Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 105

مَّا يَوَدُّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ وَلَا ٱلۡمُشۡرِكِينَ أَن يُنَزَّلَ عَلَيۡكُم مِّنۡ خَيۡرٖ مِّن رَّبِّكُمۡۚ وَٱللَّهُ يَخۡتَصُّ بِرَحۡمَتِهِۦ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ ذُو ٱلۡفَضۡلِ ٱلۡعَظِيمِ

Watu wa Kitabu waliokufuru na washirikishaji hawapendi mteremshiwe heri yoyote kutoka kwa Mola wenu. Na Allah humkusudia (kumpa) rehema zake amtakaye, na Allah ni Mwenye fadhila kubwa



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 122

يَٰبَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ ٱذۡكُرُواْ نِعۡمَتِيَ ٱلَّتِيٓ أَنۡعَمۡتُ عَلَيۡكُمۡ وَأَنِّي فَضَّلۡتُكُمۡ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ

Enyi Wana wa Israili, kum-bukeni neema zangu ambazo nime-kuneemesheni, na nimekufanyeni bora zaidi kuliko walimwengu (wa wakati wenu)



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 243

۞أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِينَ خَرَجُواْ مِن دِيَٰرِهِمۡ وَهُمۡ أُلُوفٌ حَذَرَ ٱلۡمَوۡتِ فَقَالَ لَهُمُ ٱللَّهُ مُوتُواْ ثُمَّ أَحۡيَٰهُمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَذُو فَضۡلٍ عَلَى ٱلنَّاسِ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَ ٱلنَّاسِ لَا يَشۡكُرُونَ

Hivi huwaoni wale waliotoka kwenye miji yao wakiwa maelfu wakiogopa kifo? Na Allah akawaambia kufeni, kisha akawahuisha. Hakika Allah ni mwenye fadhila kwa watu, lakini watu wengi sana hawashukuru



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 251

فَهَزَمُوهُم بِإِذۡنِ ٱللَّهِ وَقَتَلَ دَاوُۥدُ جَالُوتَ وَءَاتَىٰهُ ٱللَّهُ ٱلۡمُلۡكَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَعَلَّمَهُۥ مِمَّا يَشَآءُۗ وَلَوۡلَا دَفۡعُ ٱللَّهِ ٱلنَّاسَ بَعۡضَهُم بِبَعۡضٖ لَّفَسَدَتِ ٱلۡأَرۡضُ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ ذُو فَضۡلٍ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ

Basi waliwashinda kwa idhini ya Allah na Daudi akamuua Jaluti, na Allah akampa (Daudi) ufalme na utume na akamfundisha aliyoyataka. Na kama Allah asingewakinga watu baadhi yao kwa wengine, bila shaka ardhi ingeliharibika, lakini Allah ni Mwenye hisani kubwa mno kwa walimwengu



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 8

رَبَّنَا لَا تُزِغۡ قُلُوبَنَا بَعۡدَ إِذۡ هَدَيۡتَنَا وَهَبۡ لَنَا مِن لَّدُنكَ رَحۡمَةًۚ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡوَهَّابُ

Ewe Mola wetu, usiziache nyoyo zetu zipotee baada ya kuwa umetuongoza, na tunaomba rehema kwako. Hakika, wewe ni Mtoaji sana



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 73

وَلَا تُؤۡمِنُوٓاْ إِلَّا لِمَن تَبِعَ دِينَكُمۡ قُلۡ إِنَّ ٱلۡهُدَىٰ هُدَى ٱللَّهِ أَن يُؤۡتَىٰٓ أَحَدٞ مِّثۡلَ مَآ أُوتِيتُمۡ أَوۡ يُحَآجُّوكُمۡ عِندَ رَبِّكُمۡۗ قُلۡ إِنَّ ٱلۡفَضۡلَ بِيَدِ ٱللَّهِ يُؤۡتِيهِ مَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ وَٰسِعٌ عَلِيمٞ

Na msimuamini (yeyote) isipokuwa tu yule aliyefuata dini yenu Sema: Muongozo (sahihi) ni muongozo wa Allah tu, kwamba kuna yeyote atakayepewa mfano wa mlichopewa au atakuhojini kwacho mbele ya Mola wenu. Sema: Hakika, fadhila zote ziko mkononi mwa Allah, na Allah ni Mkunjufu, Mjuzi mno



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 74

يَخۡتَصُّ بِرَحۡمَتِهِۦ مَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ ذُو ٱلۡفَضۡلِ ٱلۡعَظِيمِ

