إِنَّمَا حَرَّمَ عَلَيۡكُمُ ٱلۡمَيۡتَةَ وَٱلدَّمَ وَلَحۡمَ ٱلۡخِنزِيرِ وَمَآ أُهِلَّ بِهِۦ لِغَيۡرِ ٱللَّهِۖ فَمَنِ ٱضۡطُرَّ غَيۡرَ بَاغٖ وَلَا عَادٖ فَلَآ إِثۡمَ عَلَيۡهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٌ
Yeye tu amekuharamishieni mzoga na damu na nyama ya nguruwe na kilichochinjwa kwa kutaja jina lisiliokuwa la Allah. Lakini, aliyefikwa na dharura bila ya kutamani wala kupitiliza kiasi, hana dhambi[1]. Hakika, Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu
1- - Kula katika hivyo vilivyo haramishwa.
أُحِلَّ لَكُمۡ لَيۡلَةَ ٱلصِّيَامِ ٱلرَّفَثُ إِلَىٰ نِسَآئِكُمۡۚ هُنَّ لِبَاسٞ لَّكُمۡ وَأَنتُمۡ لِبَاسٞ لَّهُنَّۗ عَلِمَ ٱللَّهُ أَنَّكُمۡ كُنتُمۡ تَخۡتَانُونَ أَنفُسَكُمۡ فَتَابَ عَلَيۡكُمۡ وَعَفَا عَنكُمۡۖ فَٱلۡـَٰٔنَ بَٰشِرُوهُنَّ وَٱبۡتَغُواْ مَا كَتَبَ ٱللَّهُ لَكُمۡۚ وَكُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَكُمُ ٱلۡخَيۡطُ ٱلۡأَبۡيَضُ مِنَ ٱلۡخَيۡطِ ٱلۡأَسۡوَدِ مِنَ ٱلۡفَجۡرِۖ ثُمَّ أَتِمُّواْ ٱلصِّيَامَ إِلَى ٱلَّيۡلِۚ وَلَا تُبَٰشِرُوهُنَّ وَأَنتُمۡ عَٰكِفُونَ فِي ٱلۡمَسَٰجِدِۗ تِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِ فَلَا تَقۡرَبُوهَاۗ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ ٱللَّهُ ءَايَٰتِهِۦ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمۡ يَتَّقُونَ
Mmehalalishiwa usiku wafunga kukutana kimwili na wake zenu. Wao ni vazi lenu, na nyinyi ni vazi lao. Allah amejua kwamba mlikuwa mkizihini nafsi zenu. Kwa hivyo, amekukubalieni toba yenu na amekusameheni. Basi sasa kutaneni nao kimwili natakeni aliyokuandikieni Allah. Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa Alfajiri dhidi ya weusi wa usiku. Kisha timizeni funga mpaka usiku. Wala msikutane nao kimwili, na hali mmekaa Itikafu misikitini. Hiyo ni mipaka ya Allah, basi msiisogelee. Hivi ndivyo Allah anavyobainisha hoja zake kwa watu ili wapate kumcha
ٱلطَّلَٰقُ مَرَّتَانِۖ فَإِمۡسَاكُۢ بِمَعۡرُوفٍ أَوۡ تَسۡرِيحُۢ بِإِحۡسَٰنٖۗ وَلَا يَحِلُّ لَكُمۡ أَن تَأۡخُذُواْ مِمَّآ ءَاتَيۡتُمُوهُنَّ شَيۡـًٔا إِلَّآ أَن يَخَافَآ أَلَّا يُقِيمَا حُدُودَ ٱللَّهِۖ فَإِنۡ خِفۡتُمۡ أَلَّا يُقِيمَا حُدُودَ ٱللَّهِ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡهِمَا فِيمَا ٱفۡتَدَتۡ بِهِۦۗ تِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِ فَلَا تَعۡتَدُوهَاۚ وَمَن يَتَعَدَّ حُدُودَ ٱللَّهِ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ
Talaka ni mara mbili[1]. Basi (baada ya kumrejea) akae naye kwa wema au kumuacha kwa uzuri (aendelee kumaliza Eda yake). Na si halali kwenu kuchukua chochote katika vile mlivyowapa (wake zenu) isipokuwa kama wote wawili wataogopa kukiuka sharia za Allah. Basi kama mtaogopa kuwa hawatatekeleza sharia za Allah, hakuna ubaya kwa wawili (mke kurejesha mahari na mume kupokea) katika kile mwanamke alichojikombolea. Hiyo ni mipaka ya Allah, basi msiikiuke. Na watakaoikiuka mipaka ya Allah basi hao ni madhalimu hasa
1- - Ambazo mume ana haki ya kumrejea mkewe
فَإِن طَلَّقَهَا فَلَا تَحِلُّ لَهُۥ مِنۢ بَعۡدُ حَتَّىٰ تَنكِحَ زَوۡجًا غَيۡرَهُۥۗ فَإِن طَلَّقَهَا فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡهِمَآ أَن يَتَرَاجَعَآ إِن ظَنَّآ أَن يُقِيمَا حُدُودَ ٱللَّهِۗ وَتِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِ يُبَيِّنُهَا لِقَوۡمٖ يَعۡلَمُونَ
