Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 17

إِنَّ عَلَيۡنَا جَمۡعَهُۥ وَقُرۡءَانَهُۥ

Hakika ni juu Yetu kuikusanya na kukuwezesha kuisoma kwake



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 18

فَإِذَا قَرَأۡنَٰهُ فَٱتَّبِعۡ قُرۡءَانَهُۥ

Basi Tunapoisoma (kupitia Jibrili), fuata kusomwa kwake



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 19

ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا بَيَانَهُۥ

Kisha ni juu yetu kuubainisha



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 20

كَلَّا بَلۡ تُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ

Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 21

وَتَذَرُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ

Na mnaacha maisha ya Akhera, (kwa kutoijali Akhera)



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 22

وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاضِرَةٌ

Zipo Nyuso siku hiyo zitanawiri, (zitang’aa)



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 23

إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٞ

Zikimtazama Mola wake



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 24

وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذِۭ بَاسِرَةٞ

Na nyuso (nyenginezo) siku hiyo zitakunjana



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 25

تَظُنُّ أَن يُفۡعَلَ بِهَا فَاقِرَةٞ

Zikiwa na yakini kuwa zitafikiwa na msiba unaovunja uti wa mgongo



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 26

كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِيَ

Sivyo! Itakapofika (roho) kwenye mafupa ya koo, (mitulinga)



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 27

وَقِيلَ مَنۡۜ رَاقٖ

Na itasemwa: Ni nani tabibu wa kumponya?



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 28

وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلۡفِرَاقُ

Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 29

وَٱلۡتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ

Na utakapo ambatanishwa muundi kwa muundi



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 30

إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمَسَاقُ

Siku hiyo ndiyo (ya) kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako! (ama Peponi au Motoni)



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 31

فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ

Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali, (hakumsadiki Mtume wala Qur’ani)



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 32

وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ

Lakini alikadhibisha na akakengeuka



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 33

ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ

Kisha akaenda kwa watu wake wa nyumbani kwa maringo



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 34

أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰ

Ole wako! Ole wako! (Ewe unaye kadhibisha, utaangamia!)



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 35

ثُمَّ أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰٓ

Kisha! Ole wako! Ole wako! (Ewe unaye kadhibisha, utaangamia!)



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 36

أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَن يُتۡرَكَ سُدًى

Je, mwanadamu anadhani kuwa ataachwa bure tu?



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 37

أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ

Kwani yeye hakuwa tone la manii lililotonwa?



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 38

ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ

Kisha akawa pande la damu, (Allaah) Akamuumba na Akamsawazisha?



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 39

فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ

Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke



Sura: ALQIYAAMA 

Aya : 40

أَلَيۡسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰ

Je! Huyo (aliyefanya hivyo) hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?



Sura: AL-INSAAN

Aya : 1

هَلۡ أَتَىٰ عَلَى ٱلۡإِنسَٰنِ حِينٞ مِّنَ ٱلدَّهۡرِ لَمۡ يَكُن شَيۡـٔٗا مَّذۡكُورًا

Hakika, kilimpitia binaadamu kipindi katika zama kipindi (ambacho) hakuwa kitu kinachotajwa



Sura: AL-INSAAN

Aya : 2

إِنَّا خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ مِن نُّطۡفَةٍ أَمۡشَاجٖ نَّبۡتَلِيهِ فَجَعَلۡنَٰهُ سَمِيعَۢا بَصِيرًا

Hakika, sisi tumemuumba mwanadamu kutokana na mbegu ya uhai (Manii) iliyochanganyika ili tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tumemfanya ni mwenye kusikia, mwenye kuona



Sura: AL-INSAAN

Aya : 3

إِنَّا هَدَيۡنَٰهُ ٱلسَّبِيلَ إِمَّا شَاكِرٗا وَإِمَّا كَفُورًا

Hakika, sisi tumemuongoza (tumempa mwongozo unaofikishwa na Mitume); ama awe mwenye kushukuru au mwenye kukufuru



Sura: AL-INSAAN

Aya : 4

إِنَّآ أَعۡتَدۡنَا لِلۡكَٰفِرِينَ سَلَٰسِلَاْ وَأَغۡلَٰلٗا وَسَعِيرًا

Hakika sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na moto mkali



Sura: AL-INSAAN

Aya : 5

إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ يَشۡرَبُونَ مِن كَأۡسٖ كَانَ مِزَاجُهَا كَافُورًا

Hakika, watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri



Sura: AL-INSAAN

Aya : 6

عَيۡنٗا يَشۡرَبُ بِهَا عِبَادُ ٱللَّهِ يُفَجِّرُونَهَا تَفۡجِيرٗا

Ni chemchem watakayoinywa waja wa Allah, wakiifanya imiminike kwa wingi