Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 221

وَلَا تَنكِحُواْ ٱلۡمُشۡرِكَٰتِ حَتَّىٰ يُؤۡمِنَّۚ وَلَأَمَةٞ مُّؤۡمِنَةٌ خَيۡرٞ مِّن مُّشۡرِكَةٖ وَلَوۡ أَعۡجَبَتۡكُمۡۗ وَلَا تُنكِحُواْ ٱلۡمُشۡرِكِينَ حَتَّىٰ يُؤۡمِنُواْۚ وَلَعَبۡدٞ مُّؤۡمِنٌ خَيۡرٞ مِّن مُّشۡرِكٖ وَلَوۡ أَعۡجَبَكُمۡۗ أُوْلَـٰٓئِكَ يَدۡعُونَ إِلَى ٱلنَّارِۖ وَٱللَّهُ يَدۡعُوٓاْ إِلَى ٱلۡجَنَّةِ وَٱلۡمَغۡفِرَةِ بِإِذۡنِهِۦۖ وَيُبَيِّنُ ءَايَٰتِهِۦ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمۡ يَتَذَكَّرُونَ

Na msiwaoe wanawake washi-rikina mpaka waamini. Na kwa hakika kabisa, kijakazi Muumini ni bora kuliko mshirikina, hata kama atakupendezeni. Na msiwaozeshe wanaume washirikina (makafiri) mpaka waamini. Na kwa hakika kabisa, mtumwa Muumini ni bora kuliko mshirikina hata kama atakupendezeni. Hao (Washirikina) wanahubiri kwenda motoni, na Allah anahubiri kwenda peponi na kwenye msamaha kwa idhini yake, na anazibainisha Aya zake kwa watu ili wapate kukumbuka



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 230

فَإِن طَلَّقَهَا فَلَا تَحِلُّ لَهُۥ مِنۢ بَعۡدُ حَتَّىٰ تَنكِحَ زَوۡجًا غَيۡرَهُۥۗ فَإِن طَلَّقَهَا فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡهِمَآ أَن يَتَرَاجَعَآ إِن ظَنَّآ أَن يُقِيمَا حُدُودَ ٱللَّهِۗ وَتِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِ يُبَيِّنُهَا لِقَوۡمٖ يَعۡلَمُونَ

Na kama (mume) akimpa (mkewe) Talaka (ya tatu) basi si halali kwake (kumrejea au kumuoa upya) baada ya hapo mpaka afunge ndoa na mume mwingine. Na kama akimuacha (huyo mume wa pili) basi si vibaya kurejeana (kwa kufunga ndoa upya) kama wataona wanaweza kusimamisha mipaka ya Allah. Na hiyo ni mipaka ya Allah anayoibainisha kwa watu wanaojua



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 232

وَإِذَا طَلَّقۡتُمُ ٱلنِّسَآءَ فَبَلَغۡنَ أَجَلَهُنَّ فَلَا تَعۡضُلُوهُنَّ أَن يَنكِحۡنَ أَزۡوَٰجَهُنَّ إِذَا تَرَٰضَوۡاْ بَيۡنَهُم بِٱلۡمَعۡرُوفِۗ ذَٰلِكَ يُوعَظُ بِهِۦ مَن كَانَ مِنكُمۡ يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِۗ ذَٰلِكُمۡ أَزۡكَىٰ لَكُمۡ وَأَطۡهَرُۚ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ وَأَنتُمۡ لَا تَعۡلَمُونَ

Na mnapowaacha wake na wakamaliza Eda zao, basi nyinyi mawalii msiwazuie kufunga ndoa na waume zao waliowaacha iwapo wataridhiana kwa wema. Anapewa onyo hilo yule anayemuamini Allah miongoni mwenu na Siku ya Mwisho. Hayo kwenu ni bora mno na nisafi kabisa. Na Allah anajua ilihali nyinyi hamjui



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 235

وَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ فِيمَا عَرَّضۡتُم بِهِۦ مِنۡ خِطۡبَةِ ٱلنِّسَآءِ أَوۡ أَكۡنَنتُمۡ فِيٓ أَنفُسِكُمۡۚ عَلِمَ ٱللَّهُ أَنَّكُمۡ سَتَذۡكُرُونَهُنَّ وَلَٰكِن لَّا تُوَاعِدُوهُنَّ سِرًّا إِلَّآ أَن تَقُولُواْ قَوۡلٗا مَّعۡرُوفٗاۚ وَلَا تَعۡزِمُواْ عُقۡدَةَ ٱلنِّكَاحِ حَتَّىٰ يَبۡلُغَ ٱلۡكِتَٰبُ أَجَلَهُۥۚ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا فِيٓ أَنفُسِكُمۡ فَٱحۡذَرُوهُۚ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ غَفُورٌ حَلِيمٞ

