Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 104

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَقُولُواْ رَٰعِنَا وَقُولُواْ ٱنظُرۡنَا وَٱسۡمَعُواْۗ وَلِلۡكَٰفِرِينَ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Enyi mlioamini! Msiseme: “Raainaa” na semeni “Undhurnaa”. Na sikieni. Na makafiri watapata adhabu iumizayo



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 31

قُلۡ إِن كُنتُمۡ تُحِبُّونَ ٱللَّهَ فَٱتَّبِعُونِي يُحۡبِبۡكُمُ ٱللَّهُ وَيَغۡفِرۡ لَكُمۡ ذُنُوبَكُمۡۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Allah, basi nifuateni, Allah atakupendeni na atakusameheni madhambi yenu. Na Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 32

قُلۡ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَۖ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Sema: Mtiini Allah na Mtume. Kama mkikengeuka, basi kwa hakika Allah hawapendi makafiri



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 132

وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ

Na mtiini Allah na Mtume ili mpate kupewa rehema



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 13

تِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِۚ وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ يُدۡخِلۡهُ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ وَذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Hiyo ndiyo mipaka ya Allah na yeyote mwenye kumtii Allah na Mtume wake atamuingiza katika Pepo itiririkayo mito chini yake, watabaki humo milele na huko ndiko kufaulu kuliko kukubwa



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 14

وَمَن يَعۡصِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَيَتَعَدَّ حُدُودَهُۥ يُدۡخِلۡهُ نَارًا خَٰلِدٗا فِيهَا وَلَهُۥ عَذَابٞ مُّهِينٞ

Na yeyote atakayemuasi Allah na Mtume wake na akakiuka mipaka yake atamuingiza katika Moto atabaki humo milele, na atakuwa na adhabu inayo dhalilisha



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 59

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَ وَأُوْلِي ٱلۡأَمۡرِ مِنكُمۡۖ فَإِن تَنَٰزَعۡتُمۡ فِي شَيۡءٖ فَرُدُّوهُ إِلَى ٱللَّهِ وَٱلرَّسُولِ إِن كُنتُمۡ تُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِۚ ذَٰلِكَ خَيۡرٞ وَأَحۡسَنُ تَأۡوِيلًا

Enyi mlioamini, mtiini Allah na mtiini Mtume, na wenye mamlaka katika nyinyi. Basi iwapo mtavutana[1] katika jambo lolote, lirudisheni kwa Allah na (kwa) Mtume, ikiwa mnamuamini Allah na Siku ya Mwisho. Hilo ni bora zaidi na ni mwisho mzuri sana


1- - Kuvutana ni kubishana kuhusu jambo fulani kati ya pande mbili au zaidi na kila upande huvutia kwake.


Capítulo: ANNISAI 

Verso : 64

وَمَآ أَرۡسَلۡنَا مِن رَّسُولٍ إِلَّا لِيُطَاعَ بِإِذۡنِ ٱللَّهِۚ وَلَوۡ أَنَّهُمۡ إِذ ظَّلَمُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ جَآءُوكَ فَٱسۡتَغۡفَرُواْ ٱللَّهَ وَٱسۡتَغۡفَرَ لَهُمُ ٱلرَّسُولُ لَوَجَدُواْ ٱللَّهَ تَوَّابٗا رَّحِيمٗا

Na hatukumtuma Mtume yeyote ila tu atiiwe kwa idhini ya Allah. Na lau kama walipozidhulumu nafsi zao (kwa kutenda dhambi) wangelikujia wakamuomba msamaha Allah, na Mtume (naye) akawaombea msamaha, kwa yakini kabisa, wangemkuta Allah ni Mwenye kupokea toba na Mwenye kurehemu



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 65

فَلَا وَرَبِّكَ لَا يُؤۡمِنُونَ حَتَّىٰ يُحَكِّمُوكَ فِيمَا شَجَرَ بَيۡنَهُمۡ ثُمَّ لَا يَجِدُواْ فِيٓ أَنفُسِهِمۡ حَرَجٗا مِّمَّا قَضَيۡتَ وَيُسَلِّمُواْ تَسۡلِيمٗا

