Sure: AL-BALAD 

Vers : 10

وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ

Na tukambainishia njia zote mbili?



Sure: AL-BALAD 

Vers : 11

فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ

Lakini hakujitoma (hakuingia) kwenye njia ya vikwazo vya milimani



Sure: AL-BALAD 

Vers : 12

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ

Na nini kitakujulisha ni nini njia ya vikwazo vya milimani?



Sure: AL-BALAD 

Vers : 13

فَكُّ رَقَبَةٍ

Kumkomboa mtumwa;



Sure: AL-BALAD 

Vers : 14

أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ

Au kumlisha siku ya njaa



Sure: AL-BALAD 

Vers : 15

يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ

Yatima aliye katika jamaa wa karibu (ndugu)



Sure: AL-BALAD 

Vers : 16

أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ

Au masikini aliye vumbini



Sure: AL-BALAD 

Vers : 17

ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ

Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana



Sure: AL-BALAD 

Vers : 18

أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ

Hao ndio watu wa kheri wa kuliani



Sure: AL-BALAD 

Vers : 19

وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ

Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni



Sure: AL-BALAD 

Vers : 20

عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ

Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 1

وَٱلشَّمۡسِ وَضُحَىٰهَا

Naapa kwa jua na mwangaza wake!



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 2

وَٱلۡقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا

Na kwa mwezi unapo lifuatia!



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 3

وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا

Na kwa mchana unapo lidhihirisha!



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 4

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰهَا

Na kwa usiku unapo lifunika!



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 5

وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا

Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 6

وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا طَحَىٰهَا

Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 7

وَنَفۡسٖ وَمَا سَوَّىٰهَا

Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 8

فَأَلۡهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقۡوَىٰهَا

Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 9

قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّىٰهَا

Hakika amefanikiwa aliye itakasa,



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 10

وَقَدۡ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا

Na hakika amepata hasara aliye iviza (ichafua)



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 11

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ

Kina Thamudi walikadhibisha kwasababu ya upotofu wao,



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 12

إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا

Alipo simama mwovu wao mkubwa



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 13

فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا

Hapo Mtume wa Allah alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Allah, mwacheni anywe maji fungu lake



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 14

فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا

Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwahivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwasababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa



Sure: AL-SHAMS 

Vers : 15

وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا

Wala Yeye haogopi matokeo yake



Sure: ALLAIL 

Vers : 1

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰ

Naapa kwa usiku unapo funika!



Sure: ALLAIL 

Vers : 2

وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ

Na mchana unapo dhihiri!



Sure: ALLAIL 

Vers : 3

وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ

Na kwa Aliye umba dume na jike!



Sure: ALLAIL 

Vers : 4

إِنَّ سَعۡيَكُمۡ لَشَتَّىٰ

Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni tofauti