Na si vibaya kwenu posa za fumbo mlizowafumbia au mlicho-kificha kwenye nafsi zenu. Allah amejua kuwa nyinyi mtawakumbuka hao, Na lakini msiwaahidi (ndoa) kwa siri isipokuwa mseme maneno mema. Na msiazimie kufunga nao ndoa mpaka Eda ifike mwisho wake. Na jueni kwamba Allah anajua yaliyomo katika nafsi zenu, basi jihadharini naye, najueni kwamba Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mpole mno



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 3

وَإِنۡ خِفۡتُمۡ أَلَّا تُقۡسِطُواْ فِي ٱلۡيَتَٰمَىٰ فَٱنكِحُواْ مَا طَابَ لَكُم مِّنَ ٱلنِّسَآءِ مَثۡنَىٰ وَثُلَٰثَ وَرُبَٰعَۖ فَإِنۡ خِفۡتُمۡ أَلَّا تَعۡدِلُواْ فَوَٰحِدَةً أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُكُمۡۚ ذَٰلِكَ أَدۡنَىٰٓ أَلَّا تَعُولُواْ

Na kama mtaogopa kutofanya uadilifu kwa Yatima, basi oeni wale mliowaridhia miongoni mwa wanawake, wawili wawili na watatu watatu na wane wane. Na kama mtahofia kutofanya uadilifu, basi oeni mmoja tu au (oeni vijakazi) mnaowamiliki. Kufanya hivyo kutawasogeza karibu zaidi ya kuacha dhuluma



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 4

وَءَاتُواْ ٱلنِّسَآءَ صَدُقَٰتِهِنَّ نِحۡلَةٗۚ فَإِن طِبۡنَ لَكُمۡ عَن شَيۡءٖ مِّنۡهُ نَفۡسٗا فَكُلُوهُ هَنِيٓـٔٗا مَّرِيٓـٔٗا

Na wapeni wanawake (mnaowaoa) mahari yao ikiwa ni Hadiya (waliyopewa na Allah). Ikiwa wameridhia wenyewe kuwapa chochote katika mahari hiyo, basi kuleni, kwani hicho ni halali iliyo nzuri



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 19

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا يَحِلُّ لَكُمۡ أَن تَرِثُواْ ٱلنِّسَآءَ كَرۡهٗاۖ وَلَا تَعۡضُلُوهُنَّ لِتَذۡهَبُواْ بِبَعۡضِ مَآ ءَاتَيۡتُمُوهُنَّ إِلَّآ أَن يَأۡتِينَ بِفَٰحِشَةٖ مُّبَيِّنَةٖۚ وَعَاشِرُوهُنَّ بِٱلۡمَعۡرُوفِۚ فَإِن كَرِهۡتُمُوهُنَّ فَعَسَىٰٓ أَن تَكۡرَهُواْ شَيۡـٔٗا وَيَجۡعَلَ ٱللَّهُ فِيهِ خَيۡرٗا كَثِيرٗا

Enyi mlioamini haifai kwenu kumrithi mke bila ridhaa yake[1] na msiwazuie kuolewa (sehemu nyingine) ili wasiondoke na mali mliyowapa ispokuwa kama watafanya zinaa ya wazi na ishini nao kwa wema, na endapo hamtawapenda basi (eleweni kuwa) huenda mkachukia kitu na Allah akajaalia kitu hicho kuwa na kheri nyingi


1- - Kwa kumuoa ndoa mpya na mahari mapya kinyume na ndoa ya mumewe aliyekufa. Wakati wa jahilia wanawake walilirithiwa kama zinavyorithia mali na vitu. mtu alipokufa kaka ama mtoto wa marehemu waliwafanya wake wa marehemu kuwa wake zao bila kuwaoa ndoa mpya au wao ndio waliwaozesha sehemu nyingine kwa kuchukua mahari au waliwazuia kuondoka hata kama hawakuwapenda kuishi nao kama mke ili wasiondoke na mali walizopata wakiwa kwao.


