قَالُواْ يَٰوَيۡلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَٰغِينَ
Wakasema: Ole wetu! Hakika sisi tumekuwa warukao mipaka
عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبۡدِلَنَا خَيۡرٗا مِّنۡهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ
Asaa Mola wetu akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi
كَذَٰلِكَ ٱلۡعَذَابُۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَكۡبَرُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ
Kama hivyo ndivyo inakuwa adhabu (ya hapa duniani), bila shaka adhabu ya akhera ni kubwa zaidi, laiti wangalijua!
إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Hakika wachamungu watapata Kwa Mola wao Bustani za neema
أَفَنَجۡعَلُ ٱلۡمُسۡلِمِينَ كَٱلۡمُجۡرِمِينَ
Je, Tuwafanye Waislamu (watiifu) sawa Kama wahalifu?
مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ
Mmekuwaaje Nyinyi, Vipi mnahukumu?
أَمۡ لَكُمۡ كِتَٰبٞ فِيهِ تَدۡرُسُونَ
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
إِنَّ لَكُمۡ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ
Kwamba hakika Yatakuwamo Kwa ajili yenu mnayo yachagua (mnachopendelea)?
أَمۡ لَكُمۡ أَيۡمَٰنٌ عَلَيۡنَا بَٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ إِنَّ لَكُمۡ لَمَا تَحۡكُمُونَ
Au je, mnavyo viapo juu yetu vinavyofika mpaka siku ya Kiyama ya kuwa ninyi mtapata mnayo yahukumu?
سَلۡهُمۡ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ
Waulize Hao: Ni nani miongoni mwao mdhamini wa hayo?
أَمۡ لَهُمۡ شُرَكَآءُ فَلۡيَأۡتُواْ بِشُرَكَآئِهِمۡ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli
يَوۡمَ يُكۡشَفُ عَن سَاقٖ وَيُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ
Siku ambayo yatakapokuwa mateso makali, na wataitwa kusujudu lakini hawataweza
خَٰشِعَةً أَبۡصَٰرُهُمۡ تَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۖ وَقَدۡ كَانُواْ يُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ وَهُمۡ سَٰلِمُونَ
Macho Yao yatainama chini, udhalilifu utawafunika. Na hali walikuwa wakiitwa wasujudu (kuswali duniani) walipokuwa wazima wa afya
فَذَرۡنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِۖ سَنَسۡتَدۡرِجُهُم مِّنۡ حَيۡثُ لَا يَعۡلَمُونَ
Basi Niache na anayekadhibisha Maneno haya (Qurani hii) Tutawavuta pole pole adhabuni kwa namna wasiyoijua
وَأُمۡلِي لَهُمۡۚ إِنَّ كَيۡدِي مَتِينٌ
Na Ninawapa muda, hakika mpango Wangu ni Madhubuti
أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ
Au unawaomba ujira, na wao wanaelemewa na gharama hiyo?
أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ
Au wanayo (elimu) ya ghaibu, basi wao wanaandika?
فَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلۡحُوتِ إِذۡ نَادَىٰ وَهُوَ مَكۡظُومٞ
Basi subiri hukumu ya mola wako, wala usiwe kama sahibu wa nyangumi, alipomwita (Mola wake) na hali yeye alikuwa mwenye huzuni nyingi (Amebanwa na Dhiki)
لَّوۡلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعۡمَةٞ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ مَذۡمُومٞ
Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa
فَٱجۡتَبَٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ
Lakini mola wake alimchagua na akamfanya kuwa ni miongoni mwa watu wema
وَإِن يَكَادُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَيُزۡلِقُونَكَ بِأَبۡصَٰرِهِمۡ لَمَّا سَمِعُواْ ٱلذِّكۡرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُۥ لَمَجۡنُونٞ
Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni
وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote
ٱلۡحَآقَّةُ
Tukio la haki
مَا ٱلۡحَآقَّةُ
Ni nini tukio la haki?
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحَآقَّةُ
Na ni nini kitakachokujuulisha; ni nini hilo tukio la haki?
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ وَعَادُۢ بِٱلۡقَارِعَةِ
Kina Thamudi na Adi walikadhibisha tukio (Kiyama) lenye kugonga (na kutia kiwewe)
فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهۡلِكُواْ بِٱلطَّاغِيَةِ
Ama kina Thamudi, waliangamizwa kwa ukelele mkali sana
وَأَمَّا عَادٞ فَأُهۡلِكُواْ بِرِيحٖ صَرۡصَرٍ عَاتِيَةٖ
Na ama kina Adi, waliangamizwa kwa upepo wenye baridi kali, uvumao kwa nguvu
سَخَّرَهَا عَلَيۡهِمۡ سَبۡعَ لَيَالٖ وَثَمَٰنِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومٗاۖ فَتَرَى ٱلۡقَوۡمَ فِيهَا صَرۡعَىٰ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٍ خَاوِيَةٖ
(Allah) Aliwapelekea mausiku saba na michana minane mfululizo (bila kupumzika). Basi utaona watu wameanguka kifudifudi kana kwamba ni magogo ya mitende yaliyo wazi ndani
فَهَلۡ تَرَىٰ لَهُم مِّنۢ بَاقِيَةٖ
Basi je, unamuona yeyote aliyebaki?