Sure: AL-AARAAF 

Vers : 6

فَلَنَسۡـَٔلَنَّ ٱلَّذِينَ أُرۡسِلَ إِلَيۡهِمۡ وَلَنَسۡـَٔلَنَّ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Kwa hakika kabisa, tutawauliza wale waliopelekewa (Mitume) na kwa hakika kabisa tutawauliza tuliowapeleka (Mitume)



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 7

فَلَنَقُصَّنَّ عَلَيۡهِم بِعِلۡمٖۖ وَمَا كُنَّا غَآئِبِينَ

Tena, kwa yakini kabisa, tutawasimulia (walichokifanya) kwa kujua (kwa hoja), na hatukuwa mbali nao



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 8

وَٱلۡوَزۡنُ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡحَقُّۚ فَمَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ

Na mizani siku hiyo ni haki tu. Basi yeyote ambaye uzani wake (wa matendo yakheri) utakuwa mzito (na kuelemea) basi hao ndio tu wenye kufaulu



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 9

وَمَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ فَأُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ خَسِرُوٓاْ أَنفُسَهُم بِمَا كَانُواْ بِـَٔايَٰتِنَا يَظۡلِمُونَ

Na yeyote ambaye uzani wake (wa matendo yake ya kheri) utakuwa hafifu, basi hao ndio waliozitia hasara nafsi zao kwa sababu ya walivyokuwa wanazifanyia dhulumu aya zetu (kwa kuzikataa na kuzipinga)



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 10

وَلَقَدۡ مَكَّنَّـٰكُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَجَعَلۡنَا لَكُمۡ فِيهَا مَعَٰيِشَۗ قَلِيلٗا مَّا تَشۡكُرُونَ

Na kwa hakika kabisa, tulikupeni nafasi ardhini (duniani), na tulikufanyieni humo njia za (kupata) maisha (yenu). Ni uchache mno mnavyoshukuru



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 11

وَلَقَدۡ خَلَقۡنَٰكُمۡ ثُمَّ صَوَّرۡنَٰكُمۡ ثُمَّ قُلۡنَا لِلۡمَلَـٰٓئِكَةِ ٱسۡجُدُواْ لِأٓدَمَ فَسَجَدُوٓاْ إِلَّآ إِبۡلِيسَ لَمۡ يَكُن مِّنَ ٱلسَّـٰجِدِينَ

Na kwa hakika kabisa, tulikuumbeni, kisha tulikutieni sura, kisha tuliwaambia Malaika: Msujudieni Adamu. Walisujudu isipokuwa Ibilisi tu, hakuwa miongoni mwa waliosujudu



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 12

قَالَ مَا مَنَعَكَ أَلَّا تَسۡجُدَ إِذۡ أَمَرۡتُكَۖ قَالَ أَنَا۠ خَيۡرٞ مِّنۡهُ خَلَقۡتَنِي مِن نَّارٖ وَخَلَقۡتَهُۥ مِن طِينٖ

(Allah) Alisema (akimuuliza Ibilisi): Kipi kilichokuzuia usisujudu pale nilipokuamrisha? (Ibilisi) Alisema: Mimi ni bora zaidi kuliko yeye; umeniumba kwa moto, na yeye umemuumba kwa udongo



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 13

قَالَ فَٱهۡبِطۡ مِنۡهَا فَمَا يَكُونُ لَكَ أَن تَتَكَبَّرَ فِيهَا فَٱخۡرُجۡ إِنَّكَ مِنَ ٱلصَّـٰغِرِينَ

(Allah) Akasema: Basi teremka humo. Haikustahiki kwako kufanya kiburi humo. Basi toka. Hakika, wewe ni miongoni mwa walio duni kabisa



