Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 124

۞وَإِذِ ٱبۡتَلَىٰٓ إِبۡرَٰهِـۧمَ رَبُّهُۥ بِكَلِمَٰتٖ فَأَتَمَّهُنَّۖ قَالَ إِنِّي جَاعِلُكَ لِلنَّاسِ إِمَامٗاۖ قَالَ وَمِن ذُرِّيَّتِيۖ قَالَ لَا يَنَالُ عَهۡدِي ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na (Kumbuka) Allah alipompa mtihani Ibrahimu wa maneno akayatimiza. Akasema: Hakika mimi nimekufanya kiongozi kwa watu. Akasema (Ibrahimu huku akiomba): Na katika kizazi changu? (Allah) Akasema: Ahadi yangu (hii) hawataipata madhalimu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 125

وَإِذۡ جَعَلۡنَا ٱلۡبَيۡتَ مَثَابَةٗ لِّلنَّاسِ وَأَمۡنٗا وَٱتَّخِذُواْ مِن مَّقَامِ إِبۡرَٰهِـۧمَ مُصَلّٗىۖ وَعَهِدۡنَآ إِلَىٰٓ إِبۡرَٰهِـۧمَ وَإِسۡمَٰعِيلَ أَن طَهِّرَا بَيۡتِيَ لِلطَّآئِفِينَ وَٱلۡعَٰكِفِينَ وَٱلرُّكَّعِ ٱلسُّجُودِ

Na (kumbuka) tulipoifanya Kaaba sehemu ya watu kurejea na mahali pa amani, nafanyeni mahali aliposimama Ibrahimu mahali pakuswali. Na tukawaagiza Ibrahimu na Ismaili, (kuwa) itwaharisheni Nyumba yangu kwa ajili ya wanaofanya twawafu na wanaokaa itikafu na wanaorukuu na kusujudu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 126

وَإِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِـۧمُ رَبِّ ٱجۡعَلۡ هَٰذَا بَلَدًا ءَامِنٗا وَٱرۡزُقۡ أَهۡلَهُۥ مِنَ ٱلثَّمَرَٰتِ مَنۡ ءَامَنَ مِنۡهُم بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِۚ قَالَ وَمَن كَفَرَ فَأُمَتِّعُهُۥ قَلِيلٗا ثُمَّ أَضۡطَرُّهُۥٓ إِلَىٰ عَذَابِ ٱلنَّارِۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ

Na (kumbuka) aliposema Ibrahimu: “Ewe Mola wangu, ufanye mji huu (wa Makkah) uwe wa amani, na waruzuku watu wake katika matunda; yule aliye muamini Allah miongoni mwao na kuamini Siku ya Mwisho. (Allah) akasema: Na mwenye kukufuru nitamstarehesha kidogo kisha nitamswaga kwenda kwenye adhabu ya moto, na hatima mbaya mno ni hiyo



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 127

وَإِذۡ يَرۡفَعُ إِبۡرَٰهِـۧمُ ٱلۡقَوَاعِدَ مِنَ ٱلۡبَيۡتِ وَإِسۡمَٰعِيلُ رَبَّنَا تَقَبَّلۡ مِنَّآۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Na (kumbuka wakati) Ibrahimu na Ismaili wanainua misingi ya Kaaba (wakisema): “Ewe Mola wetu, tukubalie. Hakika, wewe ndiye msikivu, mjuzi sana



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 128

رَبَّنَا وَٱجۡعَلۡنَا مُسۡلِمَيۡنِ لَكَ وَمِن ذُرِّيَّتِنَآ أُمَّةٗ مُّسۡلِمَةٗ لَّكَ وَأَرِنَا مَنَاسِكَنَا وَتُبۡ عَلَيۡنَآۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلتَّوَّابُ ٱلرَّحِيمُ

Ewe Mola wetu, tufanye sisi tuwe watiifu kwako, na katika kizazi chetu wawe umma mtiifu kwako. Na tuelekeze ibada zetu na pokea toba zetu. Hakika wewe tu ndiye mwingi wa kupokea toba mwingi wa rehema



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 129

رَبَّنَا وَٱبۡعَثۡ فِيهِمۡ رَسُولٗا مِّنۡهُمۡ يَتۡلُواْ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتِكَ وَيُعَلِّمُهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَيُزَكِّيهِمۡۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Ewe Mola wetu, na wapelekee Mtume miongoni mwao, atakayewasomea Aya zako na kuwafundisha kitabu na hekima na kuwatakasa. Hakika wewe tu ndiye mwenye nguvu kubwa mwingi wa hekima



