Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 32

قُلۡ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَۖ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Sema: Mtiini Allah na Mtume. Kama mkikengeuka, basi kwa hakika Allah hawapendi makafiri



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 132

وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ

Na mtiini Allah na Mtume ili mpate kupewa rehema



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 13

تِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِۚ وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ يُدۡخِلۡهُ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ وَذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Hiyo ndiyo mipaka ya Allah na yeyote mwenye kumtii Allah na Mtume wake atamuingiza katika Pepo itiririkayo mito chini yake, watabaki humo milele na huko ndiko kufaulu kuliko kukubwa



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 59

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَ وَأُوْلِي ٱلۡأَمۡرِ مِنكُمۡۖ فَإِن تَنَٰزَعۡتُمۡ فِي شَيۡءٖ فَرُدُّوهُ إِلَى ٱللَّهِ وَٱلرَّسُولِ إِن كُنتُمۡ تُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِۚ ذَٰلِكَ خَيۡرٞ وَأَحۡسَنُ تَأۡوِيلًا

Enyi mlioamini, mtiini Allah na mtiini Mtume, na wenye mamlaka katika nyinyi. Basi iwapo mtavutana[1] katika jambo lolote, lirudisheni kwa Allah na (kwa) Mtume, ikiwa mnamuamini Allah na Siku ya Mwisho. Hilo ni bora zaidi na ni mwisho mzuri sana


1- - Kuvutana ni kubishana kuhusu jambo fulani kati ya pande mbili au zaidi na kila upande huvutia kwake.


Capítulo: ANNISAI 

Verso : 69

وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ مَعَ ٱلَّذِينَ أَنۡعَمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ وَٱلصِّدِّيقِينَ وَٱلشُّهَدَآءِ وَٱلصَّـٰلِحِينَۚ وَحَسُنَ أُوْلَـٰٓئِكَ رَفِيقٗا

Na wenye kumtii Allah na Mtume, basi hao watakuwa pamoja na wale ambao Allah amewaneemesha ikiwa ni pamoja na Manabii na Wenye kusadikisha (Maswahaba) na Mashahidi na Watu Wema.[1] Na ni uzuri ulioje kuwa pamoja na watu hao!


1- - Aya hapa inawabainisha walioneemeshwa na ambao katika Aya ya 6 na ya 7 ya Sura Alfaatiha (1) Waislamu wametakiwa kuwaiga na kufuata njia, muongozo na sera zao. Swahaba, wakiongozwa na Abubakar, Umar, Uthman na Ali (Allah awawie radhi) wanahusika katika Aya hii kwa sababu kuna Hadithi kadhaa za Mtume (Allah amshushie rehema na amani, zinazowataja kuwa wamo Mashahidi na Wasadikishaji.


Capítulo: ANNISAI 

Verso : 80

مَّن يُطِعِ ٱلرَّسُولَ فَقَدۡ أَطَاعَ ٱللَّهَۖ وَمَن تَوَلَّىٰ فَمَآ أَرۡسَلۡنَٰكَ عَلَيۡهِمۡ حَفِيظٗا

Yeyote anayemtii Mtume basi hakika (atakuwa) amemtii Allah, na yeyote atakaye kengeuka basi (ni juu yake, kwa sababu) hatukukupeleka kwao uwe mtunzaji (wa matendo yao)



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 92

وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَ وَٱحۡذَرُواْۚ فَإِن تَوَلَّيۡتُمۡ فَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّمَا عَلَىٰ رَسُولِنَا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Na mtiini Allah na mtiini Mtume, na jihadharini (na dhambi). Na mkikengeuka basi jueni ya kuwa jukumu la Mtume wetu ni kufikisha ujumbe wenye kufafanua



Capítulo: AN-FAL 

Verso : 1

يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلۡأَنفَالِۖ قُلِ ٱلۡأَنفَالُ لِلَّهِ وَٱلرَّسُولِۖ فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَصۡلِحُواْ ذَاتَ بَيۡنِكُمۡۖ وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥٓ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ

(Ewe Nabii) Wanakuuliza kuhusu (utaratibu wa ugawaji wa) Ngawira. Sema: Ngawira ni za Allah na Mtume (wao ndio watoaji wa utaratibu wa mgao wake). Basi mcheni Allah (kwa kutekeleza amri zake na kujiepusha na makatazo yake) na tatueni migogoro baina yenu, na mtiini Allah na Mtume wake ikiwa nyinyi ni Waumini



Capítulo: AN-FAL 

Verso : 20

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَلَا تَوَلَّوۡاْ عَنۡهُ وَأَنتُمۡ تَسۡمَعُونَ

Enyi mlioamini, mtiini Allah na Mtume wake (kwa wanayo kuamrisheni au kukukatazeni), na msiigeuke (msiipinge) amri hiyo (ya kumtii Allah na Mtume wake) na ilhali mnasikia (wanayokuambieni)



Capítulo: AN-FAL 

Verso : 46

وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَلَا تَنَٰزَعُواْ فَتَفۡشَلُواْ وَتَذۡهَبَ رِيحُكُمۡۖ وَٱصۡبِرُوٓاْۚ إِنَّ ٱللَّهَ مَعَ ٱلصَّـٰبِرِينَ

Na mtiini Allah na Mtume wake, wala msizozane mtasambaratika (na woga utakutawaleni) na nguvu zenu zitatoweka. Na vumilieni. Hakika Allah yupo pamoja na wavumilivu



Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 71

وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتُ بَعۡضُهُمۡ أَوۡلِيَآءُ بَعۡضٖۚ يَأۡمُرُونَ بِٱلۡمَعۡرُوفِ وَيَنۡهَوۡنَ عَنِ ٱلۡمُنكَرِ وَيُقِيمُونَ ٱلصَّلَوٰةَ وَيُؤۡتُونَ ٱلزَّكَوٰةَ وَيُطِيعُونَ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥٓۚ أُوْلَـٰٓئِكَ سَيَرۡحَمُهُمُ ٱللَّهُۗ إِنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٌ حَكِيمٞ

Na Waumini wanaume na Waumini wanawake ni marafiki (wa kusaidiana na kuungana mkono katika kheri) wao kwa wao. Wanaamrisha mema na wanakataza maovu na wanasimamisha Swala na wanatoa Zaka na wanamtii Allah na Mtume wake. Hao Allah atawashushia rehema. Hakika, Allah ni Mwenye nguvu mno, Mwenye hekima sana



Capítulo: ANNUUR 

Verso : 51

إِنَّمَا كَانَ قَوۡلَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ إِذَا دُعُوٓاْ إِلَى ٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ لِيَحۡكُمَ بَيۡنَهُمۡ أَن يَقُولُواْ سَمِعۡنَا وَأَطَعۡنَاۚ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ

Haiwi kauli ya Waumini wanapo itwa kwa Allah na Mtume wake ili ahukumu baina yao, ila ni kusema: Tumesikia, na tumetii! Na hao ndio wenye kufanikiwa



Capítulo: ANNUUR 

Verso : 52

وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَيَخۡشَ ٱللَّهَ وَيَتَّقۡهِ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡفَآئِزُونَ

Na wenye kumtii Allah na Mtume wake, na wakamwogopa Allah na wakamcha, basi hao ndio wenye kufuzu



Capítulo: ANNUUR 

Verso : 54

قُلۡ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَۖ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّمَا عَلَيۡهِ مَا حُمِّلَ وَعَلَيۡكُم مَّا حُمِّلۡتُمۡۖ وَإِن تُطِيعُوهُ تَهۡتَدُواْۚ وَمَا عَلَى ٱلرَّسُولِ إِلَّا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Sema: Mtiini Allah, na mtiini Mtume. Na mkigeuka, basi yaliyo juu yake ni aliyo bebeshwa, na yaliyo juu yenu ni mliyo bebeshwa nyinyi. Na mkimtii yeye mtaongoka. Na hapana juu ya Mtume ila kufikisha Ujumbe wazi wazi



Capítulo: AL-AHZAAB 

Verso : 33

وَقَرۡنَ فِي بُيُوتِكُنَّ وَلَا تَبَرَّجۡنَ تَبَرُّجَ ٱلۡجَٰهِلِيَّةِ ٱلۡأُولَىٰۖ وَأَقِمۡنَ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتِينَ ٱلزَّكَوٰةَ وَأَطِعۡنَ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥٓۚ إِنَّمَا يُرِيدُ ٱللَّهُ لِيُذۡهِبَ عَنكُمُ ٱلرِّجۡسَ أَهۡلَ ٱلۡبَيۡتِ وَيُطَهِّرَكُمۡ تَطۡهِيرٗا

Na kaeni majumbani kwenu, wala msijishauwe kwa majishauwo ya kijahilia ya kizamani. Na shikeni Sala, na toeni Zaka, na mt’iini Allah na Mtume wake. Hakika Allah anataka kukuondoleeni uchafu, enyi Watu wa Nyumba ya Mtume, na kukusafisheni barabara



