Sura: ALLAIL 

Aya : 11

وَمَا يُغۡنِي عَنۡهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ

Na mali yake yatamfaa nini atakapo kuwa anadidimia?



Sura: ALLAIL 

Aya : 12

إِنَّ عَلَيۡنَا لَلۡهُدَىٰ

Hakika ni juu yetu kuonyesha uongofu



Sura: ALLAIL 

Aya : 13

وَإِنَّ لَنَا لَلۡأٓخِرَةَ وَٱلۡأُولَىٰ

Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia



Sura: ALLAIL 

Aya : 14

فَأَنذَرۡتُكُمۡ نَارٗا تَلَظَّىٰ

Basi nakuonyeni na Moto unao waka!



Sura: ALLAIL 

Aya : 15

لَا يَصۡلَىٰهَآ إِلَّا ٱلۡأَشۡقَى

Hatauingia ila mwovu kabisa!



Sura: ALLAIL 

Aya : 16

ٱلَّذِي كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ

Anaye kadhibisha na kupa mgongo



Sura: ALLAIL 

Aya : 17

وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلۡأَتۡقَى

Na mcha Mungu ataepushwa nao



Sura: ALLAIL 

Aya : 18

ٱلَّذِي يُؤۡتِي مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ

Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa



Sura: ALLAIL 

Aya : 19

وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعۡمَةٖ تُجۡزَىٰٓ

Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa



Sura: ALLAIL 

Aya : 20

إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ رَبِّهِ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa



Sura: ALLAIL 

Aya : 21

وَلَسَوۡفَ يَرۡضَىٰ

Naye atakuja ridhika!



Sura: ADH-DHUHAA 

Aya : 1

وَٱلضُّحَىٰ

Naapa kwa mchana!



Sura: ADH-DHUHAA 

Aya : 2

وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ

Na kwa usiku unapo tanda!



Sura: ADH-DHUHAA 

Aya : 3

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ

Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe



Sura: ADH-DHUHAA 

Aya : 4

وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ

Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia



Sura: ADH-DHUHAA 

Aya : 5

وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ

Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike



Sura: ADH-DHUHAA 

Aya : 6

أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ

Kwani hakukukuta yatima akakupa makazi?



Sura: ADH-DHUHAA 

Aya : 7

وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ

Na akakukuta umepotea akakuongoa?



Sura: ADH-DHUHAA 

Aya : 8

وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ

Akakukuta mhitaji akakutosheleza?



Sura: ADH-DHUHAA 

Aya : 9

فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ

Basi yatima usimwonee!



Sura: ADH-DHUHAA 

Aya : 10

وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ

Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!



Sura: ADH-DHUHAA 

Aya : 11

وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ

Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie



Sura: ASH-SHARHI 

Aya : 1

أَلَمۡ نَشۡرَحۡ لَكَ صَدۡرَكَ

Je, hatukukunjulia kifua chako?



Sura: ASH-SHARHI 

Aya : 2

وَوَضَعۡنَا عَنكَ وِزۡرَكَ

Na tukakuondolea mzigo wako?



Sura: ASH-SHARHI 

Aya : 3

ٱلَّذِيٓ أَنقَضَ ظَهۡرَكَ

Ulio vunja mgongo wako?



Sura: ASH-SHARHI 

Aya : 4

وَرَفَعۡنَا لَكَ ذِكۡرَكَ

Na tukakunyanyulia utajo wako?



Sura: ASH-SHARHI 

Aya : 5

فَإِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرًا

Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi,



Sura: ASH-SHARHI 

Aya : 6

إِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرٗا

Hakika pamoja na uzito upo wepesi



Sura: ASH-SHARHI 

Aya : 7

فَإِذَا فَرَغۡتَ فَٱنصَبۡ

Na ukipata faragha, fanya juhudi



Sura: ASH-SHARHI 

Aya : 8

وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَٱرۡغَب

Na kwa (ajili ya) Mola wako Mlezi ushughulike