Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 61

وَإِذۡ قُلۡتُمۡ يَٰمُوسَىٰ لَن نَّصۡبِرَ عَلَىٰ طَعَامٖ وَٰحِدٖ فَٱدۡعُ لَنَا رَبَّكَ يُخۡرِجۡ لَنَا مِمَّا تُنۢبِتُ ٱلۡأَرۡضُ مِنۢ بَقۡلِهَا وَقِثَّآئِهَا وَفُومِهَا وَعَدَسِهَا وَبَصَلِهَاۖ قَالَ أَتَسۡتَبۡدِلُونَ ٱلَّذِي هُوَ أَدۡنَىٰ بِٱلَّذِي هُوَ خَيۡرٌۚ ٱهۡبِطُواْ مِصۡرٗا فَإِنَّ لَكُم مَّا سَأَلۡتُمۡۗ وَضُرِبَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلذِّلَّةُ وَٱلۡمَسۡكَنَةُ وَبَآءُو بِغَضَبٖ مِّنَ ٱللَّهِۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ كَانُواْ يَكۡفُرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَيَقۡتُلُونَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ بِغَيۡرِ ٱلۡحَقِّۚ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَواْ وَّكَانُواْ يَعۡتَدُونَ

Na (kumbukeni) mliposema: Ewe Musa, hatutaweza kuvumilia (kula) chakula cha aina moja tu. Basi tuombee kwa Mola wako atutolee katika vile ambavyo ardhi inaotesha, ikiwa ni pamoja na mboga mboga zake na matango yake na vitunguu saumu vyake na dengu zake na vitunguu maji vyake. Musa akasema: Hivi, mnataka kubadilisha ambacho ni duni sana kwa ambacho ni bora zaidi? Shukeni mjini. Huko mtapata hivyo mlivyovitaka. Na wakapigwa chapa ya udhalili na umaskini na wakastahiki ghadhabu za Allah. Hayo ni kwa sababu walikuwa wakizikufuru Aya za Allah na wakiwaua Mitume pasina haki yoyote. Hayo ni kwa sababu ya kuasi kwao, na walikuwa wakichupa mipaka



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 89

وَلَمَّا جَآءَهُمۡ كِتَٰبٞ مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِ مُصَدِّقٞ لِّمَا مَعَهُمۡ وَكَانُواْ مِن قَبۡلُ يَسۡتَفۡتِحُونَ عَلَى ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فَلَمَّا جَآءَهُم مَّا عَرَفُواْ كَفَرُواْ بِهِۦۚ فَلَعۡنَةُ ٱللَّهِ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na kilipowafikia Kitabu kito-kacho kwa Allah, kinachothibitisha (yale) waliyokuwa nayo, na huko kabla walikuwa wakiomba nusra dhidi ya wale waliokufuru, basi alipowajia huyo waliye mjua, walimkataa. Basi laana ya Allah iwe juu ya makafiri



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 90

بِئۡسَمَا ٱشۡتَرَوۡاْ بِهِۦٓ أَنفُسَهُمۡ أَن يَكۡفُرُواْ بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بَغۡيًا أَن يُنَزِّلَ ٱللَّهُ مِن فَضۡلِهِۦ عَلَىٰ مَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦۖ فَبَآءُو بِغَضَبٍ عَلَىٰ غَضَبٖۚ وَلِلۡكَٰفِرِينَ عَذَابٞ مُّهِينٞ

Ni kibaya mno walichojiuzia[1] cha kukataa yale aliyoyateremsha Allah kwa husuda ya kuwa Allah anamteremshia fadhila zake amtakaye miongoni mwa waja wake. Kwa sababu hiyo, walistahiki ghadhabu juu ya ghadhabu. Na makafiri watapata adhabu yenye kudhalilisha


1- - Walichojichagulia


Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 112

ضُرِبَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلذِّلَّةُ أَيۡنَ مَا ثُقِفُوٓاْ إِلَّا بِحَبۡلٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَحَبۡلٖ مِّنَ ٱلنَّاسِ وَبَآءُو بِغَضَبٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَضُرِبَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلۡمَسۡكَنَةُۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ كَانُواْ يَكۡفُرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَيَقۡتُلُونَ ٱلۡأَنۢبِيَآءَ بِغَيۡرِ حَقّٖۚ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَواْ وَّكَانُواْ يَعۡتَدُونَ

Wamepigwa chapa ya udhalili popote wanapokutwa, isipokuwa (kama) watakuwa wameshika kamba (dini) ya Allah au kamba (misaada) ya watu (wengine). Na wamestahiki ghadhabu za Allah na pia wamepigwa chapa ya umaskini. Hiyo ni kwasababu walikuwa wakizikataa Aya za Allah na kuua Mitume pasina haki yoyote. Hiyo ni kwa sababu ya uasi wao na walikuwa wakichupa mipaka ya sheria (za Allah)