Capítulo: AL-AHZAAB 

Verso : 71

يُصۡلِحۡ لَكُمۡ أَعۡمَٰلَكُمۡ وَيَغۡفِرۡ لَكُمۡ ذُنُوبَكُمۡۗ وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ فَقَدۡ فَازَ فَوۡزًا عَظِيمًا

Apate kukutengenezeeni vitendo vyenu na akusameheni madhambi yenu. Na anaye mt’ii Allah na Mtume wake, bila ya shaka amefanikiwa mafanikio makubwa



Capítulo: MUHAMMAD 

Verso : 33

۞يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَ وَلَا تُبۡطِلُوٓاْ أَعۡمَٰلَكُمۡ

Enyi mlio amini! Mtiini Allah, na mtiini Mtume, wala msiviharibu vitendo vyenu



Capítulo: AL-FAT-HI 

Verso : 17

لَّيۡسَ عَلَى ٱلۡأَعۡمَىٰ حَرَجٞ وَلَا عَلَى ٱلۡأَعۡرَجِ حَرَجٞ وَلَا عَلَى ٱلۡمَرِيضِ حَرَجٞۗ وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ يُدۡخِلۡهُ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۖ وَمَن يَتَوَلَّ يُعَذِّبۡهُ عَذَابًا أَلِيمٗا

Kipofu hana lawama, wala kiguru hana lawama, wala mgonjwa hana lawama. Na mwenye kumtii Allah na Mtume wake, atamuingiza katika Mabustani yapitayo mito kati yake. Na atakaye geuka upande atamuadhibu kwa adhabu chungu



Capítulo: AL-HUJURAAT 

Verso : 14

۞قَالَتِ ٱلۡأَعۡرَابُ ءَامَنَّاۖ قُل لَّمۡ تُؤۡمِنُواْ وَلَٰكِن قُولُوٓاْ أَسۡلَمۡنَا وَلَمَّا يَدۡخُلِ ٱلۡإِيمَٰنُ فِي قُلُوبِكُمۡۖ وَإِن تُطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ لَا يَلِتۡكُم مِّنۡ أَعۡمَٰلِكُمۡ شَيۡـًٔاۚ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٌ

Walisema warabu tumeamini, sema hamjaamini lakini sema tumesilimu na bado haijaingia imani kwenye nyoyo zenu, na endapo mtamtii Allah na mtume wake hatowapunguzia kwenye malipo yenu chochote hakika Allah ni mwingi wakusamehe mwingi wa rehema



Capítulo: AL-MUJAADILA 

Verso : 13

ءَأَشۡفَقۡتُمۡ أَن تُقَدِّمُواْ بَيۡنَ يَدَيۡ نَجۡوَىٰكُمۡ صَدَقَٰتٖۚ فَإِذۡ لَمۡ تَفۡعَلُواْ وَتَابَ ٱللَّهُ عَلَيۡكُمۡ فَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتُواْ ٱلزَّكَوٰةَ وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥۚ وَٱللَّهُ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ

Je, mnakhofu kutanguliza hiyo swadaka kabla ya kusemezana kwenu? Ikiwa hamjafanya hayo, na Allah Akapokea toba yenu; basi simamisheni Sala, na toeni Zaka, na mtiini Allah na Mtume Wake; na Allah ni Mwenye khabari kwa yale myatendayo



Capítulo: ATTAGHAABUN 

Verso : 12

وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَۚ فَإِن تَوَلَّيۡتُمۡ فَإِنَّمَا عَلَىٰ رَسُولِنَا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Na mtiini Allah, na mt’iini Mtume. Mkigeuka, basi hakika juu ya Mtume wetu ni kufikisha (Ujumbe wake) kwa uwazi tu



Capítulo: ATTAGHAABUN 

Verso : 16

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ مَا ٱسۡتَطَعۡتُمۡ وَٱسۡمَعُواْ وَأَطِيعُواْ وَأَنفِقُواْ خَيۡرٗا لِّأَنفُسِكُمۡۗ وَمَن يُوقَ شُحَّ نَفۡسِهِۦ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ

Basi mcheni Allah muwezavyo, na sikilizeni; na tiini na toeni (kwa ajili ya Allah) itakuwa kheri kwa ajili ya nafsi zenu. Na yeyote anayeepushwa na ubakhili (tamaa ya uchu wa nafsi yake), basi hao ndio wenye kufaulu (kufanikiwa)