Sure: TWAHA 

Vers : 17

وَمَا تِلۡكَ بِيَمِينِكَ يَٰمُوسَىٰ

Na nini hicho kilichomo katika mkono wako wa kulia, ewe Mussa?



Sure: TWAHA 

Vers : 18

قَالَ هِيَ عَصَايَ أَتَوَكَّؤُاْ عَلَيۡهَا وَأَهُشُّ بِهَا عَلَىٰ غَنَمِي وَلِيَ فِيهَا مَـَٔارِبُ أُخۡرَىٰ

Akasema: Hii ni fimbo yangu; naiegemea na ninawaangushia majani kondoo na mbuzi wangu. Tena inanifaa kwa matumizi mengine



Sure: TWAHA 

Vers : 19

قَالَ أَلۡقِهَا يَٰمُوسَىٰ

(Allah) Akasema: Basi iangushe ewe Mussa



Sure: TWAHA 

Vers : 20

فَأَلۡقَىٰهَا فَإِذَا هِيَ حَيَّةٞ تَسۡعَىٰ

Akaitupa. Mara ikawa nyoka anaye kwenda mbio



Sure: TWAHA 

Vers : 21

قَالَ خُذۡهَا وَلَا تَخَفۡۖ سَنُعِيدُهَا سِيرَتَهَا ٱلۡأُولَىٰ

Akasema: Ikamate, wala usiogope! Tutairudisha hali yake ya kwanza



Sure: TWAHA 

Vers : 22

وَٱضۡمُمۡ يَدَكَ إِلَىٰ جَنَاحِكَ تَخۡرُجۡ بَيۡضَآءَ مِنۡ غَيۡرِ سُوٓءٍ ءَايَةً أُخۡرَىٰ

Na ukumbatie mkono wako kwenye ubavu wako. Utatoka mweupe pasipo kuwa na madhara yoyote. Hiyo ni ishara nyengine



Sure: TWAHA 

Vers : 23

لِنُرِيَكَ مِنۡ ءَايَٰتِنَا ٱلۡكُبۡرَى

Ili tukuonyeshe baadhi ya ishara zetu kubwa



Sure: TWAHA 

Vers : 24

ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Nenda kwa Firauni; kwani hakika yeye amepindukia mipaka



Sure: TWAHA 

Vers : 25

قَالَ رَبِّ ٱشۡرَحۡ لِي صَدۡرِي

(Mussa) akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Nikunjulie kifua changu,



Sure: TWAHA 

Vers : 26

وَيَسِّرۡ لِيٓ أَمۡرِي

Na uifanye kazi yangu (kuwa) nyepesi,



Sure: TWAHA 

Vers : 27

وَٱحۡلُلۡ عُقۡدَةٗ مِّن لِّسَانِي

Na ulifungue fundo lililo katika ulimi wangu,



Sure: TWAHA 

Vers : 28

يَفۡقَهُواْ قَوۡلِي

Wapate kufahamu maneno yangu



Sure: TWAHA 

Vers : 29

وَٱجۡعَل لِّي وَزِيرٗا مِّنۡ أَهۡلِي

Na nipe waziri katika watu wangu,



Sure: TWAHA 

Vers : 30

هَٰرُونَ أَخِي

Harun, ndugu yangu



Sure: TWAHA 

Vers : 31

ٱشۡدُدۡ بِهِۦٓ أَزۡرِي

Kwake yeye niongeze nguvu zangu



Sure: TWAHA 

Vers : 32

وَأَشۡرِكۡهُ فِيٓ أَمۡرِي

Na umshirikishe katika kazi yangu



Sure: TWAHA 

Vers : 33

كَيۡ نُسَبِّحَكَ كَثِيرٗا

Ili tukutakase sana



Sure: TWAHA 

Vers : 34

وَنَذۡكُرَكَ كَثِيرًا

Na tukukumbuke sana



Sure: TWAHA 

Vers : 35

إِنَّكَ كُنتَ بِنَا بَصِيرٗا

Hakika Wewe unatuona



Sure: TWAHA 

Vers : 36

قَالَ قَدۡ أُوتِيتَ سُؤۡلَكَ يَٰمُوسَىٰ

Akasema: Hakika Umepewa maombi yako, ewe Mussa!