Na kama (mume) akimpa (mkewe) Talaka (ya tatu) basi si halali kwake (kumrejea au kumuoa upya) baada ya hapo mpaka afunge ndoa na mume mwingine. Na kama akimuacha (huyo mume wa pili) basi si vibaya kurejeana (kwa kufunga ndoa upya) kama wataona wanaweza kusimamisha mipaka ya Allah. Na hiyo ni mipaka ya Allah anayoibainisha kwa watu wanaojua
ٱلَّذِينَ يَأۡكُلُونَ ٱلرِّبَوٰاْ لَا يَقُومُونَ إِلَّا كَمَا يَقُومُ ٱلَّذِي يَتَخَبَّطُهُ ٱلشَّيۡطَٰنُ مِنَ ٱلۡمَسِّۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ قَالُوٓاْ إِنَّمَا ٱلۡبَيۡعُ مِثۡلُ ٱلرِّبَوٰاْۗ وَأَحَلَّ ٱللَّهُ ٱلۡبَيۡعَ وَحَرَّمَ ٱلرِّبَوٰاْۚ فَمَن جَآءَهُۥ مَوۡعِظَةٞ مِّن رَّبِّهِۦ فَٱنتَهَىٰ فَلَهُۥ مَا سَلَفَ وَأَمۡرُهُۥٓ إِلَى ٱللَّهِۖ وَمَنۡ عَادَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ
Wale wanaokula riba, hawatai-nuka isipokuwa kama anavyoinuka ambaye amepagawa kwa kukumbwa na Shetani. Hayo ni kwa sababu walisema kuwa biashara ni kama riba, na Allah ameihalalisha biashara na ameiharamisha riba. Basi ambaye amefikiwa na mawaidha kutoka kwa Mola wake na akaacha, basi yake ni yale yaliyokwishapita, na jambo lake lipo kwa Allah. Na watakaorejea, basi hao ndio watu wa Motoni, wao watakaa humo milele
تِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِۚ وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ يُدۡخِلۡهُ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ وَذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
Hiyo ndiyo mipaka ya Allah na yeyote mwenye kumtii Allah na Mtume wake atamuingiza katika Pepo itiririkayo mito chini yake, watabaki humo milele na huko ndiko kufaulu kuliko kukubwa
وَمَن يَعۡصِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَيَتَعَدَّ حُدُودَهُۥ يُدۡخِلۡهُ نَارًا خَٰلِدٗا فِيهَا وَلَهُۥ عَذَابٞ مُّهِينٞ
Na yeyote atakayemuasi Allah na Mtume wake na akakiuka mipaka yake atamuingiza katika Moto atabaki humo milele, na atakuwa na adhabu inayo dhalilisha
وَلَا تَنكِحُواْ مَا نَكَحَ ءَابَآؤُكُم مِّنَ ٱلنِّسَآءِ إِلَّا مَا قَدۡ سَلَفَۚ إِنَّهُۥ كَانَ فَٰحِشَةٗ وَمَقۡتٗا وَسَآءَ سَبِيلًا
Na msiwaoe wale walio olewa na baba zenu ispokuwa yaliyopita, tendo hilo ni baya na bughdha na ni njia mbaya
حُرِّمَتۡ عَلَيۡكُمۡ أُمَّهَٰتُكُمۡ وَبَنَاتُكُمۡ وَأَخَوَٰتُكُمۡ وَعَمَّـٰتُكُمۡ وَخَٰلَٰتُكُمۡ وَبَنَاتُ ٱلۡأَخِ وَبَنَاتُ ٱلۡأُخۡتِ وَأُمَّهَٰتُكُمُ ٱلَّـٰتِيٓ أَرۡضَعۡنَكُمۡ وَأَخَوَٰتُكُم مِّنَ ٱلرَّضَٰعَةِ وَأُمَّهَٰتُ نِسَآئِكُمۡ وَرَبَـٰٓئِبُكُمُ ٱلَّـٰتِي فِي حُجُورِكُم مِّن نِّسَآئِكُمُ ٱلَّـٰتِي دَخَلۡتُم بِهِنَّ فَإِن لَّمۡ تَكُونُواْ دَخَلۡتُم بِهِنَّ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ وَحَلَـٰٓئِلُ أَبۡنَآئِكُمُ ٱلَّذِينَ مِنۡ أَصۡلَٰبِكُمۡ وَأَن تَجۡمَعُواْ بَيۡنَ ٱلۡأُخۡتَيۡنِ إِلَّا مَا قَدۡ سَلَفَۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ غَفُورٗا رَّحِيمٗا
Wameharamishwa kwenu mama zenu, na binti zenu na dada zenu na shangazi zenu, na ndugu wa mama zenu na watoto wa kaka zenu, na watoto wa dada zenu, na mama zenu ambao wamewanyonyesha na dada zenu wa kunyonya, na mama wa wake zenu, na watoto wa wake zenu ambao wapo majumbani mwenu wanaotokana na wake mlio waingilia, kama (wake hao) hamjawaingilia, basi sivibaya kwenu[1]. Na (ni haramu kwenu) wake wa watoto wenu wa kuwazaa na (ni haramu) kuwakusanya mtu na dada yake ispokua yale yaliyopita, hakika Allah ni mwenye kusamehe mpole mno
1- - Endapo mtawaacha hao kabla ya kuwaingilia mnaruhusiwa kuwaoa
