعُ عِندَهُۥٓ إِلَّا بِإِذۡنِهِۦۚ يَعۡلَمُ مَا بَيۡنَ أَيۡدِيهِمۡ وَمَا خَلۡفَهُمۡۖ وَلَا يُحِيطُونَ بِشَيۡءٖ مِّنۡ عِلۡمِهِۦٓ إِلَّا بِمَا شَآءَۚ وَسِعَ كُرۡسِيُّهُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَۖ وَلَا يَـُٔودُهُۥ حِفۡظُهُمَاۚ وَهُوَ ٱلۡعَلِيُّ ٱلۡعَظِيمُ

Allah, hakuna anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Yeye tu. Yeye ndiye Mwenye uhai wa milele, Mwenye kusimamia kila kitu. Hapatwi na kusinzia wala kulala. Ni vyake yeye tu vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Ni nani awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao, wala hawajui kitu katika elimu yake isipokuwa atakacho tu. Kursi yake imezienea mbingu na ardhi wala hakumchoshi kuzihifadhi (mbingu, ardhi na vilivyomo), na Yeye ndiye aliye juu na ndiye aliye Mkuu



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 256

لَآ إِكۡرَاهَ فِي ٱلدِّينِۖ قَد تَّبَيَّنَ ٱلرُّشۡدُ مِنَ ٱلۡغَيِّۚ فَمَن يَكۡفُرۡ بِٱلطَّـٰغُوتِ وَيُؤۡمِنۢ بِٱللَّهِ فَقَدِ ٱسۡتَمۡسَكَ بِٱلۡعُرۡوَةِ ٱلۡوُثۡقَىٰ لَا ٱنفِصَامَ لَهَاۗ وَٱللَّهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ

Hakuna kulazimisha (watu kuingia) katika dini. Hakika, uongofu umekwishajitenga na upotovu. Basi anayemkataa Twaghuti na kumuamini Allah, bila shaka yeye ameshika kishikio madhubuti kisichovunjika. Na Allah ni Mwenye kusikia sana, Mjuzi sana



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 257

ٱللَّهُ وَلِيُّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ يُخۡرِجُهُم مِّنَ ٱلظُّلُمَٰتِ إِلَى ٱلنُّورِۖ وَٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَوۡلِيَآؤُهُمُ ٱلطَّـٰغُوتُ يُخۡرِجُونَهُم مِّنَ ٱلنُّورِ إِلَى ٱلظُّلُمَٰتِۗ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Allah ni Mwenye kuwanusuru wale walioamini; huwatoa gizani na kuwapeleka kwenye mwangaza. Na ambao wamekufuru, watetezi wao ni Matwaghuti; huwatoa katika nuru na kuwaingiza kwenye giza. Hao ndio watu wa Motoni, wao humo watasalia milele



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 258

أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِي حَآجَّ إِبۡرَٰهِـۧمَ فِي رَبِّهِۦٓ أَنۡ ءَاتَىٰهُ ٱللَّهُ ٱلۡمُلۡكَ إِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِـۧمُ رَبِّيَ ٱلَّذِي يُحۡيِۦ وَيُمِيتُ قَالَ أَنَا۠ أُحۡيِۦ وَأُمِيتُۖ قَالَ إِبۡرَٰهِـۧمُ فَإِنَّ ٱللَّهَ يَأۡتِي بِٱلشَّمۡسِ مِنَ ٱلۡمَشۡرِقِ فَأۡتِ بِهَا مِنَ ٱلۡمَغۡرِبِ فَبُهِتَ ٱلَّذِي كَفَرَۗ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Je, hukumuona yule aliyehojiana na Ibrahimu kuhusu Mola wake kwa sababu Allah alimpa ufalme? Pindi Ibrahim aliposema: Mola wangu ni yule anayehuisha na kufisha. Akasema: Mimi pia nahuisha na kufisha. Ibrahim akasema: Hakika Allah hulileta jua kutokea mashariki basi wewe lilete kutokea magharibi, basi akaduwaa yule aliyekufuru. Na Allah hawaongozi watu madhalimu



