Capítulo: TWAHA 

Verso : 17

وَمَا تِلۡكَ بِيَمِينِكَ يَٰمُوسَىٰ

Na nini hicho kilichomo katika mkono wako wa kulia, ewe Mussa?



Capítulo: TWAHA 

Verso : 18

قَالَ هِيَ عَصَايَ أَتَوَكَّؤُاْ عَلَيۡهَا وَأَهُشُّ بِهَا عَلَىٰ غَنَمِي وَلِيَ فِيهَا مَـَٔارِبُ أُخۡرَىٰ

Akasema: Hii ni fimbo yangu; naiegemea na ninawaangushia majani kondoo na mbuzi wangu. Tena inanifaa kwa matumizi mengine



Capítulo: TWAHA 

Verso : 19

قَالَ أَلۡقِهَا يَٰمُوسَىٰ

(Allah) Akasema: Basi iangushe ewe Mussa



Capítulo: TWAHA 

Verso : 20

فَأَلۡقَىٰهَا فَإِذَا هِيَ حَيَّةٞ تَسۡعَىٰ

Akaitupa. Mara ikawa nyoka anaye kwenda mbio



Capítulo: TWAHA 

Verso : 21

قَالَ خُذۡهَا وَلَا تَخَفۡۖ سَنُعِيدُهَا سِيرَتَهَا ٱلۡأُولَىٰ

Akasema: Ikamate, wala usiogope! Tutairudisha hali yake ya kwanza



Capítulo: TWAHA 

Verso : 22

وَٱضۡمُمۡ يَدَكَ إِلَىٰ جَنَاحِكَ تَخۡرُجۡ بَيۡضَآءَ مِنۡ غَيۡرِ سُوٓءٍ ءَايَةً أُخۡرَىٰ

Na ukumbatie mkono wako kwenye ubavu wako. Utatoka mweupe pasipo kuwa na madhara yoyote. Hiyo ni ishara nyengine



Capítulo: TWAHA 

Verso : 23

لِنُرِيَكَ مِنۡ ءَايَٰتِنَا ٱلۡكُبۡرَى

Ili tukuonyeshe baadhi ya ishara zetu kubwa



Capítulo: TWAHA 

Verso : 24

ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Nenda kwa Firauni; kwani hakika yeye amepindukia mipaka



Capítulo: TWAHA 

Verso : 25

قَالَ رَبِّ ٱشۡرَحۡ لِي صَدۡرِي

(Mussa) akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Nikunjulie kifua changu,



Capítulo: TWAHA 

Verso : 26

وَيَسِّرۡ لِيٓ أَمۡرِي

Na uifanye kazi yangu (kuwa) nyepesi,



Capítulo: TWAHA 

Verso : 27

وَٱحۡلُلۡ عُقۡدَةٗ مِّن لِّسَانِي

Na ulifungue fundo lililo katika ulimi wangu,



Capítulo: TWAHA 

Verso : 28

يَفۡقَهُواْ قَوۡلِي

Wapate kufahamu maneno yangu



Capítulo: TWAHA 

Verso : 29

وَٱجۡعَل لِّي وَزِيرٗا مِّنۡ أَهۡلِي

Na nipe waziri katika watu wangu,



Capítulo: TWAHA 

Verso : 30

هَٰرُونَ أَخِي

Harun, ndugu yangu



Capítulo: TWAHA 

Verso : 31

ٱشۡدُدۡ بِهِۦٓ أَزۡرِي

Kwake yeye niongeze nguvu zangu



Capítulo: TWAHA 

Verso : 32

وَأَشۡرِكۡهُ فِيٓ أَمۡرِي

Na umshirikishe katika kazi yangu



Capítulo: TWAHA 

Verso : 33

كَيۡ نُسَبِّحَكَ كَثِيرٗا

Ili tukutakase sana



Capítulo: TWAHA 

Verso : 34

وَنَذۡكُرَكَ كَثِيرًا

Na tukukumbuke sana



Capítulo: TWAHA 

Verso : 35

إِنَّكَ كُنتَ بِنَا بَصِيرٗا

Hakika Wewe unatuona



Capítulo: TWAHA 

Verso : 36

قَالَ قَدۡ أُوتِيتَ سُؤۡلَكَ يَٰمُوسَىٰ

Akasema: Hakika Umepewa maombi yako, ewe Mussa!



