إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ مَفَازًا
Hakika wacha Mungu wanastahiki kufuzu
Teilnahme :
حَدَآئِقَ وَأَعۡنَٰبٗا
[watapata] Mabustani na mizabibu
وَكَوَاعِبَ أَتۡرَابٗا
Na wake wenye vifua vya kujaa, na walio lingana nao
وَكَأۡسٗا دِهَاقٗا
Na bilauri zilizo jaa,
لَّا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا كِذَّـٰبٗا
Hawatasikia humo upuuzi wala uongo
جَزَآءٗ مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابٗا
Hali yakuwa ni Malipo kutoka kwa Mola wako, ni kipawa cha kutosha
رَّبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا ٱلرَّحۡمَٰنِۖ لَا يَمۡلِكُونَ مِنۡهُ خِطَابٗا
Mola wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake Mwingi wa rehema; hawatoweza kumsemesha
يَوۡمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ صَفّٗاۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنۡ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحۡمَٰنُ وَقَالَ صَوَابٗا
Siku atakayosimama Roho (Jibrili) na Malaika hali ya kujipanga safu; Hawatasema ila aliye mruhusu Mwingi wa rehema, na atasema yaliyo sawa tu
ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمُ ٱلۡحَقُّۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ مَـَٔابًا
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anayetaka na ashike njia arejee kwa Mola wake
إِنَّآ أَنذَرۡنَٰكُمۡ عَذَابٗا قَرِيبٗا يَوۡمَ يَنظُرُ ٱلۡمَرۡءُ مَا قَدَّمَتۡ يَدَاهُ وَيَقُولُ ٱلۡكَافِرُ يَٰلَيۡتَنِي كُنتُ تُرَٰبَۢا
Hakika Sisi Tumekuonyeni adhabu ya karibu, Siku mtu atakapotazama yale yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningelikuwa mchanga
وَٱلنَّـٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا
Nina apa kwa [Malaika] wanaong’oa (roho) kwa nguvu
وَٱلنَّـٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا
Na (kwa Malaika) wanaotoa (roho) kwa upole
وَٱلسَّـٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا
Na ( kwa Malaika) wanaoogelea sana (katika anga kwa kupanda na kushuka wakitekeleza majukumu waliyopewa na Allah)
فَٱلسَّـٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا
Kisha (Nina apa kwa Malaika) wenye kuongoza (katika kushidana wakati wa kutimiza wajibu wao)
فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا
Kisha (Nina apa kwa Malaika) wenye kuendesha kila jambo (kwa maagizo ya Allah)
يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ
Siku kitakapotetemeka cha kutetemeka
تَتۡبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ
Na utafuatia mpulizo (mwingine wa pili wa baragumu)
قُلُوبٞ يَوۡمَئِذٖ وَاجِفَةٌ
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga (mapigo ya haraka haraka kwa hofu)
أَبۡصَٰرُهَا خَٰشِعَةٞ
Macho yake yatainama chini
يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرۡدُودُونَ فِي ٱلۡحَافِرَةِ
Wanasema: Je, hivi sisi kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمٗا نَّخِرَةٗ
Je, hata tukiwa ni mifupa iliyosagika na kuoza?
قَالُواْ تِلۡكَ إِذٗا كَرَّةٌ خَاسِرَةٞ
Wanasema: Basi marejeo hayo, ni marejeo yenye hasara!
فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ
Basi hakika huo ni ukelele mmoja tu
فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ
Tahamaki hao watahudhurishwa kwenye ardhi ya mkusanyiko, (wakiwa macho baada ya kufa)
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ
Je, imekufikia habarii ya Mussa?
إِذۡ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوًى
Mola wake alipo mwita katika bonde takatifu la Tuwaa, akamwambia;
ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ
Nenda kwa Firauna, hakika yeye amepindukia mipaka
فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ
Umwambie: Je, unataka utakasike?
وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ
Na nikuongoze kwa Mola wako umuogope?
فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Basi akamuonyesha Ishara (muujiza) mkubwa kabisa