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 259

أَوۡ كَٱلَّذِي مَرَّ عَلَىٰ قَرۡيَةٖ وَهِيَ خَاوِيَةٌ عَلَىٰ عُرُوشِهَا قَالَ أَنَّىٰ يُحۡيِۦ هَٰذِهِ ٱللَّهُ بَعۡدَ مَوۡتِهَاۖ فَأَمَاتَهُ ٱللَّهُ مِاْئَةَ عَامٖ ثُمَّ بَعَثَهُۥۖ قَالَ كَمۡ لَبِثۡتَۖ قَالَ لَبِثۡتُ يَوۡمًا أَوۡ بَعۡضَ يَوۡمٖۖ قَالَ بَل لَّبِثۡتَ مِاْئَةَ عَامٖ فَٱنظُرۡ إِلَىٰ طَعَامِكَ وَشَرَابِكَ لَمۡ يَتَسَنَّهۡۖ وَٱنظُرۡ إِلَىٰ حِمَارِكَ وَلِنَجۡعَلَكَ ءَايَةٗ لِّلنَّاسِۖ وَٱنظُرۡ إِلَى ٱلۡعِظَامِ كَيۡفَ نُنشِزُهَا ثُمَّ نَكۡسُوهَا لَحۡمٗاۚ فَلَمَّا تَبَيَّنَ لَهُۥ قَالَ أَعۡلَمُ أَنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ

Au kama yule aliyepita katika kitongoji nacho kikiwa kimeporomokeana mapaa yake (kimekufa). Akasema: Allah atakiuhishaje kitongoji hiki baada ya kudamirika (kuteketea) kwake? Basi Allah akamfisha miaka mia, kisha akamhuisha. Akamwambia: Je, umekaa muda gani? Akajibu: Nimekaa siku moja au baadhi ya siku. Akamwambia: Bali umekaa miaka mia. Hebu tazama chakula chako na kinywaji chako; havijavunda. Na mtazame punda wako. Na ili tukufanye ishara kwa watu, itazame mifupa jinsi tunavyoikusanya na jinsi tunavyoivika nyama. Basi ulipomdhihirikia (uweza wa Allah), akasema: Najua kwamba, Allah ni Muweza wa kila kitu



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 260

وَإِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِـۧمُ رَبِّ أَرِنِي كَيۡفَ تُحۡيِ ٱلۡمَوۡتَىٰۖ قَالَ أَوَلَمۡ تُؤۡمِنۖ قَالَ بَلَىٰ وَلَٰكِن لِّيَطۡمَئِنَّ قَلۡبِيۖ قَالَ فَخُذۡ أَرۡبَعَةٗ مِّنَ ٱلطَّيۡرِ فَصُرۡهُنَّ إِلَيۡكَ ثُمَّ ٱجۡعَلۡ عَلَىٰ كُلِّ جَبَلٖ مِّنۡهُنَّ جُزۡءٗا ثُمَّ ٱدۡعُهُنَّ يَأۡتِينَكَ سَعۡيٗاۚ وَٱعۡلَمۡ أَنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٌ حَكِيمٞ

Na kumbuka Ibrahimu aliposema: (Ewe) Mola wangu, nioneshe namna unavyofufua wafu. Akamwambia: Kwani hukuamini? Akasema: Kwanini nisiamini? Bali nimeuliza hivyo ili moyo wangu utulie. Akasema: Basi chukua ndege wanne na uwakusanye kwako kisha weka juu ya kila jabali sehemu ya ndege hao, kisha uwaite, watakujia kwa kasi. Na jua ya kwamba, Allah ni Mwenye nguvu kubwa, Mwenye hekima nyingi



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 261

مَّثَلُ ٱلَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمۡوَٰلَهُمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ كَمَثَلِ حَبَّةٍ أَنۢبَتَتۡ سَبۡعَ سَنَابِلَ فِي كُلِّ سُنۢبُلَةٖ مِّاْئَةُ حَبَّةٖۗ وَٱللَّهُ يُضَٰعِفُ لِمَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ وَٰسِعٌ عَلِيمٌ

Mfano wa wale wanaotoa mali zao katika njia ya Allah ni kama mfano wa punje iliyotoa mashuke saba, ikawa katika kila shuke mna punje mia. Na Allah humuongezea amtakaye, Na Allah ni Mwingi wa fadhila, Mjuzi mno



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 262

ٱلَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمۡوَٰلَهُمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ ثُمَّ لَا يُتۡبِعُونَ مَآ أَنفَقُواْ مَنّٗا وَلَآ أَذٗى لَّهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ وَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Wale wanaotoa mali zao katika njia ya Allah, kisha wasifuatishe yale waliyoyatoa kwa masimbulizi wala maudhi, wana malipo yao kwa Mola wao, wala hawatakuwa na hofu na hawatahuzunika