Hapana; nina apa kwa Mola wako kwamba, (watu) hawawi waumini mpaka wakufanye wewe kuwa muamuzi katika migogoro inayotokea baina yao, kisha wasihisi uzito wowote (au mashaka) katika nafsi zao kutokana na hukumu uliyoitoa na waonyeshe utiifu kamili



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 69

وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ مَعَ ٱلَّذِينَ أَنۡعَمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ وَٱلصِّدِّيقِينَ وَٱلشُّهَدَآءِ وَٱلصَّـٰلِحِينَۚ وَحَسُنَ أُوْلَـٰٓئِكَ رَفِيقٗا

Na wenye kumtii Allah na Mtume, basi hao watakuwa pamoja na wale ambao Allah amewaneemesha ikiwa ni pamoja na Manabii na Wenye kusadikisha (Maswahaba) na Mashahidi na Watu Wema.[1] Na ni uzuri ulioje kuwa pamoja na watu hao!


1- - Aya hapa inawabainisha walioneemeshwa na ambao katika Aya ya 6 na ya 7 ya Sura Alfaatiha (1) Waislamu wametakiwa kuwaiga na kufuata njia, muongozo na sera zao. Swahaba, wakiongozwa na Abubakar, Umar, Uthman na Ali (Allah awawie radhi) wanahusika katika Aya hii kwa sababu kuna Hadithi kadhaa za Mtume (Allah amshushie rehema na amani, zinazowataja kuwa wamo Mashahidi na Wasadikishaji.


Capítulo: ANNISAI 

Verso : 80

مَّن يُطِعِ ٱلرَّسُولَ فَقَدۡ أَطَاعَ ٱللَّهَۖ وَمَن تَوَلَّىٰ فَمَآ أَرۡسَلۡنَٰكَ عَلَيۡهِمۡ حَفِيظٗا

Yeyote anayemtii Mtume basi hakika (atakuwa) amemtii Allah, na yeyote atakaye kengeuka basi (ni juu yake, kwa sababu) hatukukupeleka kwao uwe mtunzaji (wa matendo yao)



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 115

وَمَن يُشَاقِقِ ٱلرَّسُولَ مِنۢ بَعۡدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُ ٱلۡهُدَىٰ وَيَتَّبِعۡ غَيۡرَ سَبِيلِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ نُوَلِّهِۦ مَا تَوَلَّىٰ وَنُصۡلِهِۦ جَهَنَّمَۖ وَسَآءَتۡ مَصِيرًا

Na yeyote anayempinga Mtume baada ya kumdhihirikia uongofu na akafuata njia isiyokuwa ya Waumini, basi tutamuelekeza huko alikoelekea, na tutamuingiza katika Jahanamu, na hayo ndio marejeo mabaya kabisa



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 92

وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَ وَٱحۡذَرُواْۚ فَإِن تَوَلَّيۡتُمۡ فَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّمَا عَلَىٰ رَسُولِنَا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Na mtiini Allah na mtiini Mtume, na jihadharini (na dhambi). Na mkikengeuka basi jueni ya kuwa jukumu la Mtume wetu ni kufikisha ujumbe wenye kufafanua



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 157

ٱلَّذِينَ يَتَّبِعُونَ ٱلرَّسُولَ ٱلنَّبِيَّ ٱلۡأُمِّيَّ ٱلَّذِي يَجِدُونَهُۥ مَكۡتُوبًا عِندَهُمۡ فِي ٱلتَّوۡرَىٰةِ وَٱلۡإِنجِيلِ يَأۡمُرُهُم بِٱلۡمَعۡرُوفِ وَيَنۡهَىٰهُمۡ عَنِ ٱلۡمُنكَرِ وَيُحِلُّ لَهُمُ ٱلطَّيِّبَٰتِ وَيُحَرِّمُ عَلَيۡهِمُ ٱلۡخَبَـٰٓئِثَ وَيَضَعُ عَنۡهُمۡ إِصۡرَهُمۡ وَٱلۡأَغۡلَٰلَ ٱلَّتِي كَانَتۡ عَلَيۡهِمۡۚ فَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ بِهِۦ وَعَزَّرُوهُ وَنَصَرُوهُ وَٱتَّبَعُواْ ٱلنُّورَ ٱلَّذِيٓ أُنزِلَ مَعَهُۥٓ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ

Ambao wanamfuata Mtume, Nabii, hasomi kilichoandikwa, ambaye kwao wanamkuta amean-dikwa katika Taurati na Injili, anawaamrisha mema na anawakataza maovu, na anawahalalishia vilivyo vizuri, na anawaharamishia vilivyo vibaya, na anawaondoshea mazito yao (sheria zao ngumu) na makongwa (minyororo ya dhambi) waliyokuwa nayo. Basi wale waliomuamini (Mtume huyo) na wakamheshimu na wakamsaidia na wakaifuata nuru aliyoteremshiwa, hao tu ndio waliofanikiwa



Capítulo: AN-FAL 

Verso : 1

يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلۡأَنفَالِۖ قُلِ ٱلۡأَنفَالُ لِلَّهِ وَٱلرَّسُولِۖ فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَصۡلِحُواْ ذَاتَ بَيۡنِكُمۡۖ وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥٓ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ

(Ewe Nabii) Wanakuuliza kuhusu (utaratibu wa ugawaji wa) Ngawira. Sema: Ngawira ni za Allah na Mtume (wao ndio watoaji wa utaratibu wa mgao wake). Basi mcheni Allah (kwa kutekeleza amri zake na kujiepusha na makatazo yake) na tatueni migogoro baina yenu, na mtiini Allah na Mtume wake ikiwa nyinyi ni Waumini



Capítulo: AN-FAL 

Verso : 13

ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ شَآقُّواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥۚ وَمَن يُشَاقِقِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ فَإِنَّ ٱللَّهَ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ

Hilo (la kuwapiga Washirikina) ni kwasababu wamemuasi Allah na Mtume wake (na kuwafurusha waumini kwenye miji yao). Na mwenye kumuasi Allah na Mtume wake basi (ajue) Allah ni Mkali wa kuadhibu



Capítulo: AN-FAL 

Verso : 20

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَلَا تَوَلَّوۡاْ عَنۡهُ وَأَنتُمۡ تَسۡمَعُونَ

Enyi mlioamini, mtiini Allah na Mtume wake (kwa wanayo kuamrisheni au kukukatazeni), na msiigeuke (msiipinge) amri hiyo (ya kumtii Allah na Mtume wake) na ilhali mnasikia (wanayokuambieni)



Capítulo: AN-FAL 

Verso : 24

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱسۡتَجِيبُواْ لِلَّهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمۡ لِمَا يُحۡيِيكُمۡۖ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ يَحُولُ بَيۡنَ ٱلۡمَرۡءِ وَقَلۡبِهِۦ وَأَنَّهُۥٓ إِلَيۡهِ تُحۡشَرُونَ

Enyi mlioamini, muitikeni Allah na Mtume wanapokuiteni kwenye jambo linalokupeni uzima. Na jueni kuwa Allah huingia kati (na kujua yanayojiri) kati ya mtu na moyo wake, na kwamba kwake Yeye tu mtakusanywa (na kulipwa)



Capítulo: AN-FAL 

Verso : 46

وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَلَا تَنَٰزَعُواْ فَتَفۡشَلُواْ وَتَذۡهَبَ رِيحُكُمۡۖ وَٱصۡبِرُوٓاْۚ إِنَّ ٱللَّهَ مَعَ ٱلصَّـٰبِرِينَ

Na mtiini Allah na Mtume wake, wala msizozane mtasambaratika (na woga utakutawaleni) na nguvu zenu zitatoweka. Na vumilieni. Hakika Allah yupo pamoja na wavumilivu



Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 24

قُلۡ إِن كَانَ ءَابَآؤُكُمۡ وَأَبۡنَآؤُكُمۡ وَإِخۡوَٰنُكُمۡ وَأَزۡوَٰجُكُمۡ وَعَشِيرَتُكُمۡ وَأَمۡوَٰلٌ ٱقۡتَرَفۡتُمُوهَا وَتِجَٰرَةٞ تَخۡشَوۡنَ كَسَادَهَا وَمَسَٰكِنُ تَرۡضَوۡنَهَآ أَحَبَّ إِلَيۡكُم مِّنَ ٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ وَجِهَادٖ فِي سَبِيلِهِۦ فَتَرَبَّصُواْ حَتَّىٰ يَأۡتِيَ ٱللَّهُ بِأَمۡرِهِۦۗ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلۡفَٰسِقِينَ

Sema: Ikiwa baba zenu na watoto wenu na ndugu zenu na wake zenu na jamaa zenu na mali mlizochuma na biashara mnazoogopa kuharibika kwake (kwa kukosa soko) na majumba mnayoyapenda ni vipendwa zaidi kwenu kuliko Allah na Mtume wake na kupigana Jihadi katika Njia yake, basi ngojeni mpaka Allah alete amri yake (adhabu yake). Na Allah hawaongozi watu waovu



Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 62

يَحۡلِفُونَ بِٱللَّهِ لَكُمۡ لِيُرۡضُوكُمۡ وَٱللَّهُ وَرَسُولُهُۥٓ أَحَقُّ أَن يُرۡضُوهُ إِن كَانُواْ مُؤۡمِنِينَ

(Wanafiki) Wanakuapieni kwa Allah ili wakuridhisheni na ilhali Allah na Mtume wake ndio wenye haki zaidi wawaridhishe ikiwa wao ni Waumini (wa kweli)



Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 63

أَلَمۡ يَعۡلَمُوٓاْ أَنَّهُۥ مَن يُحَادِدِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ فَأَنَّ لَهُۥ نَارَ جَهَنَّمَ خَٰلِدٗا فِيهَاۚ ذَٰلِكَ ٱلۡخِزۡيُ ٱلۡعَظِيمُ

Je, hawajui ya kwamba anayemfanyia uadui Allah na Mtume wake, basi huyo atapata Moto wa Jahanamu adumu humo? Hiyo ndiyo hasa hizaya kubwa kabisa



Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 71

وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتُ بَعۡضُهُمۡ أَوۡلِيَآءُ بَعۡضٖۚ يَأۡمُرُونَ بِٱلۡمَعۡرُوفِ وَيَنۡهَوۡنَ عَنِ ٱلۡمُنكَرِ وَيُقِيمُونَ ٱلصَّلَوٰةَ وَيُؤۡتُونَ ٱلزَّكَوٰةَ وَيُطِيعُونَ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥٓۚ أُوْلَـٰٓئِكَ سَيَرۡحَمُهُمُ ٱللَّهُۗ إِنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٌ حَكِيمٞ

Na Waumini wanaume na Waumini wanawake ni marafiki (wa kusaidiana na kuungana mkono katika kheri) wao kwa wao. Wanaamrisha mema na wanakataza maovu na wanasimamisha Swala na wanatoa Zaka na wanamtii Allah na Mtume wake. Hao Allah atawashushia rehema. Hakika, Allah ni Mwenye nguvu mno, Mwenye hekima sana



Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 105

وَقُلِ ٱعۡمَلُواْ فَسَيَرَى ٱللَّهُ عَمَلَكُمۡ وَرَسُولُهُۥ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَۖ وَسَتُرَدُّونَ إِلَىٰ عَٰلِمِ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَٰدَةِ فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Na sema (uwaambie wanaotubu na wengineo): Tendeni amali (kwa ikhlasi). Allah, na Mtume wake, na Waumini wataziona amali zenu. Na mtarudishwa kwa (Allah) Mwenye kujua siri na dhahiri; Naye atakuambieni yote mliyokuwa mnayatenda



Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 120

مَا كَانَ لِأَهۡلِ ٱلۡمَدِينَةِ وَمَنۡ حَوۡلَهُم مِّنَ ٱلۡأَعۡرَابِ أَن يَتَخَلَّفُواْ عَن رَّسُولِ ٱللَّهِ وَلَا يَرۡغَبُواْ بِأَنفُسِهِمۡ عَن نَّفۡسِهِۦۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ لَا يُصِيبُهُمۡ ظَمَأٞ وَلَا نَصَبٞ وَلَا مَخۡمَصَةٞ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَلَا يَطَـُٔونَ مَوۡطِئٗا يَغِيظُ ٱلۡكُفَّارَ وَلَا يَنَالُونَ مِنۡ عَدُوّٖ نَّيۡلًا إِلَّا كُتِبَ لَهُم بِهِۦ عَمَلٞ صَٰلِحٌۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُضِيعُ أَجۡرَ ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Haikupasa kwa watu wa Madina na (Mabedui) walioko pembezoni mwao kubakia nyuma wasitoke na Mtume wa Allah, wala kujipendelea nafsi zao kuliko yeye. Hayo ni kwa sababu hawapati kiu, wala uchovu wala njaa katika Njia ya Allah, wala hawakanyagi mahali panapo wachukiza makafiri, wala hawapati chochote cha kupata kwa maadui (ngawira, kuuawa au kutekwa), ila kwa hayo huandikwa kuwa ni kitendo chema kwao. Hakika, Allah haupotezi ujira wa wanaofanya mazuri



Capítulo: ANNUUR 

Verso : 52

وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَيَخۡشَ ٱللَّهَ وَيَتَّقۡهِ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡفَآئِزُونَ

Na wenye kumtii Allah na Mtume wake, na wakamwogopa Allah na wakamcha, basi hao ndio wenye kufuzu



Capítulo: ANNUUR 

Verso : 54

قُلۡ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَۖ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّمَا عَلَيۡهِ مَا حُمِّلَ وَعَلَيۡكُم مَّا حُمِّلۡتُمۡۖ وَإِن تُطِيعُوهُ تَهۡتَدُواْۚ وَمَا عَلَى ٱلرَّسُولِ إِلَّا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Sema: Mtiini Allah, na mtiini Mtume. Na mkigeuka, basi yaliyo juu yake ni aliyo bebeshwa, na yaliyo juu yenu ni mliyo bebeshwa nyinyi. Na mkimtii yeye mtaongoka. Na hapana juu ya Mtume ila kufikisha Ujumbe wazi wazi



Capítulo: ANNUUR 

Verso : 56

وَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتُواْ ٱلزَّكَوٰةَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ

Na shikeni Sala, na toeni Zaka, na mtiini Mtume, ili mpate kurehemewa



Capítulo: ANNUUR 

Verso : 63

لَّا تَجۡعَلُواْ دُعَآءَ ٱلرَّسُولِ بَيۡنَكُمۡ كَدُعَآءِ بَعۡضِكُم بَعۡضٗاۚ قَدۡ يَعۡلَمُ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ يَتَسَلَّلُونَ مِنكُمۡ لِوَاذٗاۚ فَلۡيَحۡذَرِ ٱلَّذِينَ يُخَالِفُونَ عَنۡ أَمۡرِهِۦٓ أَن تُصِيبَهُمۡ فِتۡنَةٌ أَوۡ يُصِيبَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٌ

Msifanye wito wa Mtume baina yenu kama wito wa nyinyi kwa nyinyi. Hakika Allah anawajua miongoni mwenu wanao ondoka kwa uficho. Basi nawatahadhari wanao khalifu amri yake, usije ukawapata msiba au ikawapata adhabu chungu



Capítulo: AL-AHZAAB 

Verso : 36

وَمَا كَانَ لِمُؤۡمِنٖ وَلَا مُؤۡمِنَةٍ إِذَا قَضَى ٱللَّهُ وَرَسُولُهُۥٓ أَمۡرًا أَن يَكُونَ لَهُمُ ٱلۡخِيَرَةُ مِنۡ أَمۡرِهِمۡۗ وَمَن يَعۡصِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ فَقَدۡ ضَلَّ ضَلَٰلٗا مُّبِينٗا

Haiwi kwa Muumini mwana-mume wala Muumini mwanamke kuwa na khiari katika jambo, Allah na Mtume wake wanapo kata shauri katika jambo lao. Na mwenye kumuasi Allah na Mtume wake basi hakika amepotea upotofu ulio wazi