أُحِلَّ لَكُمۡ لَيۡلَةَ ٱلصِّيَامِ ٱلرَّفَثُ إِلَىٰ نِسَآئِكُمۡۚ هُنَّ لِبَاسٞ لَّكُمۡ وَأَنتُمۡ لِبَاسٞ لَّهُنَّۗ عَلِمَ ٱللَّهُ أَنَّكُمۡ كُنتُمۡ تَخۡتَانُونَ أَنفُسَكُمۡ فَتَابَ عَلَيۡكُمۡ وَعَفَا عَنكُمۡۖ فَٱلۡـَٰٔنَ بَٰشِرُوهُنَّ وَٱبۡتَغُواْ مَا كَتَبَ ٱللَّهُ لَكُمۡۚ وَكُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَكُمُ ٱلۡخَيۡطُ ٱلۡأَبۡيَضُ مِنَ ٱلۡخَيۡطِ ٱلۡأَسۡوَدِ مِنَ ٱلۡفَجۡرِۖ ثُمَّ أَتِمُّواْ ٱلصِّيَامَ إِلَى ٱلَّيۡلِۚ وَلَا تُبَٰشِرُوهُنَّ وَأَنتُمۡ عَٰكِفُونَ فِي ٱلۡمَسَٰجِدِۗ تِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِ فَلَا تَقۡرَبُوهَاۗ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ ٱللَّهُ ءَايَٰتِهِۦ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمۡ يَتَّقُونَ
Mmehalalishiwa usiku wafunga kukutana kimwili na wake zenu. Wao ni vazi lenu, na nyinyi ni vazi lao. Allah amejua kwamba mlikuwa mkizihini nafsi zenu. Kwa hivyo, amekukubalieni toba yenu na amekusameheni. Basi sasa kutaneni nao kimwili natakeni aliyokuandikieni Allah. Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa Alfajiri dhidi ya weusi wa usiku. Kisha timizeni funga mpaka usiku. Wala msikutane nao kimwili, na hali mmekaa Itikafu misikitini. Hiyo ni mipaka ya Allah, basi msiisogelee. Hivi ndivyo Allah anavyobainisha hoja zake kwa watu ili wapate kumcha
وَيَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلۡمَحِيضِۖ قُلۡ هُوَ أَذٗى فَٱعۡتَزِلُواْ ٱلنِّسَآءَ فِي ٱلۡمَحِيضِ وَلَا تَقۡرَبُوهُنَّ حَتَّىٰ يَطۡهُرۡنَۖ فَإِذَا تَطَهَّرۡنَ فَأۡتُوهُنَّ مِنۡ حَيۡثُ أَمَرَكُمُ ٱللَّهُۚ إِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلتَّوَّـٰبِينَ وَيُحِبُّ ٱلۡمُتَطَهِّرِينَ
Na wanakuuliza kuhusu Hedhi. Sema: Huo ni uchafu. Basi waepukeni wanawake (wake zenu) katika kipindi cha Hedhi, na msiwasogelee (msifanye nao jimai) mpaka watoharike. Na watakapojitoharisha, basi waendeeni kwa kupitia alipokuamrisheni Allah. Hakika, Allah anawapenda wenye kujitoharisha na anawapenda wenye kutubu sana
نِسَآؤُكُمۡ حَرۡثٞ لَّكُمۡ فَأۡتُواْ حَرۡثَكُمۡ أَنَّىٰ شِئۡتُمۡۖ وَقَدِّمُواْ لِأَنفُسِكُمۡۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّكُم مُّلَٰقُوهُۗ وَبَشِّرِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Wake zenu ni mashamba yenu. Basi yaendeeni mashamba yenu namna mtakavyo. Na jifanyieni utangulizi. Na muogopeni Allah na jueni kuwa mtakutana naye. Na wape bishara wenye kuamini
وَٱلۡمُطَلَّقَٰتُ يَتَرَبَّصۡنَ بِأَنفُسِهِنَّ ثَلَٰثَةَ قُرُوٓءٖۚ وَلَا يَحِلُّ لَهُنَّ أَن يَكۡتُمۡنَ مَا خَلَقَ ٱللَّهُ فِيٓ أَرۡحَامِهِنَّ إِن كُنَّ يُؤۡمِنَّ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِۚ وَبُعُولَتُهُنَّ أَحَقُّ بِرَدِّهِنَّ فِي ذَٰلِكَ إِنۡ أَرَادُوٓاْ إِصۡلَٰحٗاۚ وَلَهُنَّ مِثۡلُ ٱلَّذِي عَلَيۡهِنَّ بِٱلۡمَعۡرُوفِۚ وَلِلرِّجَالِ عَلَيۡهِنَّ دَرَجَةٞۗ وَٱللَّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ
Na wanawake walioachwa wangoje Kurui tatu. Na haifai kwao kuficha alichoumba Allah kwenye mifuko yao ya uzazi ikiwa kweli wanamuamini Allah na Siku ya Mwisho. Na Waume wao wana haki zaidi ya kuwarejea katika muda huo kama wanakusudia suluhu. Na wanawake wanazo haki kwa waume wao kama walivyo na wajibu juu yao kwa wema. Na wanaume wana daraja zaidi kwa wake zao. Na Allah ni Mwenye nguvu nyingi, Mwenye hekima sana
