Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 109

وَدَّ كَثِيرٞ مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ لَوۡ يَرُدُّونَكُم مِّنۢ بَعۡدِ إِيمَٰنِكُمۡ كُفَّارًا حَسَدٗا مِّنۡ عِندِ أَنفُسِهِم مِّنۢ بَعۡدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُمُ ٱلۡحَقُّۖ فَٱعۡفُواْ وَٱصۡفَحُواْ حَتَّىٰ يَأۡتِيَ ٱللَّهُ بِأَمۡرِهِۦٓۗ إِنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ

Watu wa Kitabu wengi wanapenda laiti wakurudisheni muwe makafiri baada ya kuamini kwenu, kwa sababu ya husuda iliyomo nyoyoni mwao baada ya kuwa haki imewapambanukia. Basi sameheni na puuzeni mpaka Allah alete amri yake. Hakika, Allah ni Muweza sana wa kila jambo



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 111

وَقَالُواْ لَن يَدۡخُلَ ٱلۡجَنَّةَ إِلَّا مَن كَانَ هُودًا أَوۡ نَصَٰرَىٰۗ تِلۡكَ أَمَانِيُّهُمۡۗ قُلۡ هَاتُواْ بُرۡهَٰنَكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Na wamesema: Katu, hataingia Peponi isipokuwa tu Myahudi au Mnaswara! Hayo ndio matamanio yao. Sema: Leteni ushahidi wenu kama ninyi ni wa kweli



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 113

وَقَالَتِ ٱلۡيَهُودُ لَيۡسَتِ ٱلنَّصَٰرَىٰ عَلَىٰ شَيۡءٖ وَقَالَتِ ٱلنَّصَٰرَىٰ لَيۡسَتِ ٱلۡيَهُودُ عَلَىٰ شَيۡءٖ وَهُمۡ يَتۡلُونَ ٱلۡكِتَٰبَۗ كَذَٰلِكَ قَالَ ٱلَّذِينَ لَا يَعۡلَمُونَ مِثۡلَ قَوۡلِهِمۡۚ فَٱللَّهُ يَحۡكُمُ بَيۡنَهُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ فِيمَا كَانُواْ فِيهِ يَخۡتَلِفُونَ

Na Wayahudi wamesema: Manaswara hawa na kitu (chochote cha maana). Na Manaswara wame-sema: Wayahudi hawana kitu (chochote cha maana), na wao (wote) wanasoma Kitabu (kitakatifu kitokacho kwa Mola wao). Kama hivyo, wale ambao hawajui kitu wamesema mfano wa maneno yao. Basi Allah atahukumu baina yao Siku ya Kiyama katika yale waliyokuwa wakitafautiana



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 120

وَلَن تَرۡضَىٰ عَنكَ ٱلۡيَهُودُ وَلَا ٱلنَّصَٰرَىٰ حَتَّىٰ تَتَّبِعَ مِلَّتَهُمۡۗ قُلۡ إِنَّ هُدَى ٱللَّهِ هُوَ ٱلۡهُدَىٰۗ وَلَئِنِ ٱتَّبَعۡتَ أَهۡوَآءَهُم بَعۡدَ ٱلَّذِي جَآءَكَ مِنَ ٱلۡعِلۡمِ مَا لَكَ مِنَ ٱللَّهِ مِن وَلِيّٖ وَلَا نَصِيرٍ

Na kamwe hawatakuridhia Wayahudi na Wanaswara hadi utakapoifuata dini yao. Sema: Muongozo wa Allah ndio muongozo. Na ikiwa utafuata matamanio yao baada ya elimu iliyo kujia, basi hutampata yeyote wa kukutetea wala wa kukunusuru zaidi ya Allah



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 146

ٱلَّذِينَ ءَاتَيۡنَٰهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ يَعۡرِفُونَهُۥ كَمَا يَعۡرِفُونَ أَبۡنَآءَهُمۡۖ وَإِنَّ فَرِيقٗا مِّنۡهُمۡ لَيَكۡتُمُونَ ٱلۡحَقَّ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ

Na wale tuliowapa kitabu wanayajua hayo[1], kama wana-vyowajua watoto wao. Lakini kundi katika wao wanaificha haki ilhali wanajua


1- - Ya kuwa Muhammad ni Mtume wa kweli na Kaaba ndio kibla sahihi cha Waislamu


Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 19

إِنَّ ٱلدِّينَ عِندَ ٱللَّهِ ٱلۡإِسۡلَٰمُۗ وَمَا ٱخۡتَلَفَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَهُمُ ٱلۡعِلۡمُ بَغۡيَۢا بَيۡنَهُمۡۗ وَمَن يَكۡفُرۡ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ فَإِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ

Hakika, dini (inayokubalika) kwa Allah ni Uislamu tu. Na wale waliopewa Kitabu hawakutofautiana isipokuwa tu baada ya kuwa elimu imewafikia kwa sababu ya uovu uliokuwepo kati yao. Na yeyote anayezikataa Aya za Allah, basi hakika Allah ni Mwepesi mno wa kuhesabu



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 20

فَإِنۡ حَآجُّوكَ فَقُلۡ أَسۡلَمۡتُ وَجۡهِيَ لِلَّهِ وَمَنِ ٱتَّبَعَنِۗ وَقُل لِّلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡأُمِّيِّـۧنَ ءَأَسۡلَمۡتُمۡۚ فَإِنۡ أَسۡلَمُواْ فَقَدِ ٱهۡتَدَواْۖ وَّإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّمَا عَلَيۡكَ ٱلۡبَلَٰغُۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِٱلۡعِبَادِ

Na kama watakuletea hoja (yoyote), basi sema: Nimeukabidhi uso wangu (nimejisalimisha) kwa Allah; mimi na wale walionifuata. Na waambie waliopewa kitabu na wasio na elimu kwamba: Je, mmesilimu (Mmejisalimisha kwa Allah)? Kama wamesilimu basi hakika wameongoka, na kama wakikataa, basi wajibu wako ni kufikisha tu. Na Allah anawaona mno waja



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 64

قُلۡ يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ تَعَالَوۡاْ إِلَىٰ كَلِمَةٖ سَوَآءِۭ بَيۡنَنَا وَبَيۡنَكُمۡ أَلَّا نَعۡبُدَ إِلَّا ٱللَّهَ وَلَا نُشۡرِكَ بِهِۦ شَيۡـٔٗا وَلَا يَتَّخِذَ بَعۡضُنَا بَعۡضًا أَرۡبَابٗا مِّن دُونِ ٱللَّهِۚ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَقُولُواْ ٱشۡهَدُواْ بِأَنَّا مُسۡلِمُونَ

Sema: Enyi Watu wa Kitabu: Njooni kwenye neno la sawa kati yetu na kati yenu ya kuwa, tusimuabudu isipokuwa Allah tu, wala tusimshirikishe na chochote, na tusiwafanye baadhi yetu Miungu badala ya Allah. Na kama watapuuza, basi semeni (muwaambie): Shuhudieni kuwa sisi ni Waislamu



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 65

يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لِمَ تُحَآجُّونَ فِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَمَآ أُنزِلَتِ ٱلتَّوۡرَىٰةُ وَٱلۡإِنجِيلُ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِهِۦٓۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Enyi Watu wa Kitabu, kwanini mnaleta mijadala kuhusu Ibrahimu na ilhali Taurati na Injili hazikuteremshwa isipokuwa baada yake? Hivi hamtumii akili?



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 66

هَـٰٓأَنتُمۡ هَـٰٓؤُلَآءِ حَٰجَجۡتُمۡ فِيمَا لَكُم بِهِۦ عِلۡمٞ فَلِمَ تُحَآجُّونَ فِيمَا لَيۡسَ لَكُم بِهِۦ عِلۡمٞۚ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ وَأَنتُمۡ لَا تَعۡلَمُونَ

E nyinyi hawa! Mlihoji yale mnayoyajua, basi kwanini mnahoji msiyoyajua? Na Allah anajua na nyinyi hamjui



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 69

وَدَّت طَّآئِفَةٞ مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ لَوۡ يُضِلُّونَكُمۡ وَمَا يُضِلُّونَ إِلَّآ أَنفُسَهُمۡ وَمَا يَشۡعُرُونَ

Kundi katika Watu wa Kitabu limetamani kukupotezeni, na hawatampoteza (yeyote) isipokuwa wao wenyewe tu na ilhali hawatambui



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 70

يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لِمَ تَكۡفُرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَأَنتُمۡ تَشۡهَدُونَ

Enyi Watu wa Kitabu, kwanini mnazipinga Aya za Allah ilhali mnashuhudia?



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 71

يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لِمَ تَلۡبِسُونَ ٱلۡحَقَّ بِٱلۡبَٰطِلِ وَتَكۡتُمُونَ ٱلۡحَقَّ وَأَنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Enyi Watu wa Kitabu, kwanini mnachanganya haki na batili na mnaificha haki na ilhali nyinyi mnajua (kuwa mnachofanya sio sahihi)?



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 72

وَقَالَت طَّآئِفَةٞ مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ ءَامِنُواْ بِٱلَّذِيٓ أُنزِلَ عَلَى ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَجۡهَ ٱلنَّهَارِ وَٱكۡفُرُوٓاْ ءَاخِرَهُۥ لَعَلَّهُمۡ يَرۡجِعُونَ

Na kundi katika Watu wa Kitabu lilisema: Aminini mwanzo wa mchana (asubuhi) kile kilichoteremshwa kwa wale walioamini na kikataeni mwisho wake (jioni), huenda watarudi (nyuma)



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 73

وَلَا تُؤۡمِنُوٓاْ إِلَّا لِمَن تَبِعَ دِينَكُمۡ قُلۡ إِنَّ ٱلۡهُدَىٰ هُدَى ٱللَّهِ أَن يُؤۡتَىٰٓ أَحَدٞ مِّثۡلَ مَآ أُوتِيتُمۡ أَوۡ يُحَآجُّوكُمۡ عِندَ رَبِّكُمۡۗ قُلۡ إِنَّ ٱلۡفَضۡلَ بِيَدِ ٱللَّهِ يُؤۡتِيهِ مَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ وَٰسِعٌ عَلِيمٞ

Na msimuamini (yeyote) isipokuwa tu yule aliyefuata dini yenu Sema: Muongozo (sahihi) ni muongozo wa Allah tu, kwamba kuna yeyote atakayepewa mfano wa mlichopewa au atakuhojini kwacho mbele ya Mola wenu. Sema: Hakika, fadhila zote ziko mkononi mwa Allah, na Allah ni Mkunjufu, Mjuzi mno



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 74

يَخۡتَصُّ بِرَحۡمَتِهِۦ مَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ ذُو ٱلۡفَضۡلِ ٱلۡعَظِيمِ

Anamhusisha kwa (kumpa) rehema zake amtakaye, na Allah ni Mwenye fadhila kubwa



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 75

۞وَمِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ مَنۡ إِن تَأۡمَنۡهُ بِقِنطَارٖ يُؤَدِّهِۦٓ إِلَيۡكَ وَمِنۡهُم مَّنۡ إِن تَأۡمَنۡهُ بِدِينَارٖ لَّا يُؤَدِّهِۦٓ إِلَيۡكَ إِلَّا مَا دُمۡتَ عَلَيۡهِ قَآئِمٗاۗ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ قَالُواْ لَيۡسَ عَلَيۡنَا فِي ٱلۡأُمِّيِّـۧنَ سَبِيلٞ وَيَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ

Na miongini mwa Watu wa Kitabu wapo ambao endapo utamuamini (ukaweka kwake amana ya) mali nyingi, atakutekelezea (kwa kukurejeshea). Na miongoni mwao wapo ambao ukimuamini kwa dinari moja tu, haitekelezi (hairejeshi) isipokuwa tu kwa kumsimamia (kumdai na kumfuatilia). Hilo ni kwa sababu walisema: Hakuna lawama kwetu kwa (tunachowafanyia) Umiyina (wasiojuwa kuandika wala kusoma kilichoandikwa)[1] na wanamzulia Allah uongo ilhali wanajua


1- - Wanaokusudiwa hapa ni Waislamu Waarabu ambao kwa wakati huo hawakuwa wanajua kuandika wala
kusoma kilichoandikwa. Ni aina fulani ya dharau, ubaguzi, kejeli na udhalilishaji wa Wayahudi dhidi ya
jamii ya Waislamu; sifa ambazo Wayahudi na washirika wao wanaziendeleza hadi leo.


Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 78

وَإِنَّ مِنۡهُمۡ لَفَرِيقٗا يَلۡوُۥنَ أَلۡسِنَتَهُم بِٱلۡكِتَٰبِ لِتَحۡسَبُوهُ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ وَمَا هُوَ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ وَيَقُولُونَ هُوَ مِنۡ عِندِ ٱللَّهِ وَمَا هُوَ مِنۡ عِندِ ٱللَّهِۖ وَيَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ

Na kwa hakika kabisa, miongoni mwao lipo kundi linalopindisha ndimi zao kwenye kitabu (cha Taurati) ili mdhani hayo (wayapindishayo) yanatoka kitabuni, na (ukweli) si sehemu ya kitabu. Na wanasema: Hayo yanatoka kwa Allah na kamwe hayatoki kwa Allah, na wanamzulia Allah uongo huku wakijua



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 98

قُلۡ يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لِمَ تَكۡفُرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَٱللَّهُ شَهِيدٌ عَلَىٰ مَا تَعۡمَلُونَ

Sema: Enyi Watu wa Kitabu, kwanini mnazikanusha Aya za Allah na ilhali Allah ni Shuhuda wa mnayoyatenda?



