Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 21

فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ

Lakini aliikadhibisha na akaasi



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 22

ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ

Kisha akageuka nyuma na kufanya juhudi, (ya kukanusha)



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 23

فَحَشَرَ فَنَادَىٰ

Akakusanya watu akatangaza



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 24

فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mkuu kabisa



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 25

فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ

Basi hapo Allah akamshika na kumuadhibu kwa adhabu ya mwisho na mwanzo.[1]


1- - Allah akampa adhabu kwa kauli yake ya mwisho, nayo ni vile kusema: “Mimi ndiye Mola wenu Mlezi aliye mkubwa kabisa. Na akampa adhabu kwa kauli yake ya mwanzo, nayo ni kumkadhibisha Musa”.


Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 26

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ

Hakika katika hayo bila shaka kuna funzo kwa yule anayeogopa



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 27

ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا

Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 28

رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا

Akainua kimo chake, na akaiten-geneza vizuri



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 29

وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا

Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 30

وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ

Na ardhi baada ya hayo Akai-tandaza



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 31

أَخۡرَجَ مِنۡهَا مَآءَهَا وَمَرۡعَىٰهَا

Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 32

وَٱلۡجِبَالَ أَرۡسَىٰهَا

Na milima akaisimamisha,



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 33

مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ

Ni manufaa kwenu na kwa wanyama wenu wa mifugo



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 34

فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلۡكُبۡرَىٰ

Basi itakapokuja hilo balaa kubwa kabisa



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 35

يَوۡمَ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ

Siku ambayo mtu atakumbuka aliyoyafanya, (aliyoyakimbilia kuyafanyia juhudi)



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 36

وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ

Na moto utakapodhihirishwa wazi kwa mwenye kuona



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 37

فَأَمَّا مَن طَغَىٰ

Basi yule aliyepindukia mipaka na kuasi



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 38

وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Na akapenda zaidi maisha ya dunia



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 39

فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ

Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 40

وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ

Ama yule anayeogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake, na akaikataza nafsi yake na na matamanio



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 41

فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ

Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 42

يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرۡسَىٰهَا

Wanakuuliza kuhusu Kiyama lini kufika kwake?



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 43

فِيمَ أَنتَ مِن ذِكۡرَىٰهَآ

Una nini wewe hata ukitaje hicho kiyama?



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 44

إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ

Kwa Mola wako ndio mwisho wake



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 45

إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخۡشَىٰهَا

Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kukiogopa hicho kiyama



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 46

كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَهَا لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوۡ ضُحَىٰهَا

Siku watakapokiona, watakuwa kana kwamba hawakubaki (duniani) isipokuwa jioni moja au mchana wake



Sure: A’BASA

Vers : 1

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ

Alikunja paji lake la uso na akageuka



Sure: A’BASA

Vers : 2

أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ

Kwasababu alimjia kipofu



Sure: A’BASA

Vers : 3

وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ

Na nini kitakachokujulisha; huwenda akatakasika?



Sure: A’BASA

Vers : 4

أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ

Au akawaidhika na yakamnufaisha mawaidha?