Sure: AL-BURUJI 

Vers : 4

قُتِلَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأُخۡدُودِ

Wameangamizwa watu wa mahandaki



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 5

ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلۡوَقُودِ

Yenye moto wenye kuni nyingi,



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 6

إِذۡ هُمۡ عَلَيۡهَا قُعُودٞ

Walipo kuwa wamekaa hapo,



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 7

وَهُمۡ عَلَىٰ مَا يَفۡعَلُونَ بِٱلۡمُؤۡمِنِينَ شُهُودٞ

Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 8

وَمَا نَقَمُواْ مِنۡهُمۡ إِلَّآ أَن يُؤۡمِنُواْ بِٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَمِيدِ

Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Allah, Mwenye nguvu, Msifiwa,



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 9

ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدٌ

Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Allah ni shaahidi wa kila kitu



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 10

إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُواْ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ ثُمَّ لَمۡ يَتُوبُواْ فَلَهُمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمۡ عَذَابُ ٱلۡحَرِيقِ

Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 11

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ لَهُمۡ جَنَّـٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡكَبِيرُ

Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 12

إِنَّ بَطۡشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ

Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 13

إِنَّهُۥ هُوَ يُبۡدِئُ وَيُعِيدُ

Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejesha tena,



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 14

وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلۡوَدُودُ

Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 15

ذُو ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡمَجِيدُ

Mwenye Kiti cha Enzi,



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 16

فَعَّالٞ لِّمَا يُرِيدُ

Atendaye ayatakayo



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 17

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡجُنُودِ

Je! Zimekufikia khabari za majeshi?



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 18

فِرۡعَوۡنَ وَثَمُودَ

Ya Firauni na Thamudi?



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 19

بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي تَكۡذِيبٖ

Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 20

وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطُۢ

Na Allah nyuma yao amewazunguka



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 21

بَلۡ هُوَ قُرۡءَانٞ مَّجِيدٞ

Bali hii ni Qur’ani tukufu



Sure: AL-BURUJI 

Vers : 22

فِي لَوۡحٖ مَّحۡفُوظِۭ

Katika Ubao Ulio Hifadhiwa



Sure: ATTAARIQ 

Vers : 1

وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ

Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!



Sure: ATTAARIQ 

Vers : 2

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ

Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinachokuja usiku?



Sure: ATTAARIQ 

Vers : 3

ٱلنَّجۡمُ ٱلثَّاقِبُ

Ni Nyota yenye mwanga mkali



Sure: ATTAARIQ 

Vers : 4

إِن كُلُّ نَفۡسٖ لَّمَّا عَلَيۡهَا حَافِظٞ

Hapana nafsi ila inayo mwangalizi



Sure: ATTAARIQ 

Vers : 5

فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ

Hebu na ajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?



Sure: ATTAARIQ 

Vers : 6

خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ

Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,



Sure: ATTAARIQ 

Vers : 7

يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ

Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu



Sure: ATTAARIQ 

Vers : 8

إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجۡعِهِۦ لَقَادِرٞ

Hakika Yeye ana uwezo wa kumrudisha



Sure: ATTAARIQ 

Vers : 9

يَوۡمَ تُبۡلَى ٱلسَّرَآئِرُ

Siku zitakapo dhihirishwa siri



Sure: ATTAARIQ 

Vers : 10

فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٖ وَلَا نَاصِرٖ

Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi



Sure: ATTAARIQ 

Vers : 11

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجۡعِ

Naapa kwa mbingu yenye marejeo!