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 99

قُلۡ يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لِمَ تَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ مَنۡ ءَامَنَ تَبۡغُونَهَا عِوَجٗا وَأَنتُمۡ شُهَدَآءُۗ وَمَا ٱللَّهُ بِغَٰفِلٍ عَمَّا تَعۡمَلُونَ

Sema: Enyi Watu wa Kitabu, kwanini mnawazuia katika njia ya Allah wale ambao wameamini, mkiitafutia kasoro (njia hiyo) na ilhali nyinyi ni mashuhuda (kwamba njia hiyo haina kasoro yoyote)? Na Allah si mwenye kuyaghafilika (si Mwenye kuyapuuza) yote mnayoyatenda



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 100

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِن تُطِيعُواْ فَرِيقٗا مِّنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ يَرُدُّوكُم بَعۡدَ إِيمَٰنِكُمۡ كَٰفِرِينَ

Enyi ambao mmeamini, kama mtalitii kundi katika wale waliopewa Kitabu watakurudisheni muwe makafiri baada ya kuamini kwenu



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 113

۞لَيۡسُواْ سَوَآءٗۗ مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ أُمَّةٞ قَآئِمَةٞ يَتۡلُونَ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ ءَانَآءَ ٱلَّيۡلِ وَهُمۡ يَسۡجُدُونَ

Watu wa Kitabu hawalingani (katika uovu). Miongoni mwa Watu wa Kitabu lipo kundi lililosimama imara (katika haki) wanasoma Aya za Allah nyakati za usiku na wanasujudu



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 114

يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَيَأۡمُرُونَ بِٱلۡمَعۡرُوفِ وَيَنۡهَوۡنَ عَنِ ٱلۡمُنكَرِ وَيُسَٰرِعُونَ فِي ٱلۡخَيۡرَٰتِۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Wanamuamini Allah na Siku ya Mwisho na wanaamrisha mema na kukataza maovu na wanayaendea haraka mambo ya kheri, na hao ni katika watu wema



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 115

وَمَا يَفۡعَلُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَلَن يُكۡفَرُوهُۗ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِٱلۡمُتَّقِينَ

Na chochote cha kheri wanachokifanya hawatonyimwa malipo yake, na Allah anawajua mno wamchao (Yeye)



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 187

وَإِذۡ أَخَذَ ٱللَّهُ مِيثَٰقَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ لَتُبَيِّنُنَّهُۥ لِلنَّاسِ وَلَا تَكۡتُمُونَهُۥ فَنَبَذُوهُ وَرَآءَ ظُهُورِهِمۡ وَٱشۡتَرَوۡاْ بِهِۦ ثَمَنٗا قَلِيلٗاۖ فَبِئۡسَ مَا يَشۡتَرُونَ

Na kumbuka pale Allah alipochukua ahadi nzito, kwa ambao wamepewa kitabu kuwa lazima mtakibainisha kwa watu na hamtakificha, wakaitupa ahadi hiyo nyuma ya migongo yao, wakiuza ahadi kwa thamani ndogo, basi biashara mbaya ni hiyo waliyoifanya



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 199

وَإِنَّ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ لَمَن يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكُمۡ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡهِمۡ خَٰشِعِينَ لِلَّهِ لَا يَشۡتَرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ ثَمَنٗا قَلِيلًاۚ أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ

Na kwa hakika katika Watu wa kitabu wapo wanaomuamini Allah hasa na kilichoteremshwa kwenu na kilichoteremshwa kwao, huku wakinyenyekea kwa Allah. Hawauzi Aya za Allah kwa thamani ndogo (ya dunia). Hao malipo yao yako kwa Mola wao mlezi, hakika Allah ni mwepesi mno wa kuhesabu



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 153

يَسۡـَٔلُكَ أَهۡلُ ٱلۡكِتَٰبِ أَن تُنَزِّلَ عَلَيۡهِمۡ كِتَٰبٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِۚ فَقَدۡ سَأَلُواْ مُوسَىٰٓ أَكۡبَرَ مِن ذَٰلِكَ فَقَالُوٓاْ أَرِنَا ٱللَّهَ جَهۡرَةٗ فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّـٰعِقَةُ بِظُلۡمِهِمۡۚ ثُمَّ ٱتَّخَذُواْ ٱلۡعِجۡلَ مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَتۡهُمُ ٱلۡبَيِّنَٰتُ فَعَفَوۡنَا عَن ذَٰلِكَۚ وَءَاتَيۡنَا مُوسَىٰ سُلۡطَٰنٗا مُّبِينٗا

