Capítulo: SWAAD 

Verso : 63

أَتَّخَذۡنَٰهُمۡ سِخۡرِيًّا أَمۡ زَاغَتۡ عَنۡهُمُ ٱلۡأَبۡصَٰرُ

Tulikosea tulipo wafanyia mas-khara, au macho yetu tu hayawaoni?



Capítulo: SWAAD 

Verso : 64

إِنَّ ذَٰلِكَ لَحَقّٞ تَخَاصُمُ أَهۡلِ ٱلنَّارِ

Hakika hayo bila ya shaka ndiyo makhasimiano ya watu wa Motoni



Capítulo: SWAAD 

Verso : 65

قُلۡ إِنَّمَآ أَنَا۠ مُنذِرٞۖ وَمَا مِنۡ إِلَٰهٍ إِلَّا ٱللَّهُ ٱلۡوَٰحِدُ ٱلۡقَهَّارُ

Sema: Hakika mimi ni mwonyaji tu; na hapana mungu ila Allah Mmoja, Mwenye nguvu,



Capítulo: SWAAD 

Verso : 66

رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡغَفَّـٰرُ

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake, Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe



Capítulo: SWAAD 

Verso : 67

قُلۡ هُوَ نَبَؤٌاْ عَظِيمٌ

Sema: Hii ni habari kubwa kabisa



Capítulo: SWAAD 

Verso : 68

أَنتُمۡ عَنۡهُ مُعۡرِضُونَ

Ambayo nyinyi mnaipuuza



Capítulo: SWAAD 

Verso : 69

مَا كَانَ لِيَ مِنۡ عِلۡمِۭ بِٱلۡمَلَإِ ٱلۡأَعۡلَىٰٓ إِذۡ يَخۡتَصِمُونَ

Sikuwa na elimu ya mambo ya viumbe wakuu watukufu walipokuwa wakishindana



Capítulo: SWAAD 

Verso : 70

إِن يُوحَىٰٓ إِلَيَّ إِلَّآ أَنَّمَآ أَنَا۠ نَذِيرٞ مُّبِينٌ

Haikufunuliwa kwangu isipo kuwa ya kwamba hakika mimi ni mwonyaji dhahiri



Capítulo: SWAAD 

Verso : 71

إِذۡ قَالَ رَبُّكَ لِلۡمَلَـٰٓئِكَةِ إِنِّي خَٰلِقُۢ بَشَرٗا مِّن طِينٖ

Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitaumba mtu kutokana na udongo



Capítulo: SWAAD 

Verso : 72

فَإِذَا سَوَّيۡتُهُۥ وَنَفَخۡتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُواْ لَهُۥ سَٰجِدِينَ

Na nitakapo mkamilisha na kumpulizia roho inayo tokana nami, basi muangukieni kwa kumtii



Capítulo: SWAAD 

Verso : 73

فَسَجَدَ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ كُلُّهُمۡ أَجۡمَعُونَ

Basi Malaika wakatii wote pamoja



Capítulo: SWAAD 

Verso : 74

إِلَّآ إِبۡلِيسَ ٱسۡتَكۡبَرَ وَكَانَ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Isipo kuwa Iblisi; alijivuna na akawa katika makafiri



Capítulo: SWAAD 

Verso : 75

قَالَ يَـٰٓإِبۡلِيسُ مَا مَنَعَكَ أَن تَسۡجُدَ لِمَا خَلَقۡتُ بِيَدَيَّۖ أَسۡتَكۡبَرۡتَ أَمۡ كُنتَ مِنَ ٱلۡعَالِينَ

Allah akamwambia: Ewe Iblisi! Kipi kilicho kuzuia kumtii yule niliye muumba kwa mikono yangu? Je! Umejiona mkubwa, au umekuwa katika wakuu kweli?



Capítulo: SWAAD 

Verso : 76

قَالَ أَنَا۠ خَيۡرٞ مِّنۡهُ خَلَقۡتَنِي مِن نَّارٖ وَخَلَقۡتَهُۥ مِن طِينٖ

Akasema: Mimi ni bora kuliko yeye. Umeniumba kwa moto, na yeye umemuumba kwa udongo



Capítulo: SWAAD 

Verso : 77

قَالَ فَٱخۡرُجۡ مِنۡهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٞ

Akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umelaanika



Capítulo: SWAAD 

Verso : 78

وَإِنَّ عَلَيۡكَ لَعۡنَتِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na hakika laana yangu itakuwa juu yako mpaka Siku ya Malipo



