وَإِذۡ أَخَذۡنَا مِيثَٰقَ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ لَا تَعۡبُدُونَ إِلَّا ٱللَّهَ وَبِٱلۡوَٰلِدَيۡنِ إِحۡسَانٗا وَذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡيَتَٰمَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينِ وَقُولُواْ لِلنَّاسِ حُسۡنٗا وَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتُواْ ٱلزَّكَوٰةَ ثُمَّ تَوَلَّيۡتُمۡ إِلَّا قَلِيلٗا مِّنكُمۡ وَأَنتُم مُّعۡرِضُونَ
Na (kumbukeni) Tulipochukua ahadi kwa Wana wa Israeli kwamba, hamtamuabudu yeyote Ila Allah tu, na mtawatendea wema wazazi, na ndugu na yatima na maskini, na mseme na watu kwa maneno mazuri. Na simamisheni Swala na toeni Zaka, kisha mkakengeuka isipokuwa wachache tu kati yenu, na ilhali nyinyi mnapuuza
۞لَّيۡسَ ٱلۡبِرَّ أَن تُوَلُّواْ وُجُوهَكُمۡ قِبَلَ ٱلۡمَشۡرِقِ وَٱلۡمَغۡرِبِ وَلَٰكِنَّ ٱلۡبِرَّ مَنۡ ءَامَنَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ وَٱلۡكِتَٰبِ وَٱلنَّبِيِّـۧنَ وَءَاتَى ٱلۡمَالَ عَلَىٰ حُبِّهِۦ ذَوِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡيَتَٰمَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينَ وَٱبۡنَ ٱلسَّبِيلِ وَٱلسَّآئِلِينَ وَفِي ٱلرِّقَابِ وَأَقَامَ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتَى ٱلزَّكَوٰةَ وَٱلۡمُوفُونَ بِعَهۡدِهِمۡ إِذَا عَٰهَدُواْۖ وَٱلصَّـٰبِرِينَ فِي ٱلۡبَأۡسَآءِ وَٱلضَّرَّآءِ وَحِينَ ٱلۡبَأۡسِۗ أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ صَدَقُواْۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُتَّقُونَ
Sio wema peke yake kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa mashariki na magharibi. Bali wema ni (wa) wanaomuamini Allah na Siku ya Mwisho na Malaika na Vitabu na Manabii, na wanatoa mali pamoja na kuwa wanaipenda wakawapa ndugu na mayatima na maskini na wasafiri na waombao na katika (kuwakomboa) watumwa, na wakawa wanasimamisha swala na kutoa zaka, na watekelezao ahadi zao wanapoahidi, na wavumiliao katika shida na madhara na (katika) wakati wa vita. Hao ndio wa kweli na hao ndio wa mchao Allah
كُتِبَ عَلَيۡكُمۡ إِذَا حَضَرَ أَحَدَكُمُ ٱلۡمَوۡتُ إِن تَرَكَ خَيۡرًا ٱلۡوَصِيَّةُ لِلۡوَٰلِدَيۡنِ وَٱلۡأَقۡرَبِينَ بِٱلۡمَعۡرُوفِۖ حَقًّا عَلَى ٱلۡمُتَّقِينَ
Mmeandikiwa mmoja wenu kutoa wasia kwa wazazi na ndugu kwa namna nzuri anapofikwa na mauti kama akiacha mali, ikiwa ni haki kwa wa mchao Allah
فَمَنۢ بَدَّلَهُۥ بَعۡدَ مَا سَمِعَهُۥ فَإِنَّمَآ إِثۡمُهُۥ عَلَى ٱلَّذِينَ يُبَدِّلُونَهُۥٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَمِيعٌ عَلِيمٞ
Na atakayeubadilisha wasia huo baada ya kuusikia, basi ilivyo ni kwamba dhambi yake ipo kwa wale watakaoubadilisha. Hakika, Allah ni Msikiaji mno[1], Mjuzi mno[2]
1- - Wa kauli ya mtoa wasia.
2- - Wa kitendo chake na atamlipa.
فَمَنۡ خَافَ مِن مُّوصٖ جَنَفًا أَوۡ إِثۡمٗا فَأَصۡلَحَ بَيۡنَهُمۡ فَلَآ إِثۡمَ عَلَيۡهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Na mwenye kuchelea kwa mtoa wasia kupotoka au dhambi akarekebisha baina yao, basi hatakuwa na dhambi. Hakika, Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu
يَسۡـَٔلُونَكَ مَاذَا يُنفِقُونَۖ قُلۡ مَآ أَنفَقۡتُم مِّنۡ خَيۡرٖ فَلِلۡوَٰلِدَيۡنِ وَٱلۡأَقۡرَبِينَ وَٱلۡيَتَٰمَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينِ وَٱبۡنِ ٱلسَّبِيلِۗ وَمَا تَفۡعَلُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِهِۦ عَلِيمٞ
Wanakuuliza: Watoe nini? Sema: Chochote cha heri mtakachotoa basi wapeni wazazi na ndugu na Mayatima na masikini na Msafiri na heri yoyote muifanyayo kwa hakika Allah anaijua mno
۞وَٱلۡوَٰلِدَٰتُ يُرۡضِعۡنَ أَوۡلَٰدَهُنَّ حَوۡلَيۡنِ كَامِلَيۡنِۖ لِمَنۡ أَرَادَ أَن يُتِمَّ ٱلرَّضَاعَةَۚ وَعَلَى ٱلۡمَوۡلُودِ لَهُۥ رِزۡقُهُنَّ وَكِسۡوَتُهُنَّ بِٱلۡمَعۡرُوفِۚ لَا تُكَلَّفُ نَفۡسٌ إِلَّا وُسۡعَهَاۚ لَا تُضَآرَّ وَٰلِدَةُۢ بِوَلَدِهَا وَلَا مَوۡلُودٞ لَّهُۥ بِوَلَدِهِۦۚ وَعَلَى ٱلۡوَارِثِ مِثۡلُ ذَٰلِكَۗ فَإِنۡ أَرَادَا فِصَالًا عَن تَرَاضٖ مِّنۡهُمَا وَتَشَاوُرٖ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡهِمَاۗ وَإِنۡ أَرَدتُّمۡ أَن تَسۡتَرۡضِعُوٓاْ أَوۡلَٰدَكُمۡ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ إِذَا سَلَّمۡتُم مَّآ ءَاتَيۡتُم بِٱلۡمَعۡرُوفِۗ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ
Na wazazi wanawake wan-yonyeshe watoto wao miaka miwili kamili, kwa anayetaka kutimiza kunyonyesha. Na ni juu ya baba chakula chao (mama na mtoto) na kivazi chao kwa wema. Nafsi haikalifishwi (kufanya jambo) isipokuwa lililo ndani ya uwezo wake tu. Mama asidhuriwe kwa sababu ya mwanawe, na baba asidhuriwe kwa sababu ya mwanawe. Na ni wajibu juu ya mrithi (wa mtoto kufanya hayo). Na si vibaya kwa wawili hao (baba na mama) wakitaka kumwachisha ziwa (mtoto chini ya miaka miwili) kwa kushauriana na kuridhiana. Na mkitaka kuwapatia watoto wenu mama wa kuwanyonyesha, basi hapana ubaya kwenu mkitoa kile mlichowapa kwa njia ya wema. Na mcheni Allah na jueni kwamba Allah ni mwenye kuyaona sana yote myatendayo
لِّلرِّجَالِ نَصِيبٞ مِّمَّا تَرَكَ ٱلۡوَٰلِدَانِ وَٱلۡأَقۡرَبُونَ وَلِلنِّسَآءِ نَصِيبٞ مِّمَّا تَرَكَ ٱلۡوَٰلِدَانِ وَٱلۡأَقۡرَبُونَ مِمَّا قَلَّ مِنۡهُ أَوۡ كَثُرَۚ نَصِيبٗا مَّفۡرُوضٗا
(Watoto) wanaume wana fungu kutokana na kile alichoacha (mmoja wa) wazazi wawili na ndugu wa karibu (pia wanafungu). Na wanawake wanafungu kutokana na alichoacha (mmoja wa) wazazi wawili na ndugu wa karibu (sawa) kiwe kingi au kichache ni fungu lililofaradhishwa
وَإِذَا حَضَرَ ٱلۡقِسۡمَةَ أُوْلُواْ ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡيَتَٰمَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينُ فَٱرۡزُقُوهُم مِّنۡهُ وَقُولُواْ لَهُمۡ قَوۡلٗا مَّعۡرُوفٗا
Na kama (katika kikao cha) kugawa watahudhuria ndugu na Yatima na masikini basi waruzukuni humo chochote, na waambieni kauli nzuri
وَلۡيَخۡشَ ٱلَّذِينَ لَوۡ تَرَكُواْ مِنۡ خَلۡفِهِمۡ ذُرِّيَّةٗ ضِعَٰفًا خَافُواْ عَلَيۡهِمۡ فَلۡيَتَّقُواْ ٱللَّهَ وَلۡيَقُولُواْ قَوۡلٗا سَدِيدًا
Na waogope wale ambao lau kuwa na wao wangeacha nyuma yao kizazi (watoto) wanyonge wakiwahofia (kudhulumiwa na kunyanyaswa), basi wamuogope Allah na waseme neno la kweli
إِنَّ ٱلَّذِينَ يَأۡكُلُونَ أَمۡوَٰلَ ٱلۡيَتَٰمَىٰ ظُلۡمًا إِنَّمَا يَأۡكُلُونَ فِي بُطُونِهِمۡ نَارٗاۖ وَسَيَصۡلَوۡنَ سَعِيرٗا
Hakika wale wanaokula mali za Yatima kwa dhulma kwa hakika wanakula moto (kutia) matumboni mwao na watauingia Motoni
يُوصِيكُمُ ٱللَّهُ فِيٓ أَوۡلَٰدِكُمۡۖ لِلذَّكَرِ مِثۡلُ حَظِّ ٱلۡأُنثَيَيۡنِۚ فَإِن كُنَّ نِسَآءٗ فَوۡقَ ٱثۡنَتَيۡنِ فَلَهُنَّ ثُلُثَا مَا تَرَكَۖ وَإِن كَانَتۡ وَٰحِدَةٗ فَلَهَا ٱلنِّصۡفُۚ وَلِأَبَوَيۡهِ لِكُلِّ وَٰحِدٖ مِّنۡهُمَا ٱلسُّدُسُ مِمَّا تَرَكَ إِن كَانَ لَهُۥ وَلَدٞۚ فَإِن لَّمۡ يَكُن لَّهُۥ وَلَدٞ وَوَرِثَهُۥٓ أَبَوَاهُ فَلِأُمِّهِ ٱلثُّلُثُۚ فَإِن كَانَ لَهُۥٓ إِخۡوَةٞ فَلِأُمِّهِ ٱلسُّدُسُۚ مِنۢ بَعۡدِ وَصِيَّةٖ يُوصِي بِهَآ أَوۡ دَيۡنٍۗ ءَابَآؤُكُمۡ وَأَبۡنَآؤُكُمۡ لَا تَدۡرُونَ أَيُّهُمۡ أَقۡرَبُ لَكُمۡ نَفۡعٗاۚ فَرِيضَةٗ مِّنَ ٱللَّهِۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمٗا
Allah anawapeni agizo kwa watoto wenu (kwamba); (mtoto) mwanaume fungu lake ni sawa na mafungu ya (watoto) wanawake wawili na kama watakuwa (watoto) wanawake zaidi ya wawili basi fungu lao ni thuluthi mbili ya alicho kiacha marehemu[1]. Ikiwa binti mmoja basi fungu lake ni nusu tu (ya mali). Na wazazi wake (marehemu baba na mama) kila mmoja wao apate sudusi ikiwa ameacha mtoto (pamoja na wazazi) na ikiwa hakuwacha mtoto akarithiwa na wazazi wawili tu basi mama yake atapata thuluthi na ikiwa (ameacha pamoja na wazazi) ndugu basi mama atapata sudusi, baada ya (kutekeleza) wasia (alioacha marehemu) au deni (analodaiwa). Baba zenu na mama zenu hamjui ni yupi kati yao mwenye maslahi yaliyo karibu mno na nyinyi huo ni uwajibu kutoka kwa Allah, hakika Allah ni mjuzi mno mwenye hekima nyingi
1- - Hapa Aya imeeleza kuwa fungu la watoto wanawake wakiwa zaidi ya wawili itakuwa theluthi mbili swali ni kwamba kama watakuwa wawili? Jibu ni kwamba theluthi mbili ni fungu la mabinti kuanzia wawili na kuendelea kutokana ijimai ya wanazuoni kuwa baada ya kutaja hilo akasema akiwa mmoja fungu lake nusu bila ya kutaja fungu la wawili hiyo inamaanisha kuwa wawili watapata theluthi mbili.
۞وَلَكُمۡ نِصۡفُ مَا تَرَكَ أَزۡوَٰجُكُمۡ إِن لَّمۡ يَكُن لَّهُنَّ وَلَدٞۚ فَإِن كَانَ لَهُنَّ وَلَدٞ فَلَكُمُ ٱلرُّبُعُ مِمَّا تَرَكۡنَۚ مِنۢ بَعۡدِ وَصِيَّةٖ يُوصِينَ بِهَآ أَوۡ دَيۡنٖۚ وَلَهُنَّ ٱلرُّبُعُ مِمَّا تَرَكۡتُمۡ إِن لَّمۡ يَكُن لَّكُمۡ وَلَدٞۚ فَإِن كَانَ لَكُمۡ وَلَدٞ فَلَهُنَّ ٱلثُّمُنُ مِمَّا تَرَكۡتُمۚ مِّنۢ بَعۡدِ وَصِيَّةٖ تُوصُونَ بِهَآ أَوۡ دَيۡنٖۗ وَإِن كَانَ رَجُلٞ يُورَثُ كَلَٰلَةً أَوِ ٱمۡرَأَةٞ وَلَهُۥٓ أَخٌ أَوۡ أُخۡتٞ فَلِكُلِّ وَٰحِدٖ مِّنۡهُمَا ٱلسُّدُسُۚ فَإِن كَانُوٓاْ أَكۡثَرَ مِن ذَٰلِكَ فَهُمۡ شُرَكَآءُ فِي ٱلثُّلُثِۚ مِنۢ بَعۡدِ وَصِيَّةٖ يُوصَىٰ بِهَآ أَوۡ دَيۡنٍ غَيۡرَ مُضَآرّٖۚ وَصِيَّةٗ مِّنَ ٱللَّهِۗ وَٱللَّهُ عَلِيمٌ حَلِيمٞ
Na nyinyi mna nusu ya kile walichoacha wake zenu kama hawakuwa na mtoto na kama wakiwa na mtoto, basi fungu lenu ni robo tu ya walichoacha baada ya kutekeleza wasia wanaoweka au deni. Na wake zenu wana robo ya mlicho kiacha ikiwa tu hamkuacha mtoto, na mkiwa na mtoto basi watapata thumni ya mlichokiacha baada ya kutekeleza wasia mnaoweka au deni. Na ikiwa mtu yeyote mwanaume au mwanamke atarithiwa na kaka yake au dada yake kwa kutoacha baba na mtoto, basi kila mmoja wao anafungu la sudusi, na kama watakuwa (ndugu) zaidi ya mmoja basi hao watashirikiana katika thuluthi[1] baada ya kutoa fungu la wasia uliowekwa au deni bila ya madhara. (hili) ni agizo kutoka kwa Allah na Allah ni Mjuzi sana Mpole mno
1- - Kaka na dada waliokusudiwa hapa ni wa upande wa mama kwa dalili kwamba kaka wa baba na mama au wa baba wanachukua kilichobaki baada ya watu wa mafungu na kama hakuna basi anachukua chote. Pia dada anarithi nusu ya mali hana fungu la theluthi, hivyo ni dhahiri hapa waliolengwa ni kaka au dada wa upande wa mama.
وَلِكُلّٖ جَعَلۡنَا مَوَٰلِيَ مِمَّا تَرَكَ ٱلۡوَٰلِدَانِ وَٱلۡأَقۡرَبُونَۚ وَٱلَّذِينَ عَقَدَتۡ أَيۡمَٰنُكُمۡ فَـَٔاتُوهُمۡ نَصِيبَهُمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدًا
Na kila mtu tumemuwekea warithi katika vile ambavyo vimeachwa na wazazi na ndugu. Na wale mliofunga nao mikataba ya viapo (kuwa mtakuwa ndugu) wapeni sehemu yao (ya mirathi)[1]. Hakika, Allah ni Shahidi wa kila kitu
1- - Aya hii inazungumzia udugu wa kupanga (udugu wa Yamini). Udugu huu ulikuwepo mwanzo wa Uislamu, na ndugu wa udugu huu walikuwa wakirithiana. Urithi huu ulifutwa na Aya 11 - 12 za Sura hii.
۞وَٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ وَلَا تُشۡرِكُواْ بِهِۦ شَيۡـٔٗاۖ وَبِٱلۡوَٰلِدَيۡنِ إِحۡسَٰنٗا وَبِذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡيَتَٰمَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينِ وَٱلۡجَارِ ذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡجَارِ ٱلۡجُنُبِ وَٱلصَّاحِبِ بِٱلۡجَنۢبِ وَٱبۡنِ ٱلسَّبِيلِ وَمَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُكُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ مَن كَانَ مُخۡتَالٗا فَخُورًا
Na mwabuduni Allah na msikishirikishe naye kitu chochote. Na wazazi wawili wafanyieni mazuri, na ndugu wa karibu (wa nasaba), na Yatima na maskini na jirani wa karibu (mwenye udugu wa nasaba) na jirani wa mbali (kwa makazi au udugu) na rafiki aliyeko ubavuni (rafiki mwenye usuhuba wa karibu na pia mke) na msafiri (aliyeharibikiwa) na wale walio chini ya mikono yenu ya kuume (watumwa waliopo chini ya miliki yenu). Hakika, Allah hawapendi wenye kiburi, wenye majivuno mengi
وَيَسۡتَفۡتُونَكَ فِي ٱلنِّسَآءِۖ قُلِ ٱللَّهُ يُفۡتِيكُمۡ فِيهِنَّ وَمَا يُتۡلَىٰ عَلَيۡكُمۡ فِي ٱلۡكِتَٰبِ فِي يَتَٰمَى ٱلنِّسَآءِ ٱلَّـٰتِي لَا تُؤۡتُونَهُنَّ مَا كُتِبَ لَهُنَّ وَتَرۡغَبُونَ أَن تَنكِحُوهُنَّ وَٱلۡمُسۡتَضۡعَفِينَ مِنَ ٱلۡوِلۡدَٰنِ وَأَن تَقُومُواْ لِلۡيَتَٰمَىٰ بِٱلۡقِسۡطِۚ وَمَا تَفۡعَلُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِهِۦ عَلِيمٗا
Na wanakuuliza Fat’wa[1] kuhusu wanawake. Sema: Allah anakupeni Fat`wa kuhusu wao na (kuhusu) yale yanayosomwa kwenu katika kitabu (hiki) kuhusu Yatima wanawake ambao hamuwapi kile kilicho wajibu kupewa na mnatamani kuwaoa, na (Fat’wa kuhusu) wale wanyonge miongoni mwa watoto na kwamba muwasimamie Yatima kwa uadilifu. Na kheri yoyote mnayoifanya basi hakika Allah anaijua sana
1- - Fat’wa katika Uislamu ni kutoa maelezo ya hukumu ya sheria, kwa maana ya kufafanua na sio kulazimisha. Anayefanya hivi anaitwa Mufti. Kadhi na Mufti wanatofautiana kwamba kazi ya Kadhi ni kutoa hukumu na kulazimisha utekelezwaji wa hukumu hiyo wakati kauli ya Mufti na ufafanuzi wa hukumu yake sio lazima kutekelezwa. Rejea kitabu cha Al-Ahkaamus Sultwaaniyyah cha Imamu Almaawardi, Allah amrehemu.
۞يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُونُواْ قَوَّـٰمِينَ بِٱلۡقِسۡطِ شُهَدَآءَ لِلَّهِ وَلَوۡ عَلَىٰٓ أَنفُسِكُمۡ أَوِ ٱلۡوَٰلِدَيۡنِ وَٱلۡأَقۡرَبِينَۚ إِن يَكُنۡ غَنِيًّا أَوۡ فَقِيرٗا فَٱللَّهُ أَوۡلَىٰ بِهِمَاۖ فَلَا تَتَّبِعُواْ ٱلۡهَوَىٰٓ أَن تَعۡدِلُواْۚ وَإِن تَلۡوُۥٓاْ أَوۡ تُعۡرِضُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٗا
Enyi mlioamini, kuweni wasimamishaji uadilifu, wenye kutoa ushahidi kwa ajili ya Allah hata kama (uadilifu na ushahidi huo) ni dhidi ya nafsi zenu au wazazi na ndugu wa karibu. Ikiwa (anayetakiwa kutolewa ushahidi) ni tajiri au fukara (msipindishe ushahidi kwasababu) Allah ni bora zaidi kwao (kuliko nyinyi[1] Basi msifuate matamanio ya nafsi zenu mkaacha kutenda uadilifu. Na kama mtapotosha (ushahidi) au mtapuuza (kwa kuacha kuutoa) basi ni hakika Allah anayajua yote mnayotenda
1- - . Allah anasisitiza kuwa yeye ndiye Muumba wa Tajiri na maskini na anataka haki itendeke kwa wote. Ushahidi utolewe bila ya kuangalia utajiri wa mtu au umaskini wake.