Anamhusisha kwa (kumpa) rehema zake amtakaye, na Allah ni Mwenye fadhila kubwa



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 103

وَٱعۡتَصِمُواْ بِحَبۡلِ ٱللَّهِ جَمِيعٗا وَلَا تَفَرَّقُواْۚ وَٱذۡكُرُواْ نِعۡمَتَ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡ إِذۡ كُنتُمۡ أَعۡدَآءٗ فَأَلَّفَ بَيۡنَ قُلُوبِكُمۡ فَأَصۡبَحۡتُم بِنِعۡمَتِهِۦٓ إِخۡوَٰنٗا وَكُنتُمۡ عَلَىٰ شَفَا حُفۡرَةٖ مِّنَ ٱلنَّارِ فَأَنقَذَكُم مِّنۡهَاۗ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ ٱللَّهُ لَكُمۡ ءَايَٰتِهِۦ لَعَلَّكُمۡ تَهۡتَدُونَ

Na shikamaneni na kamba ya Allah na msifarakane, na kumbukeni neema za Allah kwenu; pale mlipokuwa maadui, akaziunganisha nyoyo zenu (na) kwa sababu hiyo mkawa ndugu kwa neema zake. Na mlikuwa katika ukingo wa shimo la Moto akakuokoeni humo. Kama hivyo Allah anazibainisha Aya zake kwenu ili mpate kuongoka



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 164

لَقَدۡ مَنَّ ٱللَّهُ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ إِذۡ بَعَثَ فِيهِمۡ رَسُولٗا مِّنۡ أَنفُسِهِمۡ يَتۡلُواْ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتِهِۦ وَيُزَكِّيهِمۡ وَيُعَلِّمُهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَإِن كَانُواْ مِن قَبۡلُ لَفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ

kwa hakika Allah amewaneemesha Waumini pale alipomtuma kwao Mtume anayetokana na wao wenyewe, anawasomea Aya zake, anawatakasa na anawafundisha kitabu na hekima japokuwa kabla ya hapo walikuwa katika uovu wa wazi



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 174

فَٱنقَلَبُواْ بِنِعۡمَةٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَفَضۡلٖ لَّمۡ يَمۡسَسۡهُمۡ سُوٓءٞ وَٱتَّبَعُواْ رِضۡوَٰنَ ٱللَّهِۗ وَٱللَّهُ ذُو فَضۡلٍ عَظِيمٍ

Basi wakarudi na neema za Allah na fadhila zake, hakuna baya lililowagusa, na wakafuata yanayomridhi Allah, na Allah ni mwenye fadhila kubwa mno



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 32

وَلَا تَتَمَنَّوۡاْ مَا فَضَّلَ ٱللَّهُ بِهِۦ بَعۡضَكُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖۚ لِّلرِّجَالِ نَصِيبٞ مِّمَّا ٱكۡتَسَبُواْۖ وَلِلنِّسَآءِ نَصِيبٞ مِّمَّا ٱكۡتَسَبۡنَۚ وَسۡـَٔلُواْ ٱللَّهَ مِن فَضۡلِهِۦٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٗا

Na msitamani (kwa husuda) vile ambavyo Allah amewazidishia baadhi yenu kuliko wengine (katika riziki na vipaji). Wanaume wana fungu katika vile walivyochuma na wanawake wana fungu katika vile walivyochuma. Na muombeni Allah (awape) katika fadhila zake. Hakika, Allah ni Mjuzi wa kila kitu



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 173

فَأَمَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ فَيُوَفِّيهِمۡ أُجُورَهُمۡ وَيَزِيدُهُم مِّن فَضۡلِهِۦۖ وَأَمَّا ٱلَّذِينَ ٱسۡتَنكَفُواْ وَٱسۡتَكۡبَرُواْ فَيُعَذِّبُهُمۡ عَذَابًا أَلِيمٗا وَلَا يَجِدُونَ لَهُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ وَلِيّٗا وَلَا نَصِيرٗا

Basi wale walioamini na kutenda mema (Allah) atawalipa ujira wao kamili na kuwaongozea fadhila zake. Na ama wale walioona kinyaa na kufanya kiburi, basi (Allah) atawaadhibu adhabu iumizayo sana, na hawatapata mlinzi wala wa kuwanusuru badala ya Allah



