Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 32

ٱلَّذِينَ يَجۡتَنِبُونَ كَبَـٰٓئِرَ ٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡفَوَٰحِشَ إِلَّا ٱللَّمَمَۚ إِنَّ رَبَّكَ وَٰسِعُ ٱلۡمَغۡفِرَةِۚ هُوَ أَعۡلَمُ بِكُمۡ إِذۡ أَنشَأَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِ وَإِذۡ أَنتُمۡ أَجِنَّةٞ فِي بُطُونِ أُمَّهَٰتِكُمۡۖ فَلَا تُزَكُّوٓاْ أَنفُسَكُمۡۖ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱتَّقَىٰٓ

Wale wanaojiepusha na madhambi makubwa na machafu isipokuwa makosa madogo-madogo. Hakika Bwana wako ni Mwingi wa msamaha. Yeye Anakujueni vyema, tangu Alipokuanzisheni kutoka katika ardhi, na pale mlipokuwa mimba changa matumboni mwa mama zenu. Basi msizitakase nafsi zenu. Yeye Anamjua zaidi aliyekuwa na taqwa



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 14

خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِن صَلۡصَٰلٖ كَٱلۡفَخَّارِ

Amemuumba mwanadamu kutokana na udongo utowao sauti kama vyombo vya udongo vilivyochomwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 57

نَحۡنُ خَلَقۡنَٰكُمۡ فَلَوۡلَا تُصَدِّقُونَ

Sisi Tumekuumbeni, basi kwa nini hamsadikishi hilo?



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 58

أَفَرَءَيۡتُم مَّا تُمۡنُونَ

Je, mnaona mbegu ya uzazi mnayo imwagia kwa nguvu?



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 59

ءَأَنتُمۡ تَخۡلُقُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡخَٰلِقُونَ

Je, nyinyi ndio mnaiumba au sisi ndio Waumbaji?



Capítulo: NUUH 

Verso : 17

وَٱللَّهُ أَنۢبَتَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِ نَبَاتٗا

Na Allah amekuotesheni (Amekuanzisheni vizuri katika udongo) wa ardhi kama mimea



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 37

أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ

Kwani yeye hakuwa tone la manii lililotonwa?



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 38

ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ

Kisha akawa pande la damu, (Allaah) Akamuumba na Akamsawazisha?



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 39

فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ

Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 1

هَلۡ أَتَىٰ عَلَى ٱلۡإِنسَٰنِ حِينٞ مِّنَ ٱلدَّهۡرِ لَمۡ يَكُن شَيۡـٔٗا مَّذۡكُورًا

Hakika, kilimpitia binaadamu kipindi katika zama kipindi (ambacho) hakuwa kitu kinachotajwa



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 2

إِنَّا خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ مِن نُّطۡفَةٍ أَمۡشَاجٖ نَّبۡتَلِيهِ فَجَعَلۡنَٰهُ سَمِيعَۢا بَصِيرًا

Hakika, sisi tumemuumba mwanadamu kutokana na mbegu ya uhai (Manii) iliyochanganyika ili tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tumemfanya ni mwenye kusikia, mwenye kuona



Capítulo: ALMURSALAAT 

Verso : 20

أَلَمۡ نَخۡلُقكُّم مِّن مَّآءٖ مَّهِينٖ

Kwani hatukukuumbeni kwa maji dhalili (manii)?



Capítulo: ALMURSALAAT 

Verso : 21

فَجَعَلۡنَٰهُ فِي قَرَارٖ مَّكِينٍ

Kisha Tukayaweka katika mahali pa kutulia, madhubuti?



Capítulo: ALMURSALAAT 

Verso : 22

إِلَىٰ قَدَرٖ مَّعۡلُومٖ

Mpaka muda maalumu?



Capítulo: ALMURSALAAT 

Verso : 23

فَقَدَرۡنَا فَنِعۡمَ ٱلۡقَٰدِرُونَ

Tukakadiria na Sisi ni wazuri walioje wa kukadiria



Capítulo: A’BASA

Verso : 18

مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ

Hivi hakumbuki! Kwa kitu gani amemuumba?



Capítulo: A’BASA

Verso : 19

مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ

Kutokana na tone la manii, Amemuumba, Akamkadiria, [Akamuwezesha]



Capítulo: ATTAARIQ 

Verso : 5

فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ

Hebu na ajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?



Capítulo: ATTAARIQ 

Verso : 6

خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ

Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,



Capítulo: ATTAARIQ 

Verso : 7

يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ

Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu



Capítulo: AL-A’LAQ 

Verso : 2

خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِنۡ عَلَقٍ

Amemuumba binaadamu kwa tone la damu