Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 185

شَهۡرُ رَمَضَانَ ٱلَّذِيٓ أُنزِلَ فِيهِ ٱلۡقُرۡءَانُ هُدٗى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَٰتٖ مِّنَ ٱلۡهُدَىٰ وَٱلۡفُرۡقَانِۚ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ ٱلشَّهۡرَ فَلۡيَصُمۡهُۖ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوۡ عَلَىٰ سَفَرٖ فَعِدَّةٞ مِّنۡ أَيَّامٍ أُخَرَۗ يُرِيدُ ٱللَّهُ بِكُمُ ٱلۡيُسۡرَ وَلَا يُرِيدُ بِكُمُ ٱلۡعُسۡرَ وَلِتُكۡمِلُواْ ٱلۡعِدَّةَ وَلِتُكَبِّرُواْ ٱللَّهَ عَلَىٰ مَا هَدَىٰكُمۡ وَلَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ

Ni mwezi wa Ramadhani ambao ndani yake imeteremshwa Qur’aniwe muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongozi na upambanuzi. Basi atakayeshuhudia mwezi (huo) miongoni mwenu afunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi[1] atimize hesabu katika siku nyingine[2]. Allah anakutakieni wepesi na hakutakieni uzito, na ili mumtukuze Allah kwa kukuongozeni na ili mpate kushukuru


1- - Anaruhusiwa kutofunga na kutimiza.


2- - Kwa kufunga zile siku ambazo hakufunga.