Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 61

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 62

وَمِن دُونِهِمَا جَنَّتَانِ

Na zaidi ya hizo mbili, ziko bustani mbili zingine



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 63

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 64

مُدۡهَآمَّتَانِ

Za rangi ya kijani iliyokoza



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 65

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 66

فِيهِمَا عَيۡنَانِ نَضَّاخَتَانِ

Mna humo chemchemu mbili zenye kububujika kwa nguvu mfululizo



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 67

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 68

فِيهِمَا فَٰكِهَةٞ وَنَخۡلٞ وَرُمَّانٞ

Mna humo matunda na mitende na makomamanga



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 69

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 70

فِيهِنَّ خَيۡرَٰتٌ حِسَانٞ

Mna humo wanawake wema wazuri



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 71

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 72

حُورٞ مَّقۡصُورَٰتٞ فِي ٱلۡخِيَامِ

weupe wakiwa na macho mapana waliotawishwa kwenye mahema



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 73

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 74

لَمۡ يَطۡمِثۡهُنَّ إِنسٞ قَبۡلَهُمۡ وَلَا جَآنّٞ

hawajaguswa na Mtu kabla yao wala Jini



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 75

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 76

مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ رَفۡرَفٍ خُضۡرٖ وَعَبۡقَرِيٍّ حِسَانٖ

Wakiegemea kwenye matakia ya kijani na mazulia ya rangi mbalimbali ya hariri mazuri mno yasiyo na kifani



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 77

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Sura: ARRAHMAAN 

Aya : 78

تَبَٰرَكَ ٱسۡمُ رَبِّكَ ذِي ٱلۡجَلَٰلِ وَٱلۡإِكۡرَامِ

Limetukuka jina la Mola wako mwenye utukufu na ukarimu



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 1

إِذَا وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ

Wakati kitakapotokea Kiyama



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 2

لَيۡسَ لِوَقۡعَتِهَا كَاذِبَةٌ

Hakuna mpingaji wa kutokea kwake



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 3

خَافِضَةٞ رَّافِعَةٌ

Ni chenye kuwashusha hadhi (makafiri) na kuwanyanyua hadhi (waumini)



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 4

إِذَا رُجَّتِ ٱلۡأَرۡضُ رَجّٗا

Wakati ardhi itakapotikiswa mtikiso mkubwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 5

وَبُسَّتِ ٱلۡجِبَالُ بَسّٗا

Na milima ikapondwa pondwa upondwaji mkubwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 6

فَكَانَتۡ هَبَآءٗ مُّنۢبَثّٗا

(Kwa sababu ya kupondwa pondwa huko, milima) ikawa vumbi lenye kutawanyika



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 7

وَكُنتُمۡ أَزۡوَٰجٗا ثَلَٰثَةٗ

Na nyinyi (watu) mtakuwa namna tatu



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 8

فَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ

Basi watakuwepo watu wa kuliani. Je, ni kina nani watu wa kuliani?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 9

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ

Na (watakuwepo) watu wa kushotoni. Je, ni kina nani watu wa kushotoni?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 10

وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ

Na (watakuwepo) waliotangulia mbele, (basi) watakua mbele.[1]


1- - Hawa ni wale ambao walitangulia mbele katika mambo ya kheri duniani ndio watakuwa mbele katika vyeo vya akhera.


Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 11

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ

Hao ndio watakao kurubishwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 12

فِي جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ

katika pepo zenye neema