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 162

أَفَمَنِ ٱتَّبَعَ رِضۡوَٰنَ ٱللَّهِ كَمَنۢ بَآءَ بِسَخَطٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَمَأۡوَىٰهُ جَهَنَّمُۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ

Je aliyefuata yanayomridhisha Allah, ni kama yule aliyestahiki ghadhabu kutoka kwa Allah na makazi yake kuwa jahannamu? Na hayo nimarejeo mabaya mno



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 93

وَمَن يَقۡتُلۡ مُؤۡمِنٗا مُّتَعَمِّدٗا فَجَزَآؤُهُۥ جَهَنَّمُ خَٰلِدٗا فِيهَا وَغَضِبَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِ وَلَعَنَهُۥ وَأَعَدَّ لَهُۥ عَذَابًا عَظِيمٗا

Na yeyote anayemuua Muumini (Muislamu) kwa kukusudia basi malipo yake ni Jahanamu, ataishi humo milele na Allah amemghadhibikia na amemlaani na amemuandalia adhabu kubwa kabisa



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 80

تَرَىٰ كَثِيرٗا مِّنۡهُمۡ يَتَوَلَّوۡنَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ لَبِئۡسَ مَا قَدَّمَتۡ لَهُمۡ أَنفُسُهُمۡ أَن سَخِطَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمۡ وَفِي ٱلۡعَذَابِ هُمۡ خَٰلِدُونَ

Utawaona wengi wao wana-wafanya makafiri marafiki (wao) wa ndani. Kwa yakini kabisa, ni maovu sana hayo yaliyotangulia kufanywa na nafsi zao hadi Allah amewakasirikia, na watadumu milele katika adhabu



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 152

إِنَّ ٱلَّذِينَ ٱتَّخَذُواْ ٱلۡعِجۡلَ سَيَنَالُهُمۡ غَضَبٞ مِّن رَّبِّهِمۡ وَذِلَّةٞ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۚ وَكَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُفۡتَرِينَ

Hakika, wale waliomfanya ndama (Mungu) itawapata adhabu ya Mola wao Mlezi na madhila katika maisha ya duniani. Na kama hivyo ndivyo tunavyowalipa wazushi



Capítulo: AN-FAL 

Verso : 16

وَمَن يُوَلِّهِمۡ يَوۡمَئِذٖ دُبُرَهُۥٓ إِلَّا مُتَحَرِّفٗا لِّقِتَالٍ أَوۡ مُتَحَيِّزًا إِلَىٰ فِئَةٖ فَقَدۡ بَآءَ بِغَضَبٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَمَأۡوَىٰهُ جَهَنَّمُۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ

Na yeyote atakayewageuzia mgongo wake siku hiyo (atakayewakimbia) isipokuwa kama (amefanya hivyo kama) mbinu za vita (geresha) au kuungana na kikosi (cha wapiganaji wenzake), basi atakuwa amestahiki ghadhabu kutoka kwa Allah na makazi yake ni Jahanamu, na huo ni mwisho mbaya mno



Capítulo: ANNAHLI 

Verso : 106

مَن كَفَرَ بِٱللَّهِ مِنۢ بَعۡدِ إِيمَٰنِهِۦٓ إِلَّا مَنۡ أُكۡرِهَ وَقَلۡبُهُۥ مُطۡمَئِنُّۢ بِٱلۡإِيمَٰنِ وَلَٰكِن مَّن شَرَحَ بِٱلۡكُفۡرِ صَدۡرٗا فَعَلَيۡهِمۡ غَضَبٞ مِّنَ ٱللَّهِ وَلَهُمۡ عَذَابٌ عَظِيمٞ

Hakika anayezusha uongo ni Yule aliyetamka neno la ukafiri baada ya imani isipokuwa tu yule aliyeshurutishwa, ilhali moyo wake unabaki imara katika imani. Lakini wale ambao mioyo yao imeridhika na ukafiri, basi ghadhabu za Allah zitawashukia, na watapata adhabu kubwa



Capítulo: TWAHA 

Verso : 81

كُلُواْ مِن طَيِّبَٰتِ مَا رَزَقۡنَٰكُمۡ وَلَا تَطۡغَوۡاْ فِيهِ فَيَحِلَّ عَلَيۡكُمۡ غَضَبِيۖ وَمَن يَحۡلِلۡ عَلَيۡهِ غَضَبِي فَقَدۡ هَوَىٰ

Kuleni katika vitu vizuri hivyo tulivyo kuruzukuni, wala msiruke mipaka katika hayo, isije ikakushukieni ghadhabu yangu. Na anayeshukiwa na ghadhabu yangu basi huyo ameangamia



Capítulo: ANNUUR 

Verso : 9

وَٱلۡخَٰمِسَةَ أَنَّ غَضَبَ ٱللَّهِ عَلَيۡهَآ إِن كَانَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ

Na mara ya tano ya kwamba ghadhabu ya Allah iwe juu yake kama mumewe yu miongoni mwa wanao sema kweli



