Capítulo: ADH-DHAARIYAAT 

Verso : 44

فَعَتَوۡاْ عَنۡ أَمۡرِ رَبِّهِمۡ فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّـٰعِقَةُ وَهُمۡ يَنظُرُونَ

Wakaasi amri ya bwana wao, basi ikawachukua adhabu ya moto hali yakuwa wao wakiangalia



Capítulo: ADH-DHAARIYAAT 

Verso : 45

فَمَا ٱسۡتَطَٰعُواْ مِن قِيَامٖ وَمَا كَانُواْ مُنتَصِرِينَ

Basi hawakuweza kusimama na hawakua wao wenye kushinda



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 51

وَثَمُودَاْ فَمَآ أَبۡقَىٰ

Na Watu wa Thamuwd kisha Hakuwabakisha



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 23

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِٱلنُّذُرِ

Kina Thamuwd waliwakadhibisha Waonyaji



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 24

فَقَالُوٓاْ أَبَشَرٗا مِّنَّا وَٰحِدٗا نَّتَّبِعُهُۥٓ إِنَّآ إِذٗا لَّفِي ضَلَٰلٖ وَسُعُرٍ

Wakasema: Ah! Tumfuate binaadamu miongoni mwetu? Hakika hapo sisi tutakuwa katika upotofu na wazimu



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 25

أَءُلۡقِيَ ٱلذِّكۡرُ عَلَيۡهِ مِنۢ بَيۡنِنَا بَلۡ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٞ

Ah! Ameteremshiwa ukumbusho (Wahyi) baina yetu? Bali yeye ni muongo mkubwa mwenye kiburi mno



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 26

سَيَعۡلَمُونَ غَدٗا مَّنِ ٱلۡكَذَّابُ ٱلۡأَشِرُ

Watakuja kujua kesho nani muongo mkubwa mwenye kiburi mno



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 27

إِنَّا مُرۡسِلُواْ ٱلنَّاقَةِ فِتۡنَةٗ لَّهُمۡ فَٱرۡتَقِبۡهُمۡ وَٱصۡطَبِرۡ

Hakika Sisi Tutawapelekea ngamia jike awe jaribio kwao, basi (Ee Nabiy Swaalih) watazame na vuta subira



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 28

وَنَبِّئۡهُمۡ أَنَّ ٱلۡمَآءَ قِسۡمَةُۢ بَيۡنَهُمۡۖ كُلُّ شِرۡبٖ مُّحۡتَضَرٞ

Na wajulishe kwamba maji ni mgawanyo baina yao (ngamia na wao), kila sehemu ya maji itahudhuriwa (kwa zamu)



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 29

فَنَادَوۡاْ صَاحِبَهُمۡ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ

Wakamuita Mtu Wao Akajipa Ushujaa Na Kumchinja



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 30

فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

Basi Vipi Ilikua Adhabu Yangu Na Maonyo yangu?



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 31

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ صَيۡحَةٗ وَٰحِدَةٗ فَكَانُواْ كَهَشِيمِ ٱلۡمُحۡتَظِرِ

Hakika Sisi Tulipeleka Kwao Ukelele Moja tu, wakawa kama mabuwa yaliyokatika-katika ya mtengenezaji zizi



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 4

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ وَعَادُۢ بِٱلۡقَارِعَةِ

Kina Thamudi na Adi walikadhibisha tukio (Kiyama) lenye kugonga (na kutia kiwewe)



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 5

فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهۡلِكُواْ بِٱلطَّاغِيَةِ

Ama kina Thamudi, waliangamizwa kwa ukelele mkali sana



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 6

وَأَمَّا عَادٞ فَأُهۡلِكُواْ بِرِيحٖ صَرۡصَرٍ عَاتِيَةٖ

Na ama kina Adi, waliangamizwa kwa upepo wenye baridi kali, uvumao kwa nguvu



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 7

سَخَّرَهَا عَلَيۡهِمۡ سَبۡعَ لَيَالٖ وَثَمَٰنِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومٗاۖ فَتَرَى ٱلۡقَوۡمَ فِيهَا صَرۡعَىٰ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٍ خَاوِيَةٖ

(Allah) Aliwapelekea mausiku saba na michana minane mfululizo (bila kupumzika). Basi utaona watu wameanguka kifudifudi kana kwamba ni magogo ya mitende yaliyo wazi ndani



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 8

فَهَلۡ تَرَىٰ لَهُم مِّنۢ بَاقِيَةٖ

Basi je, unamuona yeyote aliyebaki?



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 9

وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُواْ ٱلصَّخۡرَ بِٱلۡوَادِ

Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?



Capítulo: AL-SHAMS 

Verso : 11

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ

Kina Thamudi walikadhibisha kwasababu ya upotofu wao,



Capítulo: AL-SHAMS 

Verso : 12

إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا

Alipo simama mwovu wao mkubwa



Capítulo: AL-SHAMS 

Verso : 13

فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا

Hapo Mtume wa Allah alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Allah, mwacheni anywe maji fungu lake



Capítulo: AL-SHAMS 

Verso : 14

فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا

Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwahivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwasababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa



Capítulo: AL-SHAMS 

Verso : 15

وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا

Wala Yeye haogopi matokeo yake