Capítulo: SWAAD 

Verso : 79

قَالَ رَبِّ فَأَنظِرۡنِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ

Akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watayo fufuliwa viumbe



Capítulo: SWAAD 

Verso : 80

قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ ٱلۡمُنظَرِينَ

Allah akasema: Basi umekwisha kuwa miongoni mwa walio pewa muhula,



Capítulo: SWAAD 

Verso : 81

إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡوَقۡتِ ٱلۡمَعۡلُومِ

Mpaka siku ya wakati maalumu



Capítulo: SWAAD 

Verso : 82

قَالَ فَبِعِزَّتِكَ لَأُغۡوِيَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Akasema (Iblisi): Naapa kwa utukufu wako, bila ya shaka nitawapoteza wote,



Capítulo: SWAAD 

Verso : 83

إِلَّا عِبَادَكَ مِنۡهُمُ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipo kuwa wale waja wako miongoni mwao walio chaguliwa



Capítulo: SWAAD 

Verso : 84

قَالَ فَٱلۡحَقُّ وَٱلۡحَقَّ أَقُولُ

Akasema: Haki! Na haki ninaisema



Capítulo: SWAAD 

Verso : 85

لَأَمۡلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنكَ وَمِمَّن تَبِعَكَ مِنۡهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Bila ya shaka nitaijaza Jahannamu kwa wewe na kwa hao wote wenye kukufuata miongoni mwao



Capítulo: SWAAD 

Verso : 86

قُلۡ مَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٖ وَمَآ أَنَا۠ مِنَ ٱلۡمُتَكَلِّفِينَ

Sema (Ewe Mtume): Sikuombeni ujira juu ya haya, wala mimi si katika wadanganyifu



Capítulo: SWAAD 

Verso : 87

إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ

Hayakuwa haya ila ni mawaidha kwa walimwengu wote



Capítulo: SWAAD 

Verso : 88

وَلَتَعۡلَمُنَّ نَبَأَهُۥ بَعۡدَ حِينِۭ

Na bila ya shaka mtajua khabari zake baada ya muda



Capítulo: AZZUMAR 

Verso : 1

تَنزِيلُ ٱلۡكِتَٰبِ مِنَ ٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَكِيمِ

(Huu) Ni uteremsho wa Kitabu kutoka kwa Allah, Mwenye nguvu kubwa, Mwenye hekima sana



Capítulo: AZZUMAR 

Verso : 2

إِنَّآ أَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ فَٱعۡبُدِ ٱللَّهَ مُخۡلِصٗا لَّهُ ٱلدِّينَ

Hakika, sisi tumekuteremshia Kitabu (hiki) kwa haki. Basi muabudu Allah ukimsafia Dini Yeye tu



Capítulo: AZZUMAR 

Verso : 3

أَلَا لِلَّهِ ٱلدِّينُ ٱلۡخَالِصُۚ وَٱلَّذِينَ ٱتَّخَذُواْ مِن دُونِهِۦٓ أَوۡلِيَآءَ مَا نَعۡبُدُهُمۡ إِلَّا لِيُقَرِّبُونَآ إِلَى ٱللَّهِ زُلۡفَىٰٓ إِنَّ ٱللَّهَ يَحۡكُمُ بَيۡنَهُمۡ فِي مَا هُمۡ فِيهِ يَخۡتَلِفُونَۗ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَهۡدِي مَنۡ هُوَ كَٰذِبٞ كَفَّارٞ

Zindukeni! Dini halisi ni ya Allah tu. Na wale waliowafanya (Miungu) wapenzi badala yake (Allah walipoulizwa sababu ya kufanya hivyo walijibu kuwa): Sisi hatuwaabudu isipokuwa tu wapate kutusogeza karibu na Allah. Hakika, Allah atahukumu baina yao katika wanayo tofautiana. Hakika, Allah hamuongozi (mtu) muongo, kafiri mno



Capítulo: AZZUMAR 

Verso : 4

لَّوۡ أَرَادَ ٱللَّهُ أَن يَتَّخِذَ وَلَدٗا لَّٱصۡطَفَىٰ مِمَّا يَخۡلُقُ مَا يَشَآءُۚ سُبۡحَٰنَهُۥۖ هُوَ ٱللَّهُ ٱلۡوَٰحِدُ ٱلۡقَهَّارُ

Lau kuwa Allah angeli taka kuwa na mwana, basi bila ya shaka angeli teua amtakaye katika alio waumba. Subhanahu, Ametakasika na hayo! Yeye ni Allah Mmoja, anatenda atakalo