يَسۡتَفۡتُونَكَ قُلِ ٱللَّهُ يُفۡتِيكُمۡ فِي ٱلۡكَلَٰلَةِۚ إِنِ ٱمۡرُؤٌاْ هَلَكَ لَيۡسَ لَهُۥ وَلَدٞ وَلَهُۥٓ أُخۡتٞ فَلَهَا نِصۡفُ مَا تَرَكَۚ وَهُوَ يَرِثُهَآ إِن لَّمۡ يَكُن لَّهَا وَلَدٞۚ فَإِن كَانَتَا ٱثۡنَتَيۡنِ فَلَهُمَا ٱلثُّلُثَانِ مِمَّا تَرَكَۚ وَإِن كَانُوٓاْ إِخۡوَةٗ رِّجَالٗا وَنِسَآءٗ فَلِلذَّكَرِ مِثۡلُ حَظِّ ٱلۡأُنثَيَيۡنِۗ يُبَيِّنُ ٱللَّهُ لَكُمۡ أَن تَضِلُّواْۗ وَٱللَّهُ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمُۢ
Wanakutaka Fat’wa. Sema: Allah anakupeni Fat’wa kuhusu Kalala.[1] Ikiwa mtu aliyekufa hakuacha mtoto na amemuacha dada, basi huyo dada anastahiki kupata nusu ya mali aliyoacha. Na yeye atamrithi dada yake kama (dada naye) hakuacha mtoto. (Dada) Wakiwa wawili watapata thuluthi mbili katika mali aliyoacha (marehemu kaka yao). Na (warithi) wakiwa ndugu; wanaume na wanawake basi mwanaume mmoja anastahiki kupata fungu lililo sawa na la wanawake wawili. Allah anakubainishieni nyinyi (sheria zake) ili msipotee. Na Allah ni Mjuzi wa kila kitu
1- - Kalala ni mtu aliyekufa akiwa hakuacha mzazi wala mtoto.
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ شَهَٰدَةُ بَيۡنِكُمۡ إِذَا حَضَرَ أَحَدَكُمُ ٱلۡمَوۡتُ حِينَ ٱلۡوَصِيَّةِ ٱثۡنَانِ ذَوَا عَدۡلٖ مِّنكُمۡ أَوۡ ءَاخَرَانِ مِنۡ غَيۡرِكُمۡ إِنۡ أَنتُمۡ ضَرَبۡتُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَأَصَٰبَتۡكُم مُّصِيبَةُ ٱلۡمَوۡتِۚ تَحۡبِسُونَهُمَا مِنۢ بَعۡدِ ٱلصَّلَوٰةِ فَيُقۡسِمَانِ بِٱللَّهِ إِنِ ٱرۡتَبۡتُمۡ لَا نَشۡتَرِي بِهِۦ ثَمَنٗا وَلَوۡ كَانَ ذَا قُرۡبَىٰ وَلَا نَكۡتُمُ شَهَٰدَةَ ٱللَّهِ إِنَّآ إِذٗا لَّمِنَ ٱلۡأٓثِمِينَ
Enyi mlioamini, ushahidi wa baina yenu kinapomfikia mmoja wenu kifo wakati wa kuusia ni (mashahidi) wawili waadilifu miongoni mwenu au wawili wengine wasiokuwa katika nyinyi, mnapokuwa safarini na ukakusibuni msiba wa kifo. Mtawazuia wawili hao baada ya Swala. Waape kwa (jina la) Allah mkiwa na shaka (wakisema): Hatununui (hatupokei) thamani yoyote kwa haya (tunayoyatolea ushahidi) hata kama (tunaowatolea ushahidi dhidi yao) wakiwa ndugu wa nasaba, na hatufichi ushahidi wa Allah. Hakika, sisi tukifanya hivyo kwa yakini kabisa tutakuwa miongoni mwa wenye dhambi
۞قُلۡ تَعَالَوۡاْ أَتۡلُ مَا حَرَّمَ رَبُّكُمۡ عَلَيۡكُمۡۖ أَلَّا تُشۡرِكُواْ بِهِۦ شَيۡـٔٗاۖ وَبِٱلۡوَٰلِدَيۡنِ إِحۡسَٰنٗاۖ وَلَا تَقۡتُلُوٓاْ أَوۡلَٰدَكُم مِّنۡ إِمۡلَٰقٖ نَّحۡنُ نَرۡزُقُكُمۡ وَإِيَّاهُمۡۖ وَلَا تَقۡرَبُواْ ٱلۡفَوَٰحِشَ مَا ظَهَرَ مِنۡهَا وَمَا بَطَنَۖ وَلَا تَقۡتُلُواْ ٱلنَّفۡسَ ٱلَّتِي حَرَّمَ ٱللَّهُ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۚ ذَٰلِكُمۡ وَصَّىٰكُم بِهِۦ لَعَلَّكُمۡ تَعۡقِلُونَ
