Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 213

كَانَ ٱلنَّاسُ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ فَبَعَثَ ٱللَّهُ ٱلنَّبِيِّـۧنَ مُبَشِّرِينَ وَمُنذِرِينَ وَأَنزَلَ مَعَهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ لِيَحۡكُمَ بَيۡنَ ٱلنَّاسِ فِيمَا ٱخۡتَلَفُواْ فِيهِۚ وَمَا ٱخۡتَلَفَ فِيهِ إِلَّا ٱلَّذِينَ أُوتُوهُ مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَتۡهُمُ ٱلۡبَيِّنَٰتُ بَغۡيَۢا بَيۡنَهُمۡۖ فَهَدَى ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لِمَا ٱخۡتَلَفُواْ فِيهِ مِنَ ٱلۡحَقِّ بِإِذۡنِهِۦۗ وَٱللَّهُ يَهۡدِي مَن يَشَآءُ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٍ

Watu walikuwa umma mmoja. Allah akatuma Mitume wakitoa habari njema na wakitoa maonyo na aliteremsha vitabu pamoja nao kwa haki ili ahukumu kati ya watu katika yale ambayo wametofatiana. Na hawakutofautiana katika hayo isipokuwa wale tu waliopewa vitabu hivyo, baada ya kuwafikia hoja za waziwazi kwa sababu tu ya uovu walionao. Basi Allah akawaongoza wale ambao wameamini kwenye haki kwa idhini yake na Allah anamuongoza amtakaye kwenye njia iliyo nyooka



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 96

إِنَّ أَوَّلَ بَيۡتٖ وُضِعَ لِلنَّاسِ لَلَّذِي بِبَكَّةَ مُبَارَكٗا وَهُدٗى لِّلۡعَٰلَمِينَ

Kwa yakini kabisa, nyumba ya kwanza kabisa kuwekwa (ardhini) kwa ajili ya watu (ili kumuabudu Allah) ni ile (Alkaaba) iliyoko Makkah ikiwa imebarikiwa na ni uongofu kwa walimwengu wote



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 105

وَلَا تَكُونُواْ كَٱلَّذِينَ تَفَرَّقُواْ وَٱخۡتَلَفُواْ مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَهُمُ ٱلۡبَيِّنَٰتُۚ وَأُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمۡ عَذَابٌ عَظِيمٞ

Na msiwe kama wale waliosam-baratika na wakafarakana baada ya kuwajia hoja za wazi, na hao wana adhabu kubwa



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 138

هَٰذَا بَيَانٞ لِّلنَّاسِ وَهُدٗى وَمَوۡعِظَةٞ لِّلۡمُتَّقِينَ

Huu ni ubainifu kwa watu, na ni uongofu na ni mawaidha kwa wacha Mungu



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 165

أَوَلَمَّآ أَصَٰبَتۡكُم مُّصِيبَةٞ قَدۡ أَصَبۡتُم مِّثۡلَيۡهَا قُلۡتُمۡ أَنَّىٰ هَٰذَاۖ قُلۡ هُوَ مِنۡ عِندِ أَنفُسِكُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ

Hivi mlipopata msiba hakika mmekwishapatwa mara mbili ya huo, mlisema: umetoka wapi msiba huu? Sema huo umetoka kwenu wenyewe, hakika Allah juu ya kila kitu ni muweza



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 174

فَٱنقَلَبُواْ بِنِعۡمَةٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَفَضۡلٖ لَّمۡ يَمۡسَسۡهُمۡ سُوٓءٞ وَٱتَّبَعُواْ رِضۡوَٰنَ ٱللَّهِۗ وَٱللَّهُ ذُو فَضۡلٍ عَظِيمٍ

Basi wakarudi na neema za Allah na fadhila zake, hakuna baya lililowagusa, na wakafuata yanayomridhi Allah, na Allah ni mwenye fadhila kubwa mno



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 175

إِنَّمَا ذَٰلِكُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ يُخَوِّفُ أَوۡلِيَآءَهُۥ فَلَا تَخَافُوهُمۡ وَخَافُونِ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika huyo ni shetani anawatia khofu marafiki zake, basi msiwaogope wao, bali niogopeni mimi mkiwa nyinyi ni waumini



