فَأَمَّا مَنۡ أَعۡطَىٰ وَٱتَّقَىٰ
Ama mwenye kutoa na akamcha Allah
Teilnahme :
وَصَدَّقَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
Na akalisadikisha lilio jema,
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡيُسۡرَىٰ
Tutamsahilishia yawe mepesi
وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسۡتَغۡنَىٰ
Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,
وَكَذَّبَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
Na akakanusha lilio jema,
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡعُسۡرَىٰ
Tutamsahilishia yawe mazito!
وَمَا يُغۡنِي عَنۡهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ
Na mali yake yatamfaa nini atakapo kuwa anadidimia?
إِنَّ عَلَيۡنَا لَلۡهُدَىٰ
Hakika ni juu yetu kuonyesha uongofu
وَإِنَّ لَنَا لَلۡأٓخِرَةَ وَٱلۡأُولَىٰ
Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia
فَأَنذَرۡتُكُمۡ نَارٗا تَلَظَّىٰ
Basi nakuonyeni na Moto unao waka!
لَا يَصۡلَىٰهَآ إِلَّا ٱلۡأَشۡقَى
Hatauingia ila mwovu kabisa!
ٱلَّذِي كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Anaye kadhibisha na kupa mgongo
وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلۡأَتۡقَى
Na mcha Mungu ataepushwa nao
ٱلَّذِي يُؤۡتِي مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ
Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa
وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعۡمَةٖ تُجۡزَىٰٓ
Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa
إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ رَبِّهِ ٱلۡأَعۡلَىٰ
Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa
وَلَسَوۡفَ يَرۡضَىٰ
Naye atakuja ridhika!
وَٱلضُّحَىٰ
Naapa kwa mchana!
وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku unapo tanda!
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe
وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia
وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike
أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ
Kwani hakukukuta yatima akakupa makazi?
وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ
Na akakukuta umepotea akakuongoa?
وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ
Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ
Basi yatima usimwonee!
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie
أَلَمۡ نَشۡرَحۡ لَكَ صَدۡرَكَ
Je, hatukukunjulia kifua chako?
وَوَضَعۡنَا عَنكَ وِزۡرَكَ
Na tukakuondolea mzigo wako?