Sura: AZZUMAR 

Aya : 25

كَذَّبَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ فَأَتَىٰهُمُ ٱلۡعَذَابُ مِنۡ حَيۡثُ لَا يَشۡعُرُونَ

Waliokuwa kabla yao walika-dhibisha, na ikawajia adhabu kutoka pahala wasipo patambua



Sura: AZZUMAR 

Aya : 26

فَأَذَاقَهُمُ ٱللَّهُ ٱلۡخِزۡيَ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَكۡبَرُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ

Basi Allah akawaonjesha fedheha katika uhai wa duniani. Na bila ya shaka adhabu ya Akhera ni kubwa zaidi; laiti wangelijua!



Sura: AZZUMAR 

Aya : 27

وَلَقَدۡ ضَرَبۡنَا لِلنَّاسِ فِي هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانِ مِن كُلِّ مَثَلٖ لَّعَلَّهُمۡ يَتَذَكَّرُونَ

Na bila ya shaka tumewapigia watu mifano ya kila namna katika hii Qur’ani ili wapate kukumbuka



Sura: AZZUMAR 

Aya : 28

قُرۡءَانًا عَرَبِيًّا غَيۡرَ ذِي عِوَجٖ لَّعَلَّهُمۡ يَتَّقُونَ

Qur’ani ya Kiarabu isiyo na upogo (isiyo na mashaka), ili wamche Mungu



Sura: AZZUMAR 

Aya : 29

ضَرَبَ ٱللَّهُ مَثَلٗا رَّجُلٗا فِيهِ شُرَكَآءُ مُتَشَٰكِسُونَ وَرَجُلٗا سَلَمٗا لِّرَجُلٍ هَلۡ يَسۡتَوِيَانِ مَثَلًاۚ ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِۚ بَلۡ أَكۡثَرُهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Allah amepiga mfano wa mtu mwenye mabwana washirika wanao gombana, na wa mtu mwengine aliye husika na bwana mmoja tu. Je! Wako sawa katika hali zao? Alhamdulillahi, Sifa njema zote ni za Allah! Lakini wengi wao hawajui



Sura: AZZUMAR 

Aya : 30

إِنَّكَ مَيِّتٞ وَإِنَّهُم مَّيِّتُونَ

Kwa hakika wewe utakufa, na wao watakufa



Sura: AZZUMAR 

Aya : 31

ثُمَّ إِنَّكُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ عِندَ رَبِّكُمۡ تَخۡتَصِمُونَ

Kisha bila ya shaka mtagombana Siku ya Kiyama mbele ya Mola wenu Mlezi