Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 49

وَإِذۡ نَجَّيۡنَٰكُم مِّنۡ ءَالِ فِرۡعَوۡنَ يَسُومُونَكُمۡ سُوٓءَ ٱلۡعَذَابِ يُذَبِّحُونَ أَبۡنَآءَكُمۡ وَيَسۡتَحۡيُونَ نِسَآءَكُمۡۚ وَفِي ذَٰلِكُم بَلَآءٞ مِّن رَّبِّكُمۡ عَظِيمٞ

Na (kumbukeni) tulipokuokoeni kutoka kwenye mateso ya Firauni na watu wake waliokupeni adhabu mbaya kabisa; wakiwauwa watoto wenu wanaume kwa kuwachinjachinja na wakiwaacha hai watoto wenu wanawake. Na katika hayo kuna mtihani mkubwa sana kwenu kutoka kwa Mola wenu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 50

وَإِذۡ فَرَقۡنَا بِكُمُ ٱلۡبَحۡرَ فَأَنجَيۡنَٰكُمۡ وَأَغۡرَقۡنَآ ءَالَ فِرۡعَوۡنَ وَأَنتُمۡ تَنظُرُونَ

Na (kumbukeni) tulipokut-enganishieni bahari tukakuokoeni na tukawazamisha watu wa Firauni na nyinyi mkitazama



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 103

ثُمَّ بَعَثۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِم مُّوسَىٰ بِـَٔايَٰتِنَآ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِۦ فَظَلَمُواْ بِهَاۖ فَٱنظُرۡ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُفۡسِدِينَ

Kisha tulimtuma Musa kwa Aya zetu baada yao, aende kwa Firauni na kundi lake la mamwinyi, basi wakazidhulumu (wakazipinga) Aya hizo. Basi ona namna ulivyokuwa mwisho wa waharibifu



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 104

وَقَالَ مُوسَىٰ يَٰفِرۡعَوۡنُ إِنِّي رَسُولٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na Musa akasema: Ewe Firauni, hakika mimi ni Mtume kutoka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 105

حَقِيقٌ عَلَىٰٓ أَن لَّآ أَقُولَ عَلَى ٱللَّهِ إِلَّا ٱلۡحَقَّۚ قَدۡ جِئۡتُكُم بِبَيِّنَةٖ مِّن رَّبِّكُمۡ فَأَرۡسِلۡ مَعِيَ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ

Ni haki kwangu kutomsemea Allah ila lile la haki tu. Hakika, nimekujieni na hoja za wazi kutoka kwa Mola wenu Mlezi (zinazothibitisha ukweli wangu). Basi waachie Wana wa Israili (wawe huru) wawe pamoja na mimi (kwenda kwenye mji wa baba zao)



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 106

قَالَ إِن كُنتَ جِئۡتَ بِـَٔايَةٖ فَأۡتِ بِهَآ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ

(Firauni) Akasema: Kama umekuja na hoja basi ilete kama wewe ni miongoni mwa wasemao kweli



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 107

فَأَلۡقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعۡبَانٞ مُّبِينٞ

Basi (Musa) akaitupa chini fimbo yake na ghafla ikawa nyoka wa dhahiri



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 108

وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِيَ بَيۡضَآءُ لِلنَّـٰظِرِينَ

Na akautoa kwa nguvu mkono wake (kutoka katika nguo yake) na ghafla ukawa mweupe kwa wanaotazama



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 109

قَالَ ٱلۡمَلَأُ مِن قَوۡمِ فِرۡعَوۡنَ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٌ عَلِيمٞ

Mamwinyi katika watu wa Firauni wakasema: Hakika, huyu ni mchawi mjuzi sana



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 110

يُرِيدُ أَن يُخۡرِجَكُم مِّنۡ أَرۡضِكُمۡۖ فَمَاذَا تَأۡمُرُونَ

Anataka kukutoeni katika ardhi (nchi) yenu (kwa uchawi wake). Basi mnaniamuru (mnanishauri nifanye) nini?



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 111

قَالُوٓاْ أَرۡجِهۡ وَأَخَاهُ وَأَرۡسِلۡ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

Wakasema: Mpe muda yeye (Musa) na ndugu yake na tuma katika miji yote (watu) watakaofanya kazi ya kukusanya (wachawi)



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 112

يَأۡتُوكَ بِكُلِّ سَٰحِرٍ عَلِيمٖ

Wakuletee kila mchawi mahiri sana



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 113

وَجَآءَ ٱلسَّحَرَةُ فِرۡعَوۡنَ قَالُوٓاْ إِنَّ لَنَا لَأَجۡرًا إِن كُنَّا نَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبِينَ

Na wachawi walikuja kwa Firauni wakasema: Hivi sisi tutalipwa endapo tutashinda?



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 114

قَالَ نَعَمۡ وَإِنَّكُمۡ لَمِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

(Firauni) Akasema: Ndio, na kwa hakika kabisa, nyinyi mtakuwa miongoni mwa watu wangu wa karibu sana



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 115

قَالُواْ يَٰمُوسَىٰٓ إِمَّآ أَن تُلۡقِيَ وَإِمَّآ أَن نَّكُونَ نَحۡنُ ٱلۡمُلۡقِينَ

(Wachawi) Wakasema: Ewe Musa, ama tupa (toa wewe uchawi wako) au sisi tuwe wa mwanzo kutupa (kutoa)



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 116

قَالَ أَلۡقُواْۖ فَلَمَّآ أَلۡقَوۡاْ سَحَرُوٓاْ أَعۡيُنَ ٱلنَّاسِ وَٱسۡتَرۡهَبُوهُمۡ وَجَآءُو بِسِحۡرٍ عَظِيمٖ

(Musa) Akasema: Tupeni (Toeni). (Wachawi) Walipotupa (walipotoa uchawi wao) waliyaroga macho ya watu na waliwatisha na walikuja na uchawi mkubwa sana!



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 117

۞وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنۡ أَلۡقِ عَصَاكَۖ فَإِذَا هِيَ تَلۡقَفُ مَا يَأۡفِكُونَ

Na tulimfunulia Musa Wahyi kwamba: Tupa fimbo yako, na ghafla ikawa inameza vyote wanavyovizusha



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 118

فَوَقَعَ ٱلۡحَقُّ وَبَطَلَ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Basi haki ikathibiti na vikabatilika vyote walivyokuwa wanafanya



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 119

فَغُلِبُواْ هُنَالِكَ وَٱنقَلَبُواْ صَٰغِرِينَ

Basi (wachawi) hapo wakashindwa na wakabadilika wakawa wanyonge!



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 120

وَأُلۡقِيَ ٱلسَّحَرَةُ سَٰجِدِينَ

Na wachawi wakaporomoka chini kumsujudia (Allah)



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 121

قَالُوٓاْ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wakasema: Tumeamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 122

رَبِّ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ

Mola Mlezi wa Musa na Haruna



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 123

قَالَ فِرۡعَوۡنُ ءَامَنتُم بِهِۦ قَبۡلَ أَنۡ ءَاذَنَ لَكُمۡۖ إِنَّ هَٰذَا لَمَكۡرٞ مَّكَرۡتُمُوهُ فِي ٱلۡمَدِينَةِ لِتُخۡرِجُواْ مِنۡهَآ أَهۡلَهَاۖ فَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَ

Firauni akasema: Hivi mmemuamini kabla mimi sijakupeni idhini? Kwa hakika kabisa, hii ni njama mliyoipanga mjini ili muwatoe humo watu wake. Basi mtatambua (nitakachokufanyeni)!



