لِّلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۗ وَإِن تُبۡدُواْ مَا فِيٓ أَنفُسِكُمۡ أَوۡ تُخۡفُوهُ يُحَاسِبۡكُم بِهِ ٱللَّهُۖ فَيَغۡفِرُ لِمَن يَشَآءُ وَيُعَذِّبُ مَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٌ
Ni vya Allah tu vyote vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Na kama mkidhihirisha yaliyomo katika nyoyo zenu, au mkiyaficha, Allah atakuhojini kwayo; kwahiyo atamsamehe amtakaye, na atamuadhibu amtakaye. Na Allah ni Mwenye uweza mno wa kila kitu
لَا يُكَلِّفُ ٱللَّهُ نَفۡسًا إِلَّا وُسۡعَهَاۚ لَهَا مَا كَسَبَتۡ وَعَلَيۡهَا مَا ٱكۡتَسَبَتۡۗ رَبَّنَا لَا تُؤَاخِذۡنَآ إِن نَّسِينَآ أَوۡ أَخۡطَأۡنَاۚ رَبَّنَا وَلَا تَحۡمِلۡ عَلَيۡنَآ إِصۡرٗا كَمَا حَمَلۡتَهُۥ عَلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِنَاۚ رَبَّنَا وَلَا تُحَمِّلۡنَا مَا لَا طَاقَةَ لَنَا بِهِۦۖ وَٱعۡفُ عَنَّا وَٱغۡفِرۡ لَنَا وَٱرۡحَمۡنَآۚ أَنتَ مَوۡلَىٰنَا فَٱنصُرۡنَا عَلَى ٱلۡقَوۡمِ ٱلۡكَٰفِرِينَ
Allah haikalifishi nafsi yoyote ila (kwa) iliwezalo. Itafaidika na mema iliyoyachuma na itadhurika na mabaya iliyoyachuma. (Waumini) wanasema: “(Ewe) Mola wetu Mlezi, usitutie hatiani kama tukisahahu (kutenda yaliyo mema) au tukikosea (kwa kutenda mabaya). (Ewe) Mola wetu Mlezi, na usitubebeshe mazito kama uliyowabebesha wale waliokuwa kabla yetu. (Ewe) Mola wetu Mlezi, usitubebeshe tusiyoyaweza, na tusamehe na tughufirie na turehemu. Wewe ndiye Mola wetu. Basi tusaidie dhidi ya watu makafiri
وَمَا كَانَ لِنَفۡسٍ أَن تَمُوتَ إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِ كِتَٰبٗا مُّؤَجَّلٗاۗ وَمَن يُرِدۡ ثَوَابَ ٱلدُّنۡيَا نُؤۡتِهِۦ مِنۡهَا وَمَن يُرِدۡ ثَوَابَ ٱلۡأٓخِرَةِ نُؤۡتِهِۦ مِنۡهَاۚ وَسَنَجۡزِي ٱلشَّـٰكِرِينَ
Na nafsi yoyote haifi isipokuwa kwa idhini ya Allah tu ikiwa ni jambo lililoandikwa (na lenye) muda maalum. Na yeyote anayetaka malipo ya duniani tunampa humo, na mwenye kutaka malipo ya Akhera tutampa huko. Na tutawalipa wenye kushukuru
كُلُّ نَفۡسٖ ذَآئِقَةُ ٱلۡمَوۡتِۗ وَإِنَّمَا تُوَفَّوۡنَ أُجُورَكُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۖ فَمَن زُحۡزِحَ عَنِ ٱلنَّارِ وَأُدۡخِلَ ٱلۡجَنَّةَ فَقَدۡ فَازَۗ وَمَا ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَآ إِلَّا مَتَٰعُ ٱلۡغُرُورِ
Kila nafsi itaonja kifo, si vingine malipo yenu mtapewa yakiwa kamili siku ya kiyama, atakaye epushwa na kuwekwa mbali na Moto na akaingizwa Peponi basi huyo amefanikiwa, na haikua maisha ya dunia ila ni starehe zenye kudanganya
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ ٱتَّقُواْ رَبَّكُمُ ٱلَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفۡسٖ وَٰحِدَةٖ وَخَلَقَ مِنۡهَا زَوۡجَهَا وَبَثَّ مِنۡهُمَا رِجَالٗا كَثِيرٗا وَنِسَآءٗۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ ٱلَّذِي تَسَآءَلُونَ بِهِۦ وَٱلۡأَرۡحَامَۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلَيۡكُمۡ رَقِيبٗا