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 130

وَمَن يَرۡغَبُ عَن مِّلَّةِ إِبۡرَٰهِـۧمَ إِلَّا مَن سَفِهَ نَفۡسَهُۥۚ وَلَقَدِ ٱصۡطَفَيۡنَٰهُ فِي ٱلدُّنۡيَاۖ وَإِنَّهُۥ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ لَمِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Na hakuna anayeichukia dini ya Ibrahimu isipokuwa yule anayejitia upumbavu. Na bila shaka tumemteua duniani, na hakika akhera atakuwa miongoni mwa watu wema



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 131

إِذۡ قَالَ لَهُۥ رَبُّهُۥٓ أَسۡلِمۡۖ قَالَ أَسۡلَمۡتُ لِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na (kumbuka) Mola wake alipomwambia: Jisalimishe. Akasema: Nimejisalimisha kwa Mola wa walimwengu wote



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 132

وَوَصَّىٰ بِهَآ إِبۡرَٰهِـۧمُ بَنِيهِ وَيَعۡقُوبُ يَٰبَنِيَّ إِنَّ ٱللَّهَ ٱصۡطَفَىٰ لَكُمُ ٱلدِّينَ فَلَا تَمُوتُنَّ إِلَّا وَأَنتُم مُّسۡلِمُونَ

Na Ibrahimu aliwausia hayo watoto wake na Yakubu (kwa kuwaambia): “Enyi watoto wangu, hakika Allah amekuteulieni dini, basi msife isipokuwa mkiwa Waisilamu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 258

أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِي حَآجَّ إِبۡرَٰهِـۧمَ فِي رَبِّهِۦٓ أَنۡ ءَاتَىٰهُ ٱللَّهُ ٱلۡمُلۡكَ إِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِـۧمُ رَبِّيَ ٱلَّذِي يُحۡيِۦ وَيُمِيتُ قَالَ أَنَا۠ أُحۡيِۦ وَأُمِيتُۖ قَالَ إِبۡرَٰهِـۧمُ فَإِنَّ ٱللَّهَ يَأۡتِي بِٱلشَّمۡسِ مِنَ ٱلۡمَشۡرِقِ فَأۡتِ بِهَا مِنَ ٱلۡمَغۡرِبِ فَبُهِتَ ٱلَّذِي كَفَرَۗ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Je, hukumuona yule aliyehojiana na Ibrahimu kuhusu Mola wake kwa sababu Allah alimpa ufalme? Pindi Ibrahim aliposema: Mola wangu ni yule anayehuisha na kufisha. Akasema: Mimi pia nahuisha na kufisha. Ibrahim akasema: Hakika Allah hulileta jua kutokea mashariki basi wewe lilete kutokea magharibi, basi akaduwaa yule aliyekufuru. Na Allah hawaongozi watu madhalimu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 260

وَإِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِـۧمُ رَبِّ أَرِنِي كَيۡفَ تُحۡيِ ٱلۡمَوۡتَىٰۖ قَالَ أَوَلَمۡ تُؤۡمِنۖ قَالَ بَلَىٰ وَلَٰكِن لِّيَطۡمَئِنَّ قَلۡبِيۖ قَالَ فَخُذۡ أَرۡبَعَةٗ مِّنَ ٱلطَّيۡرِ فَصُرۡهُنَّ إِلَيۡكَ ثُمَّ ٱجۡعَلۡ عَلَىٰ كُلِّ جَبَلٖ مِّنۡهُنَّ جُزۡءٗا ثُمَّ ٱدۡعُهُنَّ يَأۡتِينَكَ سَعۡيٗاۚ وَٱعۡلَمۡ أَنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٌ حَكِيمٞ

Na kumbuka Ibrahimu aliposema: (Ewe) Mola wangu, nioneshe namna unavyofufua wafu. Akamwambia: Kwani hukuamini? Akasema: Kwanini nisiamini? Bali nimeuliza hivyo ili moyo wangu utulie. Akasema: Basi chukua ndege wanne na uwakusanye kwako kisha weka juu ya kila jabali sehemu ya ndege hao, kisha uwaite, watakujia kwa kasi. Na jua ya kwamba, Allah ni Mwenye nguvu kubwa, Mwenye hekima nyingi



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 65

يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لِمَ تُحَآجُّونَ فِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَمَآ أُنزِلَتِ ٱلتَّوۡرَىٰةُ وَٱلۡإِنجِيلُ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِهِۦٓۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Enyi Watu wa Kitabu, kwanini mnaleta mijadala kuhusu Ibrahimu na ilhali Taurati na Injili hazikuteremshwa isipokuwa baada yake? Hivi hamtumii akili?



