وَفِرۡعَوۡنَ ذِي ٱلۡأَوۡتَادِ
Na Firauni mwenye vigingi??
Teilnahme :
ٱلَّذِينَ طَغَوۡاْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ
Ambao walifanya jeuri katika nchi
فَأَكۡثَرُواْ فِيهَا ٱلۡفَسَادَ
Wakakithirisha humo ufisadi?
فَصَبَّ عَلَيۡهِمۡ رَبُّكَ سَوۡطَ عَذَابٍ
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu
إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلۡمِرۡصَادِ
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia
فَأَمَّا ٱلۡإِنسَٰنُ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكۡرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَكۡرَمَنِ
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu
وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيۡهِ رِزۡقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَهَٰنَنِ
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
كَلَّاۖ بَل لَّا تُكۡرِمُونَ ٱلۡيَتِيمَ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
وَلَا تَحَـٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Wala hamhimizani kulisha masikini;
وَتَأۡكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكۡلٗا لَّمّٗا
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبّٗا جَمّٗا
Na mnapenda mali mapenzi ya kupita kiasi
كَلَّآۖ إِذَا دُكَّتِ ٱلۡأَرۡضُ دَكّٗا دَكّٗا
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلۡمَلَكُ صَفّٗا صَفّٗا
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
وَجِاْيٓءَ يَوۡمَئِذِۭ بِجَهَنَّمَۚ يَوۡمَئِذٖ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكۡرَىٰ
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
يَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي قَدَّمۡتُ لِحَيَاتِي
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia (mema) katika uhai wangu!
فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٞ
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote kama kuadhibu kwake
وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٞ
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake
يَـٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ
Ewe nafsi iliyo tua!
ٱرۡجِعِيٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةٗ مَّرۡضِيَّةٗ
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha
فَٱدۡخُلِي فِي عِبَٰدِي
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
وَٱدۡخُلِي جَنَّتِي
Na ingia katika Pepo yangu
لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Naapa kwa Mji huu!
وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Nawe unakaa Mji huu
وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ
Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ
Hakika tumemuumba mtu katika taabu
أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ
Ati anadhani hapana yeyote atakaye muweza?
يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا
Anasema: Nimeteketeza mali chungu nzima
أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ
Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ
Kwani hatukumpa macho mawili?
وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ
Na ulimi, na midomo miwili?