Watu wa Kitabu wanakutaka (kwa inadi) uwateremshie kitabu kutoka mbinguni. Kwa hakika walimtaka (Mtume) Mussa (kwa inadi pia awaonyeshe jambo) kubwa zaidi kuliko hilo na kusema: Tuonyeshe Allah (tumuone) wazi wazi. (Kwasababu hiyo) kimondo kiliwachukua (kiliwaangamiza) kwasababu ya udhalimu wao (wa ukinzani na kukufuru). Kisha walimfanya ndama kuwa (Mungu) baada ya kuwa hoja zilizowazi zimewafikia tukasamehe hayo.[1] Na tulimpa Mussa hoja inayofafanua


1- - Madhambi ya ukaidi wa kutoamini mpaka wamuone Allah duniani na madhambi ya kuabudu ndama.


Capítulo: ANNISAI 

Verso : 159

وَإِن مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ إِلَّا لَيُؤۡمِنَنَّ بِهِۦ قَبۡلَ مَوۡتِهِۦۖ وَيَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ يَكُونُ عَلَيۡهِمۡ شَهِيدٗا

Na hakuna yeyote katika Watu wa Kitabu isipokuwa kwa yakini kabisa watamuamini tu kabla ya kufa kwake. Na Siku ya Kiama atakuwa shahidi kwao



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 171

يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لَا تَغۡلُواْ فِي دِينِكُمۡ وَلَا تَقُولُواْ عَلَى ٱللَّهِ إِلَّا ٱلۡحَقَّۚ إِنَّمَا ٱلۡمَسِيحُ عِيسَى ٱبۡنُ مَرۡيَمَ رَسُولُ ٱللَّهِ وَكَلِمَتُهُۥٓ أَلۡقَىٰهَآ إِلَىٰ مَرۡيَمَ وَرُوحٞ مِّنۡهُۖ فَـَٔامِنُواْ بِٱللَّهِ وَرُسُلِهِۦۖ وَلَا تَقُولُواْ ثَلَٰثَةٌۚ ٱنتَهُواْ خَيۡرٗا لَّكُمۡۚ إِنَّمَا ٱللَّهُ إِلَٰهٞ وَٰحِدٞۖ سُبۡحَٰنَهُۥٓ أَن يَكُونَ لَهُۥ وَلَدٞۘ لَّهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۗ وَكَفَىٰ بِٱللَّهِ وَكِيلٗا

Enyi Watu wa Kitabu, msichupe mipaka katika dini yenu na msimsemee Allah isipokuwa haki tu. Hakika, ilivyo ni kwamba Masihi, Issa Mwana wa Mariamu ni Mtume wa Allah na neno lake alilompelekea Mariamu, na ni roho iliyotoka kwake. Basi muaminini Allah na Mitume wake, na msiseme: Miungu ni watatu. Acheni (kuamini hivyo) itakuwa kheri kwenu. Hakika, ilivyo ni kwamba, Allah ni Mungu mmoja tu, ametakasika (kwa) kutokuwa na mwana. Ni vyake yeye tu vyote vilivyomo mbinguni na ardhini. Na imetosha kwamba, Allah ni Mwenye kutegemewa



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 5

ٱلۡيَوۡمَ أُحِلَّ لَكُمُ ٱلطَّيِّبَٰتُۖ وَطَعَامُ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ حِلّٞ لَّكُمۡ وَطَعَامُكُمۡ حِلّٞ لَّهُمۡۖ وَٱلۡمُحۡصَنَٰتُ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ وَٱلۡمُحۡصَنَٰتُ مِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ مِن قَبۡلِكُمۡ إِذَآ ءَاتَيۡتُمُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ مُحۡصِنِينَ غَيۡرَ مُسَٰفِحِينَ وَلَا مُتَّخِذِيٓ أَخۡدَانٖۗ وَمَن يَكۡفُرۡ بِٱلۡإِيمَٰنِ فَقَدۡ حَبِطَ عَمَلُهُۥ وَهُوَ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ مِنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ

Leo mmehalalishiwa vilivyo vizuri. Na chakula cha waliopewa Kitabu ni halali kwenu na chakula chenu ni halali kwao. Na (mmehalalishiwa kuoa) wanawake waumini waliohifadhiwa na wanawake waliohifadhiwa katika waliopewa Kitabu kabla yenu mtakapowapa malipo (mahari) yao, mkikusudia kujihifadhi (na) sio wenye kukusudia uzinzi wala kuwaweka (wanawake hao) kinyumba. Na yeyote anayekataa kuamini, bila shaka amali zake (njema) zimeporomoka (zimepotea bure) na yeye Akhera atakuwa miongoni mwa wenye hasara