Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 73

وَإِلَىٰ ثَمُودَ أَخَاهُمۡ صَٰلِحٗاۚ قَالَ يَٰقَوۡمِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مَا لَكُم مِّنۡ إِلَٰهٍ غَيۡرُهُۥۖ قَدۡ جَآءَتۡكُم بَيِّنَةٞ مِّن رَّبِّكُمۡۖ هَٰذِهِۦ نَاقَةُ ٱللَّهِ لَكُمۡ ءَايَةٗۖ فَذَرُوهَا تَأۡكُلۡ فِيٓ أَرۡضِ ٱللَّهِۖ وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوٓءٖ فَيَأۡخُذَكُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Na (tulimtuma) kwa (kabila la) Thamudi ndugu yao Swalehe akasema: Enyi watu wangu, muabuduni Allah, hamna nyinyi Mola mwingine Mlezi zaidi yake. Hakika, umekufikieni ushahidi (muujiza unaothibitisha ukweli wangu) kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Huyu ni ngamia wa Allah akiwa ushahidi kwenu. Basi mwacheni ale katika ardhi ya Allah, na msimguse kwa ubaya wowote ikawa sababu ya kukuchukueni (kukupateni) adhabu iumizayo sana



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 74

وَٱذۡكُرُوٓاْ إِذۡ جَعَلَكُمۡ خُلَفَآءَ مِنۢ بَعۡدِ عَادٖ وَبَوَّأَكُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ تَتَّخِذُونَ مِن سُهُولِهَا قُصُورٗا وَتَنۡحِتُونَ ٱلۡجِبَالَ بُيُوتٗاۖ فَٱذۡكُرُوٓاْ ءَالَآءَ ٱللَّهِ وَلَا تَعۡثَوۡاْ فِي ٱلۡأَرۡضِ مُفۡسِدِينَ

Na kumbukeni wakati (Allah) alipokufanyeni makhalifa (warithi) baada ya (watu wa) Adi na akakuwekeni vizuri ardhini; mnajenga makasri (majumba ya kifahari) katika eneo lake la tambarare, na mnachonga majabali na kuyafanya majumba. Basi kumbukeni neema za Allah, na msifanye uovu ardhini (duniani)



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 75

قَالَ ٱلۡمَلَأُ ٱلَّذِينَ ٱسۡتَكۡبَرُواْ مِن قَوۡمِهِۦ لِلَّذِينَ ٱسۡتُضۡعِفُواْ لِمَنۡ ءَامَنَ مِنۡهُمۡ أَتَعۡلَمُونَ أَنَّ صَٰلِحٗا مُّرۡسَلٞ مِّن رَّبِّهِۦۚ قَالُوٓاْ إِنَّا بِمَآ أُرۡسِلَ بِهِۦ مُؤۡمِنُونَ

Mamwinyi walio onesha kiburi katika watuwake wali-sema kuwaambia waumini walionyanyaswa: Hivi mnajua kweli kuwa Swaleh ametumwa na Mola wake? Wakasema: Hakika, sisi tunayaamini yale aliyotumwa



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 76

قَالَ ٱلَّذِينَ ٱسۡتَكۡبَرُوٓاْ إِنَّا بِٱلَّذِيٓ ءَامَنتُم بِهِۦ كَٰفِرُونَ

Wale waliotakabari wakasema: Hakika, sisi ni wenye kuyapinga (hayo) mliyoyaamini



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 77

فَعَقَرُواْ ٱلنَّاقَةَ وَعَتَوۡاْ عَنۡ أَمۡرِ رَبِّهِمۡ وَقَالُواْ يَٰصَٰلِحُ ٱئۡتِنَا بِمَا تَعِدُنَآ إِن كُنتَ مِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Wakamchinja ngamia na wakaasi amri ya Mola wao na wakasema: Ewe Swaleh, haya tuletee (hayo) unayotuahidi kama wewe ni mion-goni mwa Mitume



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 78

فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلرَّجۡفَةُ فَأَصۡبَحُواْ فِي دَارِهِمۡ جَٰثِمِينَ

Basi likawachukua tetemeko (la ardhi) na wakawa wameangamia majumbani mwao huku wamepiga magoti



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 79

فَتَوَلَّىٰ عَنۡهُمۡ وَقَالَ يَٰقَوۡمِ لَقَدۡ أَبۡلَغۡتُكُمۡ رِسَالَةَ رَبِّي وَنَصَحۡتُ لَكُمۡ وَلَٰكِن لَّا تُحِبُّونَ ٱلنَّـٰصِحِينَ

Basi akaachana nao na kusema: Enyi watu zangu, kwa Yakini kabisa nimekufikishieni ujumbe wa Mola wangu Mlezi na nimekupeni nasaha na lakini hamuwapendi wenye kunasihi



Capítulo: HUUD 

Verso : 61

۞وَإِلَىٰ ثَمُودَ أَخَاهُمۡ صَٰلِحٗاۚ قَالَ يَٰقَوۡمِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مَا لَكُم مِّنۡ إِلَٰهٍ غَيۡرُهُۥۖ هُوَ أَنشَأَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِ وَٱسۡتَعۡمَرَكُمۡ فِيهَا فَٱسۡتَغۡفِرُوهُ ثُمَّ تُوبُوٓاْ إِلَيۡهِۚ إِنَّ رَبِّي قَرِيبٞ مُّجِيبٞ

Na kwa watu wa Thamudi (tulimtuma) ndugu yao Swaleh. (Swaleh) alisema: Enyi watu wangu, mwabuduni Allah; Hamna nyinyi Mungu mwingine zaidi yake. Yeye ndiye aliyeanza kukuumbeni (kwakumuumba Adamu) kutoka ardhini, na akawaimarisheni humo, basi muombeni msamaha Yeye, kisha rudini kwake. Hakika Mola wangu mlezi yupo karibu sana, mpokeaji (wa maombi ya waja)