Enyi watu, mcheni Mola wenu Mlezi Ambaye amekuumbeni kutokana na nafsi moja tu na ameumba kutoka kwenye nafsi hiyo mke wake (Hawaa), na akaeneza kutokana na wawili hao wanaume wengi na wanawake (wengi), na mcheni Allah Ambaye mnaombana kupitia yeye, na (ogopeni kukata) udugu. Hakika, Allah amekuwa Mwenye kukufuatilieni kwa karibu sana
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَأۡكُلُوٓاْ أَمۡوَٰلَكُم بَيۡنَكُم بِٱلۡبَٰطِلِ إِلَّآ أَن تَكُونَ تِجَٰرَةً عَن تَرَاضٖ مِّنكُمۡۚ وَلَا تَقۡتُلُوٓاْ أَنفُسَكُمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِكُمۡ رَحِيمٗا
Enyi mlioamini, msile mali zenu baina yenu kwa batili, isipokuwa tu kama mali hizo ni biashara (inayofanyika) kwa maridhiano yenu. Na msijiue. Hakika, Allah ni mwenye rehema kwenu
وَإِنِ ٱمۡرَأَةٌ خَافَتۡ مِنۢ بَعۡلِهَا نُشُوزًا أَوۡ إِعۡرَاضٗا فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡهِمَآ أَن يُصۡلِحَا بَيۡنَهُمَا صُلۡحٗاۚ وَٱلصُّلۡحُ خَيۡرٞۗ وَأُحۡضِرَتِ ٱلۡأَنفُسُ ٱلشُّحَّۚ وَإِن تُحۡسِنُواْ وَتَتَّقُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٗا
Na iwapo mwanamke (mke) yeyote atachelea uasi kwa mumewe au kutojaliwa (kupuuzwa na kutelekezwa) basi si vibaya kwao kufanya suluhu baina yao, na suluhu ni jambo la kheri sana. Na nafsi zimehudhurishiwa (zimesogezewa) ubahili[1]. Na iwapo mtafanya mazuri na mkamcha Allah, basi hakika Allah anayajua vyema yote mnayoyafanya
1- - Hapa Aya inaelezea uhalisia wa nafsi ya mwanadamu wakati wa ugonvi na mivutano ambapo kila upande unakuwa na umimi, kujipendelea, kukataa kujishusha na kuwa na ugumu na uzito wa kukubali kosa, kujirudi au kusamehe haki ili kufikia suluhu na muafaka.
مِنۡ أَجۡلِ ذَٰلِكَ كَتَبۡنَا عَلَىٰ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ أَنَّهُۥ مَن قَتَلَ نَفۡسَۢا بِغَيۡرِ نَفۡسٍ أَوۡ فَسَادٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَكَأَنَّمَا قَتَلَ ٱلنَّاسَ جَمِيعٗا وَمَنۡ أَحۡيَاهَا فَكَأَنَّمَآ أَحۡيَا ٱلنَّاسَ جَمِيعٗاۚ وَلَقَدۡ جَآءَتۡهُمۡ رُسُلُنَا بِٱلۡبَيِّنَٰتِ ثُمَّ إِنَّ كَثِيرٗا مِّنۡهُم بَعۡدَ ذَٰلِكَ فِي ٱلۡأَرۡضِ لَمُسۡرِفُونَ
Kwa sababu ya hayo[1], tume-waandikia (tumewafaradhishia) Wana wa Israil ya kwamba, aliyeua nafsi (ya mtu) bila ya (yeye kuua) nafsi au kufanya uovu katika nchi, basi ni kama ameua watu wote. Na mwenye kuihuisha (kuiokoa nafsi isife) ni kama ameokoa watu wote. Na hakika waliwajia Mitume wetu na hoja za wazi, kisha wengi miongoni mwao baada ya hayo wakawa wenye kufanya yaliyovuka mipaka katika ardhi
1- - Kosa la mauaji yaliyofanywa na mmoja wa watoto wa Mtume Adamu.