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 14

قَالَ أَنظِرۡنِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ

(Ibilisi) Alisema: Nibakishe mpaka Siku (waja wako) wataka-pofufuliwa



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 15

قَالَ إِنَّكَ مِنَ ٱلۡمُنظَرِينَ

(Allah) Akasema: Hakika, wewe ni miongoni mwa watakaobakishwa



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 16

قَالَ فَبِمَآ أَغۡوَيۡتَنِي لَأَقۡعُدَنَّ لَهُمۡ صِرَٰطَكَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ

(Ibilisi) Akasema: Basi kwa sababu umenipotosha (umeniacha nipotoke), nina apa kwamba, nitawakalia (nitawawekea vikwazo) katika njia yako ya sawa



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 17

ثُمَّ لَأٓتِيَنَّهُم مِّنۢ بَيۡنِ أَيۡدِيهِمۡ وَمِنۡ خَلۡفِهِمۡ وَعَنۡ أَيۡمَٰنِهِمۡ وَعَن شَمَآئِلِهِمۡۖ وَلَا تَجِدُ أَكۡثَرَهُمۡ شَٰكِرِينَ

Kisha, kwa yakini kabisa, nitawaendea mbele yao na nyuma yao na kuliani kwao na kushotoni kwao[1]. Na hutapata wengi wao wenye kushukuru


1- - Hapa Ibilisi anakusudia kwamba, atamfuatilia mwanadamu kila alipo. Hii ni sawa na ule msemo wa Kiswahili wa mtaani usemao “Nitakula naye sahani moja”.


Sure: AL-AARAAF 

Vers : 18

قَالَ ٱخۡرُجۡ مِنۡهَا مَذۡءُومٗا مَّدۡحُورٗاۖ لَّمَن تَبِعَكَ مِنۡهُمۡ لَأَمۡلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنكُمۡ أَجۡمَعِينَ

(Allah) Akasema (kumwambia Ibilisi kwamba): Toka humo (Peponi) ukiwa umechukiwa, umelaaniwa. Kwa yakini kabisa, yeyote atakayekufuata wewe miongoni mwao hakika nitaijaza Jahanamu kwa (kukutumbukizeni humo) nyinyi nyote



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 19

وَيَـٰٓـَٔادَمُ ٱسۡكُنۡ أَنتَ وَزَوۡجُكَ ٱلۡجَنَّةَ فَكُلَا مِنۡ حَيۡثُ شِئۡتُمَا وَلَا تَقۡرَبَا هَٰذِهِ ٱلشَّجَرَةَ فَتَكُونَا مِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na ewe Adamu, kaa wewe na mkeo Peponi. Basi kuleni katika mpendavyo na msiusogelee mti huu, mtakuwa miongoni mwa madhalimu



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 20

فَوَسۡوَسَ لَهُمَا ٱلشَّيۡطَٰنُ لِيُبۡدِيَ لَهُمَا مَا وُۥرِيَ عَنۡهُمَا مِن سَوۡءَٰتِهِمَا وَقَالَ مَا نَهَىٰكُمَا رَبُّكُمَا عَنۡ هَٰذِهِ ٱلشَّجَرَةِ إِلَّآ أَن تَكُونَا مَلَكَيۡنِ أَوۡ تَكُونَا مِنَ ٱلۡخَٰلِدِينَ

Basi shetani akawashawishi wawili hao ili awafunulie tupu zao zilizohifadhiwa na kusema (akiwaambia): Mola wenu hakukukatazeni mti huu isipokuwa tu msije mkawa Malaika wawili au mkawa miongoni mwa watakaoishi milele



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 21

وَقَاسَمَهُمَآ إِنِّي لَكُمَا لَمِنَ ٱلنَّـٰصِحِينَ

Na (shetani) akawaapia (kwamba): Kwa hakika kabisa, mimi kwenu ni miongoni mwa watoaji nasaha



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 22

فَدَلَّىٰهُمَا بِغُرُورٖۚ فَلَمَّا ذَاقَا ٱلشَّجَرَةَ بَدَتۡ لَهُمَا سَوۡءَٰتُهُمَا وَطَفِقَا يَخۡصِفَانِ عَلَيۡهِمَا مِن وَرَقِ ٱلۡجَنَّةِۖ وَنَادَىٰهُمَا رَبُّهُمَآ أَلَمۡ أَنۡهَكُمَا عَن تِلۡكُمَا ٱلشَّجَرَةِ وَأَقُل لَّكُمَآ إِنَّ ٱلشَّيۡطَٰنَ لَكُمَا عَدُوّٞ مُّبِينٞ

(Shetani) Akawashusha (Kutoka katika daraja la utiifu na kuwaweka katika uovu wa kukaidi amri ya Allah) kwa njia ya hadaa. Basi walipo uonja mti ule, zilidhihiri tupu zao na wakaanza kujibandika majani ya bustanini (ili kujisitiri). Na Mola wao aliwaita: Hivi sikukukatazeni mti ule na kukuambieni ya kwamba, hakika shetani kwenu ni adui aliye dhahiri sana?



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 23

قَالَا رَبَّنَا ظَلَمۡنَآ أَنفُسَنَا وَإِن لَّمۡ تَغۡفِرۡ لَنَا وَتَرۡحَمۡنَا لَنَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ

(Adamu na mkewe) Wakasema: Ewe Mola wetu Mlezi, sisi tumezidhulumu nafsi zetu, na kama hutatusamehe na kutuhurumia kwa hakika kabisa tutakuwa miongoni mwa wenye hasara



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 24

قَالَ ٱهۡبِطُواْ بَعۡضُكُمۡ لِبَعۡضٍ عَدُوّٞۖ وَلَكُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ مُسۡتَقَرّٞ وَمَتَٰعٌ إِلَىٰ حِينٖ

(Allah) Akasema: Teremkeni, nyinyi kwa nyinyi ni maadui, na nyinyi katika ardhi (duniani) mtakuwa na makazi na starehe (burudani) mpaka muda (maalumu)



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 25

قَالَ فِيهَا تَحۡيَوۡنَ وَفِيهَا تَمُوتُونَ وَمِنۡهَا تُخۡرَجُونَ

(Allah) Akasema: Humo (duniani) mtaishi na humo mtakufa na humo mtatolewa (mtafufuliwa)



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 26

يَٰبَنِيٓ ءَادَمَ قَدۡ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكُمۡ لِبَاسٗا يُوَٰرِي سَوۡءَٰتِكُمۡ وَرِيشٗاۖ وَلِبَاسُ ٱلتَّقۡوَىٰ ذَٰلِكَ خَيۡرٞۚ ذَٰلِكَ مِنۡ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ لَعَلَّهُمۡ يَذَّكَّرُونَ

Enyi wanadamu, hakika tumekuteremshieni vazi linaloficha tupu zenu na pambo. Na vazi la kumcha Allah ndio bora zaidi. Hizo ni baadhi ya ishara za Allah ili (wanadamu) wapate kukumbuka (neema za Mola wao Mlezi na kumshukuru)



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 27

يَٰبَنِيٓ ءَادَمَ لَا يَفۡتِنَنَّكُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ كَمَآ أَخۡرَجَ أَبَوَيۡكُم مِّنَ ٱلۡجَنَّةِ يَنزِعُ عَنۡهُمَا لِبَاسَهُمَا لِيُرِيَهُمَا سَوۡءَٰتِهِمَآۚ إِنَّهُۥ يَرَىٰكُمۡ هُوَ وَقَبِيلُهُۥ مِنۡ حَيۡثُ لَا تَرَوۡنَهُمۡۗ إِنَّا جَعَلۡنَا ٱلشَّيَٰطِينَ أَوۡلِيَآءَ لِلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ

Enyi Wanadamu, kamwe shetani asikufitinisheni[1] kama alivyowatoa Peponi wazazi wenu, akiwavua nguo zao ili kuwawekea wazi tupu zao. Hakika yeye (shetani) anakuoneni yeye na jeshi lake katika namna ambayo nyinyi hamuwaoni. Hakika, sisi tumewafanya mashetani wandani wa (watu) wasioamini


1- - Shetani asikudanganyeni kwa kukupambieni maasi, kama ambavyo alimhadaa baba yenu Adamu na mkewe kwa kuwashawishi waonje mti. Matokeo yake walitolewa Peponi.


