Capítulo: ANNISAI 

Verso : 43

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَقۡرَبُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَأَنتُمۡ سُكَٰرَىٰ حَتَّىٰ تَعۡلَمُواْ مَا تَقُولُونَ وَلَا جُنُبًا إِلَّا عَابِرِي سَبِيلٍ حَتَّىٰ تَغۡتَسِلُواْۚ وَإِن كُنتُم مَّرۡضَىٰٓ أَوۡ عَلَىٰ سَفَرٍ أَوۡ جَآءَ أَحَدٞ مِّنكُم مِّنَ ٱلۡغَآئِطِ أَوۡ لَٰمَسۡتُمُ ٱلنِّسَآءَ فَلَمۡ تَجِدُواْ مَآءٗ فَتَيَمَّمُواْ صَعِيدٗا طَيِّبٗا فَٱمۡسَحُواْ بِوُجُوهِكُمۡ وَأَيۡدِيكُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَفُوًّا غَفُورًا

Enyi mlioamini, msiisogelee swala (msiswali) ilhali mmelewa, hadi mjue mnachosema.[1] Na (msiingie msikitini kwa ajili ya kuswali) mnapokuwa na janaba isipokuwa tu kama mtapita njia (kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine) hadi muoge. Na kama mkiwa wagonjwa (na hamuwezi kutawadha au kuoga kwa maji) au mkiwa safarini au mmoja wenu ametoka chooni (kukidhi haja) au mkigusana (mkiingiliana) na wake zenu na mkakosa maji, basi tayamamuni mchanga mzuri (safi); basi pakeni nyuso zenu na mikono yenu. Hakika, Allah amekuwa Msamehevu sana, Mfutaji dhambi


1- - Hapa ilikuwa pombe haijaharamishwa. Ama baada ya pombe kuharamishwa kabisa kwa aya ya 90 ya Sura Almaida (5), suala la mtu kuswali akiwa amelewa halipo, hata kama atakuwa anaelewa anachokisema na anachokifanya.


Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 6

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا قُمۡتُمۡ إِلَى ٱلصَّلَوٰةِ فَٱغۡسِلُواْ وُجُوهَكُمۡ وَأَيۡدِيَكُمۡ إِلَى ٱلۡمَرَافِقِ وَٱمۡسَحُواْ بِرُءُوسِكُمۡ وَأَرۡجُلَكُمۡ إِلَى ٱلۡكَعۡبَيۡنِۚ وَإِن كُنتُمۡ جُنُبٗا فَٱطَّهَّرُواْۚ وَإِن كُنتُم مَّرۡضَىٰٓ أَوۡ عَلَىٰ سَفَرٍ أَوۡ جَآءَ أَحَدٞ مِّنكُم مِّنَ ٱلۡغَآئِطِ أَوۡ لَٰمَسۡتُمُ ٱلنِّسَآءَ فَلَمۡ تَجِدُواْ مَآءٗ فَتَيَمَّمُواْ صَعِيدٗا طَيِّبٗا فَٱمۡسَحُواْ بِوُجُوهِكُمۡ وَأَيۡدِيكُم مِّنۡهُۚ مَا يُرِيدُ ٱللَّهُ لِيَجۡعَلَ عَلَيۡكُم مِّنۡ حَرَجٖ وَلَٰكِن يُرِيدُ لِيُطَهِّرَكُمۡ وَلِيُتِمَّ نِعۡمَتَهُۥ عَلَيۡكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ

Enyi mlioamini, mnaposimama kwenda kuswali[1], basi (tawadheni) osheni nyuso zenu na mikono yenu mpaka viwikoni na pakeni (maji) vichwa vyenu na (osheni) miguu yenu mpaka vifundoni[2]. Na mkiwa wenye Janaba basi jitwaharisheni (kwa kuoga au kutayamamu ikishindikana kuoga). Na mkiwa wagonjwa au mpo safarini au mmoja wenu ametoka msalani au mmegusana (mmejamiiana) na wanawake (wake zenu)[3] na hamkupata maji, basi tayamamuni (kusudieni) mchanga ulio safi[4] na mpake nyuso zenu na mikono yenu kwa mchanga huo[5]. Allah hataki kukuwekeeni tabu yoyote (uzito na usumbufu kwa kulazimisha kujitwaharisha kwa maji wakati maji hayapo au haiwezekani kuyatumia kwasababu ya ugonjwa au baridi kali); bali anataka kukutakaseni na kutimiza neema yake kwenu ili mpate kushukuru.[6]


1- - Hii ina maana hata kwa anayeswali kwa kuketi au kwa kulala ujumbe na utaratibu huu unamhusu pia.


2- - Kwenye Aya hii kuna visomo vikuu viwili vinavyokubalika: “Arjulakum” kwa Nasbu. Na kisomo cha pili ni “Arjulikum” kwa Jarri. Hii inamaanisha kwamba, kwa mujibu wa Qur’an na Suna sahihi za Mtume wa Allah uoshaji wa miguu una hukumu za aina mbili: (a) Kama miguu ikiwa wazi (haijavikwa kitu) faradhi yake ni kuoshwa kwa maji. (b) Kama miguu imevikwa khofu/soksi faradhi yake ni kupakwa maji.


3- - Muradi wa kugusana hapa ni kujamiiana. Kugusana tu kwa Ngozi na Ngozi hakulazimishi kutawadha.


4- - Kitendo hiki cha kutumia mchanga ulio safi na kupaka vumbi lake usoni na mikononi kinaitwa Tayamamu katika sheria ya Kiislamu.


5- - Kwa pigo la kwanza pakeni usoni na kwa pigo la pili pakeni mikononi.


6- - Aya hapa inaonesha kuwa ni lazima Muislamu kila anapotaka kuswali atawadhe. Lakini ulazima huu ni kwa yule ambaye hana Udhu. Ama mtu mwenye Udhu halazimiki kutawadha, lakini ni jambo zuri kama
atatawadha tena.