وَلَقَدۡ رَءَاهُ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡمُبِينِ
Na hakika yeye alimwona [Jibrili] kwenye upeo wa macho ulio safi
Teilnahme :
وَمَا هُوَ عَلَى ٱلۡغَيۡبِ بِضَنِينٖ
Wala yeye si bakhili kwa [kuelezea mambo ya] ghaibu
وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٖ
Na hii (Qurani) si kauli ya shetani aliye fukuzwa kutoka kwenye rehema za Allah
فَأَيۡنَ تَذۡهَبُونَ
Basi mnakwenda wapi?
إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Hii (Qurani) haikuwa isipokuwa ni ukumbusho kwa walimwengu wote
لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَسۡتَقِيمَ
Kwa yule anaye taka miongoni mwenu kwenda sawa
وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Allah Mola wa Walimwengu wote
إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتۡ
Mbingu itakapo chanika,
وَإِذَا ٱلۡكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتۡ
Na nyota zitakapo tawanyika,
وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ فُجِّرَتۡ
Na bahari zitakapo pasuliwa,
وَإِذَا ٱلۡقُبُورُ بُعۡثِرَتۡ
Na makaburi yatakapo fukuliwa,
عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ وَأَخَّرَتۡ
Hapo kila nafsi itajua ilichotanguliza, na ilicho bakisha nyuma
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلۡكَرِيمِ
Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
ٱلَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ
Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
فِيٓ أَيِّ صُورَةٖ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ
Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga
كَلَّا بَلۡ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo
وَإِنَّ عَلَيۡكُمۡ لَحَٰفِظِينَ
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
كِرَامٗا كَٰتِبِينَ
Waandishi wenye hishima,
يَعۡلَمُونَ مَا تَفۡعَلُونَ
Wanayajua mnayo yatenda
إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٖ
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
وَإِنَّ ٱلۡفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٖ
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
يَصۡلَوۡنَهَا يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Wataingia humo Siku ya Malipo
وَمَا هُمۡ عَنۡهَا بِغَآئِبِينَ
Na hawatoacha kuwamo humo
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
ثُمَّ مَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
يَوۡمَ لَا تَمۡلِكُ نَفۡسٞ لِّنَفۡسٖ شَيۡـٔٗاۖ وَٱلۡأَمۡرُ يَوۡمَئِذٖ لِّلَّهِ
(Ni) Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu
وَيۡلٞ لِّلۡمُطَفِّفِينَ
Ole wao hao wapunjao!
ٱلَّذِينَ إِذَا ٱكۡتَالُواْ عَلَى ٱلنَّاسِ يَسۡتَوۡفُونَ
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe
وَإِذَا كَالُوهُمۡ أَو وَّزَنُوهُمۡ يُخۡسِرُونَ
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza
أَلَا يَظُنُّ أُوْلَـٰٓئِكَ أَنَّهُم مَّبۡعُوثُونَ
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa