وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَنَّةِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ
Na walioamini na wakatenda yaliyo mema hao ndio watu wa Peponi; wataishi humo milele
لَٰكِنِ ٱلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْ رَبَّهُمۡ لَهُمۡ جَنَّـٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَا نُزُلٗا مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِۗ وَمَا عِندَ ٱللَّهِ خَيۡرٞ لِّلۡأَبۡرَارِ
Lakini wale wamchao Mola wao, wana Pepo zenye kutiririka chini yake mito na watabaki humo, ni makaribisho kutoka kwa Allah, na kilicho kwa Allah ni bora mno kwa wafanyao mema
تِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِۚ وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ يُدۡخِلۡهُ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ وَذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
Hiyo ndiyo mipaka ya Allah na yeyote mwenye kumtii Allah na Mtume wake atamuingiza katika Pepo itiririkayo mito chini yake, watabaki humo milele na huko ndiko kufaulu kuliko kukubwa
وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ سَنُدۡخِلُهُمۡ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۖ لَّهُمۡ فِيهَآ أَزۡوَٰجٞ مُّطَهَّرَةٞۖ وَنُدۡخِلُهُمۡ ظِلّٗا ظَلِيلًا
Na walioamini na wakatenda mema tutawaingiza katika Pepo zipitazo mito chini yake, wakibaki humo milele. Katika Pepo hizo watakuwa na wake waliotakaswa, na tutawaingiza katika vivuli vinavyofunika daima
وَمَن يَعۡمَلۡ مِنَ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ مِن ذَكَرٍ أَوۡ أُنثَىٰ وَهُوَ مُؤۡمِنٞ فَأُوْلَـٰٓئِكَ يَدۡخُلُونَ ٱلۡجَنَّةَ وَلَا يُظۡلَمُونَ نَقِيرٗا
Na yeyote anayefanya mema awe mwanaume au mwanamke na ilhali ni Muumini, basi hao wataingia Peponi na hawatadhulumiwa (jema lolote) hata kama liwe ujazo wa uwazi wa tundu ya kokwa ya tende
فَأَثَٰبَهُمُ ٱللَّهُ بِمَا قَالُواْ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ وَذَٰلِكَ جَزَآءُ ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Basi Allah, kwa yale waliyo yasema, amewalipa Pepo zipitazo mito mbele yake watadumu humo milele. Na hayo ndiyo malipo ya wafanyao mazuri
قَالَ ٱللَّهُ هَٰذَا يَوۡمُ يَنفَعُ ٱلصَّـٰدِقِينَ صِدۡقُهُمۡۚ لَهُمۡ جَنَّـٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۖ رَّضِيَ ٱللَّهُ عَنۡهُمۡ وَرَضُواْ عَنۡهُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
Allah atasema: Hii ndiyo Siku ambayo wasemao kweli utawafaa ukweli wao. Wao watapata Pepo zipitazo mito mbele yake, watadumu humo milele. Allah amewawia radhi, nao wamemuwia radhi. Huko ndiko kufuzu kukubwa sana
ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَهَاجَرُواْ وَجَٰهَدُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡ أَعۡظَمُ دَرَجَةً عِندَ ٱللَّهِۚ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡفَآئِزُونَ
Wale walioamini na wakahama na wakapigana Jihadi katika Njia ya Allah kwa mali zao na nafsi zao, hao wana hadhi kubwa zaidi mbele ya Allah na hao tu ndio wenye kufuzu
يُبَشِّرُهُمۡ رَبُّهُم بِرَحۡمَةٖ مِّنۡهُ وَرِضۡوَٰنٖ وَجَنَّـٰتٖ لَّهُمۡ فِيهَا نَعِيمٞ مُّقِيمٌ
Mola wao Mlezi anawabashiria rehema zitokazo kwake na radhi na Pepo (mbalimbali) ambazo humo watapata neema za kudumu
خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدًاۚ إِنَّ ٱللَّهَ عِندَهُۥٓ أَجۡرٌ عَظِيمٞ
Watadumu humo milele. Hakika kwa Allah yapo malipo (ya aina mbalimbali tena) makubwa mno
وَعَدَ ٱللَّهُ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَا وَمَسَٰكِنَ طَيِّبَةٗ فِي جَنَّـٰتِ عَدۡنٖۚ وَرِضۡوَٰنٞ مِّنَ ٱللَّهِ أَكۡبَرُۚ ذَٰلِكَ هُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
Allah amewaahidi Waumini wanaume na Waumini wanawake Pepo zipitazo mito mbele yake, watadumu humo milele, na (pia amewaahidi) makazi mazuri katika Pepo za kudumu. Na radhi za Allah ndio jambo kubwa zaidi. Huko ndiko hasa kufuzu kukubwa
لَٰكِنِ ٱلرَّسُولُ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مَعَهُۥ جَٰهَدُواْ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡۚ وَأُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمُ ٱلۡخَيۡرَٰتُۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ
Lakini Mtume na wale walioamini pamoja naye walipigana Jihadi kwa mali zao na nafsi zao. Na hao ndio watakaopata heri nyingi na hao ndio hasa wenye kufaulu
أَعَدَّ ٱللَّهُ لَهُمۡ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
Allah amewaandalia Pepo zipitazo mito mbele yake wadumu humo. Huko ndiko kufuzu kukubwa hasa
وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلۡأَوَّلُونَ مِنَ ٱلۡمُهَٰجِرِينَ وَٱلۡأَنصَارِ وَٱلَّذِينَ ٱتَّبَعُوهُم بِإِحۡسَٰنٖ رَّضِيَ ٱللَّهُ عَنۡهُمۡ وَرَضُواْ عَنۡهُ وَأَعَدَّ لَهُمۡ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي تَحۡتَهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
Na wale Muhajirina na Answari wa mwanzo (kuamini) nawaliowafuata wao kwa uzuri, Allah ameridhika nao (kwa utiifu wao), na wao wameridhika naye (kwa malipo mazuri atakayowapa) na amewaandalia Pepo zipitazo mito mbele yake, wadumu humo milele. Huko ndiko kufuzu kukubwa hasa.[1]
1- - Aya hii inatuonesha jinsi Allah alivyowapa Swahaba hadhi, heshima na taadhima kwa kuwatakasa na kuwaridhia. Ni Swahaba wakiongozwa na Abubakar, Umar, Uthman Ali na wengine, Tabiina na waliowafuata wao kwa wema na kwamba wote hao kwa ushahidi wa Aya hii ni Waumini na ni watu wa peponi. Na kwa upande wetu ni kuwaheshimu, kuwataja kwa wema, kuwatetea na kuwaombea dua njema. Allah anasema: “Na waliokuja baada yao wanasema: Ewe Mola wetu Mlezi, tusamehe na wasamehe ndugu zetu waliotutangulia katika imani na usitie ndani ya nyoyo zetu chuki dhidi ya yeyote miongoni mwa waumini. Ewe Mola wetu Mlezi, hakika wewe tu ndiye Mpole sana, Mwenye kurehemu”. Qur’ani 59: 10
وَٱلَّذِينَ صَبَرُواْ ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ رَبِّهِمۡ وَأَقَامُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَأَنفَقُواْ مِمَّا رَزَقۡنَٰهُمۡ سِرّٗا وَعَلَانِيَةٗ وَيَدۡرَءُونَ بِٱلۡحَسَنَةِ ٱلسَّيِّئَةَ أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمۡ عُقۡبَى ٱلدَّارِ
Na ambao husubiri kwa kutaka radhi za Mola wao Mlezi, na wakasimamisha Swala, na wakatoa katika tulivyowaruzuku kwa siri na kwa uwazi, na wakayaondoa maovu kwa mema. Hao ndio watakaopata malipo ya nyumba ya Akhera
جَنَّـٰتُ عَدۡنٖ يَدۡخُلُونَهَا وَمَن صَلَحَ مِنۡ ءَابَآئِهِمۡ وَأَزۡوَٰجِهِمۡ وَذُرِّيَّـٰتِهِمۡۖ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ يَدۡخُلُونَ عَلَيۡهِم مِّن كُلِّ بَابٖ