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 124

لَأُقَطِّعَنَّ أَيۡدِيَكُمۡ وَأَرۡجُلَكُم مِّنۡ خِلَٰفٖ ثُمَّ لَأُصَلِّبَنَّكُمۡ أَجۡمَعِينَ

Kwa hakika kabisa, nitaikatakata mikono yenu na miguu yenu kwa kupishanisha, kisha nitakutundikeni misalabani nyote



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 125

قَالُوٓاْ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ

Wakasema: Hakika, sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 126

وَمَا تَنقِمُ مِنَّآ إِلَّآ أَنۡ ءَامَنَّا بِـَٔايَٰتِ رَبِّنَا لَمَّا جَآءَتۡنَاۚ رَبَّنَآ أَفۡرِغۡ عَلَيۡنَا صَبۡرٗا وَتَوَفَّنَا مُسۡلِمِينَ

Na hakuna kosa linalopelekea ututese isipokuwa tu huku kuamini kwetu Aya za Mola wetu Mlezi zilipotufikia. (Ewe) Mola wetu Mlezi, tujaze subira na tufishe tukiwa Waislamu



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 127

وَقَالَ ٱلۡمَلَأُ مِن قَوۡمِ فِرۡعَوۡنَ أَتَذَرُ مُوسَىٰ وَقَوۡمَهُۥ لِيُفۡسِدُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَيَذَرَكَ وَءَالِهَتَكَۚ قَالَ سَنُقَتِّلُ أَبۡنَآءَهُمۡ وَنَسۡتَحۡيِۦ نِسَآءَهُمۡ وَإِنَّا فَوۡقَهُمۡ قَٰهِرُونَ

Na mamwinyi katika watu wa Firauni wakasema (kumwambia Firauni): Hivi unamuacha Musa na watu wake wafanye uharibifu katika ardhi (nchi yetu) na akuache wewe na Miungu yako? (Firauni) Akasema: Tutawaua vibaya watoto wao wanaume na tutawaacha hai watoto wao wanawake, nasi tuna uwezo mkubwa wa kuwashinda!



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 128

قَالَ مُوسَىٰ لِقَوۡمِهِ ٱسۡتَعِينُواْ بِٱللَّهِ وَٱصۡبِرُوٓاْۖ إِنَّ ٱلۡأَرۡضَ لِلَّهِ يُورِثُهَا مَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦۖ وَٱلۡعَٰقِبَةُ لِلۡمُتَّقِينَ

Musa akawaambia watu wake: Ombeni msaada kwa Allah na vumilieni[1]. Hakika, ardhi ni ya Allah tu anamrithisha amtakaye miongoni mwa waja wake. Na mwisho mwema ni wa wachaMungu tu


1- - Hapa kuna fundisho kwa Waislamu. Mtume Musa, kwa wakati huo, aliona udhaifu wa waumini na kutokuwa na maandalizi na uwezo wa kupambana. Kwa mantiki hiyo, hakuwashauri kuingia katika mapambano, lakini aliwaelekeza kuomba msaada kwa Allah na kuwa na Subira na uvumilivu na kuwaliwaza na pia kuwakumbusha ahadi ya Allah kuwa ushindi kwa waumini ni lazima pale Allah atakaporuhusu mazingira ya ushindi.


Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 129

قَالُوٓاْ أُوذِينَا مِن قَبۡلِ أَن تَأۡتِيَنَا وَمِنۢ بَعۡدِ مَا جِئۡتَنَاۚ قَالَ عَسَىٰ رَبُّكُمۡ أَن يُهۡلِكَ عَدُوَّكُمۡ وَيَسۡتَخۡلِفَكُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَيَنظُرَ كَيۡفَ تَعۡمَلُونَ

Wakasema: Tumefanyiwa maudhi kabla ya wewe kutujia na baada ya kutujia. (Musa) Akasema: Huenda Mola wenu Mlezi akamuangamiza adui yenu na akakuwekeni nyinyi badala yao katika ardhi ili aangalie: Mtafanya nini?



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 130

وَلَقَدۡ أَخَذۡنَآ ءَالَ فِرۡعَوۡنَ بِٱلسِّنِينَ وَنَقۡصٖ مِّنَ ٱلثَّمَرَٰتِ لَعَلَّهُمۡ يَذَّكَّرُونَ

Na kwa hakika kabisa, tuliwashika (tuliwatia adabu) watu wa Firauni kwa miaka ya shida mbali mbali na upungufu wa matunda (vyakula) ili waonyeke