Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 27

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ

Na watu wa kuliani, ni wepi hao watu wa kuliani?



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 28

فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ

Watakuwa kwenye mikunazi isiyo na miba



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 29

وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ

Na migomba iliyopangiliwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 30

وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ

Na kivuli kilichotandazwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 31

وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ

Na maji yenye kumiminwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 32

وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ

Na matunda mengi



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 33

لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ

Hayana kikomo na wala hayakatazwi



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 34

وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ

Na matandiko ya kupumzikia yaliyoinuliwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 35

إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ

Hakika Sisi Tutawaumba (Mahurulaini) upya



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 36

فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا

Na tukawafanya kuwa bikra



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 37

عُرُبًا أَتۡرَابٗا

Wenye mahaba kwa waume zao, na wana umri unaolingana



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 38

لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Ni kwaajili ya watu wa kuliani



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 39

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kundi kubwa katika watu wa mwanzo



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 40

وَثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na kundi kubwa katika watu wa mwishoni



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 41

وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ

Na watu wa kushotoni, je, ni wepi watu wa kushotoni?



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 42

فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ

(Watakuwa) Kwenye moto ubabuao na maji yachemkayo



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 43

وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ

Na kivuli cha moshi mweusi mnene wa joto kali mno



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 44

لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ

Si cha baridi na wala si cha kunufaisha



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 45

إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُتۡرَفِينَ

Hakika walikua kabla ya hapo kwenye maisha ya neema na anasa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 46

وَكَانُواْ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلۡحِنثِ ٱلۡعَظِيمِ

Na walikuwa wakishikilia kufanya dhambi kubwa mno



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 47

وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ

Na walikuwa wakisema: Je, hivi tutakapo kufa na tukawa udongo na mifupa, je hivi sisi hakika tutafufuliwa?



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 48

أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ

Au na wazee wetu wa mwanzo?



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 49

قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَوَّلِينَ وَٱلۡأٓخِرِينَ

Sema; Hakika wa mwanzo na wa mwisho,



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 50

لَمَجۡمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ

Hakika watakusanywa kwenye wakati na siku maalumu



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 51

ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ

Kisha hakika nyinyi enyi wapotovu mnaokadhibisha



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 52

لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ

Hakika mtakula chakula kitokanacho na mti wa mzakoum



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 53

فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ

Basi mtajaza kutokana na mti huo matumbo yenu



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 54

فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ

Na mtakunywa juu yake maji ya moto ya chemkayo



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 55

فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ

Tena mtakunywa unywaji wa ngamia mwenye kiu kubwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 56

هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Haya ndio mapokezi yao Siku ya Malipo! (Kiyama)