Sure: TWAHA 

Vers : 37

وَلَقَدۡ مَنَنَّا عَلَيۡكَ مَرَّةً أُخۡرَىٰٓ

Na hakika tulikwisha kufanyia hisani mara nyengine



Sure: TWAHA 

Vers : 38

إِذۡ أَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰٓ أُمِّكَ مَا يُوحَىٰٓ

Pale tulipo mfunulia mama yako yaliyo funuliwa,



Sure: TWAHA 

Vers : 39

أَنِ ٱقۡذِفِيهِ فِي ٱلتَّابُوتِ فَٱقۡذِفِيهِ فِي ٱلۡيَمِّ فَلۡيُلۡقِهِ ٱلۡيَمُّ بِٱلسَّاحِلِ يَأۡخُذۡهُ عَدُوّٞ لِّي وَعَدُوّٞ لَّهُۥۚ وَأَلۡقَيۡتُ عَلَيۡكَ مَحَبَّةٗ مِّنِّي وَلِتُصۡنَعَ عَلَىٰ عَيۡنِيٓ

Ya kuwa mtie katika kisanduku, na kisha kitie mtoni, na mto utamfikisha ufukweni. Atamchukua adui yangu naye ni adui yake. Na nimekutilia mapenzi yanayotoka kwangu, na ili ulelewe machoni mwangu



Sure: TWAHA 

Vers : 40

إِذۡ تَمۡشِيٓ أُخۡتُكَ فَتَقُولُ هَلۡ أَدُلُّكُمۡ عَلَىٰ مَن يَكۡفُلُهُۥۖ فَرَجَعۡنَٰكَ إِلَىٰٓ أُمِّكَ كَيۡ تَقَرَّ عَيۡنُهَا وَلَا تَحۡزَنَۚ وَقَتَلۡتَ نَفۡسٗا فَنَجَّيۡنَٰكَ مِنَ ٱلۡغَمِّ وَفَتَنَّـٰكَ فُتُونٗاۚ فَلَبِثۡتَ سِنِينَ فِيٓ أَهۡلِ مَدۡيَنَ ثُمَّ جِئۡتَ عَلَىٰ قَدَرٖ يَٰمُوسَىٰ

Dada yako alipo kwenda na akasema: Je! Nikujuulisheni mtu wa kuweza kumlea? Basi tukakurejesha kwa mama yako ili macho yake yaburudike, wala asihuzunike. Na ulimuuwa mtu, nasi tukakuokoa katika dhiki, na tukakujaribu kwa majaribio mengi. Ukakaa miaka kwa watu wa Madiyana. Kisha ukaja kama ilivyo kadiriwa, ewe Mussa!



Sure: TWAHA 

Vers : 41

وَٱصۡطَنَعۡتُكَ لِنَفۡسِي

Na nimekuteuwa kwa ajili ya nafsi yangu



Sure: TWAHA 

Vers : 42

ٱذۡهَبۡ أَنتَ وَأَخُوكَ بِـَٔايَٰتِي وَلَا تَنِيَا فِي ذِكۡرِي

Nenda, wewe na ndugu yako, pamoja na ishara zangu, wala msichoke kunikumbuka



Sure: TWAHA 

Vers : 43

ٱذۡهَبَآ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Nendeni kwa Firauni. Hakika yeye amepindukia mipaka



Sure: TWAHA 

Vers : 44

فَقُولَا لَهُۥ قَوۡلٗا لَّيِّنٗا لَّعَلَّهُۥ يَتَذَكَّرُ أَوۡ يَخۡشَىٰ

Mwambieni maneno laini, huenda akazingatia au akaogopa



Sure: TWAHA 

Vers : 45

قَالَا رَبَّنَآ إِنَّنَا نَخَافُ أَن يَفۡرُطَ عَلَيۡنَآ أَوۡ أَن يَطۡغَىٰ

Wakasema: Ewe Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tunaogopa asije akapindukia mipaka juu yetu au kufanya jeuri



Sure: TWAHA 

Vers : 46

قَالَ لَا تَخَافَآۖ إِنَّنِي مَعَكُمَآ أَسۡمَعُ وَأَرَىٰ

Akasema: Msiogope! Hakika Mimi nipo pamoja nanyi. Nasikia na ninaona