۞وَٱلۡمُحۡصَنَٰتُ مِنَ ٱلنِّسَآءِ إِلَّا مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُكُمۡۖ كِتَٰبَ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡۚ وَأُحِلَّ لَكُم مَّا وَرَآءَ ذَٰلِكُمۡ أَن تَبۡتَغُواْ بِأَمۡوَٰلِكُم مُّحۡصِنِينَ غَيۡرَ مُسَٰفِحِينَۚ فَمَا ٱسۡتَمۡتَعۡتُم بِهِۦ مِنۡهُنَّ فَـَٔاتُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ فَرِيضَةٗۚ وَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ فِيمَا تَرَٰضَيۡتُم بِهِۦ مِنۢ بَعۡدِ ٱلۡفَرِيضَةِۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمٗا
Na (ni haramu kwenu) wanawake walio katika ndoa isipokuwa wale mliowamiliki kwa mikono yenu ya kuume[1], (hili) Allah ameandika kwenu, na mmehalalishiwa (wanawake) wasiokuwa hawa mtake kwa mali zenu, kujilinda na kutofanya zinaa. Na wale (wake) mliokaa nao faragha (baada ya ndoa) kati ya hao, wapeni mahari yao ni lazima. Na si vibaya kwenu kwa mliyoridhiana katika yale yaliyotajwa[2]baada ya kutimiza wajibu, hakika Allah ni mjuzi mwenye hekima
1- - Ni haramu kumuoa mwanamke aliye katika ndoa isipokuwa kafiri endapo atatekwa katika vita ya jihadi ni halali baada ya kukaa wa kusubiria hali ya tumbo lake kuwa si mja mzito
2- - Amesema shekhe Siidy alipotafsiri aya hii wanazuoni waliyo wengi wamesema kuwa; Mwanamke kupunguza sehemu ya waliokubaliana au mwanaume kutoa zaidi ya walichoafikiana
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَوۡفُواْ بِٱلۡعُقُودِۚ أُحِلَّتۡ لَكُم بَهِيمَةُ ٱلۡأَنۡعَٰمِ إِلَّا مَا يُتۡلَىٰ عَلَيۡكُمۡ غَيۡرَ مُحِلِّي ٱلصَّيۡدِ وَأَنتُمۡ حُرُمٌۗ إِنَّ ٱللَّهَ يَحۡكُمُ مَا يُرِيدُ
Enyi mlioamini, tekelezeni makubaliano[1]. Mmehalalishiwa (kula) wanyama howa[2] (wafugwao), isipokuwa tu wale (wanyama) mnaosomewa (kwenye Qur’ani na Suna kuwa ni haramu) bila ya kuhalalisha kuwinda mkiwa katika Ihramu (utekelezaji wa ibada ya Hija au Umrah). Hakika, Allah anahukumu atakayo
1- - Allah anatuamrisha kutekeleza, makubaliano na mikataba.
2- - Wanyama howa ni ngamia, ng’ombe, kondoo na mbuzi.
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تُحِلُّواْ شَعَـٰٓئِرَ ٱللَّهِ وَلَا ٱلشَّهۡرَ ٱلۡحَرَامَ وَلَا ٱلۡهَدۡيَ وَلَا ٱلۡقَلَـٰٓئِدَ وَلَآ ءَآمِّينَ ٱلۡبَيۡتَ ٱلۡحَرَامَ يَبۡتَغُونَ فَضۡلٗا مِّن رَّبِّهِمۡ وَرِضۡوَٰنٗاۚ وَإِذَا حَلَلۡتُمۡ فَٱصۡطَادُواْۚ وَلَا يَجۡرِمَنَّكُمۡ شَنَـَٔانُ قَوۡمٍ أَن صَدُّوكُمۡ عَنِ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ أَن تَعۡتَدُواْۘ وَتَعَاوَنُواْ عَلَى ٱلۡبِرِّ وَٱلتَّقۡوَىٰۖ وَلَا تَعَاوَنُواْ عَلَى ٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡعُدۡوَٰنِۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۖ إِنَّ ٱللَّهَ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ
Enyi mlioamini, msizivunjie heshima alama za (dini) ya Allah[1] wala Miezi Mitukufu[2] wala Hadiy[3] wala vigwe[4], wala wakusudiao Nyumba Takatifu[5] wakitafuta fadhila na radhi za Mola wao. Na mkishatoka (katika Ibada ya Hija au Umrah) basi windeni (mkitaka kufanya hivyo). Na wala kule kuwachukia watu kwa kuwa walikuzuieni kufika Msikiti Mtukufu kusikupelekeeni kuwafanyia uadui (wa kuwaua na mfano wa hilo). Na saidianeni katika wema na ucha Mungu, na msisaidiane katika dhambi na uadui. Na mcheni Allah. Hakika, Allah ni Mkali sana wa kuadhibu
1- - Alama za dini ya Allah ni zile ibada kubwa kama Hija, Umra, Swala, Funga n.k.