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 263

۞قَوۡلٞ مَّعۡرُوفٞ وَمَغۡفِرَةٌ خَيۡرٞ مِّن صَدَقَةٖ يَتۡبَعُهَآ أَذٗىۗ وَٱللَّهُ غَنِيٌّ حَلِيمٞ

Kauli njema na kusamehe ni bora kuliko sadaka inayofuatishwa na maudhi, na Allah ni Mkwasi sana, Mpole mno



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 264

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تُبۡطِلُواْ صَدَقَٰتِكُم بِٱلۡمَنِّ وَٱلۡأَذَىٰ كَٱلَّذِي يُنفِقُ مَالَهُۥ رِئَآءَ ٱلنَّاسِ وَلَا يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِۖ فَمَثَلُهُۥ كَمَثَلِ صَفۡوَانٍ عَلَيۡهِ تُرَابٞ فَأَصَابَهُۥ وَابِلٞ فَتَرَكَهُۥ صَلۡدٗاۖ لَّا يَقۡدِرُونَ عَلَىٰ شَيۡءٖ مِّمَّا كَسَبُواْۗ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Enyi mlioamini, msizibatilishe sadaka zenu kwa masimbulizi na maudhi, kama yule anayetoa mali yake kwa kuwaonesha watu, na hamuamini Allah na Siku ya Mwisho. Basi mfano wake ni kama jiwe lenye kuteleza ambalo juu yake kuna mchanga, kisha likanyeshewa na mvua kubwa na ikaliacha tupu. Basi hawatakuwa na uwezo juu ya chochote katika walicho kichuma, na Allah hawaongozi watu makafiri



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 265

وَمَثَلُ ٱلَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمۡوَٰلَهُمُ ٱبۡتِغَآءَ مَرۡضَاتِ ٱللَّهِ وَتَثۡبِيتٗا مِّنۡ أَنفُسِهِمۡ كَمَثَلِ جَنَّةِۭ بِرَبۡوَةٍ أَصَابَهَا وَابِلٞ فَـَٔاتَتۡ أُكُلَهَا ضِعۡفَيۡنِ فَإِن لَّمۡ يُصِبۡهَا وَابِلٞ فَطَلّٞۗ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٌ

Na mfano wa wale wanaotoa mali zao kwa kuzitafuta radhi za Allah kwa uthabiti na yakini wa nafsi zao, ni kama mfano wa bustani iliyo katika muinuko, ipatayo mvua nyingi, na ikatoa matunda yake maradufu, na isiponyeshewa na mvua nyingi, mvua chache (hutosha) na Allah anayajua mnayoyatenda



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 266

أَيَوَدُّ أَحَدُكُمۡ أَن تَكُونَ لَهُۥ جَنَّةٞ مِّن نَّخِيلٖ وَأَعۡنَابٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ لَهُۥ فِيهَا مِن كُلِّ ٱلثَّمَرَٰتِ وَأَصَابَهُ ٱلۡكِبَرُ وَلَهُۥ ذُرِّيَّةٞ ضُعَفَآءُ فَأَصَابَهَآ إِعۡصَارٞ فِيهِ نَارٞ فَٱحۡتَرَقَتۡۗ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ ٱللَّهُ لَكُمُ ٱلۡأٓيَٰتِ لَعَلَّكُمۡ تَتَفَكَّرُونَ

Je, anapenda mmoja wenu kuwa na bustani ya mitende na mizabibu, itiririkayo mito chini yake, naye humo hupata matunda ya kila namna, na ukamfikia uzee, na ana watoto dhaifu, mara kimbunga chenye moto kikaikumba bustani hiyo na ikaungua. Hivyo ndivyo Allah anavyo kubainishieni Aya zake ili mpate kufikiri



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 267

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَنفِقُواْ مِن طَيِّبَٰتِ مَا كَسَبۡتُمۡ وَمِمَّآ أَخۡرَجۡنَا لَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِۖ وَلَا تَيَمَّمُواْ ٱلۡخَبِيثَ مِنۡهُ تُنفِقُونَ وَلَسۡتُم بِـَٔاخِذِيهِ إِلَّآ أَن تُغۡمِضُواْ فِيهِۚ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ غَنِيٌّ حَمِيدٌ

Enyi mlioamini, toeni katika vitu vizuri mlivyovichuma, na katika vile tulivyowatoleeni kutoka katika ardhi. Na msikusudie (kutoa) kibaya na hali nyinyi hamkuwa ni wenye kukipokea (kama mtapewa) ila kwa kukifumbia macho, najueni kwamba, Allah ni Mkwasi, Mwenye kuhimidiwa mno