Sema: Njooni nisome yale Mola wenu aliyokuharamishieni (nayo ni) msikishirikishenaye kitu chochote na wazazi wawili wafanyieni yaliyo mazuri na msiwaue watoto wenu kwa sababu ya ufukara (umasikini kwa sababu) sisi tunakuruzukuni nyinyi na wao. Na msiyakaribie mambo machafu yaliyo dhihiri kati ya hayo na yaliyo ya siri. Na msiiue nafsi ambayo Allah ameharamisha (kuiua) ila kwa haki tu. Hayo amekuusieni (Allah) ili myatie akilini
وَلَا تَقۡرَبُواْ مَالَ ٱلۡيَتِيمِ إِلَّا بِٱلَّتِي هِيَ أَحۡسَنُ حَتَّىٰ يَبۡلُغَ أَشُدَّهُۥۚ وَأَوۡفُواْ ٱلۡكَيۡلَ وَٱلۡمِيزَانَ بِٱلۡقِسۡطِۖ لَا نُكَلِّفُ نَفۡسًا إِلَّا وُسۡعَهَاۖ وَإِذَا قُلۡتُمۡ فَٱعۡدِلُواْ وَلَوۡ كَانَ ذَا قُرۡبَىٰۖ وَبِعَهۡدِ ٱللَّهِ أَوۡفُواْۚ ذَٰلِكُمۡ وَصَّىٰكُم بِهِۦ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ
Na msizisogelee mali za Yatima ila kwa njia iliyo nzuri sana hadi afikie utu uzima wake. Na timizeni vipimo na mizani kwa uadilifu. Hatuilazimishi nafsi (jambo lolote) isipokuwa kwa kadiri ya vile iwezavyo. Na msemapo semeni kwa uadilifu hata ikiwa (ni dhidi ya) ndugu. Na ahadi za Allah zitekelezeni. Hayo amekuusieni (Allah) ili mpate kukumbuka
مَا كَانَ لِلنَّبِيِّ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَن يَسۡتَغۡفِرُواْ لِلۡمُشۡرِكِينَ وَلَوۡ كَانُوٓاْ أُوْلِي قُرۡبَىٰ مِنۢ بَعۡدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُمۡ أَنَّهُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَحِيمِ
Haiwi (haifai) kwa Nabii na wale walioamini kuwaombea msamaha washirikina (makafiri), na hata kama watakuwa ni jamaa zao wa karibu, baada ya kuwabainikia kuwa hao ni watu wa Motoni
وَمَا كَانَ ٱسۡتِغۡفَارُ إِبۡرَٰهِيمَ لِأَبِيهِ إِلَّا عَن مَّوۡعِدَةٖ وَعَدَهَآ إِيَّاهُ فَلَمَّا تَبَيَّنَ لَهُۥٓ أَنَّهُۥ عَدُوّٞ لِّلَّهِ تَبَرَّأَ مِنۡهُۚ إِنَّ إِبۡرَٰهِيمَ لَأَوَّـٰهٌ حَلِيمٞ
Na msamaha wa Ibrahimu wa kumuombea baba yake (kafiri) haukuwa isipokuwa tu ni kwa sababu ya ahadi aliyomuahidi.[1] Basi ilipombainikia kwamba yeye ni adui wa Allah (na ni mtu wa motoni), alijiepusha naye. Hakika kabisa, Ibrahimu alikuwa mnyenyekevu sana (katika maombi), mpole mno
1- - Allah ameitaja ahadi hii ya Nabii Ibrahimu kwa baba yake katika Qur’an, Sura Almumtahina (60), Aya ya 4 pale Allah aliposema: “Kwa hakika kabisa, mmekuwa na kiigizo kizuri kwa Ibrahimu na waliokuwa pamoja naye, walipowaambia watu wao: Kwa yakini sisi tumejitenga nanyi na hayo mnayoyaabudu badala ya Allah; tumewapingeni, naumedhihiri uadui na chuki ya kudumu (kati yetu na yenu) mpaka mmuamini Allah peke yake, isipokuwa kauli ya Ibrahimu kwa baba yake (aliyomuambia kwamba): Hakika, nitakuombea msamaha…”.