Capítulo: TWAHA 

Verso : 37

وَلَقَدۡ مَنَنَّا عَلَيۡكَ مَرَّةً أُخۡرَىٰٓ

Na hakika tulikwisha kufanyia hisani mara nyengine



Capítulo: TWAHA 

Verso : 38

إِذۡ أَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰٓ أُمِّكَ مَا يُوحَىٰٓ

Pale tulipo mfunulia mama yako yaliyo funuliwa,



Capítulo: TWAHA 

Verso : 39

أَنِ ٱقۡذِفِيهِ فِي ٱلتَّابُوتِ فَٱقۡذِفِيهِ فِي ٱلۡيَمِّ فَلۡيُلۡقِهِ ٱلۡيَمُّ بِٱلسَّاحِلِ يَأۡخُذۡهُ عَدُوّٞ لِّي وَعَدُوّٞ لَّهُۥۚ وَأَلۡقَيۡتُ عَلَيۡكَ مَحَبَّةٗ مِّنِّي وَلِتُصۡنَعَ عَلَىٰ عَيۡنِيٓ

Ya kuwa mtie katika kisanduku, na kisha kitie mtoni, na mto utamfikisha ufukweni. Atamchukua adui yangu naye ni adui yake. Na nimekutilia mapenzi yanayotoka kwangu, na ili ulelewe machoni mwangu



Capítulo: TWAHA 

Verso : 40

إِذۡ تَمۡشِيٓ أُخۡتُكَ فَتَقُولُ هَلۡ أَدُلُّكُمۡ عَلَىٰ مَن يَكۡفُلُهُۥۖ فَرَجَعۡنَٰكَ إِلَىٰٓ أُمِّكَ كَيۡ تَقَرَّ عَيۡنُهَا وَلَا تَحۡزَنَۚ وَقَتَلۡتَ نَفۡسٗا فَنَجَّيۡنَٰكَ مِنَ ٱلۡغَمِّ وَفَتَنَّـٰكَ فُتُونٗاۚ فَلَبِثۡتَ سِنِينَ فِيٓ أَهۡلِ مَدۡيَنَ ثُمَّ جِئۡتَ عَلَىٰ قَدَرٖ يَٰمُوسَىٰ

Dada yako alipo kwenda na akasema: Je! Nikujuulisheni mtu wa kuweza kumlea? Basi tukakurejesha kwa mama yako ili macho yake yaburudike, wala asihuzunike. Na ulimuuwa mtu, nasi tukakuokoa katika dhiki, na tukakujaribu kwa majaribio mengi. Ukakaa miaka kwa watu wa Madiyana. Kisha ukaja kama ilivyo kadiriwa, ewe Mussa!



Capítulo: TWAHA 

Verso : 41

وَٱصۡطَنَعۡتُكَ لِنَفۡسِي

Na nimekuteuwa kwa ajili ya nafsi yangu



Capítulo: TWAHA 

Verso : 42

ٱذۡهَبۡ أَنتَ وَأَخُوكَ بِـَٔايَٰتِي وَلَا تَنِيَا فِي ذِكۡرِي

Nenda, wewe na ndugu yako, pamoja na ishara zangu, wala msichoke kunikumbuka



Capítulo: TWAHA 

Verso : 43

ٱذۡهَبَآ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Nendeni kwa Firauni. Hakika yeye amepindukia mipaka



Capítulo: TWAHA 

Verso : 44

فَقُولَا لَهُۥ قَوۡلٗا لَّيِّنٗا لَّعَلَّهُۥ يَتَذَكَّرُ أَوۡ يَخۡشَىٰ

Mwambieni maneno laini, huenda akazingatia au akaogopa



Capítulo: TWAHA 

Verso : 45

قَالَا رَبَّنَآ إِنَّنَا نَخَافُ أَن يَفۡرُطَ عَلَيۡنَآ أَوۡ أَن يَطۡغَىٰ

Wakasema: Ewe Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tunaogopa asije akapindukia mipaka juu yetu au kufanya jeuri



Capítulo: TWAHA 

Verso : 46

قَالَ لَا تَخَافَآۖ إِنَّنِي مَعَكُمَآ أَسۡمَعُ وَأَرَىٰ

Akasema: Msiogope! Hakika Mimi nipo pamoja nanyi. Nasikia na ninaona