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 66

هَـٰٓأَنتُمۡ هَـٰٓؤُلَآءِ حَٰجَجۡتُمۡ فِيمَا لَكُم بِهِۦ عِلۡمٞ فَلِمَ تُحَآجُّونَ فِيمَا لَيۡسَ لَكُم بِهِۦ عِلۡمٞۚ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ وَأَنتُمۡ لَا تَعۡلَمُونَ

E nyinyi hawa! Mlihoji yale mnayoyajua, basi kwanini mnahoji msiyoyajua? Na Allah anajua na nyinyi hamjui



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 67

مَا كَانَ إِبۡرَٰهِيمُ يَهُودِيّٗا وَلَا نَصۡرَانِيّٗا وَلَٰكِن كَانَ حَنِيفٗا مُّسۡلِمٗا وَمَا كَانَ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ

Ibrahimu hakuwa Myahudi na wala (hakuwa) Mnaswara, lakini alikuwa Muongofu, Muislamu na hakuwa miongoni mwa Washirikina



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 68

إِنَّ أَوۡلَى ٱلنَّاسِ بِإِبۡرَٰهِيمَ لَلَّذِينَ ٱتَّبَعُوهُ وَهَٰذَا ٱلنَّبِيُّ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْۗ وَٱللَّهُ وَلِيُّ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika, watu walio na haki zaidi kwa Ibrahimu ni wale tu waliomfuata yeye na (kumfuata) Mtume huyu na wale walioamini. Na Allah ni Msimamizi wa Waumini



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 125

وَمَنۡ أَحۡسَنُ دِينٗا مِّمَّنۡ أَسۡلَمَ وَجۡهَهُۥ لِلَّهِ وَهُوَ مُحۡسِنٞ وَٱتَّبَعَ مِلَّةَ إِبۡرَٰهِيمَ حَنِيفٗاۗ وَٱتَّخَذَ ٱللَّهُ إِبۡرَٰهِيمَ خَلِيلٗا

Na hakuna aliye na dini iliyo nzuri (sahihi) sana kuliko yule aliyeusalimisha uso wake kwa Allah (kwa kumtii), naye akawa mwenye kufanya mazuri na akafuata dini ya Ibrahimu akijitenga na Shirki. Na Allah amemfanya Ibrahimu kipenzi (chake)



Capítulo: ANNISAI 

Verso : 163

۞إِنَّآ أَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡكَ كَمَآ أَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ نُوحٖ وَٱلنَّبِيِّـۧنَ مِنۢ بَعۡدِهِۦۚ وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡمَٰعِيلَ وَإِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَ وَٱلۡأَسۡبَاطِ وَعِيسَىٰ وَأَيُّوبَ وَيُونُسَ وَهَٰرُونَ وَسُلَيۡمَٰنَۚ وَءَاتَيۡنَا دَاوُۥدَ زَبُورٗا

Hakika, sisi tumekufunulia (Wahyi) kama tulivyomfunulia (Wahyi) Nuhu na Manabii (wengine) baada yake. Na tumemfunulia (Wahyi) Ibrahimu na Ismail na Isihaka na Yakubu na kizazi (chake) na Issa na Ayubu na Yunus na Haruna na Sulaimani. Na tulimpa Daudi Zaburi



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 74

۞وَإِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِيمُ لِأَبِيهِ ءَازَرَ أَتَتَّخِذُ أَصۡنَامًا ءَالِهَةً إِنِّيٓ أَرَىٰكَ وَقَوۡمَكَ فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٖ

Na (kumbuka Mtume) Ibrahimu alipomwambia baba yake Azar (kwamba): Hivi unayafanya masanamu Miungu? Hakika, mimi ninakuona wewe na watu wako kwamba mmo katika upotevu ulio wazi



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 75

وَكَذَٰلِكَ نُرِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ مَلَكُوتَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَلِيَكُونَ مِنَ ٱلۡمُوقِنِينَ