Capítulo: ANNISAI 

Verso : 20

وَإِنۡ أَرَدتُّمُ ٱسۡتِبۡدَالَ زَوۡجٖ مَّكَانَ زَوۡجٖ وَءَاتَيۡتُمۡ إِحۡدَىٰهُنَّ قِنطَارٗا فَلَا تَأۡخُذُواْ مِنۡهُ شَيۡـًٔاۚ أَتَأۡخُذُونَهُۥ بُهۡتَٰنٗا وَإِثۡمٗا مُّبِينٗا

Na endapo mtataka kubadili mke sehemu ya mke aliyepo na mmoja wao mkampa mali nyingi basi msichukuwe katika mali hiyo chochote. mnakichukuaje kwa uongo na dhambi za wazi



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 21

وَكَيۡفَ تَأۡخُذُونَهُۥ وَقَدۡ أَفۡضَىٰ بَعۡضُكُمۡ إِلَىٰ بَعۡضٖ وَأَخَذۡنَ مِنكُم مِّيثَٰقًا غَلِيظٗا

Na mnazichukuaje ilhali mmekwisha ingiliana nyinyi kwa nyinyi, na (wake) wamechukuwa kwenu ahadi nzito (ya kuishi kwa wema)



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 22

وَلَا تَنكِحُواْ مَا نَكَحَ ءَابَآؤُكُم مِّنَ ٱلنِّسَآءِ إِلَّا مَا قَدۡ سَلَفَۚ إِنَّهُۥ كَانَ فَٰحِشَةٗ وَمَقۡتٗا وَسَآءَ سَبِيلًا

Na msiwaoe wale walio olewa na baba zenu ispokuwa yaliyopita, tendo hilo ni baya na bughdha na ni njia mbaya



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 23

حُرِّمَتۡ عَلَيۡكُمۡ أُمَّهَٰتُكُمۡ وَبَنَاتُكُمۡ وَأَخَوَٰتُكُمۡ وَعَمَّـٰتُكُمۡ وَخَٰلَٰتُكُمۡ وَبَنَاتُ ٱلۡأَخِ وَبَنَاتُ ٱلۡأُخۡتِ وَأُمَّهَٰتُكُمُ ٱلَّـٰتِيٓ أَرۡضَعۡنَكُمۡ وَأَخَوَٰتُكُم مِّنَ ٱلرَّضَٰعَةِ وَأُمَّهَٰتُ نِسَآئِكُمۡ وَرَبَـٰٓئِبُكُمُ ٱلَّـٰتِي فِي حُجُورِكُم مِّن نِّسَآئِكُمُ ٱلَّـٰتِي دَخَلۡتُم بِهِنَّ فَإِن لَّمۡ تَكُونُواْ دَخَلۡتُم بِهِنَّ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ وَحَلَـٰٓئِلُ أَبۡنَآئِكُمُ ٱلَّذِينَ مِنۡ أَصۡلَٰبِكُمۡ وَأَن تَجۡمَعُواْ بَيۡنَ ٱلۡأُخۡتَيۡنِ إِلَّا مَا قَدۡ سَلَفَۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ غَفُورٗا رَّحِيمٗا

Wameharamishwa kwenu mama zenu, na binti zenu na dada zenu na shangazi zenu, na ndugu wa mama zenu na watoto wa kaka zenu, na watoto wa dada zenu, na mama zenu ambao wamewanyonyesha na dada zenu wa kunyonya, na mama wa wake zenu, na watoto wa wake zenu ambao wapo majumbani mwenu wanaotokana na wake mlio waingilia, kama (wake hao) hamjawaingilia, basi sivibaya kwenu[1]. Na (ni haramu kwenu) wake wa watoto wenu wa kuwazaa na (ni haramu) kuwakusanya mtu na dada yake ispokua yale yaliyopita, hakika Allah ni mwenye kusamehe mpole mno


1- - Endapo mtawaacha hao kabla ya kuwaingilia mnaruhusiwa kuwaoa


Capítulo: ANNISAI 

Verso : 24

۞وَٱلۡمُحۡصَنَٰتُ مِنَ ٱلنِّسَآءِ إِلَّا مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُكُمۡۖ كِتَٰبَ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡۚ وَأُحِلَّ لَكُم مَّا وَرَآءَ ذَٰلِكُمۡ أَن تَبۡتَغُواْ بِأَمۡوَٰلِكُم مُّحۡصِنِينَ غَيۡرَ مُسَٰفِحِينَۚ فَمَا ٱسۡتَمۡتَعۡتُم بِهِۦ مِنۡهُنَّ فَـَٔاتُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ فَرِيضَةٗۚ وَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ فِيمَا تَرَٰضَيۡتُم بِهِۦ مِنۢ بَعۡدِ ٱلۡفَرِيضَةِۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمٗا

Na (ni haramu kwenu) wanawake walio katika ndoa isipokuwa wale mliowamiliki kwa mikono yenu ya kuume[1], (hili) Allah ameandika kwenu, na mmehalalishiwa (wanawake) wasiokuwa hawa mtake kwa mali zenu, kujilinda na kutofanya zinaa. Na wale (wake) mliokaa nao faragha (baada ya ndoa) kati ya hao, wapeni mahari yao ni lazima. Na si vibaya kwenu kwa mliyoridhiana katika yale yaliyotajwa[2]baada ya kutimiza wajibu, hakika Allah ni mjuzi mwenye hekima


1- - Ni haramu kumuoa mwanamke aliye katika ndoa isipokuwa kafiri endapo atatekwa katika vita ya jihadi ni halali baada ya kukaa wa kusubiria hali ya tumbo lake kuwa si mja mzito


2- - Amesema shekhe Siidy alipotafsiri aya hii wanazuoni waliyo wengi wamesema kuwa; Mwanamke kupunguza sehemu ya waliokubaliana au mwanaume kutoa zaidi ya walichoafikiana


Capítulo: ANNISAI 

Verso : 25

وَمَن لَّمۡ يَسۡتَطِعۡ مِنكُمۡ طَوۡلًا أَن يَنكِحَ ٱلۡمُحۡصَنَٰتِ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ فَمِن مَّا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُكُم مِّن فَتَيَٰتِكُمُ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتِۚ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِإِيمَٰنِكُمۚ بَعۡضُكُم مِّنۢ بَعۡضٖۚ فَٱنكِحُوهُنَّ بِإِذۡنِ أَهۡلِهِنَّ وَءَاتُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ بِٱلۡمَعۡرُوفِ مُحۡصَنَٰتٍ غَيۡرَ مُسَٰفِحَٰتٖ وَلَا مُتَّخِذَٰتِ أَخۡدَانٖۚ فَإِذَآ أُحۡصِنَّ فَإِنۡ أَتَيۡنَ بِفَٰحِشَةٖ فَعَلَيۡهِنَّ نِصۡفُ مَا عَلَى ٱلۡمُحۡصَنَٰتِ مِنَ ٱلۡعَذَابِۚ ذَٰلِكَ لِمَنۡ خَشِيَ ٱلۡعَنَتَ مِنكُمۡۚ وَأَن تَصۡبِرُواْ خَيۡرٞ لَّكُمۡۗ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Na asiyekuwa na uwezo wa kutosha miongoni mwenu (wa) kuoa wanawake waumini wenye kujihifadhi (waungwana), basi (oeni) wasichana (vijakazi)[1] wenu waumini mnaowamiliki. Na Allah anaijua sana imani yenu; nyinyi kwa nyinyi. Basi waoeni kwa idhini ya familia zao (zenye mamlaka ya kisheria ya kuwaozesha) na wapeni malipo (mahari) yao kwa wema wakiwa na lengo la kujihifadhi, wasio na lengo la kufanya uchafu (wa zinaa) wala kutengeneza wapenzi kinyume na sheria (mahawara). Basi wakishaingia katika hifadhi (ya ndoa), kama wakifanya uchafu (wa zinaa), basi adhabu yao ni nusu ya adhabu ya wanawake waungwana. Hayo ni kwa yule anayeogopa Zinaa miongoni mwenu. Na kama mtavumilia ni bora zaidi kwenu. Na Allah ni Mwingi wa kusamehe, mwenye huruma


1- - Kijakazi ni mtumwa wa kike. Mtumishi wa ndani wa kike nje ya utumwa hazingatiwi kuwa ni kijakazi.


Capítulo: ANNISAI 

Verso : 34

ٱلرِّجَالُ قَوَّـٰمُونَ عَلَى ٱلنِّسَآءِ بِمَا فَضَّلَ ٱللَّهُ بَعۡضَهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ وَبِمَآ أَنفَقُواْ مِنۡ أَمۡوَٰلِهِمۡۚ فَٱلصَّـٰلِحَٰتُ قَٰنِتَٰتٌ حَٰفِظَٰتٞ لِّلۡغَيۡبِ بِمَا حَفِظَ ٱللَّهُۚ وَٱلَّـٰتِي تَخَافُونَ نُشُوزَهُنَّ فَعِظُوهُنَّ وَٱهۡجُرُوهُنَّ فِي ٱلۡمَضَاجِعِ وَٱضۡرِبُوهُنَّۖ فَإِنۡ أَطَعۡنَكُمۡ فَلَا تَبۡغُواْ عَلَيۡهِنَّ سَبِيلًاۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلِيّٗا كَبِيرٗا

Wanaume ni wasimamizi wakuu wa wanawake; kwasababu ya vile Allah alivyowazidishia baadhi yao kwa wengine, na kwa sababu ya mali zao walizozitoa (mahari, makazi, mavazi, chakula na matumizi yote ya msingi kwa jumla). Basi wanawake wema ni wale wenye kutii, na wanaojihifadhi hata katika siri kwasababu Allah ameamrisha wajihifadhi. Na wale mnaochelea uasi wao, basi waonyeni na wahameni vitandani na wapigeni.[1] Na kama watakutiini msiwatafutie njia (sababu ya kuwaadhibu na kuwaonea). Hakika Allah ndiye aliye juu na Mkuu


1- - Hizi ni hatua za kumuadabisha mke aliye asi: (a) Kumnasihi (b) Kumuhama kitandani (c) Kumpiga pigo lisilodhuru.


Capítulo: ANNISAI 

Verso : 35

وَإِنۡ خِفۡتُمۡ شِقَاقَ بَيۡنِهِمَا فَٱبۡعَثُواْ حَكَمٗا مِّنۡ أَهۡلِهِۦ وَحَكَمٗا مِّنۡ أَهۡلِهَآ إِن يُرِيدَآ إِصۡلَٰحٗا يُوَفِّقِ ٱللَّهُ بَيۡنَهُمَآۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلِيمًا خَبِيرٗا

Na kama mkihofia ugomvi baina yao (mke na mume), basi tumenimuamuzi mmoja kutoka familia ya mume na muamuzi mmoja kutoka familia ya mke. Kama (wasuluhishi hao) watakusudia kusuluhisha, Allah atawapa Taufiki (Mwafaka). Hakika, Allah ni Mjuzi, Mwenye habari nyingi (za yanayojiri)



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 127

وَيَسۡتَفۡتُونَكَ فِي ٱلنِّسَآءِۖ قُلِ ٱللَّهُ يُفۡتِيكُمۡ فِيهِنَّ وَمَا يُتۡلَىٰ عَلَيۡكُمۡ فِي ٱلۡكِتَٰبِ فِي يَتَٰمَى ٱلنِّسَآءِ ٱلَّـٰتِي لَا تُؤۡتُونَهُنَّ مَا كُتِبَ لَهُنَّ وَتَرۡغَبُونَ أَن تَنكِحُوهُنَّ وَٱلۡمُسۡتَضۡعَفِينَ مِنَ ٱلۡوِلۡدَٰنِ وَأَن تَقُومُواْ لِلۡيَتَٰمَىٰ بِٱلۡقِسۡطِۚ وَمَا تَفۡعَلُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِهِۦ عَلِيمٗا

Na wanakuuliza Fat’wa[1] kuhusu wanawake. Sema: Allah anakupeni Fat`wa kuhusu wao na (kuhusu) yale yanayosomwa kwenu katika kitabu (hiki) kuhusu Yatima wanawake ambao hamuwapi kile kilicho wajibu kupewa na mnatamani kuwaoa, na (Fat’wa kuhusu) wale wanyonge miongoni mwa watoto na kwamba muwasimamie Yatima kwa uadilifu. Na kheri yoyote mnayoifanya basi hakika Allah anaijua sana


1- - Fat’wa katika Uislamu ni kutoa maelezo ya hukumu ya sheria, kwa maana ya kufafanua na sio kulazimisha. Anayefanya hivi anaitwa Mufti. Kadhi na Mufti wanatofautiana kwamba kazi ya Kadhi ni kutoa hukumu na kulazimisha utekelezwaji wa hukumu hiyo wakati kauli ya Mufti na ufafanuzi wa hukumu yake sio lazima kutekelezwa. Rejea kitabu cha Al-Ahkaamus Sultwaaniyyah cha Imamu Almaawardi, Allah amrehemu.


Capítulo: ANNISAI 

Verso : 128

وَإِنِ ٱمۡرَأَةٌ خَافَتۡ مِنۢ بَعۡلِهَا نُشُوزًا أَوۡ إِعۡرَاضٗا فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡهِمَآ أَن يُصۡلِحَا بَيۡنَهُمَا صُلۡحٗاۚ وَٱلصُّلۡحُ خَيۡرٞۗ وَأُحۡضِرَتِ ٱلۡأَنفُسُ ٱلشُّحَّۚ وَإِن تُحۡسِنُواْ وَتَتَّقُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٗا

Na iwapo mwanamke (mke) yeyote atachelea uasi kwa mumewe au kutojaliwa (kupuuzwa na kutelekezwa) basi si vibaya kwao kufanya suluhu baina yao, na suluhu ni jambo la kheri sana. Na nafsi zimehudhurishiwa (zimesogezewa) ubahili[1]. Na iwapo mtafanya mazuri na mkamcha Allah, basi hakika Allah anayajua vyema yote mnayoyafanya


1- - Hapa Aya inaelezea uhalisia wa nafsi ya mwanadamu wakati wa ugonvi na mivutano ambapo kila upande unakuwa na umimi, kujipendelea, kukataa kujishusha na kuwa na ugumu na uzito wa kukubali kosa, kujirudi au kusamehe haki ili kufikia suluhu na muafaka.


Capítulo: ANNISAI 

Verso : 129

وَلَن تَسۡتَطِيعُوٓاْ أَن تَعۡدِلُواْ بَيۡنَ ٱلنِّسَآءِ وَلَوۡ حَرَصۡتُمۡۖ فَلَا تَمِيلُواْ كُلَّ ٱلۡمَيۡلِ فَتَذَرُوهَا كَٱلۡمُعَلَّقَةِۚ وَإِن تُصۡلِحُواْ وَتَتَّقُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ غَفُورٗا رَّحِيمٗا

Na hamtaweza kufanya uadilifu baina ya wanawake (wake zenu) hata kama mtafanya jitihada. Basi (pamoja na hayo) msimili (msielemee) moja kwa moja (kwa mke mmoja), mkamuacha mwingine kama aliyetundikwa (aliyening’inizwa).[1] Na kama mtafanya usuluhishi na mkamcha Allah, hakika Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehem


1- - Waume wanakatazwa kutofanya uadilifu baina ya wake zao kwa kutotoa huduma stahiki kwa usawa au kwa kutelekeza baadhi. Hili halihusu mume mwenye wake zaidi ya mmoja tu, lakini linamhusu hata mume mwenye mke mmoja. Mume mwenye mke mmoja pia haruhusiwi kutomtendea uadilifu mkewe kwa kutompa haki zake au kwa kumtelekeza na kumuweka katika mazingira ya kutojitambua kwamba ni mke au sio mke. Uadilifu unaokusudia na sheria ni uadilifu wa huduma na sio hisia za mvuto, mahaba na mapenzi ya moyoni.


Capítulo: ANNISAI 

Verso : 130

وَإِن يَتَفَرَّقَا يُغۡنِ ٱللَّهُ كُلّٗا مِّن سَعَتِهِۦۚ وَكَانَ ٱللَّهُ وَٰسِعًا حَكِيمٗا

Na iwapo (mke na mume) watatengana (kwa kuachana baada ya suluhu kushindikana), Allah atamtosheleza kila mmoja kutoka katika wasaa (ukarimu) wake. Na Allah ni Mwingi wa wasaa, Mwingi wa hekima



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 5

وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَٰفِظُونَ

Na ambao wanazilinda tupu zao



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 6

إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٰجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُمۡ فَإِنَّهُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ

Isipokuwa kwa wake zao au kwa wale (wanawake) iliyowamiliki mikono yao ya kulia. Kwani hao si wenye kulaumiwa



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 7

فَمَنِ ٱبۡتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡعَادُونَ

Lakini anayetaka kinyume cha hayo, basi hao ndio warukao mipaka



Capítulo: ANNUUR 

Verso : 3

ٱلزَّانِي لَا يَنكِحُ إِلَّا زَانِيَةً أَوۡ مُشۡرِكَةٗ وَٱلزَّانِيَةُ لَا يَنكِحُهَآ إِلَّا زَانٍ أَوۡ مُشۡرِكٞۚ وَحُرِّمَ ذَٰلِكَ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Mwanaume mzinifu hamwoi ila na mwanamke mzinifu au mshirikina. Na mwanamke mzinifuhaolewi ila na mwanaume mzinifu au mshirikina. Na hayo yameharamishwa kwa Waumini