2- - Miezi Mitukufu ni minne: Dhul-qaada, Dhulhija, Muharram na Rajab.
3- - Hadiyu ni wanyama wanaopelekwa Makka kwa kuchinjwa katika ibada ya Hija.
4- - Vigwe ni kamba za utambulisho anayofungwa mnyama shingoni ili kumtambulisha kuwa anapelekwa Makkah kwa kuchinjwa katika ibada ya Hija.
5- - Hawa ni wale Waislamu wanaokwenda Makka kwa makusudi ya kufanya ibada ya Hija au Umra.
حُرِّمَتۡ عَلَيۡكُمُ ٱلۡمَيۡتَةُ وَٱلدَّمُ وَلَحۡمُ ٱلۡخِنزِيرِ وَمَآ أُهِلَّ لِغَيۡرِ ٱللَّهِ بِهِۦ وَٱلۡمُنۡخَنِقَةُ وَٱلۡمَوۡقُوذَةُ وَٱلۡمُتَرَدِّيَةُ وَٱلنَّطِيحَةُ وَمَآ أَكَلَ ٱلسَّبُعُ إِلَّا مَا ذَكَّيۡتُمۡ وَمَا ذُبِحَ عَلَى ٱلنُّصُبِ وَأَن تَسۡتَقۡسِمُواْ بِٱلۡأَزۡلَٰمِۚ ذَٰلِكُمۡ فِسۡقٌۗ ٱلۡيَوۡمَ يَئِسَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِن دِينِكُمۡ فَلَا تَخۡشَوۡهُمۡ وَٱخۡشَوۡنِۚ ٱلۡيَوۡمَ أَكۡمَلۡتُ لَكُمۡ دِينَكُمۡ وَأَتۡمَمۡتُ عَلَيۡكُمۡ نِعۡمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ ٱلۡإِسۡلَٰمَ دِينٗاۚ فَمَنِ ٱضۡطُرَّ فِي مَخۡمَصَةٍ غَيۡرَ مُتَجَانِفٖ لِّإِثۡمٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Mmeharamishiwa (kula) mzoga[1] na damu na nyama ya nguruwe na (mnyama) aliyechinjwa pasina (kutajwa jina la) Allah na (mnyama) aliyekufa kwa kusongeka koo (kujinyonga) na aliyekufa kwa kupigwa na aliyekufa kwa kuporomoka na aliyekufa kwa kupigwa pembe (na mwenzake) na aliyeliwa (kwa kushambuliwa) na mnyama mkali ila (mliyemuwahi akiwa hai) mkamchinja. Na (pia mmeharamishiwa kula nyama ya mnyama) aliyechinjwa katika (sehem yalipo) masanamu.[2] Na (mmeharamishiwa) kutaka kujua mambo yaliyopangwa (na Allah ikiwemo kupiga ramli na mfano wa hilo) kwa kutumia mbao. Ilivyo ni kwamba hayo (yote) ni uovu. Leo waliokufuru wameikatia tamaa dini yenu, basi msiwaogope (isipokuwa) niogopeni Mimi. Leo nimekukamilishieni dini yenu na kukutimizieni neema yangu na nimeuchagua Uislamu uwe dini yenu. Na mwenye kushikwa na dhiki ya njaa kali pasipo na kukusudia dhambi (anaruhusiwa kula hivyo vilivyoharamishwa kwa sababu) hakika, Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa huruma
1- - Mzoga ni mnyama aliyekufa mwenyewe au amechinjwa bila ya kufuata taratibu za sheria ya Kiislamu; kibudu, nyamafu.
2- - Mnyama aliyechinjwa katika sehemu za masanamu, mizimu, makaburini nk. Ni haramu kula nyama yake.
يَسۡـَٔلُونَكَ مَاذَآ أُحِلَّ لَهُمۡۖ قُلۡ أُحِلَّ لَكُمُ ٱلطَّيِّبَٰتُ وَمَا عَلَّمۡتُم مِّنَ ٱلۡجَوَارِحِ مُكَلِّبِينَ تُعَلِّمُونَهُنَّ مِمَّا عَلَّمَكُمُ ٱللَّهُۖ فَكُلُواْ مِمَّآ أَمۡسَكۡنَ عَلَيۡكُمۡ وَٱذۡكُرُواْ ٱسۡمَ ٱللَّهِ عَلَيۡهِۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ
Wanakuuliza: Wamehalalishiwa (kula) nini? Sema: Mmehalalishiwa (kula) vilivyo vizuri (ambavyo havikukatazwa) na mlichowafunza Wanyama na ndege wakali (kukiwinda) mkiwa mmewafunza aliyokufunzeni Allah (taratibu za kuwinda). Basi kuleni kile walichokukamatieni. Na tajeni jina la Allah juu ya hilo (la mnapowatuma wanyama wa kuwinda). Na muogopeni Allah. Hakika, Allah ni Mwepesi sana wa kuhesabu
ٱلۡيَوۡمَ أُحِلَّ لَكُمُ ٱلطَّيِّبَٰتُۖ وَطَعَامُ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ حِلّٞ لَّكُمۡ وَطَعَامُكُمۡ حِلّٞ لَّهُمۡۖ وَٱلۡمُحۡصَنَٰتُ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ وَٱلۡمُحۡصَنَٰتُ مِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ مِن قَبۡلِكُمۡ إِذَآ ءَاتَيۡتُمُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ مُحۡصِنِينَ غَيۡرَ مُسَٰفِحِينَ وَلَا مُتَّخِذِيٓ أَخۡدَانٖۗ وَمَن يَكۡفُرۡ بِٱلۡإِيمَٰنِ فَقَدۡ حَبِطَ عَمَلُهُۥ وَهُوَ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ مِنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ
Leo mmehalalishiwa vilivyo vizuri. Na chakula cha waliopewa Kitabu ni halali kwenu na chakula chenu ni halali kwao. Na (mmehalalishiwa kuoa) wanawake waumini waliohifadhiwa na wanawake waliohifadhiwa katika waliopewa Kitabu kabla yenu mtakapowapa malipo (mahari) yao, mkikusudia kujihifadhi (na) sio wenye kukusudia uzinzi wala kuwaweka (wanawake hao) kinyumba. Na yeyote anayekataa kuamini, bila shaka amali zake (njema) zimeporomoka (zimepotea bure) na yeye Akhera atakuwa miongoni mwa wenye hasara
إِنَّآ أَنزَلۡنَا ٱلتَّوۡرَىٰةَ فِيهَا هُدٗى وَنُورٞۚ يَحۡكُمُ بِهَا ٱلنَّبِيُّونَ ٱلَّذِينَ أَسۡلَمُواْ لِلَّذِينَ هَادُواْ وَٱلرَّبَّـٰنِيُّونَ وَٱلۡأَحۡبَارُ بِمَا ٱسۡتُحۡفِظُواْ مِن كِتَٰبِ ٱللَّهِ وَكَانُواْ عَلَيۡهِ شُهَدَآءَۚ فَلَا تَخۡشَوُاْ ٱلنَّاسَ وَٱخۡشَوۡنِ وَلَا تَشۡتَرُواْ بِـَٔايَٰتِي ثَمَنٗا قَلِيلٗاۚ وَمَن لَّمۡ يَحۡكُم بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَٰفِرُونَ
Hakika, sisi tumeiteremsha Taurati (ambayo) ndani yake kuna muongozo na nuru. Wanahukumu kwayo Manabii ambao wamejisalimisha (kwa Allah) wakiwahukumu Wayahudi. Na pia (wanahukumu kwa Taurati hiyo) wachamungu (wa Kiyahudi) na wanazuoni (wa Kiyahudi), kwa sababu ya kitabu cha Allah walichotakiwa kukilinda na wakawa mashahidi juu ya hilo. Basi msiwaogope watu na niogopeni Mimi. Na msinunue (msibadilishe) Aya zangu kwa thamani chache. Na wasiohukumu kwa (sheria) aliyoiteremsha Allah, basi hao ndio makafiri[1]
1- - Aya hapa inawahusu wenye mamlaka ya utekelezaji wa hukumu na sio kila mtu anahusika. Pia baadhi ya watu wanaichukua Aya hii kwamba ni hoja ya kumtuhumu kuwa ni kafiri kila atendaye dhambi. Watu wa Suna (Ahlu Sunna Wal Jamaa) wanamhesabu mtu ni kafiri endapo atayakataa yaliyomo ndani ya Qur’ani kwa moyo wake na mdomo wake. Ama anayeamini kwa moyo wake na kutamka kwa mdomo wake kwamba yaliyomo ndani ya Qur’ani ni maneno ya Allah na ni sahihi ila tu hatekelezi kwa vitendo huyu haingii katika hukumu ya ukafiri.