Na kama hivyo tunamuonyesha Ibrahimu ufalme wa mbinguni na ardhini, na ili awe miongoni mwa wenye yakini



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 76

فَلَمَّا جَنَّ عَلَيۡهِ ٱلَّيۡلُ رَءَا كَوۡكَبٗاۖ قَالَ هَٰذَا رَبِّيۖ فَلَمَّآ أَفَلَ قَالَ لَآ أُحِبُّ ٱلۡأٓفِلِينَ

Basi (Mtume Ibrahimu) ulipomjia usiku aliona nyota (na) akasema: Huyu ni Mola wangu Mlezi. (Nyota) Ilipozama alisema: Siwapendi wanaopotea



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 77

فَلَمَّا رَءَا ٱلۡقَمَرَ بَازِغٗا قَالَ هَٰذَا رَبِّيۖ فَلَمَّآ أَفَلَ قَالَ لَئِن لَّمۡ يَهۡدِنِي رَبِّي لَأَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلضَّآلِّينَ

Na alipoona mwezi umechomoza alisema: Huyu ni Mola wangu Mlezi. Na (mwezi) ulipozama alisema: Kama Mola wangu hataniongoza, kwa hakika kabisa nitakuwa miongoni mwa watu waliopotea



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 78

فَلَمَّا رَءَا ٱلشَّمۡسَ بَازِغَةٗ قَالَ هَٰذَا رَبِّي هَٰذَآ أَكۡبَرُۖ فَلَمَّآ أَفَلَتۡ قَالَ يَٰقَوۡمِ إِنِّي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تُشۡرِكُونَ

Na alipoliona jua limechomoza alisema: Huyu ni Mola wangu. Huyu ni mkubwa zaidi (kuliko wote). Basi (jua) lilipozama, alisema: Enyi watu wangu, mimi najitenga mbali na (Miungu yote) mnayoshirikisha (na Allah).[1]


1- - Nabii Ibrahimu katika mdahalo huu aliofanya na watu wake hakumaanisha kwamba na yeye aliamini kuwa nyota, mwezi na jua ni Miungu kama walivyoamini. Alichofanya ni maelekezo aliyopewa na Allah kama ilivyoelezwa katika Aya ya 83 ya Sura hii. Pia hiyo ni aina fulani ya mbinu za ufundishaji ya kujifanya unayemfundisha uko pamoja naye ili ufike naye kwenye ukweli na autambue kwa kutumia hoja, akili na mazingira. Nabii Ibrahimu hakuwa Mshirikishaji bali alikuwa Muumini safi anayemuamini na kumuabudu Allah tu. Rejea Aya 120-123 ya Sura Annahli (16).


Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 79

إِنِّي وَجَّهۡتُ وَجۡهِيَ لِلَّذِي فَطَرَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ حَنِيفٗاۖ وَمَآ أَنَا۠ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ

Hakika, mimi nimeelekeza uso wangu kwa (Allah) aliyeumba mbingu na ardhi, nikiacha itikadi zote potofu, na mimi si miongoni mwa washirikina



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 80

وَحَآجَّهُۥ قَوۡمُهُۥۚ قَالَ أَتُحَـٰٓجُّوٓنِّي فِي ٱللَّهِ وَقَدۡ هَدَىٰنِۚ وَلَآ أَخَافُ مَا تُشۡرِكُونَ بِهِۦٓ إِلَّآ أَن يَشَآءَ رَبِّي شَيۡـٔٗاۚ وَسِعَ رَبِّي كُلَّ شَيۡءٍ عِلۡمًاۚ أَفَلَا تَتَذَكَّرُونَ

Na watu wake wakamuwekea mdahalo. Alisema: Hivi, mnanihoji kuhusu Allah, na ilhali ameniongoa? Na siwaogopi hao mnaowashirikisha naye, isipokuwa kama Mola wangu atapenda jambo lolote (linipate). Mola wangu anajua kila kitu kwa mapana na marefu. Hivi hamuonyeki (na haya ninayokuambieni)?



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 81

وَكَيۡفَ أَخَافُ مَآ أَشۡرَكۡتُمۡ وَلَا تَخَافُونَ أَنَّكُمۡ أَشۡرَكۡتُم بِٱللَّهِ مَا لَمۡ يُنَزِّلۡ بِهِۦ عَلَيۡكُمۡ سُلۡطَٰنٗاۚ فَأَيُّ ٱلۡفَرِيقَيۡنِ أَحَقُّ بِٱلۡأَمۡنِۖ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Na vipi niwaogope wale (Miungu bandia) mliowashirikisha (na Allah) na ilhali nyinyi hamuogopi kwamba mmemshirikisha Allah na vitu ambavyo hakukuteremshieni hoja (yoyote)? Basi ni kundi lipi lililo na haki zaidi ya kuwa katika amani kati ya makundi mawili (ya mimi na nyinyi) ikiwa (kweli) mnajua?



