Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 10

وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ نُسِفَتۡ

Na milima itakapo peperushwa



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 11

وَإِذَا ٱلرُّسُلُ أُقِّتَتۡ

Na Mitume watakapo wekewa wakati wao



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 12

لِأَيِّ يَوۡمٍ أُجِّلَتۡ

Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 13

لِيَوۡمِ ٱلۡفَصۡلِ

Kwa ajili ya Siku ya hukumu na kutenganisha



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 14

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ

Na nini kitakachokujulisha Siku ya hukumu na kutenganisha?



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 15

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 16

أَلَمۡ نُهۡلِكِ ٱلۡأَوَّلِينَ

Je, kwani Hatukuangamiza watu walio tangulia?



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 17

ثُمَّ نُتۡبِعُهُمُ ٱلۡأٓخِرِينَ

Kisha Tukawafuatilishia watu wengineo?



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 18

كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ

Hivyo ndivyo Tunavyo wafanya wakosefu!



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 19

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 20

أَلَمۡ نَخۡلُقكُّم مِّن مَّآءٖ مَّهِينٖ

Kwani hatukukuumbeni kwa maji dhalili (manii)?



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 21

فَجَعَلۡنَٰهُ فِي قَرَارٖ مَّكِينٍ

Kisha Tukayaweka katika mahali pa kutulia, madhubuti?



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 22

إِلَىٰ قَدَرٖ مَّعۡلُومٖ

Mpaka muda maalumu?



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 23

فَقَدَرۡنَا فَنِعۡمَ ٱلۡقَٰدِرُونَ

Tukakadiria na Sisi ni wazuri walioje wa kukadiria



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 24

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 25

أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ كِفَاتًا

Je, kwani Hatukufanya ardhi kuwa ni chombo cha kukusanya?



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 26

أَحۡيَآءٗ وَأَمۡوَٰتٗا

Walio hai na maiti (na waliokufa)?



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 27

وَجَعَلۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ شَٰمِخَٰتٖ وَأَسۡقَيۡنَٰكُم مَّآءٗ فُرَاتٗا

Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tuna-kunywesheni maji matamu?



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 28

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 29

ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ

(wataambiwa:) Nendeni kwenye adhabu mliyokuwa mkiikanusha!



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 30

ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ ظِلّٖ ذِي ثَلَٰثِ شُعَبٖ

Nendeni kwenye kivuli chenye sehemu tatu!



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 31

لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ

Hakiwafuniki, na wala hakiwa-kingi na muwako wa moto



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 32

إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ

Hakika Moto huo hurusha macheche Kama majumba!



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 33

كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ

Kana kwamba ni ngamia waku-bwa wa rangi ya manjano!



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 34

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 35

هَٰذَا يَوۡمُ لَا يَنطِقُونَ

Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 36

وَلَا يُؤۡذَنُ لَهُمۡ فَيَعۡتَذِرُونَ

Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 37

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 38

هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِۖ جَمَعۡنَٰكُمۡ وَٱلۡأَوَّلِينَ

Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia



Sure: ALMURSALAAT 

Vers : 39

فَإِن كَانَ لَكُمۡ كَيۡدٞ فَكِيدُونِ

Ikiwa mnayo hila yoyote ile basi Nifanyieni mimi