وَكَتَبۡنَا عَلَيۡهِمۡ فِيهَآ أَنَّ ٱلنَّفۡسَ بِٱلنَّفۡسِ وَٱلۡعَيۡنَ بِٱلۡعَيۡنِ وَٱلۡأَنفَ بِٱلۡأَنفِ وَٱلۡأُذُنَ بِٱلۡأُذُنِ وَٱلسِّنَّ بِٱلسِّنِّ وَٱلۡجُرُوحَ قِصَاصٞۚ فَمَن تَصَدَّقَ بِهِۦ فَهُوَ كَفَّارَةٞ لَّهُۥۚ وَمَن لَّمۡ يَحۡكُم بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ
Na humo (ndani ya Taurati) tumewaandikia ya kwamba, roho kwa roho na jicho kwa jicho na pua kwa pua na sikio kwa sikio na jino kwa jino na majeraha ni kisasi. Basi atakayetoa sadaka (ya kusamehe haki yake kulipa kisasi) hiyo ni kafara yake (ya madhambi yake). Na wasiohukumu kwa (sheria) aliyoiteremsha Allah, basi hao ndio madhalimu
وَقَفَّيۡنَا عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِم بِعِيسَى ٱبۡنِ مَرۡيَمَ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِ مِنَ ٱلتَّوۡرَىٰةِۖ وَءَاتَيۡنَٰهُ ٱلۡإِنجِيلَ فِيهِ هُدٗى وَنُورٞ وَمُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِ مِنَ ٱلتَّوۡرَىٰةِ وَهُدٗى وَمَوۡعِظَةٗ لِّلۡمُتَّقِينَ
Na tuliwafuatishia kwa (ku-wapelekea) Issa bin Mariamu akiisadikisha Taurati iliyokuwepo kabla yake, na tukampa Injili (ambayo) ndani yake kuna muon-gozo na nuru na ikisadikisha Taurati iliyokuwepo kabla yake na ni muongozo na mawaidha kwa wacha Mungu
وَلۡيَحۡكُمۡ أَهۡلُ ٱلۡإِنجِيلِ بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ فِيهِۚ وَمَن لَّمۡ يَحۡكُم بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡفَٰسِقُونَ
Na wahukumu Watu wa Injili kwa sheria alizoziteremsha Allah humo. Na wasiohukumu kwa (sheria) aliyoiteremsha Allah basi hao ndio waovu
وَأَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ وَمُهَيۡمِنًا عَلَيۡهِۖ فَٱحۡكُم بَيۡنَهُم بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُۖ وَلَا تَتَّبِعۡ أَهۡوَآءَهُمۡ عَمَّا جَآءَكَ مِنَ ٱلۡحَقِّۚ لِكُلّٖ جَعَلۡنَا مِنكُمۡ شِرۡعَةٗ وَمِنۡهَاجٗاۚ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَجَعَلَكُمۡ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ وَلَٰكِن لِّيَبۡلُوَكُمۡ فِي مَآ ءَاتَىٰكُمۡۖ فَٱسۡتَبِقُواْ ٱلۡخَيۡرَٰتِۚ إِلَى ٱللَّهِ مَرۡجِعُكُمۡ جَمِيعٗا فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ فِيهِ تَخۡتَلِفُونَ
Na tumekuteremshia Kitabu kwa haki kikisadikisha vitabu vilivyokuwepo kabla yake na kikivitawala. Basi hukumu baina yao kwa (sheria) aliyokuteremshia Allah, na usifuate utashi wa nafsi zao ukaacha haki iliyokujia. Kila kundi katika nyinyi tumeliwekea sharia na njia. Na lau Allah angelitaka angekufanyeni (nyote) umma mmoja, lakini (amefanya hivyo) ili akujaribuni katika aliyokupeni. Basi shindaneni kwa mambo ya kheri. Kwa Allah tu ndio marejeo yenu nyote, na atakuambieni yale mliyokuwa mkitofautiana
وَأَنِ ٱحۡكُم بَيۡنَهُم بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ وَلَا تَتَّبِعۡ أَهۡوَآءَهُمۡ وَٱحۡذَرۡهُمۡ أَن يَفۡتِنُوكَ عَنۢ بَعۡضِ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ إِلَيۡكَۖ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَٱعۡلَمۡ أَنَّمَا يُرِيدُ ٱللَّهُ أَن يُصِيبَهُم بِبَعۡضِ ذُنُوبِهِمۡۗ وَإِنَّ كَثِيرٗا مِّنَ ٱلنَّاسِ لَفَٰسِقُونَ
Na hukumu baina yao kwa (sheria) aliyoiteremsha Allah, na usifuate utashi wa nafsi zao, na jihadhari nao wasije kukufitini[1] ukaacha baadhi ya aliyokuteremshia Allah. Na wakigeuka, basi jua kwamba, hakika Allah anataka kuwaadhibu kwa (sababu ya) baadhi ya dhambi zao. Na kwa hakika kabisa watu wengi ni waovu
1- - Kukupotosha na kujikuta unafuata na kutekeleza wayatakayo wao.
