Sura: ATTIIN 

Aya : 1

وَٱلتِّينِ وَٱلزَّيۡتُونِ

Naapa kwa tini na zaituni



Sura: ATTIIN 

Aya : 2

وَطُورِ سِينِينَ

Na Mlima wa Sinai



Sura: ATTIIN 

Aya : 3

وَهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ ٱلۡأَمِينِ

Na mji huu (wa Makka) wenye amani



Sura: ATTIIN 

Aya : 4

لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِيٓ أَحۡسَنِ تَقۡوِيمٖ

Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa



Sura: ATTIIN 

Aya : 5

ثُمَّ رَدَدۡنَٰهُ أَسۡفَلَ سَٰفِلِينَ

Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!



Sura: ATTIIN 

Aya : 6

إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ فَلَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونٖ

Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha



Sura: ATTIIN 

Aya : 7

فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعۡدُ بِٱلدِّينِ

Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?



Sura: ATTIIN 

Aya : 8

أَلَيۡسَ ٱللَّهُ بِأَحۡكَمِ ٱلۡحَٰكِمِينَ

Kwani Allah si muadilifu kuliko mahakimu wote?



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 1

ٱقۡرَأۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلَّذِي خَلَقَ

Soma kwa jina la Mola wako Mlezi ambaye ameumba



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 2

خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِنۡ عَلَقٍ

Amemuumba binaadamu kwa tone la damu



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 3

ٱقۡرَأۡ وَرَبُّكَ ٱلۡأَكۡرَمُ

Soma! Na Mola wako Mlezi ni Mkarimu kushinda wote!



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 4

ٱلَّذِي عَلَّمَ بِٱلۡقَلَمِ

Ambaye amefundisha kwa kalamu



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 5

عَلَّمَ ٱلۡإِنسَٰنَ مَا لَمۡ يَعۡلَمۡ

Kamfundisha mtu aliyokuwa hayajui



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 6

كَلَّآ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَيَطۡغَىٰٓ

Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 7

أَن رَّءَاهُ ٱسۡتَغۡنَىٰٓ

Akijiona katajirika



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 8

إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجۡعَىٰٓ

Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 9

أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يَنۡهَىٰ

Umemwona yule anaye mkataza



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 10

عَبۡدًا إِذَا صَلَّىٰٓ

Mja anapo sali?



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 11

أَرَءَيۡتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلۡهُدَىٰٓ

Waonaje kama yeye yuko juu ya uwongofu?



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 12

أَوۡ أَمَرَ بِٱلتَّقۡوَىٰٓ

Au anaamrisha ucha Mungu?



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 13

أَرَءَيۡتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ

Waonaje kama yeye akikanusha na akarudi nyuma?



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 14

أَلَمۡ يَعۡلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ

Hajui ya kwamba Allah anaona?



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 15

كَلَّا لَئِن لَّمۡ يَنتَهِ لَنَسۡفَعَۢا بِٱلنَّاصِيَةِ

Si hivyo! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele (nywele za mbele)!



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 16

نَاصِيَةٖ كَٰذِبَةٍ خَاطِئَةٖ

Shungi la uwongo, lenye makosa!



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 17

فَلۡيَدۡعُ نَادِيَهُۥ

Basi na awaite wenzake!



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 18

سَنَدۡعُ ٱلزَّبَانِيَةَ

Nasi tutawaita Mazabania!



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 19

كَلَّا لَا تُطِعۡهُ وَٱسۡجُدۡۤ وَٱقۡتَرِب۩

Hasha! Usimtii! Nawe sujudu na ujongee!



Sura: AL-QADRI 

Aya : 1

إِنَّآ أَنزَلۡنَٰهُ فِي لَيۡلَةِ ٱلۡقَدۡرِ

Hakika Sisi tumeiteremsha (Qur’ani) katika Laylatul Qadri (Usikuwa mtukufu wenye Cheo)



Sura: AL-QADRI 

Aya : 2

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا لَيۡلَةُ ٱلۡقَدۡرِ

Na nini kitakacho kujuulisha nini Laylatul Qadri?



Sura: AL-QADRI 

Aya : 3

لَيۡلَةُ ٱلۡقَدۡرِ خَيۡرٞ مِّنۡ أَلۡفِ شَهۡرٖ

Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu