وَمَا لَا تُبۡصِرُونَ
Na Naapa kwa yale msiyoyaona
Teilnahme :
إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ
Kwa hakika hii (Qur’ani) ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye heshima
وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَاعِرٖۚ قَلِيلٗا مَّا تُؤۡمِنُونَ
Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayoyaamini
وَلَا بِقَوۡلِ كَاهِنٖۚ قَلِيلٗا مَّا تَذَكَّرُونَ
Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka
تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Ni Uteremsho Kutoka Kwa Mola Wa Viumbe Vyote
وَلَوۡ تَقَوَّلَ عَلَيۡنَا بَعۡضَ ٱلۡأَقَاوِيلِ
Na Kama (Mtume) Angelizua Juu Yetu Baadhi Ya Maneno tu,
لَأَخَذۡنَا مِنۡهُ بِٱلۡيَمِينِ
Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia
ثُمَّ لَقَطَعۡنَا مِنۡهُ ٱلۡوَتِينَ
Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa (wa moyo!)
فَمَا مِنكُم مِّنۡ أَحَدٍ عَنۡهُ حَٰجِزِينَ
Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia
وَإِنَّهُۥ لَتَذۡكِرَةٞ لِّلۡمُتَّقِينَ
Kwa hakika hii (Qur’ani) ni ukumbusho kwa wachamungu
وَإِنَّا لَنَعۡلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ
Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha
وَإِنَّهُۥ لَحَسۡرَةٌ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na hakika hii (Qur’ani) bila shaka itakuwa ni majuto makubwa juu ya makafiri
وَإِنَّهُۥ لَحَقُّ ٱلۡيَقِينِ
Na hakika hii (Qur’an) ni haki ya yakini
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ
Basi litukuze jina la Mola Wako aliye Mkuu
سَأَلَ سَآئِلُۢ بِعَذَابٖ وَاقِعٖ
Muulizaji ameuliza kuhusu adhabu itakayotokea
لِّلۡكَٰفِرِينَ لَيۡسَ لَهُۥ دَافِعٞ
Kwa makafiri, hapana wa kuizuia
مِّنَ ٱللَّهِ ذِي ٱلۡمَعَارِجِ
Kutoka kwa Allah Mwenye madaraja ya juu (Mwenye mbingu za daraja)
تَعۡرُجُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيۡهِ فِي يَوۡمٖ كَانَ مِقۡدَارُهُۥ خَمۡسِينَ أَلۡفَ سَنَةٖ
Malaika na Roho (Jibrili) wanapanda kwenda kwake katika siku ambayo makadirio yake ni miaka hamsini elfu
فَٱصۡبِرۡ صَبۡرٗا جَمِيلًا
Basi subiri subira njema
إِنَّهُمۡ يَرَوۡنَهُۥ بَعِيدٗا
Hakika, wao wanaiona (siku hiyo) iko mbali
وَنَرَىٰهُ قَرِيبٗا
Nasi tunaiona iko karibu
يَوۡمَ تَكُونُ ٱلسَّمَآءُ كَٱلۡمُهۡلِ
Siku ambayo mbingu zitakuwa kama shaba iliyo yeyushwa
وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ
Na milima itakuwa kama sufi (iliyo chambuliwa)
وَلَا يَسۡـَٔلُ حَمِيمٌ حَمِيمٗا
Na rafiki hatomuuliza rafiki yake
يُبَصَّرُونَهُمۡۚ يَوَدُّ ٱلۡمُجۡرِمُ لَوۡ يَفۡتَدِي مِنۡ عَذَابِ يَوۡمِئِذِۭ بِبَنِيهِ
Watafanywa waonane. Mkosefu atatamani (kujikomboa) ajitolee fidia kutokana na adhabu Siku hiyo kwa kuwatoa watoto wake
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَأَخِيهِ
Na mke wake na nduguye
وَفَصِيلَتِهِ ٱلَّتِي تُـٔۡوِيهِ
Na jamaa zake wa karibu ambao wanamlinda
وَمَن فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا ثُمَّ يُنجِيهِ
Na (pia atatamani kutoa fidia kwa kulipa) vyote vilivyomo ardhini (duniani) kisha (ili) vimuokoe
كَلَّآۖ إِنَّهَا لَظَىٰ
Sio hivyo (Hayawezekani hayo). Kwa hakika, huo ni Moto mkali kabisa
نَزَّاعَةٗ لِّلشَّوَىٰ
Unaobabua kwa nguvu ngozi ya kichwani na mwilini