وَأُزۡلِفَتِ ٱلۡجَنَّةُ لِلۡمُتَّقِينَ غَيۡرَ بَعِيدٍ
Na Pepo italetwa karibu kwa kwaajili ya Wacha Mungu, haitakuwa mbali
هَٰذَا مَا تُوعَدُونَ لِكُلِّ أَوَّابٍ حَفِيظٖ
(Itasemwa): Haya ndiyo yale mliyoahidiwa kwa kila mwenye kurejea kwa Allah, kwa kutubia, mwenye kuhifadhi vyema (amri za Allah)
مَّنۡ خَشِيَ ٱلرَّحۡمَٰنَ بِٱلۡغَيۡبِ وَجَآءَ بِقَلۡبٖ مُّنِيبٍ
Anayemuogopa Allah (Mwingi wa Rehema) hali yakuwa hamuoni akaja na moyo ulioelekea kwake
ٱدۡخُلُوهَا بِسَلَٰمٖۖ ذَٰلِكَ يَوۡمُ ٱلۡخُلُودِ
Ingieni kwa amani hiyo ndiyo siku ya kukaa milele
لَهُم مَّا يَشَآءُونَ فِيهَا وَلَدَيۡنَا مَزِيدٞ
Humo watakuwa na kila wanachokitaka na kwetu sisi kuna ziada. (ya kumuona Allah)
وَكَمۡ أَهۡلَكۡنَا قَبۡلَهُم مِّن قَرۡنٍ هُمۡ أَشَدُّ مِنۡهُم بَطۡشٗا فَنَقَّبُواْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ هَلۡ مِن مَّحِيصٍ
Na Watu wa karne ngapi Tumewaaangamiza kabla yao ambao walikuwa wenye nguvu zaidi kuliko wao. Basi walitangatanga sana katika nchi nyingi. Je, kuna mahali popote pa kukimbilia?
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَذِكۡرَىٰ لِمَن كَانَ لَهُۥ قَلۡبٌ أَوۡ أَلۡقَى ٱلسَّمۡعَ وَهُوَ شَهِيدٞ
Hakika katika hayo kuna ukumbusho kwa mtu mwenye moyo au ametega sikio nae yupo anashuhudia
وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَا فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ وَمَا مَسَّنَا مِن لُّغُوبٖ
Na kwa yakini Tumeumba mbingu na ardhi na vilivyo baina yake katika siku sita, na wala Hauku-tugusa uchovu wowote
فَٱصۡبِرۡ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ قَبۡلَ طُلُوعِ ٱلشَّمۡسِ وَقَبۡلَ ٱلۡغُرُوبِ
Basi vumilia kwa hayo wanayoyasema na mtakase Mola wako kwa kumhimidi kabla kuchomoza jua na kabla ya kuchwa
وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَسَبِّحۡهُ وَأَدۡبَٰرَ ٱلسُّجُودِ
Na katika majira ya usiku pia mtakase yeye na baada ya kusujudu
وَٱسۡتَمِعۡ يَوۡمَ يُنَادِ ٱلۡمُنَادِ مِن مَّكَانٖ قَرِيبٖ
Na sikiliza kwa makini Siku atakayonadi mwenye kunadi kutoka mahali pa karibu
يَوۡمَ يَسۡمَعُونَ ٱلصَّيۡحَةَ بِٱلۡحَقِّۚ ذَٰلِكَ يَوۡمُ ٱلۡخُرُوجِ
Siku watakayosikia ukelele kwa haki. Hiyo ndio Siku ya kutoka (makaburini na kufufuka)
إِنَّا نَحۡنُ نُحۡيِۦ وَنُمِيتُ وَإِلَيۡنَا ٱلۡمَصِيرُ
Hakika sisi ndiyo tunaohuisha na tunafisha na kwetu sisi tu ndiyo marejeo
يَوۡمَ تَشَقَّقُ ٱلۡأَرۡضُ عَنۡهُمۡ سِرَاعٗاۚ ذَٰلِكَ حَشۡرٌ عَلَيۡنَا يَسِيرٞ
Siku itakayowapasukia ardhi (watoke) haraka haraka. Huo ndio mkusanyo, ni mwepesi kabisa kwetu
نَّحۡنُ أَعۡلَمُ بِمَا يَقُولُونَۖ وَمَآ أَنتَ عَلَيۡهِم بِجَبَّارٖۖ فَذَكِّرۡ بِٱلۡقُرۡءَانِ مَن يَخَافُ وَعِيدِ
Sisi tunayajua wanayoyasema na wewe hukuwa mwenye kuwatenza nguvu, basi wakumbushe kwa Qur’ani yeyote mwenye kuogopa onyo langu
وَٱلذَّـٰرِيَٰتِ ذَرۡوٗا
Ninaapa kwa upepo (mkali) unaopeperusha (kila kitu)
فَٱلۡحَٰمِلَٰتِ وِقۡرٗا
Kisha (ninaapa) wa vile vibebavyo uzito (ikiwa ni pamoja na mawingu yanayobeba maji ya mvua)
فَٱلۡجَٰرِيَٰتِ يُسۡرٗا
Kisha (ninaapa) kwa (majahazi na vyombo vingine vizito vya majini) yenye kutembea (juu ya maji) kwa wepesi
فَٱلۡمُقَسِّمَٰتِ أَمۡرًا
Kisha (ninaapa) kwa (Malaika) wanaogawa mambo (majukumu waliyopewa na Allah)
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٞ
(Kwamba) Hakika ilivyo ni kwamba, mnachoahidiwa ni kweli kabisa
وَإِنَّ ٱلدِّينَ لَوَٰقِعٞ
Na Hakika, malipo (Siku ya Kiyama) kwa yakini kabisa yatakuwepo
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلۡحُبُكِ
Nina apa kwa mbingu yenye njia
إِنَّكُمۡ لَفِي قَوۡلٖ مُّخۡتَلِفٖ
(Kwamba) Hakika, nyinyi mmo katika zinazotofautiana.[1]
1- - Mara mseme Muhammad ni muongo, mara mchawi n.k.
يُؤۡفَكُ عَنۡهُ مَنۡ أُفِكَ
Huondolewa Humo Yule Anaye-ondolewa
قُتِلَ ٱلۡخَرَّـٰصُونَ
Wamelaaniwa Wakadhibishaji
ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي غَمۡرَةٖ سَاهُونَ
Wale Ambao Wamezama Katika Ujinga Hali Ya Kujisahau
يَسۡـَٔلُونَ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Wanauliza Ni Lini Hiyo Siku Ya Malipo
يَوۡمَ هُمۡ عَلَى ٱلنَّارِ يُفۡتَنُونَ
Siku Hiyo Wao Katika Moto Watachomwa
ذُوقُواْ فِتۡنَتَكُمۡ هَٰذَا ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تَسۡتَعۡجِلُونَ
Onjeni Adhabu Yenu Hii Ambayo Mlikua Kwayo Mnaiharakisha
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٍ
Hakika Ya Wachamungu Watakua Ndani Ya Pepo Na Chemchem