Nazo ni Bustani za milele, wataingia wao na waliyo wema miongoni mwa Baba zao, na wake zao, na vizazi vyao (hata kama hawakufikia daraja za ucha Mungu). Na Malaika wanaingia kwao wao katika kila mlango
وَأُدۡخِلَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَا بِإِذۡنِ رَبِّهِمۡۖ تَحِيَّتُهُمۡ فِيهَا سَلَٰمٌ
Na (Allah) atawaingiza walioamini na waliotenda mema katika Pepo ipitayo mito mbele yake, watadumu humo kwa idhini ya Mola wao Mlezi. Maamkizi yao humo (kutoka kwa Allah na Malaika) yatakuwa: Salaam[1]
1- - Rejea Sura ArRa’d 13: 24 “Amani iwe kwenu, kwa sababu mlisubiri, basi ni mema yaliyoje matokeo ya
nyumba ya Akhera
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٍ
Hakika wanaomuogopa Mola wao watakuwa katika Pepo na chemchem
ٱدۡخُلُوهَا بِسَلَٰمٍ ءَامِنِينَ
(Wamchao Allah wataambiwa:) Ingieni (Peponi) kwa salama na amani
وَنَزَعۡنَا مَا فِي صُدُورِهِم مِّنۡ غِلٍّ إِخۡوَٰنًا عَلَىٰ سُرُرٖ مُّتَقَٰبِلِينَ
Na tutaondoa (kwa watu wa Peponi) chuki iliyokuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya fahari wakiwa wameelekeana
إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ كَانَتۡ لَهُمۡ جَنَّـٰتُ ٱلۡفِرۡدَوۡسِ نُزُلًا
Hakika wale walio amini na wakatenda mema mashukio yao yatakuwa kwenye Pepo za Firdausi
خَٰلِدِينَ فِيهَا لَا يَبۡغُونَ عَنۡهَا حِوَلٗا
Watadumu humo; hawatataka kuondoka
إِلَّا مَن تَابَ وَءَامَنَ وَعَمِلَ صَٰلِحٗا فَأُوْلَـٰٓئِكَ يَدۡخُلُونَ ٱلۡجَنَّةَ وَلَا يُظۡلَمُونَ شَيۡـٔٗا
Isipokuwa walio tubu, wakaamini, na wakatenda mema. Hao, basi, wataingia Peponi wala hawatadhulumiwa chochote
إِنَّ ٱللَّهَ يُدۡخِلُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ إِنَّ ٱللَّهَ يَفۡعَلُ مَا يُرِيدُ
Hakika Allah atawaingiza walio amini na wakatenda mema katika Bustani zipitazo mito kati yake. Hakika Allah hutenda atakayo
إِنَّ ٱللَّهَ يُدۡخِلُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ يُحَلَّوۡنَ فِيهَا مِنۡ أَسَاوِرَ مِن ذَهَبٖ وَلُؤۡلُؤٗاۖ وَلِبَاسُهُمۡ فِيهَا حَرِيرٞ
Hakika Allah atawaingiza walio amini na wakatenda mema katika Bustani zipitiwazo na mito kati yake. Watapambwa humo kwa mapambo ya mikononi ya dhahabu na lulu. Na mavazi yao humo ni hariri
وَهُدُوٓاْ إِلَى ٱلطَّيِّبِ مِنَ ٱلۡقَوۡلِ وَهُدُوٓاْ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلۡحَمِيدِ
Na wataongozwa kwenye maneno mazuri, na wataongozwa kwenye Njia ya Msifiwa
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٖ
Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani
لَّيۡسَ عَلَى ٱلۡأَعۡمَىٰ حَرَجٞ وَلَا عَلَى ٱلۡأَعۡرَجِ حَرَجٞ وَلَا عَلَى ٱلۡمَرِيضِ حَرَجٞۗ وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ يُدۡخِلۡهُ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۖ وَمَن يَتَوَلَّ يُعَذِّبۡهُ عَذَابًا أَلِيمٗا
Kipofu hana lawama, wala kiguru hana lawama, wala mgonjwa hana lawama. Na mwenye kumtii Allah na Mtume wake, atamuingiza katika Mabustani yapitayo mito kati yake. Na atakaye geuka upande atamuadhibu kwa adhabu chungu
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَنَعِيمٖ
Hakika ya wacha mungu watakua katika bustani na neema
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَنَهَرٖ
Hakika Waliomcha Allah watakua kwenye mabustani Na Mito