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 82

ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَلَمۡ يَلۡبِسُوٓاْ إِيمَٰنَهُم بِظُلۡمٍ أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمُ ٱلۡأَمۡنُ وَهُم مُّهۡتَدُونَ

Wale walioamini na imani zao hawakuzichanganya na dhuluma (ushirikina), hao ndio wenye amani na hao ndio waongofu



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 83

وَتِلۡكَ حُجَّتُنَآ ءَاتَيۡنَٰهَآ إِبۡرَٰهِيمَ عَلَىٰ قَوۡمِهِۦۚ نَرۡفَعُ دَرَجَٰتٖ مَّن نَّشَآءُۗ إِنَّ رَبَّكَ حَكِيمٌ عَلِيمٞ

Na hizo ndio hoja zetu tulizompa (Mtume) Ibrahimu ajadiliane na watu wake[1]. Tunampandisha vyeo tumtakae. Hakika, Mola wako ni Mwenye hekima sana, Mjuzi mno


1- - Hapa Aya inathibitisha kuwa, mdahalo wa Nabii Ibrahimu na watu ni maelekezo ya Allah na hoja zote na mpangilio mzima ameelekezwa na Mola wake.


Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 161

قُلۡ إِنَّنِي هَدَىٰنِي رَبِّيٓ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ دِينٗا قِيَمٗا مِّلَّةَ إِبۡرَٰهِيمَ حَنِيفٗاۚ وَمَا كَانَ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ

Sema: Kwa hakika, mimi ameniongoza Mola wangu Mlezi kwenye njia iliyo nyooka; dini iliyo sawa kabisa, mila ya Ibrahimu aliyeacha itikadi zote potofu na hakuwa miongoni mwa washirikina



Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 114

وَمَا كَانَ ٱسۡتِغۡفَارُ إِبۡرَٰهِيمَ لِأَبِيهِ إِلَّا عَن مَّوۡعِدَةٖ وَعَدَهَآ إِيَّاهُ فَلَمَّا تَبَيَّنَ لَهُۥٓ أَنَّهُۥ عَدُوّٞ لِّلَّهِ تَبَرَّأَ مِنۡهُۚ إِنَّ إِبۡرَٰهِيمَ لَأَوَّـٰهٌ حَلِيمٞ

Na msamaha wa Ibrahimu wa kumuombea baba yake (kafiri) haukuwa isipokuwa tu ni kwa sababu ya ahadi aliyomuahidi.[1] Basi ilipombainikia kwamba yeye ni adui wa Allah (na ni mtu wa motoni), alijiepusha naye. Hakika kabisa, Ibrahimu alikuwa mnyenyekevu sana (katika maombi), mpole mno


1- - Allah ameitaja ahadi hii ya Nabii Ibrahimu kwa baba yake katika Qur’an, Sura Almumtahina (60), Aya ya 4 pale Allah aliposema: “Kwa hakika kabisa, mmekuwa na kiigizo kizuri kwa Ibrahimu na waliokuwa pamoja naye, walipowaambia watu wao: Kwa yakini sisi tumejitenga nanyi na hayo mnayoyaabudu badala ya Allah; tumewapingeni, naumedhihiri uadui na chuki ya kudumu (kati yetu na yenu) mpaka mmuamini Allah peke yake, isipokuwa kauli ya Ibrahimu kwa baba yake (aliyomuambia kwamba): Hakika, nitakuombea msamaha…”.


Capítulo: HUUD 

Verso : 69

وَلَقَدۡ جَآءَتۡ رُسُلُنَآ إِبۡرَٰهِيمَ بِٱلۡبُشۡرَىٰ قَالُواْ سَلَٰمٗاۖ قَالَ سَلَٰمٞۖ فَمَا لَبِثَ أَن جَآءَ بِعِجۡلٍ حَنِيذٖ

Na hakika walikuja wajumbe wetu kwa Ibrahimu kwa bishara njema, wakasema: Salama! Naye akasema: salama! Haukupita muda akaleta ndama wa kuchoma