ٱلطَّلَٰقُ مَرَّتَانِۖ فَإِمۡسَاكُۢ بِمَعۡرُوفٍ أَوۡ تَسۡرِيحُۢ بِإِحۡسَٰنٖۗ وَلَا يَحِلُّ لَكُمۡ أَن تَأۡخُذُواْ مِمَّآ ءَاتَيۡتُمُوهُنَّ شَيۡـًٔا إِلَّآ أَن يَخَافَآ أَلَّا يُقِيمَا حُدُودَ ٱللَّهِۖ فَإِنۡ خِفۡتُمۡ أَلَّا يُقِيمَا حُدُودَ ٱللَّهِ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡهِمَا فِيمَا ٱفۡتَدَتۡ بِهِۦۗ تِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِ فَلَا تَعۡتَدُوهَاۚ وَمَن يَتَعَدَّ حُدُودَ ٱللَّهِ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ
Talaka ni mara mbili[1]. Basi (baada ya kumrejea) akae naye kwa wema au kumuacha kwa uzuri (aendelee kumaliza Eda yake). Na si halali kwenu kuchukua chochote katika vile mlivyowapa (wake zenu) isipokuwa kama wote wawili wataogopa kukiuka sharia za Allah. Basi kama mtaogopa kuwa hawatatekeleza sharia za Allah, hakuna ubaya kwa wawili (mke kurejesha mahari na mume kupokea) katika kile mwanamke alichojikombolea. Hiyo ni mipaka ya Allah, basi msiikiuke. Na watakaoikiuka mipaka ya Allah basi hao ni madhalimu hasa
1- - Ambazo mume ana haki ya kumrejea mkewe
وَإِذَا طَلَّقۡتُمُ ٱلنِّسَآءَ فَبَلَغۡنَ أَجَلَهُنَّ فَأَمۡسِكُوهُنَّ بِمَعۡرُوفٍ أَوۡ سَرِّحُوهُنَّ بِمَعۡرُوفٖۚ وَلَا تُمۡسِكُوهُنَّ ضِرَارٗا لِّتَعۡتَدُواْۚ وَمَن يَفۡعَلۡ ذَٰلِكَ فَقَدۡ ظَلَمَ نَفۡسَهُۥۚ وَلَا تَتَّخِذُوٓاْ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ هُزُوٗاۚ وَٱذۡكُرُواْ نِعۡمَتَ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡ وَمَآ أَنزَلَ عَلَيۡكُم مِّنَ ٱلۡكِتَٰبِ وَٱلۡحِكۡمَةِ يَعِظُكُم بِهِۦۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ
Na mtakapowaacha wake na wakakaribia kumaliza muda wa Eda zao, basi ishini nao kwa wema (kwa kuwarejea) au muwaachie (wamalize Eda zao na wawe huru) kwa wema. Na msibaki nao kwa lengo la kuwadhuru ili kuwafanyia uonevu. Na yeyote atakaye fanya hivyo basi kwa hakika atakuwa amejidhulumu mwenyewe. Na msizifanyie mzaha Aya za Allah. Na kumbukeni neema za Allah kwenu, na kitabu na hekima alizokuteremshieni. Allah anakuonyeni kwa hayo, na mcheni Allah na jueni kwamba, Allah ni Mjuzi mno wa kila kitu
وَإِذَا طَلَّقۡتُمُ ٱلنِّسَآءَ فَبَلَغۡنَ أَجَلَهُنَّ فَلَا تَعۡضُلُوهُنَّ أَن يَنكِحۡنَ أَزۡوَٰجَهُنَّ إِذَا تَرَٰضَوۡاْ بَيۡنَهُم بِٱلۡمَعۡرُوفِۗ ذَٰلِكَ يُوعَظُ بِهِۦ مَن كَانَ مِنكُمۡ يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِۗ ذَٰلِكُمۡ أَزۡكَىٰ لَكُمۡ وَأَطۡهَرُۚ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ وَأَنتُمۡ لَا تَعۡلَمُونَ
Na mnapowaacha wake na wakamaliza Eda zao, basi nyinyi mawalii msiwazuie kufunga ndoa na waume zao waliowaacha iwapo wataridhiana kwa wema. Anapewa onyo hilo yule anayemuamini Allah miongoni mwenu na Siku ya Mwisho. Hayo kwenu ni bora mno na nisafi kabisa. Na Allah anajua ilihali nyinyi hamjui
۞وَٱلۡوَٰلِدَٰتُ يُرۡضِعۡنَ أَوۡلَٰدَهُنَّ حَوۡلَيۡنِ كَامِلَيۡنِۖ لِمَنۡ أَرَادَ أَن يُتِمَّ ٱلرَّضَاعَةَۚ وَعَلَى ٱلۡمَوۡلُودِ لَهُۥ رِزۡقُهُنَّ وَكِسۡوَتُهُنَّ بِٱلۡمَعۡرُوفِۚ لَا تُكَلَّفُ نَفۡسٌ إِلَّا وُسۡعَهَاۚ لَا تُضَآرَّ وَٰلِدَةُۢ بِوَلَدِهَا وَلَا مَوۡلُودٞ لَّهُۥ بِوَلَدِهِۦۚ وَعَلَى ٱلۡوَارِثِ مِثۡلُ ذَٰلِكَۗ فَإِنۡ أَرَادَا فِصَالًا عَن تَرَاضٖ مِّنۡهُمَا وَتَشَاوُرٖ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡهِمَاۗ وَإِنۡ أَرَدتُّمۡ أَن تَسۡتَرۡضِعُوٓاْ أَوۡلَٰدَكُمۡ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ إِذَا سَلَّمۡتُم مَّآ ءَاتَيۡتُم بِٱلۡمَعۡرُوفِۗ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ
Na wazazi wanawake wan-yonyeshe watoto wao miaka miwili kamili, kwa anayetaka kutimiza kunyonyesha. Na ni juu ya baba chakula chao (mama na mtoto) na kivazi chao kwa wema. Nafsi haikalifishwi (kufanya jambo) isipokuwa lililo ndani ya uwezo wake tu. Mama asidhuriwe kwa sababu ya mwanawe, na baba asidhuriwe kwa sababu ya mwanawe. Na ni wajibu juu ya mrithi (wa mtoto kufanya hayo). Na si vibaya kwa wawili hao (baba na mama) wakitaka kumwachisha ziwa (mtoto chini ya miaka miwili) kwa kushauriana na kuridhiana. Na mkitaka kuwapatia watoto wenu mama wa kuwanyonyesha, basi hapana ubaya kwenu mkitoa kile mlichowapa kwa njia ya wema. Na mcheni Allah na jueni kwamba Allah ni mwenye kuyaona sana yote myatendayo
وَٱلَّذِينَ يُتَوَفَّوۡنَ مِنكُمۡ وَيَذَرُونَ أَزۡوَٰجٗا يَتَرَبَّصۡنَ بِأَنفُسِهِنَّ أَرۡبَعَةَ أَشۡهُرٖ وَعَشۡرٗاۖ فَإِذَا بَلَغۡنَ أَجَلَهُنَّ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ فِيمَا فَعَلۡنَ فِيٓ أَنفُسِهِنَّ بِٱلۡمَعۡرُوفِۗ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ
Na wanaokufa miongoni mwenu na kuacha wake, wangoje wao wenyewe miezi minne na siku kumi. Na watakapotimiza Eda zao, basi hapana ubaya kwenu katika waliyojifanyia kwa wema. Na Allah anayajua vilivyo myafanyayo
وَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ فِيمَا عَرَّضۡتُم بِهِۦ مِنۡ خِطۡبَةِ ٱلنِّسَآءِ أَوۡ أَكۡنَنتُمۡ فِيٓ أَنفُسِكُمۡۚ عَلِمَ ٱللَّهُ أَنَّكُمۡ سَتَذۡكُرُونَهُنَّ وَلَٰكِن لَّا تُوَاعِدُوهُنَّ سِرًّا إِلَّآ أَن تَقُولُواْ قَوۡلٗا مَّعۡرُوفٗاۚ وَلَا تَعۡزِمُواْ عُقۡدَةَ ٱلنِّكَاحِ حَتَّىٰ يَبۡلُغَ ٱلۡكِتَٰبُ أَجَلَهُۥۚ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا فِيٓ أَنفُسِكُمۡ فَٱحۡذَرُوهُۚ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ غَفُورٌ حَلِيمٞ
Na si vibaya kwenu posa za fumbo mlizowafumbia au mlicho-kificha kwenye nafsi zenu. Allah amejua kuwa nyinyi mtawakumbuka hao, Na lakini msiwaahidi (ndoa) kwa siri isipokuwa mseme maneno mema. Na msiazimie kufunga nao ndoa mpaka Eda ifike mwisho wake. Na jueni kwamba Allah anajua yaliyomo katika nafsi zenu, basi jihadharini naye, najueni kwamba Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mpole mno
وَٱلَّذِينَ يُتَوَفَّوۡنَ مِنكُمۡ وَيَذَرُونَ أَزۡوَٰجٗا وَصِيَّةٗ لِّأَزۡوَٰجِهِم مَّتَٰعًا إِلَى ٱلۡحَوۡلِ غَيۡرَ إِخۡرَاجٖۚ فَإِنۡ خَرَجۡنَ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ فِي مَا فَعَلۡنَ فِيٓ أَنفُسِهِنَّ مِن مَّعۡرُوفٖۗ وَٱللَّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٞ
Na wale wanaokufa miongoni mwenu na wakaacha wake, waache Usia kwa ajili ya wake zao wapatiwe matunzo kwa mwaka mzima bila ya kuwatoa (majumbani). Na kama watatoka wenyewe, basi hakuna ubaya kwenu kwa kile walichokifanya kwenye nafsi zao. Na Allah ni Mwenye nguvu mno, Mwingi mno wa hekima
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا تَدَايَنتُم بِدَيۡنٍ إِلَىٰٓ أَجَلٖ مُّسَمّٗى فَٱكۡتُبُوهُۚ وَلۡيَكۡتُب بَّيۡنَكُمۡ كَاتِبُۢ بِٱلۡعَدۡلِۚ وَلَا يَأۡبَ كَاتِبٌ أَن يَكۡتُبَ كَمَا عَلَّمَهُ ٱللَّهُۚ فَلۡيَكۡتُبۡ وَلۡيُمۡلِلِ ٱلَّذِي عَلَيۡهِ ٱلۡحَقُّ وَلۡيَتَّقِ ٱللَّهَ رَبَّهُۥ وَلَا يَبۡخَسۡ مِنۡهُ شَيۡـٔٗاۚ فَإِن كَانَ ٱلَّذِي عَلَيۡهِ ٱلۡحَقُّ سَفِيهًا أَوۡ ضَعِيفًا أَوۡ لَا يَسۡتَطِيعُ أَن يُمِلَّ هُوَ فَلۡيُمۡلِلۡ وَلِيُّهُۥ بِٱلۡعَدۡلِۚ وَٱسۡتَشۡهِدُواْ شَهِيدَيۡنِ مِن رِّجَالِكُمۡۖ فَإِن لَّمۡ يَكُونَا رَجُلَيۡنِ فَرَجُلٞ وَٱمۡرَأَتَانِ مِمَّن تَرۡضَوۡنَ مِنَ ٱلشُّهَدَآءِ أَن تَضِلَّ إِحۡدَىٰهُمَا فَتُذَكِّرَ إِحۡدَىٰهُمَا ٱلۡأُخۡرَىٰۚ وَلَا يَأۡبَ ٱلشُّهَدَآءُ إِذَا مَا دُعُواْۚ وَلَا تَسۡـَٔمُوٓاْ أَن تَكۡتُبُوهُ صَغِيرًا أَوۡ كَبِيرًا إِلَىٰٓ أَجَلِهِۦۚ ذَٰلِكُمۡ أَقۡسَطُ عِندَ ٱللَّهِ وَأَقۡوَمُ لِلشَّهَٰدَةِ وَأَدۡنَىٰٓ أَلَّا تَرۡتَابُوٓاْ إِلَّآ أَن تَكُونَ تِجَٰرَةً حَاضِرَةٗ تُدِيرُونَهَا بَيۡنَكُمۡ فَلَيۡسَ عَلَيۡكُمۡ جُنَاحٌ أَلَّا تَكۡتُبُوهَاۗ وَأَشۡهِدُوٓاْ إِذَا تَبَايَعۡتُمۡۚ وَلَا يُضَآرَّ كَاتِبٞ وَلَا شَهِيدٞۚ وَإِن تَفۡعَلُواْ فَإِنَّهُۥ فُسُوقُۢ بِكُمۡۗ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۖ وَيُعَلِّمُكُمُ ٱللَّهُۗ وَٱللَّهُ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ
Enyi mliyoamini, mnapoko-peshana mkopo wowote kwa muda maalum, basi uandikeni. Na mwandishi aandike baina yenu kwa uadilifu. Na mwandishi asikatae kuandika. Aandike kama Allah alivyomfunza. Hivyo basi, aandike na ni juu ya mdaiwa kutoa maneno ya kuandikwa na amwogope Allah, Mola wake Mlezi, na asipunguze chochote ndani yake. Na kama yule anayedaiwa ni alie pumbaa mnyonge, au hawezi kuandikisha mwenyewe, basi msimamizi wake aandikishe kwa uadilifu. Na shuhudisheni mashahidi wawili wanaume waaminifu sana miongoni mwenu. Na iwapo hakuna wanaume wawili, basi (apatikane) mwanaume mmoja na wanawake wawili katika wale mnaowaridhia kuwa mashahidi, ili kama atasahau mmoja wa wanawake wawili, yule mwingine amkumbushe mwenzake. Na mashahidi wasikatae wanapoitwa. Na msikimwe kuliandika deni, likiwa dogo au kubwa, mpaka muda wake. Jambo hilo kwenu ni uadilifu zaidi mbele ya Allah, na sahihi zaidi kwa ushahidi, na pia inakurubisha mno kutokuwa na shaka, isipokuwa kama ni biashara mnayofanya kati yenu papo hapo, basi si dhambi kwenu msipoiandika. Na mnapouziana wekeni mashahidi. Wala asitiwe matatani mwandishi wala shahidi, na kama mkifanya hivyo (kuwatia matatani), basi kwa hakika huo ni uovu mkubwa kwenu. Na mwogopeni Allah, na Allah ndiye ana kuelimisheni; na Allah ni Mjuzi mno wa kila kitu
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا يَحِلُّ لَكُمۡ أَن تَرِثُواْ ٱلنِّسَآءَ كَرۡهٗاۖ وَلَا تَعۡضُلُوهُنَّ لِتَذۡهَبُواْ بِبَعۡضِ مَآ ءَاتَيۡتُمُوهُنَّ إِلَّآ أَن يَأۡتِينَ بِفَٰحِشَةٖ مُّبَيِّنَةٖۚ وَعَاشِرُوهُنَّ بِٱلۡمَعۡرُوفِۚ فَإِن كَرِهۡتُمُوهُنَّ فَعَسَىٰٓ أَن تَكۡرَهُواْ شَيۡـٔٗا وَيَجۡعَلَ ٱللَّهُ فِيهِ خَيۡرٗا كَثِيرٗا
Enyi mlioamini haifai kwenu kumrithi mke bila ridhaa yake[1] na msiwazuie kuolewa (sehemu nyingine) ili wasiondoke na mali mliyowapa ispokuwa kama watafanya zinaa ya wazi na ishini nao kwa wema, na endapo hamtawapenda basi (eleweni kuwa) huenda mkachukia kitu na Allah akajaalia kitu hicho kuwa na kheri nyingi
1- - Kwa kumuoa ndoa mpya na mahari mapya kinyume na ndoa ya mumewe aliyekufa. Wakati wa jahilia wanawake walilirithiwa kama zinavyorithia mali na vitu. mtu alipokufa kaka ama mtoto wa marehemu waliwafanya wake wa marehemu kuwa wake zao bila kuwaoa ndoa mpya au wao ndio waliwaozesha sehemu nyingine kwa kuchukua mahari au waliwazuia kuondoka hata kama hawakuwapenda kuishi nao kama mke ili wasiondoke na mali walizopata wakiwa kwao.
وَإِنۡ أَرَدتُّمُ ٱسۡتِبۡدَالَ زَوۡجٖ مَّكَانَ زَوۡجٖ وَءَاتَيۡتُمۡ إِحۡدَىٰهُنَّ قِنطَارٗا فَلَا تَأۡخُذُواْ مِنۡهُ شَيۡـًٔاۚ أَتَأۡخُذُونَهُۥ بُهۡتَٰنٗا وَإِثۡمٗا مُّبِينٗا
Na endapo mtataka kubadili mke sehemu ya mke aliyepo na mmoja wao mkampa mali nyingi basi msichukuwe katika mali hiyo chochote. mnakichukuaje kwa uongo na dhambi za wazi
وَلَا تَنكِحُواْ مَا نَكَحَ ءَابَآؤُكُم مِّنَ ٱلنِّسَآءِ إِلَّا مَا قَدۡ سَلَفَۚ إِنَّهُۥ كَانَ فَٰحِشَةٗ وَمَقۡتٗا وَسَآءَ سَبِيلًا
Na msiwaoe wale walio olewa na baba zenu ispokuwa yaliyopita, tendo hilo ni baya na bughdha na ni njia mbaya
حُرِّمَتۡ عَلَيۡكُمۡ أُمَّهَٰتُكُمۡ وَبَنَاتُكُمۡ وَأَخَوَٰتُكُمۡ وَعَمَّـٰتُكُمۡ وَخَٰلَٰتُكُمۡ وَبَنَاتُ ٱلۡأَخِ وَبَنَاتُ ٱلۡأُخۡتِ وَأُمَّهَٰتُكُمُ ٱلَّـٰتِيٓ أَرۡضَعۡنَكُمۡ وَأَخَوَٰتُكُم مِّنَ ٱلرَّضَٰعَةِ وَأُمَّهَٰتُ نِسَآئِكُمۡ وَرَبَـٰٓئِبُكُمُ ٱلَّـٰتِي فِي حُجُورِكُم مِّن نِّسَآئِكُمُ ٱلَّـٰتِي دَخَلۡتُم بِهِنَّ فَإِن لَّمۡ تَكُونُواْ دَخَلۡتُم بِهِنَّ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ وَحَلَـٰٓئِلُ أَبۡنَآئِكُمُ ٱلَّذِينَ مِنۡ أَصۡلَٰبِكُمۡ وَأَن تَجۡمَعُواْ بَيۡنَ ٱلۡأُخۡتَيۡنِ إِلَّا مَا قَدۡ سَلَفَۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ غَفُورٗا رَّحِيمٗا
Wameharamishwa kwenu mama zenu, na binti zenu na dada zenu na shangazi zenu, na ndugu wa mama zenu na watoto wa kaka zenu, na watoto wa dada zenu, na mama zenu ambao wamewanyonyesha na dada zenu wa kunyonya, na mama wa wake zenu, na watoto wa wake zenu ambao wapo majumbani mwenu wanaotokana na wake mlio waingilia, kama (wake hao) hamjawaingilia, basi sivibaya kwenu[1]. Na (ni haramu kwenu) wake wa watoto wenu wa kuwazaa na (ni haramu) kuwakusanya mtu na dada yake ispokua yale yaliyopita, hakika Allah ni mwenye kusamehe mpole mno
1- - Endapo mtawaacha hao kabla ya kuwaingilia mnaruhusiwa kuwaoa
۞وَٱلۡمُحۡصَنَٰتُ مِنَ ٱلنِّسَآءِ إِلَّا مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُكُمۡۖ كِتَٰبَ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡۚ وَأُحِلَّ لَكُم مَّا وَرَآءَ ذَٰلِكُمۡ أَن تَبۡتَغُواْ بِأَمۡوَٰلِكُم مُّحۡصِنِينَ غَيۡرَ مُسَٰفِحِينَۚ فَمَا ٱسۡتَمۡتَعۡتُم بِهِۦ مِنۡهُنَّ فَـَٔاتُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ فَرِيضَةٗۚ وَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ فِيمَا تَرَٰضَيۡتُم بِهِۦ مِنۢ بَعۡدِ ٱلۡفَرِيضَةِۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمٗا
Na (ni haramu kwenu) wanawake walio katika ndoa isipokuwa wale mliowamiliki kwa mikono yenu ya kuume[1], (hili) Allah ameandika kwenu, na mmehalalishiwa (wanawake) wasiokuwa hawa mtake kwa mali zenu, kujilinda na kutofanya zinaa. Na wale (wake) mliokaa nao faragha (baada ya ndoa) kati ya hao, wapeni mahari yao ni lazima. Na si vibaya kwenu kwa mliyoridhiana katika yale yaliyotajwa[2]baada ya kutimiza wajibu, hakika Allah ni mjuzi mwenye hekima
1- - Ni haramu kumuoa mwanamke aliye katika ndoa isipokuwa kafiri endapo atatekwa katika vita ya jihadi ni halali baada ya kukaa wa kusubiria hali ya tumbo lake kuwa si mja mzito
2- - Amesema shekhe Siidy alipotafsiri aya hii wanazuoni waliyo wengi wamesema kuwa; Mwanamke kupunguza sehemu ya waliokubaliana au mwanaume kutoa zaidi ya walichoafikiana
وَمَن لَّمۡ يَسۡتَطِعۡ مِنكُمۡ طَوۡلًا أَن يَنكِحَ ٱلۡمُحۡصَنَٰتِ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ فَمِن مَّا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُكُم مِّن فَتَيَٰتِكُمُ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتِۚ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِإِيمَٰنِكُمۚ بَعۡضُكُم مِّنۢ بَعۡضٖۚ فَٱنكِحُوهُنَّ بِإِذۡنِ أَهۡلِهِنَّ وَءَاتُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ بِٱلۡمَعۡرُوفِ مُحۡصَنَٰتٍ غَيۡرَ مُسَٰفِحَٰتٖ وَلَا مُتَّخِذَٰتِ أَخۡدَانٖۚ فَإِذَآ أُحۡصِنَّ فَإِنۡ أَتَيۡنَ بِفَٰحِشَةٖ فَعَلَيۡهِنَّ نِصۡفُ مَا عَلَى ٱلۡمُحۡصَنَٰتِ مِنَ ٱلۡعَذَابِۚ ذَٰلِكَ لِمَنۡ خَشِيَ ٱلۡعَنَتَ مِنكُمۡۚ وَأَن تَصۡبِرُواْ خَيۡرٞ لَّكُمۡۗ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Na asiyekuwa na uwezo wa kutosha miongoni mwenu (wa) kuoa wanawake waumini wenye kujihifadhi (waungwana), basi (oeni) wasichana (vijakazi)[1] wenu waumini mnaowamiliki. Na Allah anaijua sana imani yenu; nyinyi kwa nyinyi. Basi waoeni kwa idhini ya familia zao (zenye mamlaka ya kisheria ya kuwaozesha) na wapeni malipo (mahari) yao kwa wema wakiwa na lengo la kujihifadhi, wasio na lengo la kufanya uchafu (wa zinaa) wala kutengeneza wapenzi kinyume na sheria (mahawara). Basi wakishaingia katika hifadhi (ya ndoa), kama wakifanya uchafu (wa zinaa), basi adhabu yao ni nusu ya adhabu ya wanawake waungwana. Hayo ni kwa yule anayeogopa Zinaa miongoni mwenu. Na kama mtavumilia ni bora zaidi kwenu. Na Allah ni Mwingi wa kusamehe, mwenye huruma
1- - Kijakazi ni mtumwa wa kike. Mtumishi wa ndani wa kike nje ya utumwa hazingatiwi kuwa ni kijakazi.
وَلَا تَتَمَنَّوۡاْ مَا فَضَّلَ ٱللَّهُ بِهِۦ بَعۡضَكُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖۚ لِّلرِّجَالِ نَصِيبٞ مِّمَّا ٱكۡتَسَبُواْۖ وَلِلنِّسَآءِ نَصِيبٞ مِّمَّا ٱكۡتَسَبۡنَۚ وَسۡـَٔلُواْ ٱللَّهَ مِن فَضۡلِهِۦٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٗا
Na msitamani (kwa husuda) vile ambavyo Allah amewazidishia baadhi yenu kuliko wengine (katika riziki na vipaji). Wanaume wana fungu katika vile walivyochuma na wanawake wana fungu katika vile walivyochuma. Na muombeni Allah (awape) katika fadhila zake. Hakika, Allah ni Mjuzi wa kila kitu
ٱلرِّجَالُ قَوَّـٰمُونَ عَلَى ٱلنِّسَآءِ بِمَا فَضَّلَ ٱللَّهُ بَعۡضَهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ وَبِمَآ أَنفَقُواْ مِنۡ أَمۡوَٰلِهِمۡۚ فَٱلصَّـٰلِحَٰتُ قَٰنِتَٰتٌ حَٰفِظَٰتٞ لِّلۡغَيۡبِ بِمَا حَفِظَ ٱللَّهُۚ وَٱلَّـٰتِي تَخَافُونَ نُشُوزَهُنَّ فَعِظُوهُنَّ وَٱهۡجُرُوهُنَّ فِي ٱلۡمَضَاجِعِ وَٱضۡرِبُوهُنَّۖ فَإِنۡ أَطَعۡنَكُمۡ فَلَا تَبۡغُواْ عَلَيۡهِنَّ سَبِيلًاۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلِيّٗا كَبِيرٗا
Wanaume ni wasimamizi wakuu wa wanawake; kwasababu ya vile Allah alivyowazidishia baadhi yao kwa wengine, na kwa sababu ya mali zao walizozitoa (mahari, makazi, mavazi, chakula na matumizi yote ya msingi kwa jumla). Basi wanawake wema ni wale wenye kutii, na wanaojihifadhi hata katika siri kwasababu Allah ameamrisha wajihifadhi. Na wale mnaochelea uasi wao, basi waonyeni na wahameni vitandani na wapigeni.[1] Na kama watakutiini msiwatafutie njia (sababu ya kuwaadhibu na kuwaonea). Hakika Allah ndiye aliye juu na Mkuu
1- - Hizi ni hatua za kumuadabisha mke aliye asi: (a) Kumnasihi (b) Kumuhama kitandani (c) Kumpiga pigo lisilodhuru.
۞وَٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ وَلَا تُشۡرِكُواْ بِهِۦ شَيۡـٔٗاۖ وَبِٱلۡوَٰلِدَيۡنِ إِحۡسَٰنٗا وَبِذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡيَتَٰمَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينِ وَٱلۡجَارِ ذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡجَارِ ٱلۡجُنُبِ وَٱلصَّاحِبِ بِٱلۡجَنۢبِ وَٱبۡنِ ٱلسَّبِيلِ وَمَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُكُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ مَن كَانَ مُخۡتَالٗا فَخُورًا
Na mwabuduni Allah na msikishirikishe naye kitu chochote. Na wazazi wawili wafanyieni mazuri, na ndugu wa karibu (wa nasaba), na Yatima na maskini na jirani wa karibu (mwenye udugu wa nasaba) na jirani wa mbali (kwa makazi au udugu) na rafiki aliyeko ubavuni (rafiki mwenye usuhuba wa karibu na pia mke) na msafiri (aliyeharibikiwa) na wale walio chini ya mikono yenu ya kuume (watumwa waliopo chini ya miliki yenu). Hakika, Allah hawapendi wenye kiburi, wenye majivuno mengi
وَيَسۡتَفۡتُونَكَ فِي ٱلنِّسَآءِۖ قُلِ ٱللَّهُ يُفۡتِيكُمۡ فِيهِنَّ وَمَا يُتۡلَىٰ عَلَيۡكُمۡ فِي ٱلۡكِتَٰبِ فِي يَتَٰمَى ٱلنِّسَآءِ ٱلَّـٰتِي لَا تُؤۡتُونَهُنَّ مَا كُتِبَ لَهُنَّ وَتَرۡغَبُونَ أَن تَنكِحُوهُنَّ وَٱلۡمُسۡتَضۡعَفِينَ مِنَ ٱلۡوِلۡدَٰنِ وَأَن تَقُومُواْ لِلۡيَتَٰمَىٰ بِٱلۡقِسۡطِۚ وَمَا تَفۡعَلُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِهِۦ عَلِيمٗا
Na wanakuuliza Fat’wa[1] kuhusu wanawake. Sema: Allah anakupeni Fat`wa kuhusu wao na (kuhusu) yale yanayosomwa kwenu katika kitabu (hiki) kuhusu Yatima wanawake ambao hamuwapi kile kilicho wajibu kupewa na mnatamani kuwaoa, na (Fat’wa kuhusu) wale wanyonge miongoni mwa watoto na kwamba muwasimamie Yatima kwa uadilifu. Na kheri yoyote mnayoifanya basi hakika Allah anaijua sana
1- - Fat’wa katika Uislamu ni kutoa maelezo ya hukumu ya sheria, kwa maana ya kufafanua na sio kulazimisha. Anayefanya hivi anaitwa Mufti. Kadhi na Mufti wanatofautiana kwamba kazi ya Kadhi ni kutoa hukumu na kulazimisha utekelezwaji wa hukumu hiyo wakati kauli ya Mufti na ufafanuzi wa hukumu yake sio lazima kutekelezwa. Rejea kitabu cha Al-Ahkaamus Sultwaaniyyah cha Imamu Almaawardi, Allah amrehemu.
وَإِنِ ٱمۡرَأَةٌ خَافَتۡ مِنۢ بَعۡلِهَا نُشُوزًا أَوۡ إِعۡرَاضٗا فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡهِمَآ أَن يُصۡلِحَا بَيۡنَهُمَا صُلۡحٗاۚ وَٱلصُّلۡحُ خَيۡرٞۗ وَأُحۡضِرَتِ ٱلۡأَنفُسُ ٱلشُّحَّۚ وَإِن تُحۡسِنُواْ وَتَتَّقُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٗا
Na iwapo mwanamke (mke) yeyote atachelea uasi kwa mumewe au kutojaliwa (kupuuzwa na kutelekezwa) basi si vibaya kwao kufanya suluhu baina yao, na suluhu ni jambo la kheri sana. Na nafsi zimehudhurishiwa (zimesogezewa) ubahili[1]. Na iwapo mtafanya mazuri na mkamcha Allah, basi hakika Allah anayajua vyema yote mnayoyafanya
1- - Hapa Aya inaelezea uhalisia wa nafsi ya mwanadamu wakati wa ugonvi na mivutano ambapo kila upande unakuwa na umimi, kujipendelea, kukataa kujishusha na kuwa na ugumu na uzito wa kukubali kosa, kujirudi au kusamehe haki ili kufikia suluhu na muafaka.
وَلَن تَسۡتَطِيعُوٓاْ أَن تَعۡدِلُواْ بَيۡنَ ٱلنِّسَآءِ وَلَوۡ حَرَصۡتُمۡۖ فَلَا تَمِيلُواْ كُلَّ ٱلۡمَيۡلِ فَتَذَرُوهَا كَٱلۡمُعَلَّقَةِۚ وَإِن تُصۡلِحُواْ وَتَتَّقُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ غَفُورٗا رَّحِيمٗا
Na hamtaweza kufanya uadilifu baina ya wanawake (wake zenu) hata kama mtafanya jitihada. Basi (pamoja na hayo) msimili (msielemee) moja kwa moja (kwa mke mmoja), mkamuacha mwingine kama aliyetundikwa (aliyening’inizwa).[1] Na kama mtafanya usuluhishi na mkamcha Allah, hakika Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehem
1- - Waume wanakatazwa kutofanya uadilifu baina ya wake zao kwa kutotoa huduma stahiki kwa usawa au kwa kutelekeza baadhi. Hili halihusu mume mwenye wake zaidi ya mmoja tu, lakini linamhusu hata mume mwenye mke mmoja. Mume mwenye mke mmoja pia haruhusiwi kutomtendea uadilifu mkewe kwa kutompa haki zake au kwa kumtelekeza na kumuweka katika mazingira ya kutojitambua kwamba ni mke au sio mke. Uadilifu unaokusudia na sheria ni uadilifu wa huduma na sio hisia za mvuto, mahaba na mapenzi ya moyoni.
۞هُوَ ٱلَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفۡسٖ وَٰحِدَةٖ وَجَعَلَ مِنۡهَا زَوۡجَهَا لِيَسۡكُنَ إِلَيۡهَاۖ فَلَمَّا تَغَشَّىٰهَا حَمَلَتۡ حَمۡلًا خَفِيفٗا فَمَرَّتۡ بِهِۦۖ فَلَمَّآ أَثۡقَلَت دَّعَوَا ٱللَّهَ رَبَّهُمَا لَئِنۡ ءَاتَيۡتَنَا صَٰلِحٗا لَّنَكُونَنَّ مِنَ ٱلشَّـٰكِرِينَ
Yeye (Allah) Ndiye aliyeku-umbeni kutokana na nafsi moja (Adamu), na akajaalia kutoka katika nafsi hiyo mkewe ili apate utulivu kwake. Na (Adamu) alipomuingilia (mkewe) tu alibeba mimba nyepesi (kwa sababu ndio kwanza ilitunga) na aliweza kutembea nayo. Basi alipopata uzito (wa mimba kwa sababu ilikuwa kubwa) wote wawili (Adamu na mkewe) walimuomba Allah Mola wao Mlezi (na kusema): Kwa yakini kabisa (ewe Mola wetu), kama utatupa (mtoto) mwema bila shaka tutakuwa miongoni mwa wenye kushukuru
قَالَ رَبِّ ٱلسِّجۡنُ أَحَبُّ إِلَيَّ مِمَّا يَدۡعُونَنِيٓ إِلَيۡهِۖ وَإِلَّا تَصۡرِفۡ عَنِّي كَيۡدَهُنَّ أَصۡبُ إِلَيۡهِنَّ وَأَكُن مِّنَ ٱلۡجَٰهِلِينَ
(Yusuf) Alisema: “Ewe Mola wangu Mlezi, napenda zaidi kufungwa gerezani kuliko hili (hawa wanawake) wanaloniitia. Na usiponiondoshea vitimbi vyao (hawa wanawake) mimi nitavutika kwao na nitakuwa miongoni mwa wajinga
وَيَجۡعَلُونَ لِلَّهِ ٱلۡبَنَٰتِ سُبۡحَٰنَهُۥ وَلَهُم مَّا يَشۡتَهُونَ
Na wanamfanyia Allah mabinti (kwa kusema Malaika ni mabinti wa Allah!) utakasifu ni wake!(Allah ametakasika na kauli yao hiyo) Ilhali wanajifanyia wanachotaka
وَإِذَا بُشِّرَ أَحَدُهُم بِٱلۡأُنثَىٰ ظَلَّ وَجۡهُهُۥ مُسۡوَدّٗا وَهُوَ كَظِيمٞ
Na pindi mmoja wao anapopewa habari ya (kuzaliwa mtoto) mwa-namke, uso wake hugeuka mweusi, nakujawa na huzuni mno
يَتَوَٰرَىٰ مِنَ ٱلۡقَوۡمِ مِن سُوٓءِ مَا بُشِّرَ بِهِۦٓۚ أَيُمۡسِكُهُۥ عَلَىٰ هُونٍ أَمۡ يَدُسُّهُۥ فِي ٱلتُّرَابِۗ أَلَا سَآءَ مَا يَحۡكُمُونَ
Hujificha (asionekane) na watu kwasababu ya kujihisi vibaya kutokana na ile bishara aliyoiona kwake mbaya. (huku akijishauri kuhusu binti huyo) hivi, amchukue na avumilie fedheha au amfukie ardhini akiwa hai? Sikilizeni! Ni mabaya wanayoyahukumu
إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٰجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُمۡ فَإِنَّهُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ
Isipokuwa kwa wake zao au kwa wale (wanawake) iliyowamiliki mikono yao ya kulia. Kwani hao si wenye kulaumiwa