وَكَتَبۡنَا عَلَيۡهِمۡ فِيهَآ أَنَّ ٱلنَّفۡسَ بِٱلنَّفۡسِ وَٱلۡعَيۡنَ بِٱلۡعَيۡنِ وَٱلۡأَنفَ بِٱلۡأَنفِ وَٱلۡأُذُنَ بِٱلۡأُذُنِ وَٱلسِّنَّ بِٱلسِّنِّ وَٱلۡجُرُوحَ قِصَاصٞۚ فَمَن تَصَدَّقَ بِهِۦ فَهُوَ كَفَّارَةٞ لَّهُۥۚ وَمَن لَّمۡ يَحۡكُم بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ
Na humo (ndani ya Taurati) tumewaandikia ya kwamba, roho kwa roho na jicho kwa jicho na pua kwa pua na sikio kwa sikio na jino kwa jino na majeraha ni kisasi. Basi atakayetoa sadaka (ya kusamehe haki yake kulipa kisasi) hiyo ni kafara yake (ya madhambi yake). Na wasiohukumu kwa (sheria) aliyoiteremsha Allah, basi hao ndio madhalimu
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ عَلَيۡكُمۡ أَنفُسَكُمۡۖ لَا يَضُرُّكُم مَّن ضَلَّ إِذَا ٱهۡتَدَيۡتُمۡۚ إِلَى ٱللَّهِ مَرۡجِعُكُمۡ جَمِيعٗا فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Enyi mlioamini, zijalini nafsi zenu. Hawakudhuruni waliopotea ikiwa nyinyi mmeongoka. Kwa Allah tu ndio marejeo yenu nyote; basi atakuambieni yale yote mliyokuwa mnayatenda
وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًا أَوۡ قَالَ أُوحِيَ إِلَيَّ وَلَمۡ يُوحَ إِلَيۡهِ شَيۡءٞ وَمَن قَالَ سَأُنزِلُ مِثۡلَ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُۗ وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذِ ٱلظَّـٰلِمُونَ فِي غَمَرَٰتِ ٱلۡمَوۡتِ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ بَاسِطُوٓاْ أَيۡدِيهِمۡ أَخۡرِجُوٓاْ أَنفُسَكُمُۖ ٱلۡيَوۡمَ تُجۡزَوۡنَ عَذَابَ ٱلۡهُونِ بِمَا كُنتُمۡ تَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ غَيۡرَ ٱلۡحَقِّ وَكُنتُمۡ عَنۡ ءَايَٰتِهِۦ تَسۡتَكۡبِرُونَ
Na ni nani dhalimu zaidi kuliko yule aliyemzushia Allah uongo (kuwa amempa Utume) au aliyesema kuwa: Nimeletewa Wahyi na ilhali hakuletewa Wahyi wowote? Na (ni nani dhalimu zaidi kuliko) yule aliyesema kuwa: Nitateremsha mfano wa aliyoteremsha Allah? Na lau ungeona wakati madhalimu wamo katika mahangaiko ya mauti na Malaika wamenyoosha mikono yao (wakiwa tayari kuchukua roho zao wakiwaambia): Zitoeni (ziokoeni) roho zenu (kutoka mikononi mwetu kama mnaweza kwa sababu) leo mtalipwa adhabu ya fedheha kwa sababu ya yale yasiyokuwa ya haki mliyomsingizia Allah, na mlikuwa mnazifanyia kiburi Aya zake
وَهُوَ ٱلَّذِيٓ أَنشَأَكُم مِّن نَّفۡسٖ وَٰحِدَةٖ فَمُسۡتَقَرّٞ وَمُسۡتَوۡدَعٞۗ قَدۡ فَصَّلۡنَا ٱلۡأٓيَٰتِ لِقَوۡمٖ يَفۡقَهُونَ
Na yeye (Allah) ndiye aliye-kuumbeni kwa mara ya kwanza kutoka katika nafsi moja[1]. Basi pakomahali pa kutulizana (kwa ajili yenukatika matumbo ya mama zenu) na pako mahali pa hifadhi (makaburini). Hakika tumezifafanua Aya (hizi) kwa watu wanaofahamu