Capítulo: FAATWIR 

Verso : 39

هُوَ ٱلَّذِي جَعَلَكُمۡ خَلَـٰٓئِفَ فِي ٱلۡأَرۡضِۚ فَمَن كَفَرَ فَعَلَيۡهِ كُفۡرُهُۥۖ وَلَا يَزِيدُ ٱلۡكَٰفِرِينَ كُفۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ إِلَّا مَقۡتٗاۖ وَلَا يَزِيدُ ٱلۡكَٰفِرِينَ كُفۡرُهُمۡ إِلَّا خَسَارٗا

Yeye ndiye aliye kufanyeni manaibu katika ardhi. Na anaye kufuru, basi kufuru yake ni juu yake; na kufuru za makafiri haziwazidishii kwa Mola wao Mlezi ila kuchukiwa. Wala kufuru za makafiri haziwazidishii ila khasara



Capítulo: GHAAFIR 

Verso : 10

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يُنَادَوۡنَ لَمَقۡتُ ٱللَّهِ أَكۡبَرُ مِن مَّقۡتِكُمۡ أَنفُسَكُمۡ إِذۡ تُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلۡإِيمَٰنِ فَتَكۡفُرُونَ

Kwa hakika wale walio kufuru watanadiwa: Bila ya shaka Allah kukuchukieni ni kukubwa kuliko kujichukia nyinyi nafsi zenu, mlipo kuwa mnaitwa kwenye Imani nanyi mkakataa



Capítulo: GHAAFIR 

Verso : 35

ٱلَّذِينَ يُجَٰدِلُونَ فِيٓ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ بِغَيۡرِ سُلۡطَٰنٍ أَتَىٰهُمۡۖ كَبُرَ مَقۡتًا عِندَ ٱللَّهِ وَعِندَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْۚ كَذَٰلِكَ يَطۡبَعُ ٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ قَلۡبِ مُتَكَبِّرٖ جَبَّارٖ

Hao ambao wanajadiliana katika Ishara za Allah pasipo ushahidi wowote ulio wafikia, ni chukizo kubwa mbele ya Allah na mbele ya walio amini. Hivi ndivyo Allah apigavyo muhuri juu ya kila moyo wa jeuri anaye jivuna



Capítulo: ASH-SHUURAA 

Verso : 16

وَٱلَّذِينَ يُحَآجُّونَ فِي ٱللَّهِ مِنۢ بَعۡدِ مَا ٱسۡتُجِيبَ لَهُۥ حُجَّتُهُمۡ دَاحِضَةٌ عِندَ رَبِّهِمۡ وَعَلَيۡهِمۡ غَضَبٞ وَلَهُمۡ عَذَابٞ شَدِيدٌ

Na wanaohojiana juu ya Allah baada ya kukubaliwa, hoja za hawa ni baatili mbele ya Mola wao Mlezi, na juu yao ipo ghadhabu, na itakuwa kwao adhabu kali



Capítulo: MUHAMMAD 

Verso : 27

فَكَيۡفَ إِذَا تَوَفَّتۡهُمُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ يَضۡرِبُونَ وُجُوهَهُمۡ وَأَدۡبَٰرَهُمۡ

Basi itakuwaje Malaika watakapo wafisha wakawa wanawapiga nyuso zao na migongo yao!



Capítulo: MUHAMMAD 

Verso : 28

ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمُ ٱتَّبَعُواْ مَآ أَسۡخَطَ ٱللَّهَ وَكَرِهُواْ رِضۡوَٰنَهُۥ فَأَحۡبَطَ أَعۡمَٰلَهُمۡ

Hayo ni kwasababu wao waliyafuata yaliyo mchukiza Allah na wakachukia yanayo mridhisha, basi akaviangusha vitendo vyao



Capítulo: AL-FAT-HI 

Verso : 6

وَيُعَذِّبَ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱلۡمُنَٰفِقَٰتِ وَٱلۡمُشۡرِكِينَ وَٱلۡمُشۡرِكَٰتِ ٱلظَّآنِّينَ بِٱللَّهِ ظَنَّ ٱلسَّوۡءِۚ عَلَيۡهِمۡ دَآئِرَةُ ٱلسَّوۡءِۖ وَغَضِبَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمۡ وَلَعَنَهُمۡ وَأَعَدَّ لَهُمۡ جَهَنَّمَۖ وَسَآءَتۡ مَصِيرٗا

Na awape adhabu wanafiki wanaume na wanaafiki wanawake, na washirikina wanaume na washirikina wanawake, wanao mdhania Allah dhana mbaya. Utawafikia mgeuko mbaya, na Allah awakasirikie, na awalaani, na awaandalie Jahannamu. Na hayo ni marudio maovu kabisa



Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 3

كَبُرَ مَقۡتًا عِندَ ٱللَّهِ أَن تَقُولُواْ مَا لَا تَفۡعَلُونَ

Imekuwa chukizo kubwa mno mbele ya Allah kwamba mnasema msiyoyafanya