أَفَحُكۡمَ ٱلۡجَٰهِلِيَّةِ يَبۡغُونَۚ وَمَنۡ أَحۡسَنُ مِنَ ٱللَّهِ حُكۡمٗا لِّقَوۡمٖ يُوقِنُونَ
Je, ni hukumu za Kijahiliya tu wanazozitaka? Na ni nani mwenye sheria nzuri zaidi kuliko Allah, kwa watu wenye yakini?
۞قُلۡ تَعَالَوۡاْ أَتۡلُ مَا حَرَّمَ رَبُّكُمۡ عَلَيۡكُمۡۖ أَلَّا تُشۡرِكُواْ بِهِۦ شَيۡـٔٗاۖ وَبِٱلۡوَٰلِدَيۡنِ إِحۡسَٰنٗاۖ وَلَا تَقۡتُلُوٓاْ أَوۡلَٰدَكُم مِّنۡ إِمۡلَٰقٖ نَّحۡنُ نَرۡزُقُكُمۡ وَإِيَّاهُمۡۖ وَلَا تَقۡرَبُواْ ٱلۡفَوَٰحِشَ مَا ظَهَرَ مِنۡهَا وَمَا بَطَنَۖ وَلَا تَقۡتُلُواْ ٱلنَّفۡسَ ٱلَّتِي حَرَّمَ ٱللَّهُ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۚ ذَٰلِكُمۡ وَصَّىٰكُم بِهِۦ لَعَلَّكُمۡ تَعۡقِلُونَ
Sema: Njooni nisome yale Mola wenu aliyokuharamishieni (nayo ni) msikishirikishenaye kitu chochote na wazazi wawili wafanyieni yaliyo mazuri na msiwaue watoto wenu kwa sababu ya ufukara (umasikini kwa sababu) sisi tunakuruzukuni nyinyi na wao. Na msiyakaribie mambo machafu yaliyo dhihiri kati ya hayo na yaliyo ya siri. Na msiiue nafsi ambayo Allah ameharamisha (kuiua) ila kwa haki tu. Hayo amekuusieni (Allah) ili myatie akilini
وَلَا تَقۡرَبُواْ مَالَ ٱلۡيَتِيمِ إِلَّا بِٱلَّتِي هِيَ أَحۡسَنُ حَتَّىٰ يَبۡلُغَ أَشُدَّهُۥۚ وَأَوۡفُواْ ٱلۡكَيۡلَ وَٱلۡمِيزَانَ بِٱلۡقِسۡطِۖ لَا نُكَلِّفُ نَفۡسًا إِلَّا وُسۡعَهَاۖ وَإِذَا قُلۡتُمۡ فَٱعۡدِلُواْ وَلَوۡ كَانَ ذَا قُرۡبَىٰۖ وَبِعَهۡدِ ٱللَّهِ أَوۡفُواْۚ ذَٰلِكُمۡ وَصَّىٰكُم بِهِۦ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ
Na msizisogelee mali za Yatima ila kwa njia iliyo nzuri sana hadi afikie utu uzima wake. Na timizeni vipimo na mizani kwa uadilifu. Hatuilazimishi nafsi (jambo lolote) isipokuwa kwa kadiri ya vile iwezavyo. Na msemapo semeni kwa uadilifu hata ikiwa (ni dhidi ya) ndugu. Na ahadi za Allah zitekelezeni. Hayo amekuusieni (Allah) ili mpate kukumbuka
وَأَنَّ هَٰذَا صِرَٰطِي مُسۡتَقِيمٗا فَٱتَّبِعُوهُۖ وَلَا تَتَّبِعُواْ ٱلسُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمۡ عَن سَبِيلِهِۦۚ ذَٰلِكُمۡ وَصَّىٰكُم بِهِۦ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ
Na kwa hakika, hii ni njia yangu iliyonyooka, basi ifuateni. Na msifuate njia nyingine zikaku-farakanisheni muiache njia yake. Hayo amekuusieni (Allah) ili muwe wachaMungu
قُلۡ إِنَّمَا حَرَّمَ رَبِّيَ ٱلۡفَوَٰحِشَ مَا ظَهَرَ مِنۡهَا وَمَا بَطَنَ وَٱلۡإِثۡمَ وَٱلۡبَغۡيَ بِغَيۡرِ ٱلۡحَقِّ وَأَن تُشۡرِكُواْ بِٱللَّهِ مَا لَمۡ يُنَزِّلۡ بِهِۦ سُلۡطَٰنٗا وَأَن تَقُولُواْ عَلَى ٱللَّهِ مَا لَا تَعۡلَمُونَ
Sema: Hakika, ilivyo ni kwamba, Mola wangu Mlezi ameharamisha (mambo) machafu; ya dhahiri katika hayo na ya siri na dhambi na dhuluma bila ya haki yoyote,[1] na kuvishirikisha na Allah vitu ambavyo hakuviteremshia dalili (hoja) yoyote na (pia Allah ameharamisha) kumsemea Allah msiyoyajua
1- - Dhuluma bila ya haki ni dhuluma isiyokuwa na msingi wa kisheria. Ama kutekeleza haki kwa msingi wa sheria sio dhuluma wala ukandamizaji, ila tu limetumika neno dhuluma kwa ulinganifu wa lugha. Inayo onekana kama ni dhuluma kwenye macho ya wapingaji wa sheria za Allah ni kama kuuawa kwa mtu aliyethibitika kuua, kukatwa mkono mtu aliyethibitika kuiba n.k. Lakini hii sio dhuluma ila ni haki kwa sababu ni utekelezaji wa sheria.