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 3

حُرِّمَتۡ عَلَيۡكُمُ ٱلۡمَيۡتَةُ وَٱلدَّمُ وَلَحۡمُ ٱلۡخِنزِيرِ وَمَآ أُهِلَّ لِغَيۡرِ ٱللَّهِ بِهِۦ وَٱلۡمُنۡخَنِقَةُ وَٱلۡمَوۡقُوذَةُ وَٱلۡمُتَرَدِّيَةُ وَٱلنَّطِيحَةُ وَمَآ أَكَلَ ٱلسَّبُعُ إِلَّا مَا ذَكَّيۡتُمۡ وَمَا ذُبِحَ عَلَى ٱلنُّصُبِ وَأَن تَسۡتَقۡسِمُواْ بِٱلۡأَزۡلَٰمِۚ ذَٰلِكُمۡ فِسۡقٌۗ ٱلۡيَوۡمَ يَئِسَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِن دِينِكُمۡ فَلَا تَخۡشَوۡهُمۡ وَٱخۡشَوۡنِۚ ٱلۡيَوۡمَ أَكۡمَلۡتُ لَكُمۡ دِينَكُمۡ وَأَتۡمَمۡتُ عَلَيۡكُمۡ نِعۡمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ ٱلۡإِسۡلَٰمَ دِينٗاۚ فَمَنِ ٱضۡطُرَّ فِي مَخۡمَصَةٍ غَيۡرَ مُتَجَانِفٖ لِّإِثۡمٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Mmeharamishiwa (kula) mzoga[1] na damu na nyama ya nguruwe na (mnyama) aliyechinjwa pasina (kutajwa jina la) Allah na (mnyama) aliyekufa kwa kusongeka koo (kujinyonga) na aliyekufa kwa kupigwa na aliyekufa kwa kuporomoka na aliyekufa kwa kupigwa pembe (na mwenzake) na aliyeliwa (kwa kushambuliwa) na mnyama mkali ila (mliyemuwahi akiwa hai) mkamchinja. Na (pia mmeharamishiwa kula nyama ya mnyama) aliyechinjwa katika (sehem yalipo) masanamu.[2] Na (mmeharamishiwa) kutaka kujua mambo yaliyopangwa (na Allah ikiwemo kupiga ramli na mfano wa hilo) kwa kutumia mbao. Ilivyo ni kwamba hayo (yote) ni uovu. Leo waliokufuru wameikatia tamaa dini yenu, basi msiwaogope (isipokuwa) niogopeni Mimi. Leo nimekukamilishieni dini yenu na kukutimizieni neema yangu na nimeuchagua Uislamu uwe dini yenu. Na mwenye kushikwa na dhiki ya njaa kali pasipo na kukusudia dhambi (anaruhusiwa kula hivyo vilivyoharamishwa kwa sababu) hakika, Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa huruma


1- - Mzoga ni mnyama aliyekufa mwenyewe au amechinjwa bila ya kufuata taratibu za sheria ya Kiislamu; kibudu, nyamafu.


2- - Mnyama aliyechinjwa katika sehemu za masanamu, mizimu, makaburini nk. Ni haramu kula nyama yake.


Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 6

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا قُمۡتُمۡ إِلَى ٱلصَّلَوٰةِ فَٱغۡسِلُواْ وُجُوهَكُمۡ وَأَيۡدِيَكُمۡ إِلَى ٱلۡمَرَافِقِ وَٱمۡسَحُواْ بِرُءُوسِكُمۡ وَأَرۡجُلَكُمۡ إِلَى ٱلۡكَعۡبَيۡنِۚ وَإِن كُنتُمۡ جُنُبٗا فَٱطَّهَّرُواْۚ وَإِن كُنتُم مَّرۡضَىٰٓ أَوۡ عَلَىٰ سَفَرٍ أَوۡ جَآءَ أَحَدٞ مِّنكُم مِّنَ ٱلۡغَآئِطِ أَوۡ لَٰمَسۡتُمُ ٱلنِّسَآءَ فَلَمۡ تَجِدُواْ مَآءٗ فَتَيَمَّمُواْ صَعِيدٗا طَيِّبٗا فَٱمۡسَحُواْ بِوُجُوهِكُمۡ وَأَيۡدِيكُم مِّنۡهُۚ مَا يُرِيدُ ٱللَّهُ لِيَجۡعَلَ عَلَيۡكُم مِّنۡ حَرَجٖ وَلَٰكِن يُرِيدُ لِيُطَهِّرَكُمۡ وَلِيُتِمَّ نِعۡمَتَهُۥ عَلَيۡكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ

Enyi mlioamini, mnaposimama kwenda kuswali[1], basi (tawadheni) osheni nyuso zenu na mikono yenu mpaka viwikoni na pakeni (maji) vichwa vyenu na (osheni) miguu yenu mpaka vifundoni[2]. Na mkiwa wenye Janaba basi jitwaharisheni (kwa kuoga au kutayamamu ikishindikana kuoga). Na mkiwa wagonjwa au mpo safarini au mmoja wenu ametoka msalani au mmegusana (mmejamiiana) na wanawake (wake zenu)[3] na hamkupata maji, basi tayamamuni (kusudieni) mchanga ulio safi[4] na mpake nyuso zenu na mikono yenu kwa mchanga huo[5]. Allah hataki kukuwekeeni tabu yoyote (uzito na usumbufu kwa kulazimisha kujitwaharisha kwa maji wakati maji hayapo au haiwezekani kuyatumia kwasababu ya ugonjwa au baridi kali); bali anataka kukutakaseni na kutimiza neema yake kwenu ili mpate kushukuru.[6]


1- - Hii ina maana hata kwa anayeswali kwa kuketi au kwa kulala ujumbe na utaratibu huu unamhusu pia.


2- - Kwenye Aya hii kuna visomo vikuu viwili vinavyokubalika: “Arjulakum” kwa Nasbu. Na kisomo cha pili ni “Arjulikum” kwa Jarri. Hii inamaanisha kwamba, kwa mujibu wa Qur’an na Suna sahihi za Mtume wa Allah uoshaji wa miguu una hukumu za aina mbili: (a) Kama miguu ikiwa wazi (haijavikwa kitu) faradhi yake ni kuoshwa kwa maji. (b) Kama miguu imevikwa khofu/soksi faradhi yake ni kupakwa maji.


3- - Muradi wa kugusana hapa ni kujamiiana. Kugusana tu kwa Ngozi na Ngozi hakulazimishi kutawadha.


4- - Kitendo hiki cha kutumia mchanga ulio safi na kupaka vumbi lake usoni na mikononi kinaitwa Tayamamu katika sheria ya Kiislamu.


5- - Kwa pigo la kwanza pakeni usoni na kwa pigo la pili pakeni mikononi.


6- - Aya hapa inaonesha kuwa ni lazima Muislamu kila anapotaka kuswali atawadhe. Lakini ulazima huu ni kwa yule ambaye hana Udhu. Ama mtu mwenye Udhu halazimiki kutawadha, lakini ni jambo zuri kama
atatawadha tena.


Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 54

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مَن يَرۡتَدَّ مِنكُمۡ عَن دِينِهِۦ فَسَوۡفَ يَأۡتِي ٱللَّهُ بِقَوۡمٖ يُحِبُّهُمۡ وَيُحِبُّونَهُۥٓ أَذِلَّةٍ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ أَعِزَّةٍ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ يُجَٰهِدُونَ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَلَا يَخَافُونَ لَوۡمَةَ لَآئِمٖۚ ذَٰلِكَ فَضۡلُ ٱللَّهِ يُؤۡتِيهِ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ وَٰسِعٌ عَلِيمٌ

Enyi mlioamini, yeyote ataka-yeritadi miongoni mwenu kwa kuiacha Dini yake (ya Uislamu), basi Allah ataleta watu anaowapenda nao wanampenda, wanyenyekevu mno kwa waumini (wenzao) na wenye nguvu sana mbele ya makafiri, wanapigania Jihadi katika Njia ya Allah, na hawaogopi lawama za mwenye kulaumu. Hizo ni fadhila za Allah humpa amtakaye. Na Allah ni Mkunjufu, Mwenye kujua sana



Capítulo: AN-FAL 

Verso : 53

ذَٰلِكَ بِأَنَّ ٱللَّهَ لَمۡ يَكُ مُغَيِّرٗا نِّعۡمَةً أَنۡعَمَهَا عَلَىٰ قَوۡمٍ حَتَّىٰ يُغَيِّرُواْ مَا بِأَنفُسِهِمۡ وَأَنَّ ٱللَّهَ سَمِيعٌ عَلِيمٞ

Hiyo (ada ya kuwaadhibu makafiri au kuchukua neema zake) ni kwasababu Allah habadilishi neema zozote alizo waneemesha watu, mpaka wao wabadilishe yaliyomo nafsini mwao. Na hakika Allah ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua



Capítulo: YUNUS 

Verso : 58

قُلۡ بِفَضۡلِ ٱللَّهِ وَبِرَحۡمَتِهِۦ فَبِذَٰلِكَ فَلۡيَفۡرَحُواْ هُوَ خَيۡرٞ مِّمَّا يَجۡمَعُونَ

Sema: Fadhila za Allah na rehema zake, basi wafurahie hayo. Hilo ni bora zaidi kwao kuliko wanavyovikusanya



Capítulo: YUNUS 

Verso : 60

وَمَا ظَنُّ ٱلَّذِينَ يَفۡتَرُونَ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۗ إِنَّ ٱللَّهَ لَذُو فَضۡلٍ عَلَى ٱلنَّاسِ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَشۡكُرُونَ

Na ni ipi dhana ya wanaomzushia Allah uongo Siku ya Kiyama? (Wanadhani hali yao itakuwaje siku hiyo?). Hakika kabisa, Allah ndiye mwenye fadhila kwa watu, na lakini wengi wao sana hawashukuru



Capítulo: YUNUS 

Verso : 107

وَإِن يَمۡسَسۡكَ ٱللَّهُ بِضُرّٖ فَلَا كَاشِفَ لَهُۥٓ إِلَّا هُوَۖ وَإِن يُرِدۡكَ بِخَيۡرٖ فَلَا رَآدَّ لِفَضۡلِهِۦۚ يُصِيبُ بِهِۦ مَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦۚ وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ

Na kama Allah atakugusisha madhara (yoyote), basi hakuna yeyote wa kuyaondoa isipokuwa yeye tu na akikutakia kheri, basi hakuna wa kurudisha (kuzuia) fadhila zake. (Allah) Anamlenga (anampa fadhila zake) amtakaye katika waja wake, na yeye tu ndiye Mwenye kusamehe, mwenye kurehemu



Capítulo: YUSUF 

Verso : 38

وَٱتَّبَعۡتُ مِلَّةَ ءَابَآءِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَۚ مَا كَانَ لَنَآ أَن نُّشۡرِكَ بِٱللَّهِ مِن شَيۡءٖۚ ذَٰلِكَ مِن فَضۡلِ ٱللَّهِ عَلَيۡنَا وَعَلَى ٱلنَّاسِ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَ ٱلنَّاسِ لَا يَشۡكُرُونَ

Na nilifuata mila (dini) ya Baba zangu, Ibrahim na Is-hak na Yakubu. Sisi hatukuwa na haki ya kumshirikisha Allah kwa chochote. Hayo ni katika fadhila za Allah kwetu na kwa watu (wengine) lakini watu wengi sana hawashukuru



Capítulo: IBRAHIM 

Verso : 34

وَءَاتَىٰكُم مِّن كُلِّ مَا سَأَلۡتُمُوهُۚ وَإِن تَعُدُّواْ نِعۡمَتَ ٱللَّهِ لَا تُحۡصُوهَآۗ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَظَلُومٞ كَفَّارٞ

Na akakupeni kila mlicho-muomba. Na mkizihesabu neema za Allah hamuwezi kuzidhibiti. Hakika mwanadamu ni dhalimu mkubwa, mwenye kuzikufuru sana neema



Capítulo: ANNAHLI 

Verso : 18

وَإِن تَعُدُّواْ نِعۡمَةَ ٱللَّهِ لَا تُحۡصُوهَآۗ إِنَّ ٱللَّهَ لَغَفُورٞ رَّحِيمٞ

Na kama mkihesabu neema za Allah (kwenu) hamtaweza kuzidhibiti. Hakika Allah ni msamehevu sana mwenye rehema



Capítulo: ANNAHLI 

Verso : 53

وَمَا بِكُم مِّن نِّعۡمَةٖ فَمِنَ ٱللَّهِۖ ثُمَّ إِذَا مَسَّكُمُ ٱلضُّرُّ فَإِلَيۡهِ تَجۡـَٔرُونَ

Na neema yeyote mliyonayo imetoka kwa Allah. Kisha inapowaguseni dhara, basi yeye tu mnamlilia



Capítulo: ANNAHLI 

Verso : 81

وَٱللَّهُ جَعَلَ لَكُم مِّمَّا خَلَقَ ظِلَٰلٗا وَجَعَلَ لَكُم مِّنَ ٱلۡجِبَالِ أَكۡنَٰنٗا وَجَعَلَ لَكُمۡ سَرَٰبِيلَ تَقِيكُمُ ٱلۡحَرَّ وَسَرَٰبِيلَ تَقِيكُم بَأۡسَكُمۡۚ كَذَٰلِكَ يُتِمُّ نِعۡمَتَهُۥ عَلَيۡكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تُسۡلِمُونَ