Capítulo: ANNUUR 

Verso : 32

وَأَنكِحُواْ ٱلۡأَيَٰمَىٰ مِنكُمۡ وَٱلصَّـٰلِحِينَ مِنۡ عِبَادِكُمۡ وَإِمَآئِكُمۡۚ إِن يَكُونُواْ فُقَرَآءَ يُغۡنِهِمُ ٱللَّهُ مِن فَضۡلِهِۦۗ وَٱللَّهُ وَٰسِعٌ عَلِيمٞ

Na waozesheni wajane miongoni mwenu na wema katika watumwa wenu na wajakazi wenu. Wakiwa mafakiri Allah atawatajirisha kwa fadhila yake. Na Allah ni Mwenye wasaa Mwenye kujua



Capítulo: ANNUUR 

Verso : 33

وَلۡيَسۡتَعۡفِفِ ٱلَّذِينَ لَا يَجِدُونَ نِكَاحًا حَتَّىٰ يُغۡنِيَهُمُ ٱللَّهُ مِن فَضۡلِهِۦۗ وَٱلَّذِينَ يَبۡتَغُونَ ٱلۡكِتَٰبَ مِمَّا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُكُمۡ فَكَاتِبُوهُمۡ إِنۡ عَلِمۡتُمۡ فِيهِمۡ خَيۡرٗاۖ وَءَاتُوهُم مِّن مَّالِ ٱللَّهِ ٱلَّذِيٓ ءَاتَىٰكُمۡۚ وَلَا تُكۡرِهُواْ فَتَيَٰتِكُمۡ عَلَى ٱلۡبِغَآءِ إِنۡ أَرَدۡنَ تَحَصُّنٗا لِّتَبۡتَغُواْ عَرَضَ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۚ وَمَن يُكۡرِههُّنَّ فَإِنَّ ٱللَّهَ مِنۢ بَعۡدِ إِكۡرَٰهِهِنَّ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Na wajizuilie na machafu wale wasiopata cha kuolea, mpaka Allah awatajirishe kwa fadhila yake. Na wanao taka kuandikiwa uhuru katika wale ambao mikono yenu ya kulia imewamiliki, basi waandikieni kama mkiona wema kwao. Na wapeni katika mali ya Allah aliyo kupeni. Wala msiwashurutishe vijakazi wenu kufanya zina kwa ajili ya kutafuta pato la maisha ya dunia, ilhali wao wanataka kujiheshimu. Na atakaye walazimisha basi Allah baada ya kulazimishwa kwao huko, atawasamehe, kwani Allah ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu



Capítulo: ARRUUM 

Verso : 21

وَمِنۡ ءَايَٰتِهِۦٓ أَنۡ خَلَقَ لَكُم مِّنۡ أَنفُسِكُمۡ أَزۡوَٰجٗا لِّتَسۡكُنُوٓاْ إِلَيۡهَا وَجَعَلَ بَيۡنَكُم مَّوَدَّةٗ وَرَحۡمَةًۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّقَوۡمٖ يَتَفَكَّرُونَ

Na katika Ishara zake ni kuwa amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. Naye amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanao fikiri



Capítulo: AL-AHZAAB 

Verso : 37

وَإِذۡ تَقُولُ لِلَّذِيٓ أَنۡعَمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِ وَأَنۡعَمۡتَ عَلَيۡهِ أَمۡسِكۡ عَلَيۡكَ زَوۡجَكَ وَٱتَّقِ ٱللَّهَ وَتُخۡفِي فِي نَفۡسِكَ مَا ٱللَّهُ مُبۡدِيهِ وَتَخۡشَى ٱلنَّاسَ وَٱللَّهُ أَحَقُّ أَن تَخۡشَىٰهُۖ فَلَمَّا قَضَىٰ زَيۡدٞ مِّنۡهَا وَطَرٗا زَوَّجۡنَٰكَهَا لِكَيۡ لَا يَكُونَ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ حَرَجٞ فِيٓ أَزۡوَٰجِ أَدۡعِيَآئِهِمۡ إِذَا قَضَوۡاْ مِنۡهُنَّ وَطَرٗاۚ وَكَانَ أَمۡرُ ٱللَّهِ مَفۡعُولٗا

kumbuka pindi ulipo mwambia mtu ambae aliye neemeshwa na Allah neema ya uislam, nawe ukamneemesha kwa kumuacha huru kutokana na utumwa: mshikilie mke usimpe talaka, na mche Allah. Na ukaficha katika nafsi yako siri ya kumpenda mkeo ambayo hukupenda watu waijuwe lakini Allah aliifichua, Allah ndiye mwenye haki zaidi ya kuogopwa. Basi ilipo kwisha haja ya Zaidi kwa mkeo waakaachana, tulikuoza wewe, ili isiwe taabu kwa Waumini kuwaoa wake wa watoto wao wa kupanga[1] watapokuwa wamekwisha timiza nao shuruti za talaka. na amri ya Allah ni yenye kutekelezwa


1- - Watoto wa kupanga niwale ambao wamelelewa na wazazi ambao sio wazazi wao wa kuwazaa mpaka ikafikia mototo anamwita alie mlea Baba. Kwa mfano Swahaba Zaid bin Haarith alilelewa na mtume mpaka akawa anaitwa Zaid Bin Muhamad, zaidi alipo muacha mkeo Hindu Aliolewa na Mtume kuonyesha kuwa mke wa mototo wa kupanga akiachwa wewe babayake wa kupanga inajuzu kumuoa.


Capítulo: AL-AHZAAB 

Verso : 49

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا نَكَحۡتُمُ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ ثُمَّ طَلَّقۡتُمُوهُنَّ مِن قَبۡلِ أَن تَمَسُّوهُنَّ فَمَا لَكُمۡ عَلَيۡهِنَّ مِنۡ عِدَّةٖ تَعۡتَدُّونَهَاۖ فَمَتِّعُوهُنَّ وَسَرِّحُوهُنَّ سَرَاحٗا جَمِيلٗا

nyie mlioamini! Mkiwaoa wana-wake, Waumini, kisha mkawapa talaka kabla ya kuwagusa, basi hamna eda juu yao mtakayo ihesabu. Basi wapeni cha kuwaliwaza, na muwaache kwa wema



Capítulo: AL-AHZAAB 

Verso : 52

لَّا يَحِلُّ لَكَ ٱلنِّسَآءُ مِنۢ بَعۡدُ وَلَآ أَن تَبَدَّلَ بِهِنَّ مِنۡ أَزۡوَٰجٖ وَلَوۡ أَعۡجَبَكَ حُسۡنُهُنَّ إِلَّا مَا مَلَكَتۡ يَمِينُكَۗ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ رَّقِيبٗا

Baada ya hawa hawakuhalalikii wewe wanawake wengine, wala kuwabadilisha kwa wake wengine ingawa uzuri wao ukikupendeza; isipo kuwa yule uliye mmiliki kwa mkono wako wa kulia. Na Allah anachunga kila kitu



Capítulo: AL-MUMTAHINA 

Verso : 10

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا جَآءَكُمُ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتُ مُهَٰجِرَٰتٖ فَٱمۡتَحِنُوهُنَّۖ ٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِإِيمَٰنِهِنَّۖ فَإِنۡ عَلِمۡتُمُوهُنَّ مُؤۡمِنَٰتٖ فَلَا تَرۡجِعُوهُنَّ إِلَى ٱلۡكُفَّارِۖ لَا هُنَّ حِلّٞ لَّهُمۡ وَلَا هُمۡ يَحِلُّونَ لَهُنَّۖ وَءَاتُوهُم مَّآ أَنفَقُواْۚ وَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ أَن تَنكِحُوهُنَّ إِذَآ ءَاتَيۡتُمُوهُنَّ أُجُورَهُنَّۚ وَلَا تُمۡسِكُواْ بِعِصَمِ ٱلۡكَوَافِرِ وَسۡـَٔلُواْ مَآ أَنفَقۡتُمۡ وَلۡيَسۡـَٔلُواْ مَآ أَنفَقُواْۚ ذَٰلِكُمۡ حُكۡمُ ٱللَّهِ يَحۡكُمُ بَيۡنَكُمۡۖ وَٱللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٞ

Enyi walioamini! Wanapokujieni Waumini wa kike waliohajiri (waliohama) basi wajaribuni. Allah ndiye Mwenye kujua zaidi Imani yao. Kisha mkiwatambua kuwa ni Waumini basi msiwarejeshe kwa makafiri. Wao si wake halaal kwao, wala hao makafiri hawahalalikii wanawake Waumini. Na wapeni (makafiri mahari) waliyotoa. Na wala si dhambi kufunga nao ndoa mkiwapa mahari yao. Na wala msiwaweke wanawake makafiri katika fungamano la ndoa; na takeni mlichotoa (katika mahari), nao watake walichotoa. Hiyo ndio hukumu ya Allah, Ana hukumu baina yenu, na Allah ni Mwenye kujua, Mwenye hekima