مَا تَعۡبُدُونَ مِن دُونِهِۦٓ إِلَّآ أَسۡمَآءٗ سَمَّيۡتُمُوهَآ أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُم مَّآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بِهَا مِن سُلۡطَٰنٍۚ إِنِ ٱلۡحُكۡمُ إِلَّا لِلَّهِ أَمَرَ أَلَّا تَعۡبُدُوٓاْ إِلَّآ إِيَّاهُۚ ذَٰلِكَ ٱلدِّينُ ٱلۡقَيِّمُ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَ ٱلنَّاسِ لَا يَعۡلَمُونَ
(Nyinyi) Hamuabudu badala yake (Allah) ila majina tu mliyoyaita nyinyi na Baba zenu (kuwa ni Miungu). Allah hakuyateremshia majina hayo hoja yoyote. Hapana hukumu ila ya Allah tu. Ameamrisha msimuabudu yeyote isipokuwa Yeye tu. Hiyo ndiyo Dini sahihi lakini watu wengi hawajui
وَكَذَٰلِكَ أَنزَلۡنَٰهُ حُكۡمًا عَرَبِيّٗاۚ وَلَئِنِ ٱتَّبَعۡتَ أَهۡوَآءَهُم بَعۡدَ مَا جَآءَكَ مِنَ ٱلۡعِلۡمِ مَا لَكَ مِنَ ٱللَّهِ مِن وَلِيّٖ وَلَا وَاقٖ
Na kama hivi (tulivyoiteremsha hii Qur’an ikiwa imesheheni misingi ya dini) tumeiteremsha (pia hii) Qur’ani kuwa ni hukumu (kwa lugha ya) Kiarabu (ili ifahamike na kuhifadhiwa kwa wepesi). Na ukifuata matamanio yao baada ya kukujia elimu, hutakuwa na rafiki wala mlinzi wa kukukinga (na adhabu ya Allah
إِنَّمَا حَرَّمَ عَلَيۡكُمُ ٱلۡمَيۡتَةَ وَٱلدَّمَ وَلَحۡمَ ٱلۡخِنزِيرِ وَمَآ أُهِلَّ لِغَيۡرِ ٱللَّهِ بِهِۦۖ فَمَنِ ٱضۡطُرَّ غَيۡرَ بَاغٖ وَلَا عَادٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Kwa hakika (Allah) amewa-haramishia (katika wanyama) mzoga na damu (iliyomwagika baada ya mnyama kuchinjwa) na nyama ya nguruwe na (mnyama) aliyechinjwa si kwa ajili ya Allah (kama kuchinja kwa ajili ya mashetani). Lakini atakayelazimika (kula nyama hiyo kwa njaa asife kwa kukosa mbadala), bila kuasi wala kuchupa mipaka, basi hakika Allah ni msamehevu, mwenye rehema
وَلَا تَقُولُواْ لِمَا تَصِفُ أَلۡسِنَتُكُمُ ٱلۡكَذِبَ هَٰذَا حَلَٰلٞ وَهَٰذَا حَرَامٞ لِّتَفۡتَرُواْ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَۚ إِنَّ ٱلَّذِينَ يَفۡتَرُونَ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَ لَا يُفۡلِحُونَ
Na msiseme (enyi washirikina), kwa uongo ambao usemwao na ndimi zenu kuwa, hii halali (kwanini Allah ameiharamisha) na hii haramu (kwanini ameihalalisha), ili kumzulia Allah uongo. Hakika wale wamzuliao Allah uongo hawatafaulu[1]
1- - Katika Aya hii Allah anabainisha kuwa uhalali wa kitu na uharamu hatokani na utashi wa mtu ama watu, bali ni msingi uliyowekwa na Allah mwenyewe kwa viumbe wake, hivyo anawakemea washirikishaji na Makafiri kwa ujumla, wasihalalishe au kuharamisha kitu kwa utashi wa nafsi zao. Kilicho halali ni kile alicha halalisha Allah, na haramu ni kile alicho kiharamisha Allah.