Na Allah amewafanyieni katika vile alivyoviumba, vitiavyo kivuli (kama miti na milima) na amewafanyieni milima kuwa sehemu ya kukimbilia, na amewafanyieni kanzu zinazowakingeni na joto, na dereya[1] zinazowakingeni katika vita vyenu. Hivi ndivyo (Allah) anatimiza neema zake kwenu ili mpate kutii


1- - Ni vazi la chuma linalovaliwa vitani kujikinga na mikuki na silaha zote (proof)


Capítulo: ANNAHLI 

Verso : 83

يَعۡرِفُونَ نِعۡمَتَ ٱللَّهِ ثُمَّ يُنكِرُونَهَا وَأَكۡثَرُهُمُ ٱلۡكَٰفِرُونَ

Wanazijua neema za Allah kisha wanazipinga na wengi wao ni makafiri



Capítulo: ANNAHLI 

Verso : 114

فَكُلُواْ مِمَّا رَزَقَكُمُ ٱللَّهُ حَلَٰلٗا طَيِّبٗا وَٱشۡكُرُواْ نِعۡمَتَ ٱللَّهِ إِن كُنتُمۡ إِيَّاهُ تَعۡبُدُونَ

Na kuleni katika vile alivyo-waruzukuni Allah, vilivyo halali na vizuri na shukuruni neema za Allah ikiwa nyinyi mnamuabudu yeye tu



Capítulo: AL-ISRAA 

Verso : 12

وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ وَٱلنَّهَارَ ءَايَتَيۡنِۖ فَمَحَوۡنَآ ءَايَةَ ٱلَّيۡلِ وَجَعَلۡنَآ ءَايَةَ ٱلنَّهَارِ مُبۡصِرَةٗ لِّتَبۡتَغُواْ فَضۡلٗا مِّن رَّبِّكُمۡ وَلِتَعۡلَمُواْ عَدَدَ ٱلسِّنِينَ وَٱلۡحِسَابَۚ وَكُلَّ شَيۡءٖ فَصَّلۡنَٰهُ تَفۡصِيلٗا

Na tumefanya usiku na mchana kuwa ishara mbili. Tena tukaifuta ishara ya usiku, na tukaifanya ishara ya mchana ni yenye mwangaza ili mtafute fadhila itokayo kwa Mola wenu Mlezi, na mpate kujua idadi ya miaka na hesabu. Na kila kitu tumekifafanua waziwazi



Capítulo: AL-ISRAA 

Verso : 20

كُلّٗا نُّمِدُّ هَـٰٓؤُلَآءِ وَهَـٰٓؤُلَآءِ مِنۡ عَطَآءِ رَبِّكَۚ وَمَا كَانَ عَطَآءُ رَبِّكَ مَحۡظُورًا

Wote hao tunawakunjulia - hawa na hao - katika neema za Mola wako Mlezi. Wala neema za Mola wako Mlezi hazizuiliki



Capítulo: AL-ISRAA 

Verso : 66

رَّبُّكُمُ ٱلَّذِي يُزۡجِي لَكُمُ ٱلۡفُلۡكَ فِي ٱلۡبَحۡرِ لِتَبۡتَغُواْ مِن فَضۡلِهِۦٓۚ إِنَّهُۥ كَانَ بِكُمۡ رَحِيمٗا

Mola wenu Mlezi ndiye anaye kuendesheeni marikebu katika bahari ili mtafute katika fadhila zake. Hakika Yeye ni Mwenye kukurehemuni nyinyi



Capítulo: AL-ISRAA 

Verso : 70

۞وَلَقَدۡ كَرَّمۡنَا بَنِيٓ ءَادَمَ وَحَمَلۡنَٰهُمۡ فِي ٱلۡبَرِّ وَٱلۡبَحۡرِ وَرَزَقۡنَٰهُم مِّنَ ٱلطَّيِّبَٰتِ وَفَضَّلۡنَٰهُمۡ عَلَىٰ كَثِيرٖ مِّمَّنۡ خَلَقۡنَا تَفۡضِيلٗا

Na hakika tumewatukuza wanaadamu, na tumewapa vya kupanda nchi kavu na baharini, na tumewaruzuku vitu vizuri vizuri, na tumewafadhilisha kwa fadhila kubwa kuliko wengi miongoni mwa tulio waumba