Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 17

تَدۡعُواْ مَنۡ أَدۡبَرَ وَتَوَلَّىٰ

Unamwita yule aliyegeuza mgongo (aliyepuuza muongozo wa Allah) na akakengeuka



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 18

وَجَمَعَ فَأَوۡعَىٰٓ

Na akakusanya (mali) kisha akayahifadhi (katika makasha)



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 19

۞إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ خُلِقَ هَلُوعًا

Hakika, mwanadamu ameumbwa akiwa mwenye pupa (mwenye kukosa subira)



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 20

إِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ جَزُوعٗا

Inapomgusa shari anakuwa mwingi wa kupapatika (kulalamika na kuhuzunika)



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 21

وَإِذَا مَسَّهُ ٱلۡخَيۡرُ مَنُوعًا

Na inapomgusa kheri (anakuwa) mwingi wa kuzuia (bahili)



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 22

إِلَّا ٱلۡمُصَلِّينَ

Isipokuwa wenye kuswali



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 23

ٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ دَآئِمُونَ

Ambao wenye kudumisha Sala zao



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 24

وَٱلَّذِينَ فِيٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ حَقّٞ مَّعۡلُومٞ

Na wale ambao katika Mali zao kuna haki maalumu



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 25

لِّلسَّآئِلِ وَٱلۡمَحۡرُومِ

Kwa (Masikini) mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 26

وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na ambao wanasadikisha Siku ya Malipo, (siku ya Kiyama)



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 27

وَٱلَّذِينَ هُم مِّنۡ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشۡفِقُونَ

Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 28

إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمۡ غَيۡرُ مَأۡمُونٖ

Hakika adhabu ya Mola wao si ya kusalimika nayo



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 29

وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَٰفِظُونَ

Na ambao wanahifadhi tupu zao



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 30

إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٰجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُمۡ فَإِنَّهُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ

Isipokuwa kwa wake zao, au wale iliyowamiliki mikono yao ya kuume, basi hao si wenye kulaumiwa



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 31

فَمَنِ ٱبۡتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡعَادُونَ

Basi yeyote yule atakayetaka kinyume ya hayo, basi hao ndio warukao mipaka



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 32

وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِأَمَٰنَٰتِهِمۡ وَعَهۡدِهِمۡ رَٰعُونَ

Na ambao amana zao na ahadi zao ni wenye kuzichunga (na kuzitimiza)



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 33

وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَٰدَٰتِهِمۡ قَآئِمُونَ

Na ambao wanasimama imara katika kutoa ushahidi wao,



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 34

وَٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ يُحَافِظُونَ

Na ambao kwenye Sala zao ni wenye kuzilinda



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 35

أُوْلَـٰٓئِكَ فِي جَنَّـٰتٖ مُّكۡرَمُونَ

Hao ndio watakao heshimiwa Peponi



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 36

فَمَالِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ قِبَلَكَ مُهۡطِعِينَ

Wana nini wale walio kufuru (wanaharakiza mbele yako) na wanakutumbulia macho tu?



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 37

عَنِ ٱلۡيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ عِزِينَ

(Kukukalia) makundi kwa makundi kuliani na kushotoni.[1]


1- - Kitu gani kinawapelekea hao walio kufuru kukujia mbio mbio kutoka kuliani na kushotoni kwa makundi?.


Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 38

أَيَطۡمَعُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُدۡخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٖ

Je, kwani kila mmoja wao ana tamaa ya kuingia kwenye Pepo yenye neema?



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 39

كَلَّآۖ إِنَّا خَلَقۡنَٰهُم مِّمَّا يَعۡلَمُونَ

Sivyo hivyo! Hakika Sisi Tumewaumba kutokana na kile wanachokijua.[1]


1- - Basi nawaache hiyo tamaa yao ya kuingia Peponi. Hakika Sisi tumewaumba wao kutokana na maji ya kudharauliwa (dhalili).


Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 40

فَلَآ أُقۡسِمُ بِرَبِّ ٱلۡمَشَٰرِقِ وَٱلۡمَغَٰرِبِ إِنَّا لَقَٰدِرُونَ

Basi Naapa kwa Mola wa Mashariki zote na Magharibi zote, hakika Sisi bila shaka ni Wenye kuweza



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 41

عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ خَيۡرٗا مِّنۡهُمۡ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ

(Tuna uwezo wa) Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 42

فَذَرۡهُمۡ يَخُوضُواْ وَيَلۡعَبُواْ حَتَّىٰ يُلَٰقُواْ يَوۡمَهُمُ ٱلَّذِي يُوعَدُونَ

Basi waachilie mbali watumbukie katika porojo na upuuzi, na wacheze, mpaka wakutane na Siku yao ambayo wanayo ahidiwa



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 43

يَوۡمَ يَخۡرُجُونَ مِنَ ٱلۡأَجۡدَاثِ سِرَاعٗا كَأَنَّهُمۡ إِلَىٰ نُصُبٖ يُوفِضُونَ

Siku watapotoka makaburini haraka haraka kana kwamba wanakimbilia kushindana kuifikia kwenye Lengo



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 44

خَٰشِعَةً أَبۡصَٰرُهُمۡ تَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۚ ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمُ ٱلَّذِي كَانُواْ يُوعَدُونَ

Macho yao yatainama chini, udhalili utawafunika. Hiyo ndio ile siku waliyokuwa wakiahidiwa



Capítulo: NUUH 

Verso : 1

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوۡمِهِۦٓ أَنۡ أَنذِرۡ قَوۡمَكَ مِن قَبۡلِ أَن يَأۡتِيَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Hakika, Sisi Tulimtuma Nuhu kwa watu wake (tukamwambia) kwamba: Waonye watu wako kabla haijawafikia adhabu iumizayo sana



Capítulo: NUUH 

Verso : 2

قَالَ يَٰقَوۡمِ إِنِّي لَكُمۡ نَذِيرٞ مُّبِينٌ

(Nuhu) Akasema: Enyi watu wangu, hakika mimi kwenu ni muonyaji wa dhahiri (wa wazi) kwenu