1- - (ambae ni Adamu, Allah amshushie amani)
قَدۡ جَآءَكُم بَصَآئِرُ مِن رَّبِّكُمۡۖ فَمَنۡ أَبۡصَرَ فَلِنَفۡسِهِۦۖ وَمَنۡ عَمِيَ فَعَلَيۡهَاۚ وَمَآ أَنَا۠ عَلَيۡكُم بِحَفِيظٖ
Hakika, zimekujieni (hoja) zifunguazo macho kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Basi atakaeziona ni kwa faida yake na atakaejifanya kipofu basi ni hasara yake, na mimi si mlinzi wenu (sikuamrishwa kuwa mlinzi wenu)
وَلَا تَقۡرَبُواْ مَالَ ٱلۡيَتِيمِ إِلَّا بِٱلَّتِي هِيَ أَحۡسَنُ حَتَّىٰ يَبۡلُغَ أَشُدَّهُۥۚ وَأَوۡفُواْ ٱلۡكَيۡلَ وَٱلۡمِيزَانَ بِٱلۡقِسۡطِۖ لَا نُكَلِّفُ نَفۡسًا إِلَّا وُسۡعَهَاۖ وَإِذَا قُلۡتُمۡ فَٱعۡدِلُواْ وَلَوۡ كَانَ ذَا قُرۡبَىٰۖ وَبِعَهۡدِ ٱللَّهِ أَوۡفُواْۚ ذَٰلِكُمۡ وَصَّىٰكُم بِهِۦ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ
Na msizisogelee mali za Yatima ila kwa njia iliyo nzuri sana hadi afikie utu uzima wake. Na timizeni vipimo na mizani kwa uadilifu. Hatuilazimishi nafsi (jambo lolote) isipokuwa kwa kadiri ya vile iwezavyo. Na msemapo semeni kwa uadilifu hata ikiwa (ni dhidi ya) ndugu. Na ahadi za Allah zitekelezeni. Hayo amekuusieni (Allah) ili mpate kukumbuka
هَلۡ يَنظُرُونَ إِلَّآ أَن تَأۡتِيَهُمُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ أَوۡ يَأۡتِيَ رَبُّكَ أَوۡ يَأۡتِيَ بَعۡضُ ءَايَٰتِ رَبِّكَۗ يَوۡمَ يَأۡتِي بَعۡضُ ءَايَٰتِ رَبِّكَ لَا يَنفَعُ نَفۡسًا إِيمَٰنُهَا لَمۡ تَكُنۡ ءَامَنَتۡ مِن قَبۡلُ أَوۡ كَسَبَتۡ فِيٓ إِيمَٰنِهَا خَيۡرٗاۗ قُلِ ٱنتَظِرُوٓاْ إِنَّا مُنتَظِرُونَ
Hakuna wanacho kingoja isipokuwa tu wanangoja wawajie Malaika au aje Mola wako Mlezi au zije baadhi ya ishara za Mola wako. Siku zitakapokuja baadhi ya ishara za Mola wako haitamfaa mtu imani yake ikiwa hakuamini kabla ya hapo au hakuchuma kheri yoyote katika kuamini kwake. Sema: Ngojeni, nasi (pia) ni wenye kungoja
قُلۡ أَغَيۡرَ ٱللَّهِ أَبۡغِي رَبّٗا وَهُوَ رَبُّ كُلِّ شَيۡءٖۚ وَلَا تَكۡسِبُ كُلُّ نَفۡسٍ إِلَّا عَلَيۡهَاۚ وَلَا تَزِرُ وَازِرَةٞ وِزۡرَ أُخۡرَىٰۚ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّكُم مَّرۡجِعُكُمۡ فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ فِيهِ تَخۡتَلِفُونَ
Sema: Je nitafute Mola mlezi asiekuwa Allah! na ilhali yeye (Allah) ni Mola Mlezi wa kila kitu? Na kila nafsi haitachuma (jambo la kheri au la shari) isipokuwa litarudi kwake mwenyewe. Na hatabeba mtu yeyote mzigo wa (dhambi za) mwengine. Kisha (nyote) marejeo yenu ni kwa Mola wenu tu, na atakuelezeni yote mliyokuwa mkitofautiana
۞هُوَ ٱلَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفۡسٖ وَٰحِدَةٖ وَجَعَلَ مِنۡهَا زَوۡجَهَا لِيَسۡكُنَ إِلَيۡهَاۖ فَلَمَّا تَغَشَّىٰهَا حَمَلَتۡ حَمۡلًا خَفِيفٗا فَمَرَّتۡ بِهِۦۖ فَلَمَّآ أَثۡقَلَت دَّعَوَا ٱللَّهَ رَبَّهُمَا لَئِنۡ ءَاتَيۡتَنَا صَٰلِحٗا لَّنَكُونَنَّ مِنَ ٱلشَّـٰكِرِينَ
Yeye (Allah) Ndiye aliyeku-umbeni kutokana na nafsi moja (Adamu), na akajaalia kutoka katika nafsi hiyo mkewe ili apate utulivu kwake. Na (Adamu) alipomuingilia (mkewe) tu alibeba mimba nyepesi (kwa sababu ndio kwanza ilitunga) na aliweza kutembea nayo. Basi alipopata uzito (wa mimba kwa sababu ilikuwa kubwa) wote wawili (Adamu na mkewe) walimuomba Allah Mola wao Mlezi (na kusema): Kwa yakini kabisa (ewe Mola wetu), kama utatupa (mtoto) mwema bila shaka tutakuwa miongoni mwa wenye kushukuru
فَلَا تُعۡجِبۡكَ أَمۡوَٰلُهُمۡ وَلَآ أَوۡلَٰدُهُمۡۚ إِنَّمَا يُرِيدُ ٱللَّهُ لِيُعَذِّبَهُم بِهَا فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَتَزۡهَقَ أَنفُسُهُمۡ وَهُمۡ كَٰفِرُونَ
Zisikupendeze (zisikushangaze) mali zao wala watoto wao. Hakika ilivyo ni kwamba, Allah anataka kuwaadhibu kwazo hapa duniani[1], na roho zao zitoke (kwa uchungu) na wao wakiwa makafiri
1- - Adhabu inayotajwa hapa kwa wanafiki na makafiri kwa jumla wanaojikusanyia mali na kukataa kumuamini Allah ni tabu wanayoipata katika kutafuta mali, tabu wanayoipata katika kuilinda na tabu wanayoipata katika kukosa amani.
وَلَا تُعۡجِبۡكَ أَمۡوَٰلُهُمۡ وَأَوۡلَٰدُهُمۡۚ إِنَّمَا يُرِيدُ ٱللَّهُ أَن يُعَذِّبَهُم بِهَا فِي ٱلدُّنۡيَا وَتَزۡهَقَ أَنفُسُهُمۡ وَهُمۡ كَٰفِرُونَ
Na zisikushangaze mali zao na watoto wao (hapa duniani). Ilivyo ni kwamba, Allah anataka kuwaadhibu kwazo duniani[1] na zitoke kwa nguvu roho zao na ilhali wao ni makafiri
1- - Rejea dokezo katika Aya ya 55 ya Sura hii.
وَمَا كَانَ لِنَفۡسٍ أَن تُؤۡمِنَ إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۚ وَيَجۡعَلُ ٱلرِّجۡسَ عَلَى ٱلَّذِينَ لَا يَعۡقِلُونَ
Na haiwi kwa nafsi yoyote kuamini, isipokuwa tu kwa idhini ya Allah. Na (Allah) anaweka uchafu (wa uovu na upotevu) kwa wale wasiotumia akili (na kumtambua Allah na kumuamini)
قُلۡ يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ قَدۡ جَآءَكُمُ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّكُمۡۖ فَمَنِ ٱهۡتَدَىٰ فَإِنَّمَا يَهۡتَدِي لِنَفۡسِهِۦۖ وَمَن ضَلَّ فَإِنَّمَا يَضِلُّ عَلَيۡهَاۖ وَمَآ أَنَا۠ عَلَيۡكُم بِوَكِيلٖ
Sema: Enyi watu, hakika imekujieni haki kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Basi yeyote anayeongoka, anaongoka kwa faida ya nafsi yake, na anayepotea, basi kwa hakika anapotea kwa hasara ya nafsi yake. Na mimi si msaidizi kwenu
