Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 184

أَيَّامٗا مَّعۡدُودَٰتٖۚ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوۡ عَلَىٰ سَفَرٖ فَعِدَّةٞ مِّنۡ أَيَّامٍ أُخَرَۚ وَعَلَى ٱلَّذِينَ يُطِيقُونَهُۥ فِدۡيَةٞ طَعَامُ مِسۡكِينٖۖ فَمَن تَطَوَّعَ خَيۡرٗا فَهُوَ خَيۡرٞ لَّهُۥۚ وَأَن تَصُومُواْ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Ni siku chache za kuhesabika tu. Na atakayekuwa mgonjwa miongoni mwenu au safarini, basi[1] atimize hesabu katika siku nyingine. Na wale wasioiweza (funga), watoe fidia kwa kumlisha maskini. Na atakayefanya wema kwa ridhaa ya nafsi yake, basi ni bora kwake, na kufunga ni bora kwenu, ikiwa mnajua


1- - Anaruhusiwa kuacha kufunga na atimize.


Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 196

وَأَتِمُّواْ ٱلۡحَجَّ وَٱلۡعُمۡرَةَ لِلَّهِۚ فَإِنۡ أُحۡصِرۡتُمۡ فَمَا ٱسۡتَيۡسَرَ مِنَ ٱلۡهَدۡيِۖ وَلَا تَحۡلِقُواْ رُءُوسَكُمۡ حَتَّىٰ يَبۡلُغَ ٱلۡهَدۡيُ مَحِلَّهُۥۚ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوۡ بِهِۦٓ أَذٗى مِّن رَّأۡسِهِۦ فَفِدۡيَةٞ مِّن صِيَامٍ أَوۡ صَدَقَةٍ أَوۡ نُسُكٖۚ فَإِذَآ أَمِنتُمۡ فَمَن تَمَتَّعَ بِٱلۡعُمۡرَةِ إِلَى ٱلۡحَجِّ فَمَا ٱسۡتَيۡسَرَ مِنَ ٱلۡهَدۡيِۚ فَمَن لَّمۡ يَجِدۡ فَصِيَامُ ثَلَٰثَةِ أَيَّامٖ فِي ٱلۡحَجِّ وَسَبۡعَةٍ إِذَا رَجَعۡتُمۡۗ تِلۡكَ عَشَرَةٞ كَامِلَةٞۗ ذَٰلِكَ لِمَن لَّمۡ يَكُنۡ أَهۡلُهُۥ حَاضِرِي ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ

Na timizeni Hija na Umra kwa ajili ya Allah. Na ikiwa mmezuiwa[1], basi chinjeni wanyama watakaokuwa rahisi kupatikana. Na wala msinyoe vichwa vyenu, hadi mnyama afike mahali pake. Basi ambaye atakuwa mgonjwa miongoni mwenu, au ana tatizo kichwani kwake, basi atoe fidia ya kufunga au sadaka au mnyama. Na mtakapokuwa katika hali ya amani, atakayefanya Umra kabla ya Hija[2] basi afunge siku tatu katika Hija na siku saba mtakaporejea kwenu. Hizo ni siku kumi kamili. Hilo ni kwa ambaye familia yake sio wakazi wa (mji wa) Msikiti Mtukufu (wa Makka). Na mcheni Allah, na jueni kwamba, Allah ni mkali wa kuadhibu


1- - Kutimiza ibada hizo


2- - Bila kuunganisha Umra na Hija


Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 107

وَفَدَيۡنَٰهُ بِذِبۡحٍ عَظِيمٖ

Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu (mnyama wa kuchinja) mtukufu