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 268

ٱلشَّيۡطَٰنُ يَعِدُكُمُ ٱلۡفَقۡرَ وَيَأۡمُرُكُم بِٱلۡفَحۡشَآءِۖ وَٱللَّهُ يَعِدُكُم مَّغۡفِرَةٗ مِّنۡهُ وَفَضۡلٗاۗ وَٱللَّهُ وَٰسِعٌ عَلِيمٞ

Shetani anakutieni hofu ya ufukara na anakuamrisheni uovu, na Allah anakuahidini msamaha utokao kwake na ziada, na Allah ni Mwenye wasaa sana, Mwenye kujua mno



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 269

يُؤۡتِي ٱلۡحِكۡمَةَ مَن يَشَآءُۚ وَمَن يُؤۡتَ ٱلۡحِكۡمَةَ فَقَدۡ أُوتِيَ خَيۡرٗا كَثِيرٗاۗ وَمَا يَذَّكَّرُ إِلَّآ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَٰبِ

Humpa hekima amtakaye. Na aliyepewa hekima bila shaka amepewa heri nyingi, na hawakumbuki ila wenye akili



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 270

وَمَآ أَنفَقۡتُم مِّن نَّفَقَةٍ أَوۡ نَذَرۡتُم مِّن نَّذۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُهُۥۗ وَمَا لِلظَّـٰلِمِينَ مِنۡ أَنصَارٍ

Na chochote mkitoacho au nadhiri yoyote muiwekayo kwa hakika Allah anaijua, na madhalimu hawana yeyote wa kuwanusuru



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 271

إِن تُبۡدُواْ ٱلصَّدَقَٰتِ فَنِعِمَّا هِيَۖ وَإِن تُخۡفُوهَا وَتُؤۡتُوهَا ٱلۡفُقَرَآءَ فَهُوَ خَيۡرٞ لَّكُمۡۚ وَيُكَفِّرُ عَنكُم مِّن سَيِّـَٔاتِكُمۡۗ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ

Iwapo mtadhihirisha sadaka ni vizuri sana, na kama mtatoa kwa siri na kuwapa mafukara basi hilo ni bora zaidi kwenu na atakufutieni baadhi ya maovu yenu na Allah anayajua mno mnayoyatenda



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 272

۞لَّيۡسَ عَلَيۡكَ هُدَىٰهُمۡ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ يَهۡدِي مَن يَشَآءُۗ وَمَا تُنفِقُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَلِأَنفُسِكُمۡۚ وَمَا تُنفِقُونَ إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ ٱللَّهِۚ وَمَا تُنفِقُواْ مِنۡ خَيۡرٖ يُوَفَّ إِلَيۡكُمۡ وَأَنتُمۡ لَا تُظۡلَمُونَ

Si jukumu lako kuwaongoa, lakini Allah humuongoa amtakaye. Na heri yoyote muitoayo, basi ni kwa (manufaa ya) nafsi zenu. Na msitoe ila kwa kutafuta wajihi (radhi) za Allah, na heri yoyote mtakayotoa mtarudishiwa kamili, nanyi hamtadhulumiwa



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 273

لِلۡفُقَرَآءِ ٱلَّذِينَ أُحۡصِرُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ لَا يَسۡتَطِيعُونَ ضَرۡبٗا فِي ٱلۡأَرۡضِ يَحۡسَبُهُمُ ٱلۡجَاهِلُ أَغۡنِيَآءَ مِنَ ٱلتَّعَفُّفِ تَعۡرِفُهُم بِسِيمَٰهُمۡ لَا يَسۡـَٔلُونَ ٱلنَّاسَ إِلۡحَافٗاۗ وَمَا تُنفِقُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِهِۦ عَلِيمٌ

(Heri na sadaka hizo) Wapewe mafakiri waliofungwa katika njia ya Allah wasioweza kusafiri katika ardhi (kwa kujitafutia riziki), asiyewajua huwadhania ni wakwasi kwa kujizuia kuomba. Utawatambua kwa alama zao, hawawaombi watu kwa ung’ang’anizi. Na heri yoyote mnayoitoa, basi kwa hakika Allah anaijua sana



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 274

ٱلَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمۡوَٰلَهُم بِٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِ سِرّٗا وَعَلَانِيَةٗ فَلَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ وَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Wale watoao mali zao usiku na mchana, kwa siri na kwa dhahiri, basi wana malipo yao kwa Mola wao, na hawatakuwa na hofu yoyote na hawatahuzunika



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 275

ٱلَّذِينَ يَأۡكُلُونَ ٱلرِّبَوٰاْ لَا يَقُومُونَ إِلَّا كَمَا يَقُومُ ٱلَّذِي يَتَخَبَّطُهُ ٱلشَّيۡطَٰنُ مِنَ ٱلۡمَسِّۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ قَالُوٓاْ إِنَّمَا ٱلۡبَيۡعُ مِثۡلُ ٱلرِّبَوٰاْۗ وَأَحَلَّ ٱللَّهُ ٱلۡبَيۡعَ وَحَرَّمَ ٱلرِّبَوٰاْۚ فَمَن جَآءَهُۥ مَوۡعِظَةٞ مِّن رَّبِّهِۦ فَٱنتَهَىٰ فَلَهُۥ مَا سَلَفَ وَأَمۡرُهُۥٓ إِلَى ٱللَّهِۖ وَمَنۡ عَادَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Wale wanaokula riba, hawatai-nuka isipokuwa kama anavyoinuka ambaye amepagawa kwa kukumbwa na Shetani. Hayo ni kwa sababu walisema kuwa biashara ni kama riba, na Allah ameihalalisha biashara na ameiharamisha riba. Basi ambaye amefikiwa na mawaidha kutoka kwa Mola wake na akaacha, basi yake ni yale yaliyokwishapita, na jambo lake lipo kwa Allah. Na watakaorejea, basi hao ndio watu wa Motoni, wao watakaa humo milele



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 276

يَمۡحَقُ ٱللَّهُ ٱلرِّبَوٰاْ وَيُرۡبِي ٱلصَّدَقَٰتِۗ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ كُلَّ كَفَّارٍ أَثِيمٍ

Allah huiondolea baraka riba na huzibariki sadaka, na Allah hampendi kila kafiri mno mwingi wa dhambi



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 277

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ وَأَقَامُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتَوُاْ ٱلزَّكَوٰةَ لَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ وَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Hakika wale walioamini na kutenda vitendo vizuri na kusimamisha Swala na kutoa Zaka, wanamalipo mema mbele ya Mola wao, na hawana hofu yoyote, na hawahuzuniki



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 278

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَذَرُواْ مَا بَقِيَ مِنَ ٱلرِّبَوٰٓاْ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ

Enyi mlioamini, mcheni Allah, na acheni yaliyobakia katika riba ikiwa ninyi ni waumini



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 279

فَإِن لَّمۡ تَفۡعَلُواْ فَأۡذَنُواْ بِحَرۡبٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦۖ وَإِن تُبۡتُمۡ فَلَكُمۡ رُءُوسُ أَمۡوَٰلِكُمۡ لَا تَظۡلِمُونَ وَلَا تُظۡلَمُونَ

Na msipofanya (hivyo) basi tangazeni vita na Allah na Mtume wake, na kama mkitubu, basi ni stahiki yenu rasilimali zenu, hamtadhulumu wala hamtadhulumiwa



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 280

وَإِن كَانَ ذُو عُسۡرَةٖ فَنَظِرَةٌ إِلَىٰ مَيۡسَرَةٖۚ وَأَن تَصَدَّقُواْ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Na kama (mdeni) ni mwenye hali ngumu, basi (mdai) angoje mpaka wakati wa uwezo. Na kulifanya sadaka (hilo deni) ni heri kwenu (kuliko kungoja mpaka mdaiwa kupata uwezo), ikiwa mnajua



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 281

وَٱتَّقُواْ يَوۡمٗا تُرۡجَعُونَ فِيهِ إِلَى ٱللَّهِۖ ثُمَّ تُوَفَّىٰ كُلُّ نَفۡسٖ مَّا كَسَبَتۡ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Na iogopeni siku ambayo mtarejeshwa kwa Allah, kisha kila mtu atalipwa kikamilifu aliyoyachuma, nao hawatadhulumiwa