۞إِنَّ ٱللَّهَ يَأۡمُرُ بِٱلۡعَدۡلِ وَٱلۡإِحۡسَٰنِ وَإِيتَآيِٕ ذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَيَنۡهَىٰ عَنِ ٱلۡفَحۡشَآءِ وَٱلۡمُنكَرِ وَٱلۡبَغۡيِۚ يَعِظُكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ
Kwa hakika Allah anaamuru uadilifu, na ihsani, na kuwapa (sadaka) ndugu wa karibu na anakataza uchafu, na uovu, na uasi. Anawanasihini ili mpate kukumbuka
۞وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعۡبُدُوٓاْ إِلَّآ إِيَّاهُ وَبِٱلۡوَٰلِدَيۡنِ إِحۡسَٰنًاۚ إِمَّا يَبۡلُغَنَّ عِندَكَ ٱلۡكِبَرَ أَحَدُهُمَآ أَوۡ كِلَاهُمَا فَلَا تَقُل لَّهُمَآ أُفّٖ وَلَا تَنۡهَرۡهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوۡلٗا كَرِيمٗا
Na Mola wako Mlezi ameam-risha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu, na wazazi wawili muwa-tendee wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa heshima
وَٱخۡفِضۡ لَهُمَا جَنَاحَ ٱلذُّلِّ مِنَ ٱلرَّحۡمَةِ وَقُل رَّبِّ ٱرۡحَمۡهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرٗا
Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma. Na useme: Mola wangu Mlezi! Warehemu kama walivyo nilea utotoni
وَءَاتِ ذَا ٱلۡقُرۡبَىٰ حَقَّهُۥ وَٱلۡمِسۡكِينَ وَٱبۡنَ ٱلسَّبِيلِ وَلَا تُبَذِّرۡ تَبۡذِيرًا
Na mpe aliye jamaa yako haki yake, na masikini, na msafiri; wala usitumie ovyo kwa fujo
وَلَا تَقۡتُلُوٓاْ أَوۡلَٰدَكُمۡ خَشۡيَةَ إِمۡلَٰقٖۖ نَّحۡنُ نَرۡزُقُهُمۡ وَإِيَّاكُمۡۚ إِنَّ قَتۡلَهُمۡ كَانَ خِطۡـٔٗا كَبِيرٗا
Wala msiwauwe watoto wenu kwa kuogopa umasikini. Sisi tunawaruzuku wao na nyinyi. Hakika kuwaua hao ni hatia (kosa) kubwa sana
وَلَا يَأۡتَلِ أُوْلُواْ ٱلۡفَضۡلِ مِنكُمۡ وَٱلسَّعَةِ أَن يُؤۡتُوٓاْ أُوْلِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينَ وَٱلۡمُهَٰجِرِينَ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِۖ وَلۡيَعۡفُواْ وَلۡيَصۡفَحُوٓاْۗ أَلَا تُحِبُّونَ أَن يَغۡفِرَ ٱللَّهُ لَكُمۡۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٌ
Na wale katika nyinyi wenye fadhila na wasaa wasiape kutowapa jamaa zao na masikini na walio hama katika Njia ya Allah. Na wasamehe, na waachilie mbali. Je! Nyinyi hampendi Allah akusameheni? Na Allah ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu
وَوَصَّيۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ بِوَٰلِدَيۡهِ حُسۡنٗاۖ وَإِن جَٰهَدَاكَ لِتُشۡرِكَ بِي مَا لَيۡسَ لَكَ بِهِۦ عِلۡمٞ فَلَا تُطِعۡهُمَآۚ إِلَيَّ مَرۡجِعُكُمۡ فَأُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Na tumemuusia mwanaadamu kuwafanyia wema wazazi wake. Na ikiwa watakushikilia unishirikishe Mimi na usiyo kuwa na ujuzi nayo, basi usiwat’ii. Kwangu Mimi ndio marejeo yenu, na nitakwambieni mliyokuwa mkiyatenda