تَدۡعُواْ مَنۡ أَدۡبَرَ وَتَوَلَّىٰ
Unamwita yule aliyegeuza mgongo (aliyepuuza muongozo wa Allah) na akakengeuka
وَجَمَعَ فَأَوۡعَىٰٓ
Na akakusanya (mali) kisha akayahifadhi (katika makasha)
۞إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ خُلِقَ هَلُوعًا
Hakika, mwanadamu ameumbwa akiwa mwenye pupa (mwenye kukosa subira)
إِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ جَزُوعٗا
Inapomgusa shari anakuwa mwingi wa kupapatika (kulalamika na kuhuzunika)
وَإِذَا مَسَّهُ ٱلۡخَيۡرُ مَنُوعًا
Na inapomgusa kheri (anakuwa) mwingi wa kuzuia (bahili)
إِلَّا ٱلۡمُصَلِّينَ
Isipokuwa wenye kuswali
ٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ دَآئِمُونَ
Ambao wenye kudumisha Sala zao
وَٱلَّذِينَ فِيٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ حَقّٞ مَّعۡلُومٞ
Na wale ambao katika Mali zao kuna haki maalumu
لِّلسَّآئِلِ وَٱلۡمَحۡرُومِ
Kwa (Masikini) mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba
وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ
Na ambao wanasadikisha Siku ya Malipo, (siku ya Kiyama)
وَٱلَّذِينَ هُم مِّنۡ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشۡفِقُونَ
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao
إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمۡ غَيۡرُ مَأۡمُونٖ
Hakika adhabu ya Mola wao si ya kusalimika nayo
وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَٰفِظُونَ
Na ambao wanahifadhi tupu zao
إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٰجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُمۡ فَإِنَّهُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ
Isipokuwa kwa wake zao, au wale iliyowamiliki mikono yao ya kuume, basi hao si wenye kulaumiwa
فَمَنِ ٱبۡتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡعَادُونَ
Basi yeyote yule atakayetaka kinyume ya hayo, basi hao ndio warukao mipaka
وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِأَمَٰنَٰتِهِمۡ وَعَهۡدِهِمۡ رَٰعُونَ
Na ambao amana zao na ahadi zao ni wenye kuzichunga (na kuzitimiza)
وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَٰدَٰتِهِمۡ قَآئِمُونَ
Na ambao wanasimama imara katika kutoa ushahidi wao,
وَٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ يُحَافِظُونَ
Na ambao kwenye Sala zao ni wenye kuzilinda
أُوْلَـٰٓئِكَ فِي جَنَّـٰتٖ مُّكۡرَمُونَ
Hao ndio watakao heshimiwa Peponi
فَمَالِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ قِبَلَكَ مُهۡطِعِينَ
Wana nini wale walio kufuru (wanaharakiza mbele yako) na wanakutumbulia macho tu?
عَنِ ٱلۡيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ عِزِينَ
(Kukukalia) makundi kwa makundi kuliani na kushotoni.[1]
1- - Kitu gani kinawapelekea hao walio kufuru kukujia mbio mbio kutoka kuliani na kushotoni kwa makundi?.
أَيَطۡمَعُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُدۡخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٖ
Je, kwani kila mmoja wao ana tamaa ya kuingia kwenye Pepo yenye neema?
كَلَّآۖ إِنَّا خَلَقۡنَٰهُم مِّمَّا يَعۡلَمُونَ
Sivyo hivyo! Hakika Sisi Tumewaumba kutokana na kile wanachokijua.[1]
1- - Basi nawaache hiyo tamaa yao ya kuingia Peponi. Hakika Sisi tumewaumba wao kutokana na maji ya kudharauliwa (dhalili).
فَلَآ أُقۡسِمُ بِرَبِّ ٱلۡمَشَٰرِقِ وَٱلۡمَغَٰرِبِ إِنَّا لَقَٰدِرُونَ
Basi Naapa kwa Mola wa Mashariki zote na Magharibi zote, hakika Sisi bila shaka ni Wenye kuweza
عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ خَيۡرٗا مِّنۡهُمۡ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ
(Tuna uwezo wa) Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi
فَذَرۡهُمۡ يَخُوضُواْ وَيَلۡعَبُواْ حَتَّىٰ يُلَٰقُواْ يَوۡمَهُمُ ٱلَّذِي يُوعَدُونَ
Basi waachilie mbali watumbukie katika porojo na upuuzi, na wacheze, mpaka wakutane na Siku yao ambayo wanayo ahidiwa
يَوۡمَ يَخۡرُجُونَ مِنَ ٱلۡأَجۡدَاثِ سِرَاعٗا كَأَنَّهُمۡ إِلَىٰ نُصُبٖ يُوفِضُونَ
Siku watapotoka makaburini haraka haraka kana kwamba wanakimbilia kushindana kuifikia kwenye Lengo
خَٰشِعَةً أَبۡصَٰرُهُمۡ تَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۚ ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمُ ٱلَّذِي كَانُواْ يُوعَدُونَ
Macho yao yatainama chini, udhalili utawafunika. Hiyo ndio ile siku waliyokuwa wakiahidiwa
إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوۡمِهِۦٓ أَنۡ أَنذِرۡ قَوۡمَكَ مِن قَبۡلِ أَن يَأۡتِيَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ
Hakika, Sisi Tulimtuma Nuhu kwa watu wake (tukamwambia) kwamba: Waonye watu wako kabla haijawafikia adhabu iumizayo sana
قَالَ يَٰقَوۡمِ إِنِّي لَكُمۡ نَذِيرٞ مُّبِينٌ
(Nuhu) Akasema: Enyi watu wangu, hakika mimi kwenu ni muonyaji wa dhahiri (wa wazi) kwenu