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 97

۞جَعَلَ ٱللَّهُ ٱلۡكَعۡبَةَ ٱلۡبَيۡتَ ٱلۡحَرَامَ قِيَٰمٗا لِّلنَّاسِ وَٱلشَّهۡرَ ٱلۡحَرَامَ وَٱلۡهَدۡيَ وَٱلۡقَلَـٰٓئِدَۚ ذَٰلِكَ لِتَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ وَأَنَّ ٱللَّهَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٌ

Allah ameifanya Al-Kaaba, Nyumba Tukufu kuwa tegemeo la watu, na kadhalika (ameifanya) Miezi Mitukufu (tegemeo kwa kusitishwa vita) na wanyama wa hadiyi (dhabihu) waliovikwa koja. (Allah amefanya) Hayo ili mjue kwamba Allah anayajua yaliyomo mbinguni na yaliyomo ardhini, na kwamba Allah ni Mjuzi wa kila kitu



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 158

قُلۡ يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ إِنِّي رَسُولُ ٱللَّهِ إِلَيۡكُمۡ جَمِيعًا ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ يُحۡيِۦ وَيُمِيتُۖ فَـَٔامِنُواْ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِ ٱلنَّبِيِّ ٱلۡأُمِّيِّ ٱلَّذِي يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَكَلِمَٰتِهِۦ وَٱتَّبِعُوهُ لَعَلَّكُمۡ تَهۡتَدُونَ

Sema: Enyi watu, hakika mimi ni Mtume wa Allah kwenu nyote[1]. (Allah) Ambaye ni wake pekee ufalme wa mbinguni na ardhini. Hapana mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa yeye tu. Anahuisha na anafisha. Basi muaminini Allah na Mtume wake, Nabii ambaye hasomi kilichoandikwa, ambaye anamuamini Allah na maneno yake, na mfuateni ili mpate kuongoka


1- - Aya hii ni tangazo rasmi kwamba, Uislamu ni dini ya ulimwengu wote na sio ya taifa fulani, kabila fulani au jamii fulani.


Capítulo: YUNUS 

Verso : 19

وَمَا كَانَ ٱلنَّاسُ إِلَّآ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ فَٱخۡتَلَفُواْۚ وَلَوۡلَا كَلِمَةٞ سَبَقَتۡ مِن رَّبِّكَ لَقُضِيَ بَيۡنَهُمۡ فِيمَا فِيهِ يَخۡتَلِفُونَ

Na hawakuwa watu isipokuwa ni Umma mmoja tu, basi wakatofautiana.[1] Na lau kama sio neno lililotangulia[2] kutoka kwa Mola wako Mlezi bila shaka wangekwisha hukumiwa kati yao katika yale wanayo tofautiana humo


1- - Aya hapa inaeleza kuwa binadamu wote walikuwa kitu kimoja wakiwa katika dini moja. Lakini baadae walitofautiana na baadhi yao kupotoka ndio Allah akatuma Mitume ili kuwarudisha katika dini sahihi.


2- - Neno lililokusudiwa hapa ni ule uamuzi wa Allah wa kutowahukumu watu hapa duniani kwa dhambi wanazofanya kama ilivyokuwa kwa mataifa yaliyopita. Amewapa muda hadi Siku ya Kiama. Uamuzi huu umetajwa katika Aya ya 14 ya Sura Ash-shuuraa (42).


Capítulo: YUNUS 

Verso : 57

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ قَدۡ جَآءَتۡكُم مَّوۡعِظَةٞ مِّن رَّبِّكُمۡ وَشِفَآءٞ لِّمَا فِي ٱلصُّدُورِ وَهُدٗى وَرَحۡمَةٞ لِّلۡمُؤۡمِنِينَ

Enyi watu, hakika yamekujieni mawaidha kutoka kwa Mola wenu Mlezi na ponyo (dawa) ya (maradhi) yaliyomo vifuani (mwenu) na muongozo na rehema kwa Waumini



