Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 21

وَتَذَرُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ

Na mnaacha maisha ya Akhera, (kwa kutoijali Akhera)



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 22

وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاضِرَةٌ

Zipo Nyuso siku hiyo zitanawiri, (zitang’aa)



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 23

إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٞ

Zikimtazama Mola wake



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 24

وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذِۭ بَاسِرَةٞ

Na nyuso (nyenginezo) siku hiyo zitakunjana



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 25

تَظُنُّ أَن يُفۡعَلَ بِهَا فَاقِرَةٞ

Zikiwa na yakini kuwa zitafikiwa na msiba unaovunja uti wa mgongo



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 26

كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِيَ

Sivyo! Itakapofika (roho) kwenye mafupa ya koo, (mitulinga)



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 27

وَقِيلَ مَنۡۜ رَاقٖ

Na itasemwa: Ni nani tabibu wa kumponya?



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 28

وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلۡفِرَاقُ

Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 29

وَٱلۡتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ

Na utakapo ambatanishwa muundi kwa muundi



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 30

إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمَسَاقُ

Siku hiyo ndiyo (ya) kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako! (ama Peponi au Motoni)



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 31

فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ

Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali, (hakumsadiki Mtume wala Qur’ani)



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 32

وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ

Lakini alikadhibisha na akakengeuka



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 33

ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ

Kisha akaenda kwa watu wake wa nyumbani kwa maringo



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 34

أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰ

Ole wako! Ole wako! (Ewe unaye kadhibisha, utaangamia!)



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 35

ثُمَّ أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰٓ

Kisha! Ole wako! Ole wako! (Ewe unaye kadhibisha, utaangamia!)



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 36

أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَن يُتۡرَكَ سُدًى

Je, mwanadamu anadhani kuwa ataachwa bure tu?



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 37

أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ

Kwani yeye hakuwa tone la manii lililotonwa?



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 38

ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ

Kisha akawa pande la damu, (Allaah) Akamuumba na Akamsawazisha?



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 39

فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ

Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke



Sure: ALQIYAAMA 

Vers : 40

أَلَيۡسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰ

Je! Huyo (aliyefanya hivyo) hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?



Sure: AL-INSAAN

Vers : 1

هَلۡ أَتَىٰ عَلَى ٱلۡإِنسَٰنِ حِينٞ مِّنَ ٱلدَّهۡرِ لَمۡ يَكُن شَيۡـٔٗا مَّذۡكُورًا

Hakika, kilimpitia binaadamu kipindi katika zama kipindi (ambacho) hakuwa kitu kinachotajwa



Sure: AL-INSAAN

Vers : 2

إِنَّا خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ مِن نُّطۡفَةٍ أَمۡشَاجٖ نَّبۡتَلِيهِ فَجَعَلۡنَٰهُ سَمِيعَۢا بَصِيرًا

Hakika, sisi tumemuumba mwanadamu kutokana na mbegu ya uhai (Manii) iliyochanganyika ili tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tumemfanya ni mwenye kusikia, mwenye kuona



Sure: AL-INSAAN

Vers : 3

إِنَّا هَدَيۡنَٰهُ ٱلسَّبِيلَ إِمَّا شَاكِرٗا وَإِمَّا كَفُورًا

Hakika, sisi tumemuongoza (tumempa mwongozo unaofikishwa na Mitume); ama awe mwenye kushukuru au mwenye kukufuru



Sure: AL-INSAAN

Vers : 4

إِنَّآ أَعۡتَدۡنَا لِلۡكَٰفِرِينَ سَلَٰسِلَاْ وَأَغۡلَٰلٗا وَسَعِيرًا

Hakika sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na moto mkali



Sure: AL-INSAAN

Vers : 5

إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ يَشۡرَبُونَ مِن كَأۡسٖ كَانَ مِزَاجُهَا كَافُورًا

Hakika, watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri



Sure: AL-INSAAN

Vers : 6

عَيۡنٗا يَشۡرَبُ بِهَا عِبَادُ ٱللَّهِ يُفَجِّرُونَهَا تَفۡجِيرٗا

Ni chemchem watakayoinywa waja wa Allah, wakiifanya imiminike kwa wingi



Sure: AL-INSAAN

Vers : 7

يُوفُونَ بِٱلنَّذۡرِ وَيَخَافُونَ يَوۡمٗا كَانَ شَرُّهُۥ مُسۡتَطِيرٗا

Wanatimiza ahadi, na wanaiogopa siku ambayo shari yake ni yenye kuenea sana



Sure: AL-INSAAN

Vers : 8

وَيُطۡعِمُونَ ٱلطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِۦ مِسۡكِينٗا وَيَتِيمٗا وَأَسِيرًا

Na wanalisha chakula, pamoja na kukipenda kwake, (wanawalisha) masikini na mayatima na mateka



Sure: AL-INSAAN

Vers : 9

إِنَّمَا نُطۡعِمُكُمۡ لِوَجۡهِ ٱللَّهِ لَا نُرِيدُ مِنكُمۡ جَزَآءٗ وَلَا شُكُورًا

Hakika sisi tunakulisheni kwa ajili ya kutaka radhi za Allah. Hatutaki kwenu malipo wala shukrani



Sure: AL-INSAAN

Vers : 10

إِنَّا نَخَافُ مِن رَّبِّنَا يَوۡمًا عَبُوسٗا قَمۡطَرِيرٗا

Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu hiyo siku yenye shida na taabu