Sure: AL-MAIDA 

Vers : 62

وَتَرَىٰ كَثِيرٗا مِّنۡهُمۡ يُسَٰرِعُونَ فِي ٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡعُدۡوَٰنِ وَأَكۡلِهِمُ ٱلسُّحۡتَۚ لَبِئۡسَ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Na utawaona wengi kati yao wanakimbilia kwenye dhambi na uadui na ulaji wao wa vya haramu. Kwa yakini kabisa, ni maovu mno hayo waliyokuwa wanayatenda



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 63

لَوۡلَا يَنۡهَىٰهُمُ ٱلرَّبَّـٰنِيُّونَ وَٱلۡأَحۡبَارُ عَن قَوۡلِهِمُ ٱلۡإِثۡمَ وَأَكۡلِهِمُ ٱلسُّحۡتَۚ لَبِئۡسَ مَا كَانُواْ يَصۡنَعُونَ

Mbona wachamungu (wao) na wanazuoni (wao) hawawakatazi kusema maneno ya dhambi na ulaji wao wa vya haramu? Kwa yakini kabisa, ni maovu mno hayo waliyokuwa wanayafanya



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 64

وَقَالَتِ ٱلۡيَهُودُ يَدُ ٱللَّهِ مَغۡلُولَةٌۚ غُلَّتۡ أَيۡدِيهِمۡ وَلُعِنُواْ بِمَا قَالُواْۘ بَلۡ يَدَاهُ مَبۡسُوطَتَانِ يُنفِقُ كَيۡفَ يَشَآءُۚ وَلَيَزِيدَنَّ كَثِيرٗا مِّنۡهُم مَّآ أُنزِلَ إِلَيۡكَ مِن رَّبِّكَ طُغۡيَٰنٗا وَكُفۡرٗاۚ وَأَلۡقَيۡنَا بَيۡنَهُمُ ٱلۡعَدَٰوَةَ وَٱلۡبَغۡضَآءَ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِۚ كُلَّمَآ أَوۡقَدُواْ نَارٗا لِّلۡحَرۡبِ أَطۡفَأَهَا ٱللَّهُۚ وَيَسۡعَوۡنَ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَسَادٗاۚ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ ٱلۡمُفۡسِدِينَ

Na Wayahudi walisema: Mkono wa Allah umefumba (kwa ubahili). Mikono yao ndio iliyofumba na wamelaaniwa (kwasababu ya hayo) waliyoyasema. Bali mikono yake (Allah) ni yenye kukunjuka; anatoa atakavyo. Na kwa yakini kabisa, yaliyoteremshwa kwako kutoka kwa Mola wako Mlezi yatawazidisha wengi wao uasi na ukafiri. Na tumerusha baina yao uadui na chuki mpaka Siku ya Kiama. Kila wanapowasha moto wa vita, Allah anauzima. Na wanakimbilia kufanya uovu katika ardhi. Na Allah hawapendi wafanyao uovu



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 65

وَلَوۡ أَنَّ أَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ ءَامَنُواْ وَٱتَّقَوۡاْ لَكَفَّرۡنَا عَنۡهُمۡ سَيِّـَٔاتِهِمۡ وَلَأَدۡخَلۡنَٰهُمۡ جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Na lau kama Watu wa Kitabu wangeamini na wakawa wachamungu bila shaka tungewafutia makosa yao, na tungewaingiza kwenye Pepo za neema



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 66

وَلَوۡ أَنَّهُمۡ أَقَامُواْ ٱلتَّوۡرَىٰةَ وَٱلۡإِنجِيلَ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡهِم مِّن رَّبِّهِمۡ لَأَكَلُواْ مِن فَوۡقِهِمۡ وَمِن تَحۡتِ أَرۡجُلِهِمۚ مِّنۡهُمۡ أُمَّةٞ مُّقۡتَصِدَةٞۖ وَكَثِيرٞ مِّنۡهُمۡ سَآءَ مَا يَعۡمَلُونَ

Na lau kama wangeliisimamisha Taurati na Injili na yote waliyo-teremshiwa kutoka kwa Mola wao Mlezi (kwa kuyafanyia kazi), bila shaka wangekula vitokavyo juu yao na vya chini ya miguu yao (wangepata riziki zao kwa wasaa na maisha yao kuwa ya furaha). Miongoni mwao wapo wenye msimamo wa wastani, na wengi miongoni mwao wayafanyayo ni mabaya sana



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 67

۞يَـٰٓأَيُّهَا ٱلرَّسُولُ بَلِّغۡ مَآ أُنزِلَ إِلَيۡكَ مِن رَّبِّكَۖ وَإِن لَّمۡ تَفۡعَلۡ فَمَا بَلَّغۡتَ رِسَالَتَهُۥۚ وَٱللَّهُ يَعۡصِمُكَ مِنَ ٱلنَّاسِۗ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Ewe Mtume, fikisha uliyotere-mshiwa kutoka kwa Mola wako Mlezi. Na usipofanya (hivyo) basi (utakuwa) hukufikisha ujumbe wake. Na Allah atakulinda dhidi ya watu. Hakika, Allah hawaongozi (njia ya sawa) watu makafiri