Capítulo: HUUD 

Verso : 62

قَالُواْ يَٰصَٰلِحُ قَدۡ كُنتَ فِينَا مَرۡجُوّٗا قَبۡلَ هَٰذَآۖ أَتَنۡهَىٰنَآ أَن نَّعۡبُدَ مَا يَعۡبُدُ ءَابَآؤُنَا وَإِنَّنَا لَفِي شَكّٖ مِّمَّا تَدۡعُونَآ إِلَيۡهِ مُرِيبٖ

Wakasema: Ewe Swaleh! Hakika ulikuwa mtu unayetegemewa sana kwetu kabla ya haya, hivi unatukataza kuabudu walichokiabudu baba zetu? Na kwa hakika sisi tuna shaka na wasiwasi kwa hayo unayo tuitia



Capítulo: HUUD 

Verso : 63

قَالَ يَٰقَوۡمِ أَرَءَيۡتُمۡ إِن كُنتُ عَلَىٰ بَيِّنَةٖ مِّن رَّبِّي وَءَاتَىٰنِي مِنۡهُ رَحۡمَةٗ فَمَن يَنصُرُنِي مِنَ ٱللَّهِ إِنۡ عَصَيۡتُهُۥۖ فَمَا تَزِيدُونَنِي غَيۡرَ تَخۡسِيرٖ

(Swaleh) akasema: Enyi watu wangu! Mwaonaje kama ninayo dalili kutoka kwa Mola wangu mlezi? Na amenipa rehema kutoka kwake, basi ni nani atakayeninusuru kwa Allah endapo nitamuasi? Basi hamtanizidishia chochote isipokuwa kunitia hasara tu



Capítulo: HUUD 

Verso : 64

وَيَٰقَوۡمِ هَٰذِهِۦ نَاقَةُ ٱللَّهِ لَكُمۡ ءَايَةٗۖ فَذَرُوهَا تَأۡكُلۡ فِيٓ أَرۡضِ ٱللَّهِۖ وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوٓءٖ فَيَأۡخُذَكُمۡ عَذَابٞ قَرِيبٞ

Na enyi watu wangu, huyu ni ngamia wa Allah ni ishara kwenu, basi mwacheni ale katika ardhi ya Allah, na msimguse kwa ubaya isije kuwashikeni adhabu iliyo karibu mno



Capítulo: HUUD 

Verso : 65

فَعَقَرُوهَا فَقَالَ تَمَتَّعُواْ فِي دَارِكُمۡ ثَلَٰثَةَ أَيَّامٖۖ ذَٰلِكَ وَعۡدٌ غَيۡرُ مَكۡذُوبٖ

Basi walimchinja; Na (Swaleh) akasema, stareheni majumbani mwenu kwa siku tatu; hiyo ni ahadi isiyokadhibishwa



Capítulo: HUUD 

Verso : 66

فَلَمَّا جَآءَ أَمۡرُنَا نَجَّيۡنَا صَٰلِحٗا وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مَعَهُۥ بِرَحۡمَةٖ مِّنَّا وَمِنۡ خِزۡيِ يَوۡمِئِذٍۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ ٱلۡقَوِيُّ ٱلۡعَزِيزُ

Basi ilipokuja amri yetu tulimuokoa Swaleh na wale walio amini pamoja naye kwa rehema kutoka kwetu na kutokana na fedheha ya siku hiyo. Hakika Mola wako mlezi ndiye mwenye nguvu zaidi mwenye ushindi



Capítulo: HUUD 

Verso : 67

وَأَخَذَ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ ٱلصَّيۡحَةُ فَأَصۡبَحُواْ فِي دِيَٰرِهِمۡ جَٰثِمِينَ

Na ukelele ukawaangamiza wale waliodhulumu, na wakapambazukiwa wakiwa maiti ndani ya majumba yao



Capítulo: HUUD 

Verso : 68

كَأَن لَّمۡ يَغۡنَوۡاْ فِيهَآۗ أَلَآ إِنَّ ثَمُودَاْ كَفَرُواْ رَبَّهُمۡۗ أَلَا بُعۡدٗا لِّثَمُودَ

Kana kwamba hawakuwepo humo. Elewa! Hakika Thamud walimkufuru Mola wao mlezi. Eleweni! Maangamizi yawafike watu wa Thamudi



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 141

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Kina Thamud waliwakanusha Mitume



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 142

إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ صَٰلِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchi Allah?



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 143

إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 144

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Allah, na nitiini



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 145

وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 146

أَتُتۡرَكُونَ فِي مَا هَٰهُنَآ ءَامِنِينَ

Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 147

فِي جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٖ

Katika mabustani, na chemchem?



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 148

وَزُرُوعٖ وَنَخۡلٖ طَلۡعُهَا هَضِيمٞ

Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 149

وَتَنۡحِتُونَ مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتٗا فَٰرِهِينَ

Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 150

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Allah, na nitiini mimi



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 151

وَلَا تُطِيعُوٓاْ أَمۡرَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ

Wala msitii amri za walio pindukia mipaka,



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 152

ٱلَّذِينَ يُفۡسِدُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا يُصۡلِحُونَ

Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 153

قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلۡمُسَحَّرِينَ

Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 154

مَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا فَأۡتِ بِـَٔايَةٍ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ

Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 155

قَالَ هَٰذِهِۦ نَاقَةٞ لَّهَا شِرۡبٞ وَلَكُمۡ شِرۡبُ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ

Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu