إِلَّا تَنصُرُوهُ فَقَدۡ نَصَرَهُ ٱللَّهُ إِذۡ أَخۡرَجَهُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ ثَانِيَ ٱثۡنَيۡنِ إِذۡ هُمَا فِي ٱلۡغَارِ إِذۡ يَقُولُ لِصَٰحِبِهِۦ لَا تَحۡزَنۡ إِنَّ ٱللَّهَ مَعَنَاۖ فَأَنزَلَ ٱللَّهُ سَكِينَتَهُۥ عَلَيۡهِ وَأَيَّدَهُۥ بِجُنُودٖ لَّمۡ تَرَوۡهَا وَجَعَلَ كَلِمَةَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ ٱلسُّفۡلَىٰۗ وَكَلِمَةُ ٱللَّهِ هِيَ ٱلۡعُلۡيَاۗ وَٱللَّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ
Ikiwa nyinyi hamtamnusuru Mtume (Muhammad), basi Allah alikwishamnusuru pale waliokufuru walipomtoa (walipomfukuza) akiwa mmoja kati ya wawili wakati walipokuwa kwenye pango (la mlima Thaur), wakati akimwambia Swahibawake[1]: “Usihuzunike. Hakika, Allah yupo pamoja nasi”. Allah alimteremshia utulivu wake, na akampa nguvu kwa majeshi ambayo hamkuyaona, na akalifanya neno la waliokufuru kuwa chini sana, na Neno la Allah ndilo lililo juu zaidi. Na Allah ndiye Mwenye nguvu mno, Mwenye hekima sana[2]
1- - Alikuwa Swahaba Abubakar, Allah amuwie radhi.
2- - Aya hii inatutajia tukio adhimu la kuhama kwa Nabii Muhammad (Allah amshushie rehema na amani)
kutoka kwenye mji Mtukufu wa Makkah na kwenda kujificha kwenye pango (Ghari Thaur) kwa muda wa
siku tatu, na hatimae kuelekea uhamishoni kwenye Mji wa Madina. Aidha, Allah kupitia Aya hii
ametudhihirishia wazi utukufu wa Nabii wake na utukufu wa Swahaba Abubakar Allah amridhie ambaye
Alifuatana na Nabii kwenye msafara huo.
ٱنفِرُواْ خِفَافٗا وَثِقَالٗا وَجَٰهِدُواْ بِأَمۡوَٰلِكُمۡ وَأَنفُسِكُمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِۚ ذَٰلِكُمۡ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ
Tokeni haraka (kwenda kwenye Jihadi katika mazingira yoyote) mkiwa wepesi (wa hali, mali, maandalizi n.k.) na wazito (wa hali, mali, maandalizi n.k.) na piganeni Jihadi kwa mali zenu na nafsi zenu katika Njia ya Allah. Hiyo ni heri kwenu iwapo mnajua
لَوۡ كَانَ عَرَضٗا قَرِيبٗا وَسَفَرٗا قَاصِدٗا لَّٱتَّبَعُوكَ وَلَٰكِنۢ بَعُدَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلشُّقَّةُۚ وَسَيَحۡلِفُونَ بِٱللَّهِ لَوِ ٱسۡتَطَعۡنَا لَخَرَجۡنَا مَعَكُمۡ يُهۡلِكُونَ أَنفُسَهُمۡ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ إِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ
Lau kama ingekuwa (hilo wanaloitiwa) ni faida ya papo kwa papo na safari fupi, kwa yakini kabisa wangelikufuata (ili nao wapate ngawira), na lakini kipande (cha safari ya eneo la vita la Tabuk) kimekuwa cha mbali (ndio maana wamekuwa wazito). Na wataapia Allah (mtakaporejea) kwamba: Lau kama tungeweza, bila ya shaka tungelitoka pamoja nanyi. Wanaziangamiza nafsi zao, na Allah anajua fika kuwa wao ni waongo
عَفَا ٱللَّهُ عَنكَ لِمَ أَذِنتَ لَهُمۡ حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَكَ ٱلَّذِينَ صَدَقُواْ وَتَعۡلَمَ ٱلۡكَٰذِبِينَ
Allah alishakusamehe. Kwa nini uliwaruhusu (wasiende kwenye vita vya Tabuki) kabla ya kukubainikia wasemao kweli, na ukawajua waongo?
لَا يَسۡتَـٔۡذِنُكَ ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ أَن يُجَٰهِدُواْ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡۗ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِٱلۡمُتَّقِينَ
Hawakuombi ruhusa wale wanaomuamini Allah na Siku ya Mwisho, wasiende kupigana Jihadi kwa mali zao na nafsi zao. Na Allah ni Mwenye kuwajua mno wachaMungu
إِنَّمَا يَسۡتَـٔۡذِنُكَ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَٱرۡتَابَتۡ قُلُوبُهُمۡ فَهُمۡ فِي رَيۡبِهِمۡ يَتَرَدَّدُونَ
Hakika wanaokuomba ruhusa ni wale wasiomuamini Allah na Siku ya Mwisho na nyoyo zao zina shaka (Wanafiki). Basi hao wanataradadi katika shaka zao
۞وَلَوۡ أَرَادُواْ ٱلۡخُرُوجَ لَأَعَدُّواْ لَهُۥ عُدَّةٗ وَلَٰكِن كَرِهَ ٱللَّهُ ٱنۢبِعَاثَهُمۡ فَثَبَّطَهُمۡ وَقِيلَ ٱقۡعُدُواْ مَعَ ٱلۡقَٰعِدِينَ
Na kama ingelikuwa kweli walitaka kutoka, bila ya shaka wangeliandalia hilo maandalizi, na lakini Allah amechukia kutoka kwao, na kwa hiyo akawakwaza na ikasemwa: Kaeni pamoja na wanaokaa
لَوۡ خَرَجُواْ فِيكُم مَّا زَادُوكُمۡ إِلَّا خَبَالٗا وَلَأَوۡضَعُواْ خِلَٰلَكُمۡ يَبۡغُونَكُمُ ٱلۡفِتۡنَةَ وَفِيكُمۡ سَمَّـٰعُونَ لَهُمۡۗ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِٱلظَّـٰلِمِينَ
Lau kama (wanafiki) wangetoka (kwenda Jihadi) pamoja nanyi wasingekuzidishieni isipokuwa mchafuko (mvurugano) tu, na wangekwenda mbio kati yenu wakikutilieni fitina. Na miongoni mwenu wapo (wapelelezi) wanaosikiliza sana (habari kwenu) na kuzipeleka kwao. Na Allah anawajua mno madhalimu
لَقَدِ ٱبۡتَغَوُاْ ٱلۡفِتۡنَةَ مِن قَبۡلُ وَقَلَّبُواْ لَكَ ٱلۡأُمُورَ حَتَّىٰ جَآءَ ٱلۡحَقُّ وَظَهَرَ أَمۡرُ ٱللَّهِ وَهُمۡ كَٰرِهُونَ
Kwa hakika kabisa, (wanafiki) hapo awali (kabla ya vita vya Tabuki) walitaka fitina, na wakakupindulia pindulia mambo (kihila ili ukubaliane nao), mpaka ilipokuja haki na likadhihiri jambo la Allah (Dini yake), na ilhali wao ni wenye kuchukia
وَمِنۡهُم مَّن يَقُولُ ٱئۡذَن لِّي وَلَا تَفۡتِنِّيٓۚ أَلَا فِي ٱلۡفِتۡنَةِ سَقَطُواْۗ وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمُحِيطَةُۢ بِٱلۡكَٰفِرِينَ
Na miongoni mwao (hao wanafiki) wapo wanaosema: Niruhusu (nisiende Jihadi) wala usinitie katika fitina. Zinduka! Wameshatumbukia katika fitina (kwa kuhalifu Jihadi na kutoa udhuru wa uongo). Na hakika kabisa, Jahanamu ni yenye kuwazingira makafiri
إِن تُصِبۡكَ حَسَنَةٞ تَسُؤۡهُمۡۖ وَإِن تُصِبۡكَ مُصِيبَةٞ يَقُولُواْ قَدۡ أَخَذۡنَآ أَمۡرَنَا مِن قَبۡلُ وَيَتَوَلَّواْ وَّهُمۡ فَرِحُونَ
Likikupata jambo zuri (mafanikio, wema, nusura au ngawira) linawachukiza, na yakikusibu maafa, wanasema: Sisi tulilichukulia (tahadhari) jambo letu tokea awali (kwa kujiweka mbali) na wanageuka (kwenda zao) na ilhali wakifurahia sana (kilichowasibu Waislamu)
قُل لَّن يُصِيبَنَآ إِلَّا مَا كَتَبَ ٱللَّهُ لَنَا هُوَ مَوۡلَىٰنَاۚ وَعَلَى ٱللَّهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ
Sema: Katu halitusibu ila tu alilotuandikia Allah. Yeye ndiye Mola wetu Mlinzi. Na waumini (wa kweli) wamtegemee Allah tu
قُلۡ هَلۡ تَرَبَّصُونَ بِنَآ إِلَّآ إِحۡدَى ٱلۡحُسۡنَيَيۡنِۖ وَنَحۡنُ نَتَرَبَّصُ بِكُمۡ أَن يُصِيبَكُمُ ٱللَّهُ بِعَذَابٖ مِّنۡ عِندِهِۦٓ أَوۡ بِأَيۡدِينَاۖ فَتَرَبَّصُوٓاْ إِنَّا مَعَكُم مُّتَرَبِّصُونَ
Sema (ewe Nabii Muhammad uwaambie wanafiki kuwa): Hivi mnatutazamia litupate moja ya mema mawili (kufa mashahidi au kupata ushindi)? Nasi tunakutazamieni Allah akufikishieni adhabu kutoka kwake au kwa (kupitia) mikono yetu. Basi ngojeni, nasi pamoja nanyi tunangoja
قُلۡ أَنفِقُواْ طَوۡعًا أَوۡ كَرۡهٗا لَّن يُتَقَبَّلَ مِنكُمۡ إِنَّكُمۡ كُنتُمۡ قَوۡمٗا فَٰسِقِينَ
Sema (uwaambie wanafiki kuwa): Toeni mkipenda au msipende. Katu hakitopokelewa kitu kwenu. Hakika, nyinyi mmekuwa watu waovu
وَمَا مَنَعَهُمۡ أَن تُقۡبَلَ مِنۡهُمۡ نَفَقَٰتُهُمۡ إِلَّآ أَنَّهُمۡ كَفَرُواْ بِٱللَّهِ وَبِرَسُولِهِۦ وَلَا يَأۡتُونَ ٱلصَّلَوٰةَ إِلَّا وَهُمۡ كُسَالَىٰ وَلَا يُنفِقُونَ إِلَّا وَهُمۡ كَٰرِهُونَ
Na hakuna kilichowazuia kukubaliwa michango yao ila tu kwamba, walimkufuru Allah na Mtume wake na hawaendikuswali ila wakiwa wavivu, na wala hawatoi (michango kwenye Jihadi n.k.) ila wakiwa wamechukia
فَلَا تُعۡجِبۡكَ أَمۡوَٰلُهُمۡ وَلَآ أَوۡلَٰدُهُمۡۚ إِنَّمَا يُرِيدُ ٱللَّهُ لِيُعَذِّبَهُم بِهَا فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَتَزۡهَقَ أَنفُسُهُمۡ وَهُمۡ كَٰفِرُونَ
Zisikupendeze (zisikushangaze) mali zao wala watoto wao. Hakika ilivyo ni kwamba, Allah anataka kuwaadhibu kwazo hapa duniani[1], na roho zao zitoke (kwa uchungu) na wao wakiwa makafiri
1- - Adhabu inayotajwa hapa kwa wanafiki na makafiri kwa jumla wanaojikusanyia mali na kukataa kumuamini Allah ni tabu wanayoipata katika kutafuta mali, tabu wanayoipata katika kuilinda na tabu wanayoipata katika kukosa amani.
وَيَحۡلِفُونَ بِٱللَّهِ إِنَّهُمۡ لَمِنكُمۡ وَمَا هُم مِّنكُمۡ وَلَٰكِنَّهُمۡ قَوۡمٞ يَفۡرَقُونَ
Na wanaapa kwa Allah (kwa uongo) kwamba wao ni katika nyinyi, na wala wao si katika nyinyi. Lakini wao ni watu wanaoishi kwa hofu
لَوۡ يَجِدُونَ مَلۡجَـًٔا أَوۡ مَغَٰرَٰتٍ أَوۡ مُدَّخَلٗا لَّوَلَّوۡاْ إِلَيۡهِ وَهُمۡ يَجۡمَحُونَ
Laiti kama (hawa wanafiki) wangepata mahali pa kukimbilia au ngome au pango la kuingia (ili wasiende Jihadi) basi wangekwenda huko na huku wakikimbilia
وَمِنۡهُم مَّن يَلۡمِزُكَ فِي ٱلصَّدَقَٰتِ فَإِنۡ أُعۡطُواْ مِنۡهَا رَضُواْ وَإِن لَّمۡ يُعۡطَوۡاْ مِنۡهَآ إِذَا هُمۡ يَسۡخَطُونَ
Na miongoni mwao wapo (wanafiki) wanaokubeua (wanaokubeza) katika (kugawa) sadaka. Wanapopewa sadaka katika sadaka hizo (kama walivyotarajia) wanaridhika. Na wasipopewa katika sadaka hizo (kama walivyotarajia) haraka wanakasirika
وَلَوۡ أَنَّهُمۡ رَضُواْ مَآ ءَاتَىٰهُمُ ٱللَّهُ وَرَسُولُهُۥ وَقَالُواْ حَسۡبُنَا ٱللَّهُ سَيُؤۡتِينَا ٱللَّهُ مِن فَضۡلِهِۦ وَرَسُولُهُۥٓ إِنَّآ إِلَى ٱللَّهِ رَٰغِبُونَ
Na laiti kama (wanafiki) wangeridhia kile walichopewa na Allah na Mtume wake na wakasema: “Allah anatutosha, Allah atatupa (vingi) katika fadhila zake na pia Mtume wake (atatupa zaidi ya alivyotupa), (ingekuwa bora zaidi kwao). Hakika sisi ni wenye kumtaraji Allah tu (atupe fadhila zake)”
فَرِحَ ٱلۡمُخَلَّفُونَ بِمَقۡعَدِهِمۡ خِلَٰفَ رَسُولِ ٱللَّهِ وَكَرِهُوٓاْ أَن يُجَٰهِدُواْ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَقَالُواْ لَا تَنفِرُواْ فِي ٱلۡحَرِّۗ قُلۡ نَارُ جَهَنَّمَ أَشَدُّ حَرّٗاۚ لَّوۡ كَانُواْ يَفۡقَهُونَ
Walioachwa nyuma walifurahia kwa kule kubakia kwao nyuma na kumuacha Mtume wa Allah na walichukia (kwenda) kupigana Jihadi kwa mali zao na nafsi zao katika Njia ya Allah na wakasema: Msiende katika (Jihadi kipindi) cha joto. Sema: Moto wa Jahanamu una joto kali zaidi, laiti kama wangekuwa wanafahamu
فَلۡيَضۡحَكُواْ قَلِيلٗا وَلۡيَبۡكُواْ كَثِيرٗا جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ
Basi wacheke kidogo (hapa duniani) na walie sana (huko Akhera) ikiwa ni malipo ya yale waliyokuwa wakiyachuma
فَإِن رَّجَعَكَ ٱللَّهُ إِلَىٰ طَآئِفَةٖ مِّنۡهُمۡ فَٱسۡتَـٔۡذَنُوكَ لِلۡخُرُوجِ فَقُل لَّن تَخۡرُجُواْ مَعِيَ أَبَدٗا وَلَن تُقَٰتِلُواْ مَعِيَ عَدُوًّاۖ إِنَّكُمۡ رَضِيتُم بِٱلۡقُعُودِ أَوَّلَ مَرَّةٖ فَٱقۡعُدُواْ مَعَ ٱلۡخَٰلِفِينَ
Basi (Ewe Mtume Muhammad) Allah akikurudisha (salama) kwenye kundi moja miongoni mwao (hao wanafiki) na wakakuomba idhini ya kutoka (nawe kwenda vitani) sema: Nyinyi katu hamuwezi kutoka pamoja nami, na asilani hamuwezi kupigana na adui pamoja nami. Hakika, nyinyi mmeridhia kukaa nyuma mara ya kwanza, basi kaeni pamoja na hao wabakiao nyuma (wanawake, watoto na wasiojiweza)
وَلَا تُصَلِّ عَلَىٰٓ أَحَدٖ مِّنۡهُم مَّاتَ أَبَدٗا وَلَا تَقُمۡ عَلَىٰ قَبۡرِهِۦٓۖ إِنَّهُمۡ كَفَرُواْ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ وَمَاتُواْ وَهُمۡ فَٰسِقُونَ
Na kamwe usimswalie yeyote katika wao (wanafiki) akifa wala usisimame kaburini kwake (na kumuombea dua). Hakika, hao wamemkufuru Allah na Mtume wake na wamekufa ilhali ni waovu
وَلَا تُعۡجِبۡكَ أَمۡوَٰلُهُمۡ وَأَوۡلَٰدُهُمۡۚ إِنَّمَا يُرِيدُ ٱللَّهُ أَن يُعَذِّبَهُم بِهَا فِي ٱلدُّنۡيَا وَتَزۡهَقَ أَنفُسُهُمۡ وَهُمۡ كَٰفِرُونَ
Na zisikushangaze mali zao na watoto wao (hapa duniani). Ilivyo ni kwamba, Allah anataka kuwaadhibu kwazo duniani[1] na zitoke kwa nguvu roho zao na ilhali wao ni makafiri
1- - Rejea dokezo katika Aya ya 55 ya Sura hii.
وَإِذَآ أُنزِلَتۡ سُورَةٌ أَنۡ ءَامِنُواْ بِٱللَّهِ وَجَٰهِدُواْ مَعَ رَسُولِهِ ٱسۡتَـٔۡذَنَكَ أُوْلُواْ ٱلطَّوۡلِ مِنۡهُمۡ وَقَالُواْ ذَرۡنَا نَكُن مَّعَ ٱلۡقَٰعِدِينَ
Na inapoteremshwa Sura (inayowaamrisha) kwamba: Muaminini Allah na piganeni Jihadi pamoja na Mtume wake, wale wenye uwezo (wa mali na nguvu) miongoni mwao wanakuomba ruhusa na kusema: Tuache tuwe pamoja na wanaokaa nyuma
رَضُواْ بِأَن يَكُونُواْ مَعَ ٱلۡخَوَالِفِ وَطُبِعَ عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ فَهُمۡ لَا يَفۡقَهُونَ
Wameridhia kuwa pamoja na wabakiao nyuma (wenye nyudhuru), na nyoyo zao zikapigwa chapa kwa hivyo hawafahamu
لَٰكِنِ ٱلرَّسُولُ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مَعَهُۥ جَٰهَدُواْ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡۚ وَأُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمُ ٱلۡخَيۡرَٰتُۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ
Lakini Mtume na wale walioamini pamoja naye walipigana Jihadi kwa mali zao na nafsi zao. Na hao ndio watakaopata heri nyingi na hao ndio hasa wenye kufaulu
أَعَدَّ ٱللَّهُ لَهُمۡ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
Allah amewaandalia Pepo zipitazo mito mbele yake wadumu humo. Huko ndiko kufuzu kukubwa hasa
وَجَآءَ ٱلۡمُعَذِّرُونَ مِنَ ٱلۡأَعۡرَابِ لِيُؤۡذَنَ لَهُمۡ وَقَعَدَ ٱلَّذِينَ كَذَبُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥۚ سَيُصِيبُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ
Na walikuja wenye kujitia udhuru katika Mabedui ili wapewe ruhusa (ya kutokwenda vitani), na walikaa wale (wanafiki) waliomwambia uwongo Allah na Mtume wake. Itawafika (wale) waliokufuru katika wao (na kusema uongo) adhabu iumizayo sana