Sure: AL-BAQARAH 

Vers : 282

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا تَدَايَنتُم بِدَيۡنٍ إِلَىٰٓ أَجَلٖ مُّسَمّٗى فَٱكۡتُبُوهُۚ وَلۡيَكۡتُب بَّيۡنَكُمۡ كَاتِبُۢ بِٱلۡعَدۡلِۚ وَلَا يَأۡبَ كَاتِبٌ أَن يَكۡتُبَ كَمَا عَلَّمَهُ ٱللَّهُۚ فَلۡيَكۡتُبۡ وَلۡيُمۡلِلِ ٱلَّذِي عَلَيۡهِ ٱلۡحَقُّ وَلۡيَتَّقِ ٱللَّهَ رَبَّهُۥ وَلَا يَبۡخَسۡ مِنۡهُ شَيۡـٔٗاۚ فَإِن كَانَ ٱلَّذِي عَلَيۡهِ ٱلۡحَقُّ سَفِيهًا أَوۡ ضَعِيفًا أَوۡ لَا يَسۡتَطِيعُ أَن يُمِلَّ هُوَ فَلۡيُمۡلِلۡ وَلِيُّهُۥ بِٱلۡعَدۡلِۚ وَٱسۡتَشۡهِدُواْ شَهِيدَيۡنِ مِن رِّجَالِكُمۡۖ فَإِن لَّمۡ يَكُونَا رَجُلَيۡنِ فَرَجُلٞ وَٱمۡرَأَتَانِ مِمَّن تَرۡضَوۡنَ مِنَ ٱلشُّهَدَآءِ أَن تَضِلَّ إِحۡدَىٰهُمَا فَتُذَكِّرَ إِحۡدَىٰهُمَا ٱلۡأُخۡرَىٰۚ وَلَا يَأۡبَ ٱلشُّهَدَآءُ إِذَا مَا دُعُواْۚ وَلَا تَسۡـَٔمُوٓاْ أَن تَكۡتُبُوهُ صَغِيرًا أَوۡ كَبِيرًا إِلَىٰٓ أَجَلِهِۦۚ ذَٰلِكُمۡ أَقۡسَطُ عِندَ ٱللَّهِ وَأَقۡوَمُ لِلشَّهَٰدَةِ وَأَدۡنَىٰٓ أَلَّا تَرۡتَابُوٓاْ إِلَّآ أَن تَكُونَ تِجَٰرَةً حَاضِرَةٗ تُدِيرُونَهَا بَيۡنَكُمۡ فَلَيۡسَ عَلَيۡكُمۡ جُنَاحٌ أَلَّا تَكۡتُبُوهَاۗ وَأَشۡهِدُوٓاْ إِذَا تَبَايَعۡتُمۡۚ وَلَا يُضَآرَّ كَاتِبٞ وَلَا شَهِيدٞۚ وَإِن تَفۡعَلُواْ فَإِنَّهُۥ فُسُوقُۢ بِكُمۡۗ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۖ وَيُعَلِّمُكُمُ ٱللَّهُۗ وَٱللَّهُ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ

Enyi mliyoamini, mnapoko-peshana mkopo wowote kwa muda maalum, basi uandikeni. Na mwandishi aandike baina yenu kwa uadilifu. Na mwandishi asikatae kuandika. Aandike kama Allah alivyomfunza. Hivyo basi, aandike na ni juu ya mdaiwa kutoa maneno ya kuandikwa na amwogope Allah, Mola wake Mlezi, na asipunguze chochote ndani yake. Na kama yule anayedaiwa ni alie pumbaa mnyonge, au hawezi kuandikisha mwenyewe, basi msimamizi wake aandikishe kwa uadilifu. Na shuhudisheni mashahidi wawili wanaume waaminifu sana miongoni mwenu. Na iwapo hakuna wanaume wawili, basi (apatikane) mwanaume mmoja na wanawake wawili katika wale mnaowaridhia kuwa mashahidi, ili kama atasahau mmoja wa wanawake wawili, yule mwingine amkumbushe mwenzake. Na mashahidi wasikatae wanapoitwa. Na msikimwe kuliandika deni, likiwa dogo au kubwa, mpaka muda wake. Jambo hilo kwenu ni uadilifu zaidi mbele ya Allah, na sahihi zaidi kwa ushahidi, na pia inakurubisha mno kutokuwa na shaka, isipokuwa kama ni biashara mnayofanya kati yenu papo hapo, basi si dhambi kwenu msipoiandika. Na mnapouziana wekeni mashahidi. Wala asitiwe matatani mwandishi wala shahidi, na kama mkifanya hivyo (kuwatia matatani), basi kwa hakika huo ni uovu mkubwa kwenu. Na mwogopeni Allah, na Allah ndiye ana kuelimisheni; na Allah ni Mjuzi mno wa kila kitu