Sure: AL-AARAAF 

Vers : 28

وَإِذَا فَعَلُواْ فَٰحِشَةٗ قَالُواْ وَجَدۡنَا عَلَيۡهَآ ءَابَآءَنَا وَٱللَّهُ أَمَرَنَا بِهَاۗ قُلۡ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَأۡمُرُ بِٱلۡفَحۡشَآءِۖ أَتَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ مَا لَا تَعۡلَمُونَ

Na wafanyapo mambo machafu wanasema: (Haya tuyafanyayo) Tumewakuta nayo baba zetu na Allah ametuamuru hayo. Sema: Hakika, Allah haamrishi machafu. Hivi mnamzushia Allah msiyoyajua?



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 29

قُلۡ أَمَرَ رَبِّي بِٱلۡقِسۡطِۖ وَأَقِيمُواْ وُجُوهَكُمۡ عِندَ كُلِّ مَسۡجِدٖ وَٱدۡعُوهُ مُخۡلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَۚ كَمَا بَدَأَكُمۡ تَعُودُونَ

Sema: Mola wangu Mlezi ameamrisha (kufanya) uadilifu. Na elekezeni nyuso zenu kila mnaposwali (mkusudieni Allah kila mfanyapo ibada) na muabuduni yeye tu mkimtakasia dini. Kama (Allah) ambavyo amekuumbeni mwanzo ndivyo mtakavyorudi



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 30

فَرِيقًا هَدَىٰ وَفَرِيقًا حَقَّ عَلَيۡهِمُ ٱلضَّلَٰلَةُۚ إِنَّهُمُ ٱتَّخَذُواْ ٱلشَّيَٰطِينَ أَوۡلِيَآءَ مِن دُونِ ٱللَّهِ وَيَحۡسَبُونَ أَنَّهُم مُّهۡتَدُونَ

Kundi moja (Allah) ameliongoa na kundi (lingine) limestahiki kupotea. Hakika, wao wamewafanya mashetani wandani (wao) badala ya Allah na wanadhani kwamba wameongoka



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 31

۞يَٰبَنِيٓ ءَادَمَ خُذُواْ زِينَتَكُمۡ عِندَ كُلِّ مَسۡجِدٖ وَكُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ وَلَا تُسۡرِفُوٓاْۚ إِنَّهُۥ لَا يُحِبُّ ٱلۡمُسۡرِفِينَ

Enyi wanadamu, chukueni mapambo yenu kila muendapo msikitini (kila mnaposwali)[1] na kuleni na kunyweni na msifanye ubadhirifu. Hakika, yeye (Allah) hawapendi wabadhirifu


1- - Aya hii ndio iliyoweka sharti la Muislamu kujisitiri kwa kuvaa nguo za heshima na sitara katika Swala. Na sio kuvaa nguo tu, lakini kuvaa nguo ya sitara, safi na inayopendeza. Kwa msingi huu, sio vyema kwa Muislamu kuswali akiwa amevaa nguo chafu au zenye michoro, picha na mandishi yasiyokuwa na lazima.


