لَّيۡسَ لَهُمۡ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٖ
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba
Teilnahme :
لَّا يُسۡمِنُ وَلَا يُغۡنِي مِن جُوعٖ
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاعِمَةٞ
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu
لِّسَعۡيِهَا رَاضِيَةٞ
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ
Katika Bustani ya juu
لَّا تَسۡمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةٗ
Hawatasikia humo upuuzi. Humo imo chemchem inayo miminika
فِيهَا عَيۡنٞ جَارِيَةٞ
Humo imo chemchem inayo miminika
فِيهَا سُرُرٞ مَّرۡفُوعَةٞ
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
وَأَكۡوَابٞ مَّوۡضُوعَةٞ
Na bilauri zilizo pangwa,
وَنَمَارِقُ مَصۡفُوفَةٞ
Na matakia (yakiwa) safu safu,
وَزَرَابِيُّ مَبۡثُوثَةٌ
Na mazulia yaliyo tandikwa
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلۡإِبِلِ كَيۡفَ خُلِقَتۡ
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ رُفِعَتۡ
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
وَإِلَى ٱلۡجِبَالِ كَيۡفَ نُصِبَتۡ
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa (simamishwa)?
وَإِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَيۡفَ سُطِحَتۡ
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
فَذَكِّرۡ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٞ
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji
لَّسۡتَ عَلَيۡهِم بِمُصَيۡطِرٍ
Wewe si mwenye kuwatawalia
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
Lakini anaye rudi nyuma na kukufuru,
فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَكۡبَرَ
Basi Allah Atamuadhibu adhabu kubwa kabisa
إِنَّ إِلَيۡنَآ إِيَابَهُمۡ
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا حِسَابَهُم
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hesabu yao!
وَٱلۡفَجۡرِ
Naapa kwa alfajiri,
وَلَيَالٍ عَشۡرٖ
Na kwa masiku kumi,
وَٱلشَّفۡعِ وَٱلۡوَتۡرِ
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَسۡرِ
Na kwa usiku unapo pita,
هَلۡ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٞ لِّذِي حِجۡرٍ
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A’di?
إِرَمَ ذَاتِ ٱلۡعِمَادِ
Wa Iram, wenye majumba marefu?
ٱلَّتِي لَمۡ يُخۡلَقۡ مِثۡلُهَا فِي ٱلۡبِلَٰدِ
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُواْ ٱلصَّخۡرَ بِٱلۡوَادِ
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?