Capítulo: YUNUS 

Verso : 108

قُلۡ يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ قَدۡ جَآءَكُمُ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّكُمۡۖ فَمَنِ ٱهۡتَدَىٰ فَإِنَّمَا يَهۡتَدِي لِنَفۡسِهِۦۖ وَمَن ضَلَّ فَإِنَّمَا يَضِلُّ عَلَيۡهَاۖ وَمَآ أَنَا۠ عَلَيۡكُم بِوَكِيلٖ

Sema: Enyi watu, hakika imekujieni haki kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Basi yeyote anayeongoka, anaongoka kwa faida ya nafsi yake, na anayepotea, basi kwa hakika anapotea kwa hasara ya nafsi yake. Na mimi si msaidizi kwenu



Capítulo: YUSUF 

Verso : 38

وَٱتَّبَعۡتُ مِلَّةَ ءَابَآءِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَۚ مَا كَانَ لَنَآ أَن نُّشۡرِكَ بِٱللَّهِ مِن شَيۡءٖۚ ذَٰلِكَ مِن فَضۡلِ ٱللَّهِ عَلَيۡنَا وَعَلَى ٱلنَّاسِ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَ ٱلنَّاسِ لَا يَشۡكُرُونَ

Na nilifuata mila (dini) ya Baba zangu, Ibrahim na Is-hak na Yakubu. Sisi hatukuwa na haki ya kumshirikisha Allah kwa chochote. Hayo ni katika fadhila za Allah kwetu na kwa watu (wengine) lakini watu wengi sana hawashukuru



Capítulo: IBRAHIM 

Verso : 1

الٓرۚ كِتَٰبٌ أَنزَلۡنَٰهُ إِلَيۡكَ لِتُخۡرِجَ ٱلنَّاسَ مِنَ ٱلظُّلُمَٰتِ إِلَى ٱلنُّورِ بِإِذۡنِ رَبِّهِمۡ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَمِيدِ

Alif Lam Raa[1]. Hiki ni Kitabu tulichokiteremsha kwako ili kwacho uwatowe watu kwenye giza uwapeleke kwenye muangaza, kwa idhini ya Mola wao Mlezi, uwafikishe kwenye Njia ya Mwenye nguvu, Msifiwa


1- - Allah ndiye ajuaye maana halisi ya herufi hizi.


Capítulo: ANNAHLI 

Verso : 44

بِٱلۡبَيِّنَٰتِ وَٱلزُّبُرِۗ وَأَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ ٱلذِّكۡرَ لِتُبَيِّنَ لِلنَّاسِ مَا نُزِّلَ إِلَيۡهِمۡ وَلَعَلَّهُمۡ يَتَفَكَّرُونَ

(Tuliwatuma) wakiwa na dalili za wazi. Na tumekuteremshia (ewe Muhammad) ukumbusho (Qur’ani) ili uwabainishie watu (kilichojificha katika maana na hukumu zake), na ili wapate kutafakari



Capítulo: AL-ISRAA 

Verso : 89

وَلَقَدۡ صَرَّفۡنَا لِلنَّاسِ فِي هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانِ مِن كُلِّ مَثَلٖ فَأَبَىٰٓ أَكۡثَرُ ٱلنَّاسِ إِلَّا كُفُورٗا

Na hakika tumewaeleza watu katika hii Qur’ani kwa kila mfano. Lakini watu wengi wanakataa isipo kuwa kukanusha tu



Capítulo: AL-HAJJ 

Verso : 49

قُلۡ يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ إِنَّمَآ أَنَا۠ لَكُمۡ نَذِيرٞ مُّبِينٞ

Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni mwonyaji kwenu niliye dhaahiri



Capítulo: ARRUUM 

Verso : 30

فَأَقِمۡ وَجۡهَكَ لِلدِّينِ حَنِيفٗاۚ فِطۡرَتَ ٱللَّهِ ٱلَّتِي فَطَرَ ٱلنَّاسَ عَلَيۡهَاۚ لَا تَبۡدِيلَ لِخَلۡقِ ٱللَّهِۚ ذَٰلِكَ ٱلدِّينُ ٱلۡقَيِّمُ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَ ٱلنَّاسِ لَا يَعۡلَمُونَ

Basi uelekeze uso wako sawasawa kwenye Dini. Ndyo umbile la Mwenyezi Mungu alilo waumbia watu, hapana mabadiliko katika uumbaji wa Mwenyezi Mungu. Hiyo ndiyo dini iliyo sawa, lakini watu wengi hawajui.



Capítulo: SABAA 

Verso : 28

وَمَآ أَرۡسَلۡنَٰكَ إِلَّا كَآفَّةٗ لِّلنَّاسِ بَشِيرٗا وَنَذِيرٗا وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَ ٱلنَّاسِ لَا يَعۡلَمُونَ

Na hatukukutuma ila kwa watu wote, uwe mbashiri, na muonyaji. Lakini watu wengi hawajui



Capítulo: AZZUMAR 

Verso : 41

إِنَّآ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ لِلنَّاسِ بِٱلۡحَقِّۖ فَمَنِ ٱهۡتَدَىٰ فَلِنَفۡسِهِۦۖ وَمَن ضَلَّ فَإِنَّمَا يَضِلُّ عَلَيۡهَاۖ وَمَآ أَنتَ عَلَيۡهِم بِوَكِيلٍ

Hakika Sisi tumekuteremshia Kitabu kwa ajili ya watu wote kwa Haki. Basi mwenye kuongoka ni kwa nafsi yake, na mwenye kupotoka bila ya shaka amepotoka kwa hasara yake. Na wewe si mlinzi juu yao



Capítulo: ASH-SHUURAA 

Verso : 13

۞شَرَعَ لَكُم مِّنَ ٱلدِّينِ مَا وَصَّىٰ بِهِۦ نُوحٗا وَٱلَّذِيٓ أَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡكَ وَمَا وَصَّيۡنَا بِهِۦٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ وَعِيسَىٰٓۖ أَنۡ أَقِيمُواْ ٱلدِّينَ وَلَا تَتَفَرَّقُواْ فِيهِۚ كَبُرَ عَلَى ٱلۡمُشۡرِكِينَ مَا تَدۡعُوهُمۡ إِلَيۡهِۚ ٱللَّهُ يَجۡتَبِيٓ إِلَيۡهِ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِيٓ إِلَيۡهِ مَن يُنِيبُ

Amekuamrisheni Dini ile ile aliyo muusia Nuhu na tuliyo kufunulia wewe, na tuliyo wausia Ibrahim na Mussa na Issa, kwamba shikeni Dini wala msifarakane kwayo. Ni magumu kwa washirikina hayo unayo waitia. Allah humteua amtakaye, na humwongoa aelekeaye



Capítulo: AL-JAATHIYA 

Verso : 20

هَٰذَا بَصَـٰٓئِرُ لِلنَّاسِ وَهُدٗى وَرَحۡمَةٞ لِّقَوۡمٖ يُوقِنُونَ

Hizi ni dalili zilizo wazi kwa watu wote, na ni uongofu, na rehema kwa watu wenye yakini



Capítulo: AL-HADIID

Verso : 25

لَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا رُسُلَنَا بِٱلۡبَيِّنَٰتِ وَأَنزَلۡنَا مَعَهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمِيزَانَ لِيَقُومَ ٱلنَّاسُ بِٱلۡقِسۡطِۖ وَأَنزَلۡنَا ٱلۡحَدِيدَ فِيهِ بَأۡسٞ شَدِيدٞ وَمَنَٰفِعُ لِلنَّاسِ وَلِيَعۡلَمَ ٱللَّهُ مَن يَنصُرُهُۥ وَرُسُلَهُۥ بِٱلۡغَيۡبِۚ إِنَّ ٱللَّهَ قَوِيٌّ عَزِيزٞ

Kwa yakini Tuliwapeleka Mitume Wetu kwa hoja zilizo wazi wazi, na Tukateremsha pamoja nao Kitabu na Mizani (shariy’ah) ili watu wasimamie kwa uadilifu. Na Tukateremsha chuma chenye nguvu nyingi na manufaa kwa watu, na ili Allah Ajue nani atakayeinusuru (Dini Yake) na Mtume Wake hali ya kuwa ni ghaibu. Hakika Allah ni Mwenye nguvu zote, Mwenye kushinda