Sure: AL-AARAAF 

Vers : 32

قُلۡ مَنۡ حَرَّمَ زِينَةَ ٱللَّهِ ٱلَّتِيٓ أَخۡرَجَ لِعِبَادِهِۦ وَٱلطَّيِّبَٰتِ مِنَ ٱلرِّزۡقِۚ قُلۡ هِيَ لِلَّذِينَ ءَامَنُواْ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا خَالِصَةٗ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۗ كَذَٰلِكَ نُفَصِّلُ ٱلۡأٓيَٰتِ لِقَوۡمٖ يَعۡلَمُونَ

Sema: Hivi ni nani aliyeharamisha mapambo ya Allah ambayo ameyatoa kwa waja wake na riziki nzuri? Sema: Hayo (mapambo na riziki nzuri) ni kwa ajili ya wale walioamini katika maisha (yao) ya dunia, yakiwa halisi (ya peke yao) Siku ya Kiyama. Kama hivyo tunazifafanua Aya (zetu) kwa watu wanaojua



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 33

قُلۡ إِنَّمَا حَرَّمَ رَبِّيَ ٱلۡفَوَٰحِشَ مَا ظَهَرَ مِنۡهَا وَمَا بَطَنَ وَٱلۡإِثۡمَ وَٱلۡبَغۡيَ بِغَيۡرِ ٱلۡحَقِّ وَأَن تُشۡرِكُواْ بِٱللَّهِ مَا لَمۡ يُنَزِّلۡ بِهِۦ سُلۡطَٰنٗا وَأَن تَقُولُواْ عَلَى ٱللَّهِ مَا لَا تَعۡلَمُونَ

Sema: Hakika, ilivyo ni kwamba, Mola wangu Mlezi ameharamisha (mambo) machafu; ya dhahiri katika hayo na ya siri na dhambi na dhuluma bila ya haki yoyote,[1] na kuvishirikisha na Allah vitu ambavyo hakuviteremshia dalili (hoja) yoyote na (pia Allah ameharamisha) kumsemea Allah msiyoyajua


1- - Dhuluma bila ya haki ni dhuluma isiyokuwa na msingi wa kisheria. Ama kutekeleza haki kwa msingi wa sheria sio dhuluma wala ukandamizaji, ila tu limetumika neno dhuluma kwa ulinganifu wa lugha. Inayo onekana kama ni dhuluma kwenye macho ya wapingaji wa sheria za Allah ni kama kuuawa kwa mtu aliyethibitika kuua, kukatwa mkono mtu aliyethibitika kuiba n.k. Lakini hii sio dhuluma ila ni haki kwa sababu ni utekelezaji wa sheria.


Sure: AL-AARAAF 

Vers : 34

وَلِكُلِّ أُمَّةٍ أَجَلٞۖ فَإِذَا جَآءَ أَجَلُهُمۡ لَا يَسۡتَأۡخِرُونَ سَاعَةٗ وَلَا يَسۡتَقۡدِمُونَ

Na kila umma una muda (wake); basi utakapofika muda wao hawatachelewesha hata saa moja wala hawatasogeza



Sure: AL-AARAAF 

Vers : 35

يَٰبَنِيٓ ءَادَمَ إِمَّا يَأۡتِيَنَّكُمۡ رُسُلٞ مِّنكُمۡ يَقُصُّونَ عَلَيۡكُمۡ ءَايَٰتِي فَمَنِ ٱتَّقَىٰ وَأَصۡلَحَ فَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Enyi wanadamu, watakapo kufikieni Mitume watokanao na nyinyi wakikuhadithieni Aya zangu[1], basi yeyote atakayekuwa na uchaMungu na akafanya mema basi hawatakuwa na hofu yoyote, na hawatahuzunika


1- - Aya hii wanaitumia baadhi ya watu ili kupotosha. Wanadai kwamba, utume bado unaendelea. Itikadi ya Watu wa Sun ana Jama a ni kwamba, utume umekoma kwa Mtume Muhammad. Hakuna Mtume mwingine baada yake. Tujiulize swali la msingi. Aya hapa kama inasema kuwa Mitume wanaendelea kuja je, hizo Aya za Allah wanazotakiwa kutusomea ziko wapi? Rejea Aya ya 40, Sura Al-ahzab (33). Pia rejea Aya ya 158 ya Sura Al-aaraf (7).