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 68

قُلۡ يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لَسۡتُمۡ عَلَىٰ شَيۡءٍ حَتَّىٰ تُقِيمُواْ ٱلتَّوۡرَىٰةَ وَٱلۡإِنجِيلَ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكُم مِّن رَّبِّكُمۡۗ وَلَيَزِيدَنَّ كَثِيرٗا مِّنۡهُم مَّآ أُنزِلَ إِلَيۡكَ مِن رَّبِّكَ طُغۡيَٰنٗا وَكُفۡرٗاۖ فَلَا تَأۡسَ عَلَى ٱلۡقَوۡمِ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Sema: Enyi Watu wa Kitabu, hamna lolote (la maana) mpaka muisimamishe Taurati na Injili na yote mliyoteremshiwa kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Na hakika ulioteremshiwa kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Na kwa yakini kabisa, yale uliyoteremshiwa na Mola wako Mlezi yatawazidishia wengi wao uasi na ukafiri. Basi usiwasikitikie watu makafiri



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 69

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَٱلَّذِينَ هَادُواْ وَٱلصَّـٰبِـُٔونَ وَٱلنَّصَٰرَىٰ مَنۡ ءَامَنَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَعَمِلَ صَٰلِحٗا فَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Hakika, walioamini na Wayahudi na Wasabai[1] na Wanaswara (Wakristo); waliomuamini Allah na Siku ya Mwisho na wakatenda mema, basi hawatakuwa na hofu na hawatahuzunika.[2]


1- - Ni watu wanaoabudu Malaika/nyota


2- - Aya hapa inawatangazia watu wa dini zote kwamba salama yao huko Akhera ni kuwa na Imani sahihi ya Uislamu inayosisitiza kumuamini Allah kwa usahihi wake na Siku ya Kiama na kutenda amali njema. Aya haimaanishi kuwa dini zote ni sahihi kama baadhi ya watu wanavyodhani. Ikumbukwe kuwa Aya ya 85 ya Sura Aal-imran (3) inaweka wazi kuwa dini inayokubalika ni Uislamu tu na asiyekuwa na Imani hiyo atakuwa katika hasara huko Akhera.


Sure: AL-MAIDA 

Vers : 70

لَقَدۡ أَخَذۡنَا مِيثَٰقَ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ وَأَرۡسَلۡنَآ إِلَيۡهِمۡ رُسُلٗاۖ كُلَّمَا جَآءَهُمۡ رَسُولُۢ بِمَا لَا تَهۡوَىٰٓ أَنفُسُهُمۡ فَرِيقٗا كَذَّبُواْ وَفَرِيقٗا يَقۡتُلُونَ

Kwa hakika kabisa, tulichukua ahadi ya Wana wa Israili[1] na tuliwapelekea Mitume. Kila alipowajia Mtume na yale ambayo nafsi zao haziyapendi wengine waliwapinga na wengine waliwauwa


1- - Ya kumuamini Allah na Mtume wake.


Sure: AL-MAIDA 

Vers : 71

وَحَسِبُوٓاْ أَلَّا تَكُونَ فِتۡنَةٞ فَعَمُواْ وَصَمُّواْ ثُمَّ تَابَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمۡ ثُمَّ عَمُواْ وَصَمُّواْ كَثِيرٞ مِّنۡهُمۡۚ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِمَا يَعۡمَلُونَ

Na walidhani kuwa hakutakuwa na mtihani (adhabu yoyote); kwasababu hiyo wakawa vipofu (wa kutoiona haki) na viziwi (wa kutoisikia haki). Kisha Allah akapokea Toba yao. Kisha wengi katika wao wakawa tena vipofu na viziwi. Na Allah ni Mwenye kuyaona hayo wayatendayo



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 72

لَقَدۡ كَفَرَ ٱلَّذِينَ قَالُوٓاْ إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلۡمَسِيحُ ٱبۡنُ مَرۡيَمَۖ وَقَالَ ٱلۡمَسِيحُ يَٰبَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ رَبِّي وَرَبَّكُمۡۖ إِنَّهُۥ مَن يُشۡرِكۡ بِٱللَّهِ فَقَدۡ حَرَّمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِ ٱلۡجَنَّةَ وَمَأۡوَىٰهُ ٱلنَّارُۖ وَمَا لِلظَّـٰلِمِينَ مِنۡ أَنصَارٖ

Kwa hakika kabisa, wamekufuru waliosema: Hakika, Allah ni Masihi Mwana wa Mariamu. Na Masihi (mwenyewe) alisema: Enyi Wana wa Israili, muabuduni Allah, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Ilivyo ni kwamba, yeyote anayemfanyia ushirika Allah, hakika Allah amemharamishia Pepo, na makazi yake ni Motoni. Na madhalimu hawatakuwa na watetezi wowote



