Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 43

وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ

Na kivuli cha moshi mweusi mnene wa joto kali mno



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 44

لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ

Si cha baridi na wala si cha kunufaisha



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 45

إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُتۡرَفِينَ

Hakika walikua kabla ya hapo kwenye maisha ya neema na anasa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 46

وَكَانُواْ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلۡحِنثِ ٱلۡعَظِيمِ

Na walikuwa wakishikilia kufanya dhambi kubwa mno



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 47

وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ

Na walikuwa wakisema: Je, hivi tutakapo kufa na tukawa udongo na mifupa, je hivi sisi hakika tutafufuliwa?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 48

أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ

Au na wazee wetu wa mwanzo?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 49

قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَوَّلِينَ وَٱلۡأٓخِرِينَ

Sema; Hakika wa mwanzo na wa mwisho,



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 50

لَمَجۡمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ

Hakika watakusanywa kwenye wakati na siku maalumu



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 51

ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ

Kisha hakika nyinyi enyi wapotovu mnaokadhibisha



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 52

لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ

Hakika mtakula chakula kitokanacho na mti wa mzakoum



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 53

فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ

Basi mtajaza kutokana na mti huo matumbo yenu



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 54

فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ

Na mtakunywa juu yake maji ya moto ya chemkayo



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 55

فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ

Tena mtakunywa unywaji wa ngamia mwenye kiu kubwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 56

هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Haya ndio mapokezi yao Siku ya Malipo! (Kiyama)



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 57

نَحۡنُ خَلَقۡنَٰكُمۡ فَلَوۡلَا تُصَدِّقُونَ

Sisi Tumekuumbeni, basi kwa nini hamsadikishi hilo?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 58

أَفَرَءَيۡتُم مَّا تُمۡنُونَ

Je, mnaona mbegu ya uzazi mnayo imwagia kwa nguvu?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 59

ءَأَنتُمۡ تَخۡلُقُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡخَٰلِقُونَ

Je, nyinyi ndio mnaiumba au sisi ndio Waumbaji?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 60

نَحۡنُ قَدَّرۡنَا بَيۡنَكُمُ ٱلۡمَوۡتَ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ

Sisi tumekadiria kati yenu umauti na haikua sisi wenye kukimbiwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 61

عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمۡثَٰلَكُمۡ وَنُنشِئَكُمۡ فِي مَا لَا تَعۡلَمُونَ

Kwamba Tuwabadilishe wengine mfano wenu, na Tukuumbeni katika umbo msilolijua



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 62

وَلَقَدۡ عَلِمۡتُمُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُولَىٰ فَلَوۡلَا تَذَكَّرُونَ

Na bila shaka mmejua umbo la kwanza, basi kwanini hamkumbuki?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 63

أَفَرَءَيۡتُم مَّا تَحۡرُثُونَ

Je, mnaona mbegu mnazo-zipanda?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 64

ءَأَنتُمۡ تَزۡرَعُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلزَّـٰرِعُونَ

Je, ni nyinyi ndio mnaziotesha, au Sisi ndio Wenye kuotesha mimea?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 65

لَوۡ نَشَآءُ لَجَعَلۡنَٰهُ حُطَٰمٗا فَظَلۡتُمۡ تَفَكَّهُونَ

Lau Tungelitaka, Tungelifanya mabua yaliyonyauka na mkabaki mnashangaa na kusikitika



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 66

إِنَّا لَمُغۡرَمُونَ

(Mkisema): Hakika sisi tumegharimika



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 67

بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ

Bali sisi tumenyimwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 68

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلۡمَآءَ ٱلَّذِي تَشۡرَبُونَ

Je, mnaona maji ambayo mnakunywa?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 69

ءَأَنتُمۡ أَنزَلۡتُمُوهُ مِنَ ٱلۡمُزۡنِ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنزِلُونَ

Je, ni nyinyi ndio mliyoyateremsha kutoka katika mawingu ya mvua au Sisi ndio Wateremshaji?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 70

لَوۡ نَشَآءُ جَعَلۡنَٰهُ أُجَاجٗا فَلَوۡلَا تَشۡكُرُونَ

Lau Tungelitaka, Tungeliyafanya ya chumvi kali chungu basi kwa nini hamshukuru?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 71

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِي تُورُونَ

Je, mnaona moto ambao mnauwasha?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 72

ءَأَنتُمۡ أَنشَأۡتُمۡ شَجَرَتَهَآ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنشِـُٔونَ

Je, ni nyinyi ndio mliouumba mti wake, au Sisi ndio Waumbaji wa mti huo?