۞وَمَآ أُبَرِّئُ نَفۡسِيٓۚ إِنَّ ٱلنَّفۡسَ لَأَمَّارَةُۢ بِٱلسُّوٓءِ إِلَّا مَا رَحِمَ رَبِّيٓۚ إِنَّ رَبِّي غَفُورٞ رَّحِيمٞ
(Yusuf aliendelea kusema) Nami siisafishi nafsi yangu (sijitoi lawamani). Kwa hakika nafsi inaamrisha mno maovu, isipokuwa ile tu aliyoirehemu Mola wangu Mlezi. Hakika, Mola wangu Mlezi ni Msamehevu, mwingi wa rehema
وَكُلَّ إِنسَٰنٍ أَلۡزَمۡنَٰهُ طَـٰٓئِرَهُۥ فِي عُنُقِهِۦۖ وَنُخۡرِجُ لَهُۥ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ كِتَٰبٗا يَلۡقَىٰهُ مَنشُورًا
Na kila mtu tumemfungia a’mali yake shingoni mwake. Na Siku ya Kiyama tutamtolea kitabu atakacho kikuta kiwazi kimekunjuliwa
رَّبُّكُمۡ أَعۡلَمُ بِمَا فِي نُفُوسِكُمۡۚ إِن تَكُونُواْ صَٰلِحِينَ فَإِنَّهُۥ كَانَ لِلۡأَوَّـٰبِينَ غَفُورٗا
Mola wenu anajua kabisa yaliyo nyoyoni mwenu. Ikiwa nyinyi mtakuwa wema, basi hakika Yeye ni Mwenye kuwasamehe wanao tubia kwake
وَلَا تَقۡتُلُواْ ٱلنَّفۡسَ ٱلَّتِي حَرَّمَ ٱللَّهُ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۗ وَمَن قُتِلَ مَظۡلُومٗا فَقَدۡ جَعَلۡنَا لِوَلِيِّهِۦ سُلۡطَٰنٗا فَلَا يُسۡرِف فِّي ٱلۡقَتۡلِۖ إِنَّهُۥ كَانَ مَنصُورٗا
Wala msiuwe nafsi ambayo Allah amekataza isipo kuwa kwa haki. Na aliye uliwa kwa kudhulumiwa basi tumempa madaraka mrithi wake. Lakini asipite mpaka katika kuuwa. Kwani yeye anasaidiwa
كُلُّ نَفۡسٖ ذَآئِقَةُ ٱلۡمَوۡتِۗ وَنَبۡلُوكُم بِٱلشَّرِّ وَٱلۡخَيۡرِ فِتۡنَةٗۖ وَإِلَيۡنَا تُرۡجَعُونَ
Kila nafsi itaonja mauti; na tunakujaribuni kwa mtihani wa shari na kheri. Na kwetu Sisi mtarejeshwa
وَلَا نُكَلِّفُ نَفۡسًا إِلَّا وُسۡعَهَاۚ وَلَدَيۡنَا كِتَٰبٞ يَنطِقُ بِٱلۡحَقِّ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ
Na hatuilazimishi nafsi ila kwa kadri ya uwezo wake. Na tunacho kitabu kisemacho kweli. Nao hawatadhulumiwa
وَٱلَّذِينَ لَا يَدۡعُونَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ وَلَا يَقۡتُلُونَ ٱلنَّفۡسَ ٱلَّتِي حَرَّمَ ٱللَّهُ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَلَا يَزۡنُونَۚ وَمَن يَفۡعَلۡ ذَٰلِكَ يَلۡقَ أَثَامٗا
Na ambao hawamuombi Mungu Mwengine pamoja na Allah, wala hawaui nafsi aliyoiharimisha Allah isipokuwa kwa haki tu, wala hawazini (hawafanyi Zinaa) - na atakayefanya hayo atapata madhara,
وَمَن جَٰهَدَ فَإِنَّمَا يُجَٰهِدُ لِنَفۡسِهِۦٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَغَنِيٌّ عَنِ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na anaye fanya juhudi basi bila ya shaka anafanya juhudi kwa ajili ya nafsi yake. Hakika Allah si mhitaji wa walimwengu
كُلُّ نَفۡسٖ ذَآئِقَةُ ٱلۡمَوۡتِۖ ثُمَّ إِلَيۡنَا تُرۡجَعُونَ
Kila nafsi itaonja mauti. Kisha mtarudishwa kwetu