Sure: AL-KAAFIRUUN 

Vers : 6

لَكُمۡ دِينُكُمۡ وَلِيَ دِينِ

Nyinyi mna dini yenu, nami nina dini yangu



Sure: ANASRI 

Vers : 1

إِذَا جَآءَ نَصۡرُ ٱللَّهِ وَٱلۡفَتۡحُ

Itakapokuja nusra ya Allah na ushindi (ukombozi wa mji wa Makka)



Sure: ANASRI 

Vers : 2

وَرَأَيۡتَ ٱلنَّاسَ يَدۡخُلُونَ فِي دِينِ ٱللَّهِ أَفۡوَاجٗا

Na ukaona watu wanaingia katika Dini ya Allah kwa makundi



Sure: ANASRI 

Vers : 3

فَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ وَٱسۡتَغۡفِرۡهُۚ إِنَّهُۥ كَانَ تَوَّابَۢا

Basi zitakase sifa za Mola wako Mlezi na muombe msamaha. Hakika, Yeye (Allah) amekuwa Mwenye kukubali sana toba. Sura imetoa utabiri wa kifo cha Mtume rehma na amani ziwe juu yake



Sure: AL-MASAD

Vers : 1

تَبَّتۡ يَدَآ أَبِي لَهَبٖ وَتَبَّ

Imeangamia mikono ya Abulahab na yeye (kwa maana hiyo) ameangamia



Sure: AL-MASAD

Vers : 2

مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُ مَالُهُۥ وَمَا كَسَبَ

Haitamfaa mali yake na (vitendo) alivyovichuma (alivyovifanya)



Sure: AL-MASAD

Vers : 3

سَيَصۡلَىٰ نَارٗا ذَاتَ لَهَبٖ

Atauingia moto wenye muwako



Sure: AL-MASAD

Vers : 4

وَٱمۡرَأَتُهُۥ حَمَّالَةَ ٱلۡحَطَبِ

(Ataingia Motoni yeye) Na mkewe, mchukuzi mkubwa wa kuni



Sure: AL-MASAD

Vers : 5

فِي جِيدِهَا حَبۡلٞ مِّن مَّسَدِۭ

Shingoni mwake iko kamba ya kusokotwa



Sure: AL-IKHLAAS 

Vers : 1

قُلۡ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ

Sema: Yeye Allah ni wa pekee



Sure: AL-IKHLAAS 

Vers : 2

ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ

Allah ndiye tu Mkusudiwa (katika kuabudiwa, kutegemewa na kutatua shida za watu)



Sure: AL-IKHLAAS 

Vers : 3

لَمۡ يَلِدۡ وَلَمۡ يُولَدۡ

Hakuzaa[1] na hakuzaliwa.[2]


1- - Kwa maana hiyo hana mtoto.


2- - Kwa maana hiyo hana baba wala mama.

---------------

------------------------------------------------------------

---------------

------------------------------------------------------------


Sure: AL-IKHLAAS 

Vers : 4

وَلَمۡ يَكُن لَّهُۥ كُفُوًا أَحَدُۢ

Na hakuna yeyote anaye fanana naye



Sure: AL-FALAQ

Vers : 1

قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلۡفَلَقِ

Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko



Sure: AL-FALAQ

Vers : 2

مِن شَرِّ مَا خَلَقَ

(Najikinga) Dhidi ya shari ya alivyoviumba



Sure: AL-FALAQ

Vers : 3

وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ

Na (najikinga) dhidi ya shari ya giza la usiku liingiapo



Sure: AL-FALAQ

Vers : 4

وَمِن شَرِّ ٱلنَّفَّـٰثَٰتِ فِي ٱلۡعُقَدِ

Na (najikinga) dhidi ya shari ya (wanawake) wanaopulizia mafundoni



Sure: AL-FALAQ

Vers : 5

وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ

Na (najikinga) dhidi ya shari ya hasidi anapo husudu



Sure: ANNAAS

Vers : 1

قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ

Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa watu



Sure: ANNAAS

Vers : 2

مَلِكِ ٱلنَّاسِ

Mfalme wa watu



Sure: ANNAAS

Vers : 3

إِلَٰهِ ٱلنَّاسِ

Muabudiwa wa haki wa watu (Mwenye haki ya kuabudiwa na watu)



Sure: ANNAAS

Vers : 4

مِن شَرِّ ٱلۡوَسۡوَاسِ ٱلۡخَنَّاسِ

(Najilinda dhidi ya shari ya (shetani) mwenye kutia wasiwasi, mwenye kurejea nyuma



Sure: ANNAAS

Vers : 5

ٱلَّذِي يُوَسۡوِسُ فِي صُدُورِ ٱلنَّاسِ

Anayetia wasiwasi katika vifua vya watu



Sure: ANNAAS

Vers : 6

مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ

(Shetani) Anayetokana na majini na watu