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 73

لَّقَدۡ كَفَرَ ٱلَّذِينَ قَالُوٓاْ إِنَّ ٱللَّهَ ثَالِثُ ثَلَٰثَةٖۘ وَمَا مِنۡ إِلَٰهٍ إِلَّآ إِلَٰهٞ وَٰحِدٞۚ وَإِن لَّمۡ يَنتَهُواْ عَمَّا يَقُولُونَ لَيَمَسَّنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٌ

Kwa hakika kabisa, wamekufuru waliosema: Allah ni Watatu wa utatu. Na (ilivyo ni kwamba) hakuna yeyote mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa Muabudiwa Mmoja tu. Na wasipokoma (kusema) hayo wanayoyasema, kwa yakini kabisa itawashika wale waliokufuru miongoni mwao adhabu iumizayo sana



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 74

أَفَلَا يَتُوبُونَ إِلَى ٱللَّهِ وَيَسۡتَغۡفِرُونَهُۥۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Hivi, ni kwanini hawatubu kwa Allah na kumuomba msamaha? Na Allah ni Mwingi wa kusamehe mwenye kurehemu



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 75

مَّا ٱلۡمَسِيحُ ٱبۡنُ مَرۡيَمَ إِلَّا رَسُولٞ قَدۡ خَلَتۡ مِن قَبۡلِهِ ٱلرُّسُلُ وَأُمُّهُۥ صِدِّيقَةٞۖ كَانَا يَأۡكُلَانِ ٱلطَّعَامَۗ ٱنظُرۡ كَيۡفَ نُبَيِّنُ لَهُمُ ٱلۡأٓيَٰتِ ثُمَّ ٱنظُرۡ أَنَّىٰ يُؤۡفَكُونَ

Hakuwa Masihi Mwana wa Mariamu isipokuwa ni Mtume tu. Walishapita Mitume (wengi) kabla yake, na mama yake ni mwanamke msadikishaji mno. (Wote wawili) Walikuwa wanakula chakula (kama binadamu wengine). Angalia namna tunavyowabainishia (watu) hoja (mbalimbali), kisha angalia namna wanavyopotoshwa!



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 76

قُلۡ أَتَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ مَا لَا يَمۡلِكُ لَكُمۡ ضَرّٗا وَلَا نَفۡعٗاۚ وَٱللَّهُ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Sema: Hivi, mnaaabudu, badala ya Allah, wale (Miungu) ambao hawawezi kukuleteeni madhara wala manufaa? Na Allah ndiye hasa Msikiaji sana, Mwenye kujua



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 77

قُلۡ يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لَا تَغۡلُواْ فِي دِينِكُمۡ غَيۡرَ ٱلۡحَقِّ وَلَا تَتَّبِعُوٓاْ أَهۡوَآءَ قَوۡمٖ قَدۡ ضَلُّواْ مِن قَبۡلُ وَأَضَلُّواْ كَثِيرٗا وَضَلُّواْ عَن سَوَآءِ ٱلسَّبِيلِ

Sema: Enyi Watu wa Kitabu, msivuke mipaka katika dini yenu bila ya haki, na msifuate utashi wa nafsi wa watu waliokwishapotea tangu zamani, na wakawapoteza wengi, na wenyewe wakapotea njia ya sawa



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 78

لُعِنَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۢ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ عَلَىٰ لِسَانِ دَاوُۥدَ وَعِيسَى ٱبۡنِ مَرۡيَمَۚ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَواْ وَّكَانُواْ يَعۡتَدُونَ

Wamelaaniwa waliokufuru miongoni mwa Wana wa Israili kupitia ulimi wa Daudi na Issa Mwana wa Mariamu. Hayo ni kwasababu waliasi na walikuwa wanachupa mipaka



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 79

كَانُواْ لَا يَتَنَاهَوۡنَ عَن مُّنكَرٖ فَعَلُوهُۚ لَبِئۡسَ مَا كَانُواْ يَفۡعَلُونَ

Walikuwa hawakatazani maovu waliyokuwa wakiyafanya. Kwa yakini kabisa, ni maovu makubwa sana hayo waliyokuwa wanayafanya!



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 80

تَرَىٰ كَثِيرٗا مِّنۡهُمۡ يَتَوَلَّوۡنَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ لَبِئۡسَ مَا قَدَّمَتۡ لَهُمۡ أَنفُسُهُمۡ أَن سَخِطَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمۡ وَفِي ٱلۡعَذَابِ هُمۡ خَٰلِدُونَ

Utawaona wengi wao wana-wafanya makafiri marafiki (wao) wa ndani. Kwa yakini kabisa, ni maovu sana hayo yaliyotangulia kufanywa na nafsi zao hadi Allah amewakasirikia, na watadumu milele katika adhabu



Sure: AL-MAIDA 

Vers : 81

وَلَوۡ كَانُواْ يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلنَّبِيِّ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡهِ مَا ٱتَّخَذُوهُمۡ أَوۡلِيَآءَ وَلَٰكِنَّ كَثِيرٗا مِّنۡهُمۡ فَٰسِقُونَ

Na lau wangelimwamini Allah, na (huyu) Nabii, na yaliyoteremshwa kwake, wasingewafanya hao (makafiri) wapenzi wa ndani, lakini wengi katika wao ni waovu